Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mbaroni kwa kuoa mtoto wa miaka minane

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Mbaroni kwa kuoa mtoto wa miaka minane

      Mbaroni kwa kuoa mtoto wa miaka minane



      na Grace Macha, Arusha

      MFANYABIASHARA wa jijini Arusha, Joseph Ngisha (24), anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuoa mtoto wa kike (jina limehifadhiwa) akiwa na umri wa miaka minane mwaka 2010 baada ya kumlipia mahari ya ng’ombe wanne kwa wazazi wake.

      Aidha baba wa mtoto huyo ambaye kwa sasa ana ujauzito wa miezi mitatu, Lemomomo Olokuto (42) mkazi wa Mto wa Mbu wilayani Monduli, naye anashikiliwa kwa tuhuma za kumuoza mtoto huyo kinyume cha sheria na haki za malezi ya watoto.
      Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, aliwaeleza waandishi wa habari jana kuwa walimkamata Ngisha, Julai 18 mwaka huu, saa 3:45 akiwa nyumbani kwake pamoja na mtoto huyo maeneo ya Sakina, Songambele.
      Alisema kuwa Ngisha alipohojiwa na polisi alikiri kumuoa binti huyo kwa kutoa mahari ya ng’ombe wanne huku akikanusha taarifa zilizotolewa na baba wa mtoto huyo, Olokuto aliyedai kuwa alimuoza mtoto huyo kwa mahari ya ngombe watatu.
      Alisema Ngisha alitiwa mbaroni Julai 18 mwaka huu, saa 3.45 asubuhi nyumbani kwake baada polisi kupata taarifa za siri na kumkuta akiishi na mtoto huyo huku akiwa amembebesha ujauzito wenye miezi mitatu.
      “Ngisha alianza kumchumbia mtoto huyo baada ya kuacha kunyonya kwa mama yake, alipofikisha umri wa miaka minane aliwafuata wazazi wake na kuwaeleza nia ya kutaka kumuoa,” alisema Sabas.
      Hata hivyo mama wa mtoto huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, inadaiwa kuwa hakukubaliana na mpango huo ambapo Ngisha alimdanganya kuwa anakwenda kumpeleka shule.
      “Taarifa za Ngisha kuishi na mtoto huyo kama mke ziligunduliwa na majirani kwani mara nyingi alikuwa akimfungia ndani bila mtu kujua huku akiwaeleza baadhi ya jamaa zake kuwa ni mdogo wake,” alisema.
      Kwa sasa mtoto huyo yuko chini ya uangalizi wa ofisi ya ustawi wa jamii jijini Arusha, akiendelea na uchunguzi wa afya kuangalia endapo amepata madhara yoyote kiafya zaidi ya hiyo mimba aliyo nayo kwa sasa.
      Kamanda Sabas alisema kuwa polisi wanaendelea na upelelezi juu ya tukio hilo ambapo ukikamilika watuhumiwa hao ambao kwa sasa wanashikiliwa na jeshi hilo watafikishwa mahakamani.


    2. #2
      mbalapala's Avatar
      Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 30
      Rep Power : 363
      Likes Received
      8
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Mpesapesa View Post
      Mbaroni kwa kuoa mtoto wa miaka minane


      na Grace Macha, Arusha

      MFANYABIASHARA wa jijini Arusha, Joseph Ngisha (24), anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuoa mtoto wa kike (jina limehifadhiwa) akiwa na umri wa miaka minane mwaka 2010 baada ya kumlipia mahari ya ng’ombe wanne kwa wazazi wake.

      Aidha baba wa mtoto huyo ambaye kwa sasa ana ujauzito wa miezi mitatu, Lemomomo Olokuto (42) mkazi wa Mto wa Mbu wilayani Monduli, naye anashikiliwa kwa tuhuma za kumuoza mtoto huyo kinyume cha sheria na haki za malezi ya watoto.
      Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, aliwaeleza waandishi wa habari jana kuwa walimkamata Ngisha, Julai 18 mwaka huu, saa 3:45 akiwa nyumbani kwake pamoja na mtoto huyo maeneo ya Sakina, Songambele.
      Alisema kuwa Ngisha alipohojiwa na polisi alikiri kumuoa binti huyo kwa kutoa mahari ya ng’ombe wanne huku akikanusha taarifa zilizotolewa na baba wa mtoto huyo, Olokuto aliyedai kuwa alimuoza mtoto huyo kwa mahari ya ngombe watatu.
      Alisema Ngisha alitiwa mbaroni Julai 18 mwaka huu, saa 3.45 asubuhi nyumbani kwake baada polisi kupata taarifa za siri na kumkuta akiishi na mtoto huyo huku akiwa amembebesha ujauzito wenye miezi mitatu.
      “Ngisha alianza kumchumbia mtoto huyo baada ya kuacha kunyonya kwa mama yake, alipofikisha umri wa miaka minane aliwafuata wazazi wake na kuwaeleza nia ya kutaka kumuoa,” alisema Sabas.
      Hata hivyo mama wa mtoto huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, inadaiwa kuwa hakukubaliana na mpango huo ambapo Ngisha alimdanganya kuwa anakwenda kumpeleka shule.
      “Taarifa za Ngisha kuishi na mtoto huyo kama mke ziligunduliwa na majirani kwani mara nyingi alikuwa akimfungia ndani bila mtu kujua huku akiwaeleza baadhi ya jamaa zake kuwa ni mdogo wake,” alisema.
      Kwa sasa mtoto huyo yuko chini ya uangalizi wa ofisi ya ustawi wa jamii jijini Arusha, akiendelea na uchunguzi wa afya kuangalia endapo amepata madhara yoyote kiafya zaidi ya hiyo mimba aliyo nayo kwa sasa.
      Kamanda Sabas alisema kuwa polisi wanaendelea na upelelezi juu ya tukio hilo ambapo ukikamilika watuhumiwa hao ambao kwa sasa wanashikiliwa na jeshi hilo watafikishwa mahakamani.
      Duu miaka nane kishabeba mimba! Sasa ile kitu ungo aliuvunja lini jamani? Makubwa ya Joseph Ngisha!

    3. #3
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,989
      Rep Power : 16312
      Likes Received
      3404
      Likes Given
      4352

      Default Re: Mbaroni kwa kuoa mtoto wa miaka minane

      oh my god hizi mila zitatuumbua jamani mtoto wa miaka minee hawa wamasai hawabadiliki kumbe kale katabia chakuchumbia toka tumboni bado kipo maski ni kasha mwaribia maisha hivi wazazi wengine wakoje?hasa wanaume ni balaa kabisa ndio sababu kumpa baba mtoto wa kike akae nae ataishiwa kubakwa tu jamani maana hawatabirirki ina maana huyo baba kaona huyo mtoto kashafikia kulala na mwanaume?
      SODOMA NA GOMORA HII IMERUDI WATOTO WENGI CHINI YA 12 YEARS HAPA TZ WANATENDEWA VITENDO VIOVU SANA PIA NI KUTOKANA NA MAADILI MABAYA YA NDOA ZETU NA SHERIA ZA NDOA KUBADILIKA BADILIKA KILA SIKU MFANO YULE MAMA ANANYANGANYA MTOTO WA 4MONTH MAHAKAMA INAPEWA PESA WANAHALALISHA MTOTO HUYO AKAISHI KWA BABA YAKE JE BABA HUYO ATAMNYONYESHA? ONA NDOA ZINAVUNJIKA KILA SIKU WANAWAKE HUKIMBIA NAKUWAACHIA WANAUME WATOTO WANAISHIA KUBAKWA NAKULAWITIWA INABIDI KUMWOMBA MUNGU SANA NA SHERIA ZA NDOA KUREKEBISHWA.
      Kosea njia utaelekezwa,lakini usikosee mtu wakuoa /kuolewa naye,vinginevyo majuto yatakuwa sehemu ya maisha yako.tuliza kichwa unapochagua mwenzi wa maisha.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...