Nitaanza kwa kusema kwamba kilichofanyika sio sahihi. Kabla hatujaenda kwenye vifungu vya sheria Civil Service Act, 2003 na pengine Employment and Labour Relations Act, 2004 ili kuona kama Mwajiri anayo mandate ya kushusha mshahara wa mwajiriwa, tujiulize haya:
Kwamba, ajira ni mkataba/ makubaliano kati ya mwajiri na mwajiriwa. Mwajiri alipotangaza kazi alitoa sifa na pengine masharti ya ajira. Mwajiriwa akaona kuwa anazo sifa, akaomba kazi hiyo. Akasahiliwa na kufaulu. Baada ya hapo, bila shaka alipewa barua ya kufaulu kwake na kuonyesha kuwa amekubaliwa kuajiriwa. Barua hiyo ndio inatoa masharti ya ajira ikiwemo malipo (yaani mshahara). Kwa stage hii, muomba kazi halazimishwi au halazimiki kuajiriwa. Anaangalia masharti ya ajira yenyewe lakini kikubwa anaangalia mshahara (How much do you offer me). Hiki ni kigezo kikubwa sana cha mtu kukubali kuajiriwa. Inawezekana kuwa wakati wa ajira hii, mtu alishwahi kupata offer nyingine mahali pengine. Kwa kulinganisha mishahara ya sehemu mbili tofauti, bilashaka unachagua sehemeu iliyonona kidogo. Mtu huyu (Mwajiri) akikubadilikia kesho na kutoa mshahara tofauti atakuwa amekuumiza na kukupotezea opportunities za mahali pengine.
Hivyo basi, kwa mantiki hiyo, Mwajiriwa hawezi kukurupuka na akasema leo nashusha msharahara wako bila kukushirikisha na wewe ukatoa idhini au maoni yako. Akifanya hivyo, atakuwa amevunja mkataba wa ajira na atakuwa amekiuka sheria na hata katiba ya nchi. Mwajiriwa hana budi kuchukua hatua.
Follow Us Here