TiGo Says
    Show/Hide This

    Topic: Muokoeni mama yangu

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 30 of 37
    1. #1
      Mazeejoh's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th January 2011
      Posts : 8
      Rep Power : 372
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Muokoeni mama yangu

      Ahsante kwa kufungua hii mail. Nimatumaini yangu utapata muda wa kunisikiliza na kuguswa kiasi cha kunishauri haraka iwezekanavyo kwani hali ni mbaya...

      Nalazimika kuanza kwa maelezo yafuatayo ili base of argument and the problem itself ieleweke.


      Sisi tumezaliwa watatu wote wakiwa ni wannaume (1978,1980,1985), Baba ni Mtanzania na Mama ni mtanzania. Tulilelewa kenya wote baada ya kuwa mama alikuwa ana fanya kazi kama mwalimu wa HIgh School kule. Baba alikuwa anafanya kazi kama mwalimu pia lakini 1985 aliachishwa kazi baada ya kuwa mlevi na mgomvi mgomvi tofauti na nidhamu ya taaluma inavyotaka. Alipoachishwa kazi mama akawa yeye ndiyo bread winner wa familia. In 1987 baba alituaga kwamba anakwenda nyumbani (TZ) atakuja baada ya wiki moja huyo ukawa mwanzo wa story iliyojaa Hasira, maudhi, kilio, hofu, upweke n.k. maishani mwa kila mmoja wetu.




      Wiki moja ikazaa mwezi, mwaka, miaka 2,5, 10 hadi 13.


      Ndani ya maika hii yote mateso mama aliyopitia sipati maneno ya kutosha kuelezea, maana hata niandikapo hii post roho inauma sana. Alifanya kila awezalo kutuelimisha, kutulisha, kutuvisha na kutulea katika maadili mema. Alijinyima kila aina ya starehe ili tupate mahitaji yetu, alijituma hadi kununua ngombe wa maziwa ili kujiongezea kipato cha kuendesha familia huku gharama zingine zikimuelemea, kidogo kidogo akapata shamba la eka mbili hili likawa tulizo kwani tulilima vyakula na kahawa ambayo ilimsaidia kulipa ada za shule kwa sisi wote. Yalikuwa ni maisha ya taabu sana, Namshukuru mungu hamna kati yetu aliyemuongezea maudhi kwa kuhitaji kisichowezekana. Raha nyingi za ujanani tulizikosa kwani hela ya kuvaa vizuri, kusoma shule bora, kula vizuri, na vitu vingine vizuri vizuri ambavyo wenzetu walikuwa wakivipata hatukapata, T.V. yenyewe hatukuwa nayo, radio ilikuwa ni hadi betri zipatikane sana sana mwisho wa mwezi. Hali iliendelea hivyo hadi mimi nilipomaliza Form 4 ilibidi nimpumzishe mama kwa kualisha miaka miwili ili wadogo zangu wapate ada ya kumalizia masomo yao. Nilibaki nyumbani na mama yangu nikiwa kama house boy sasa kwani kazi zote zilikuwa zangu mama akienda shule. Hapo ndo mama hata afya yake ikiwa afadhali kwani alipata mda wa kupumzika. Baada ya miaka miwili nikapata nafasi ya kujiunga na college ya Printing and Press Operation, mama akauza ngombe mmoja ilinipate fees ya kujiunga, kweli nikajitahidi kadri ya uwezo wangu na baada ya miaka miwili nikahitimu kwa CREDIT jambo ambalo lilimtia mama furaha sana.




      Mapenzi kama upofu fulani


      Katika kupekua barua zake, mama akakuta barua ya zamani sana ikitokea Tanzania. Mama akapata wazo la kufatilia senders postal address ili kujua hatma ya Baba kwani kwa kipindi chote hichi hatujawahi kusikia lolote kutoka kwake. Mara nyingi tulifikir kwamba kafa. Akakusanya hela ya kutosha na kutuaga kwamba anakwenda kumtafuta baba. Alifanikiwa kuja hadi Dar es Salaam na baada ya kufuatilia mwenye anuani ya barua akabahatika kufika kwa Baba Mkubwa wangu. Baba alipatwa na shock ya kufa mtu baada ya kumkuta mama kule jioni aliporudi. Alishindwa cha kusema na kujielezea ikabaki ameduwaa. Baada ya maongezi na mealewano ikaeleweka kwamba lazima sisi (watoto) turudi kwenye chimbuko letu (TANZANIA) ukizingatia wote ni wakiume. Basi mama akarudi na kutupa habari yote, ilikuwa vingumu kuamini na kuelewa eti baada ya miaka Ishirini na Miwili tungeweza kuondoka na kuacha kila kitu lakini kutokana na kuweka furaha ya mama mbele ikabidi tukubaliane nalo.


      BABA ANARUDI
      Baada ya mwezi mmoja toka mama arudi toka Dar es salaam. Baba akawasili, lakini tofauti na mategemeo yetu alikuwa hafanani na mafanikio ambayo tulidhani angekuwa nayo baada ya miaka yote hiyo. Tukampokea na kuamini huu ndo mwanzo mpya wa maisha na familia kwa ujumla. Cha kushangaza wote wawili waliamua kuuza kila kitu ambacho mama yangu alikuwa nacho ilikuja Tanzania waanze upya. Hiyo kwangu ilikuwa dalili ya baba hayupo hali njema ki fedha. Tukauza kila kitu na kuhamia Tanzania. Fedha iliyopatikana ndiyo ikawa kianzio, ikumbukwe mama hajastaafu hivyo ukasukwa mpango ahamishiwe shule jirani na mpaka wa TARIME na KENYA ili aweze kumalizia miaka yake na kupata pension yake. Mama akawa anakwenda asubuhi Kenya anafundisha na jioni anarejea Tanzania. Mshahara wake ukawa unalisha familia kwa sababu Baba hana kazi, mshahara huo huo ukawa unatumika kuwalipia wadogo zangu shule za sekondari hapa Tanzania. Baada ya miaka miwili mama akaja na idea ya kuanzisha shule, ikabidi baba atumie uwenyeji wake na wakapata eneo, mama akatoa hela ikawa kodi ya jengo na baby care class ikaanzishwa. Mama akalazimika kupata mkopo ilikuwezesha Baby Class itabuke ikiwa pamoja na huduma zake, waalimu wawili, uji na chakula cha mchana vikawa vivutio vvya vya wanafunzi kuongezeka. Pakawa na ongezeko kubwa la wanafunzi hadi wazo likawa kuanzisha shule kubwa. Basi Mama aakarudi benki tena na kuchukua mkopo mkubwa zaidi, likapatikana eneo kubwa na majengo matatu yakajengwa.


      Wazazi wangu walienda hatua moja mbele wakafunga ndoa kanisani, hili lilitokea baada ya kubaini baba anawatoto wengine hapa Dar es salaam. (3 watatu wakike 1 dume) baba alibisha sana na kumshawishi mama kwamba ili aamini yupo naye tu na hana mpango wa kado basi wafunge ndoa.. Mama alipostaafu pension yake ilikuwa nzuri sana kiasi kwamba Baba akawa anaitamani. Akaanza visa kwamba haheshimiki kwenye familia kwa sababu hana kazi maalum, akaanza kumlaumu mama eti ndiye anayeharibu familia, eti anatushawishi sisi watoto tudharau baba. Haya yote kwa sababu baba anapenda sana pombe, mara kadhaa amekutwa na vimwana akijirusha, hadi disko, aibu kweli kwa mama na familia kwani wote ni watu wazima na mama ni mzee wa kanisa. Sasa sisi hatukulelewa katika misingi ya ulevi na kujirusha kiasi hicho lazim tutofautiane naye. Lakini hili likawa chanzop cha kuleta vurugu za kumnyima mama usingizi. Ili kumtuliza mama akamnunulia Canter ambayo angeweza kufanyia biashara ya kusafirisha samaki na mazao, yeye akawa akipata hela haonekani nyumbani analewa hadi mtaji, zikiisha analianzisha nyumbani ili apate hela na kuendelea na ufuska wake. Upande wa pili shule imehsakuwa ngumzo katika wilaya ya MARA, kwani hivi sasa ina Boarding na DAY hadi darasa la SABA, ina magari matatu ya kusafirisha watoto na zaidi ya yote matokeo yake yamekuwa ngumzo MARA nzima. Kwa miaka miwili mfululizo imekuwa imeshikilia nafasi ya kwanza wilayani na kufaulisha wanafunzi asilimia 85%. Credit zote ni kwa mama kwa sababu she has been behind the steering all the way. Baba kazi kubwa bi kunywa na kuspend. Anaiba hadi ATM kadi ya account ya shule na ku draw hela bila ridhaa ya mtu yeyote an kuspend anavyotaka.


      Sasa ametangaza kwamba vyote ni vyake, nyumba, magari shule kila kitu ni chake. Anauwezo wa kufanya chochote awezalo bila ushauri wa yeyote yule. Mimi nimeoa na nina motto mmoja hapa DAR, mdogo wangu ameoa ni mwalimu na ana mtoto mmoja anaishi nyumbani tarime, mdogo wetu wa mwisho yupo SAUT Mwanza mwaka wa tatu. Kwangu na wote tunaamini huku nikumuonea mama kwani jasho lote ni lake.




      SWALI LANGU NI JINSI GANI NITAMUOKOA MAMA ILI?


      Kumuajibisha baba kwani ni dhahili siyo responsible but in human?


      Mali ziwe salama?


      Baba asiweze kuuza au kuingia mkataba wowote bila kuhusisha familia yote.?


      Kumdhibiti baba asifanye vurugu?


      Kuhakikisha nia ya mama kwamba vyote vifaidi watoto wa tumbo lake tu litimie.?
      Ahsante kwa kufungua hii mail. Nimatumaini yangu utapata muda wa kunisikiliza na kuguswa kiasi cha kunishauri haraka iwezekanavyo kwani hali ni mbaya...

      Nalazimika kuanza kwa maelezo yafuatayo ili base of argument and the problem itself ieleweke.

      Sisi tumezaliwa watatu wote wakiwa ni wannaume (1978,1980,1985), Baba ni Mtanzania na Mama ni mtanzania. Tulilelewa kenya wote baada ya kuwa mama alikuwa ana fanya kazi kama mwalimu wa HIgh School kule. Baba alikuwa anafanya kazi kama mwalimu pia lakini 1985 aliachishwa kazi baada ya kuwa mlevi na mgomvi mgomvi tofauti na nidhamu ya taaluma inavyotaka. Alipoachishwa kazi mama akawa yeye ndiyo bread winner wa familia. In 1987 baba alituaga kwamba anakwenda nyumbani (TZ) atakuja baada ya wiki moja huyo ukawa mwanzo wa story iliyojaa Hasira, maudhi, kilio, hofu, upweke n.k. maishani mwa kila mmoja wetu.



      Wiki moja ikazaa mwezi, mwaka, miaka 2,5, 10 hadi 13.


      Ndani ya maika hii yote mateso mama aliyopitia sipati maneno ya kutosha kuelezea, maana hata niandikapo hii post roho inauma sana. Alifanya kila awezalo kutuelimisha, kutulisha, kutuvisha na kutulea katika maadili mema. Alijinyima kila aina ya starehe ili tupate mahitaji yetu, alijituma hadi kununua ngombe wa maziwa ili kujiongezea kipato cha kuendesha familia huku gharama zingine zikimuelemea, kidogo kidogo akapata shamba la eka mbili hili likawa tulizo kwani tulilima vyakula na kahawa ambayo ilimsaidia kulipa ada za shule kwa sisi wote. Yalikuwa ni maisha ya taabu sana, Namshukuru mungu hamna kati yetu aliyemuongezea maudhi kwa kuhitaji kisichowezekana. Raha nyingi za ujanani tulizikosa kwani hela ya kuvaa vizuri, kusoma shule bora, kula vizuri, na vitu vingine vizuri vizuri ambavyo wenzetu walikuwa wakivipata hatukapata, T.V. yenyewe hatukuwa nayo, radio ilikuwa ni hadi betri zipatikane sana sana mwisho wa mwezi. Hali iliendelea hivyo hadi mimi nilipomaliza Form 4 ilibidi nimpumzishe mama kwa kualisha miaka miwili ili wadogo zangu wapate ada ya kumalizia masomo yao. Nilibaki nyumbani na mama yangu nikiwa kama house boy sasa kwani kazi zote zilikuwa zangu mama akienda shule. Hapo ndo mama hata afya yake ikiwa afadhali kwani alipata mda wa kupumzika. Baada ya miaka miwili nikapata nafasi ya kujiunga na college ya Printing and Press Operation, mama akauza ngombe mmoja ilinipate fees ya kujiunga, kweli nikajitahidi kadri ya uwezo wangu na baada ya miaka miwili nikahitimu kwa CREDIT jambo ambalo lilimtia mama furaha sana.



      Mapenzi kama upofu fulani

      Katika kupekua barua zake, mama akakuta barua ya zamani sana ikitokea Tanzania. Mama akapata wazo la kufatilia senders postal address ili kujua hatma ya Baba kwani kwa kipindi chote hichi hatujawahi kusikia lolote kutoka kwake. Mara nyingi tulifikir kwamba kafa. Akakusanya hela ya kutosha na kutuaga kwamba anakwenda kumtafuta baba. Alifanikiwa kuja hadi Dar es Salaam na baada ya kufuatilia mwenye anuani ya barua akabahatika kufika kwa Baba Mkubwa wangu. Baba alipatwa na shock ya kufa mtu baada ya kumkuta mama kule jioni aliporudi. Alishindwa cha kusema na kujielezea ikabaki ameduwaa. Baada ya maongezi na mealewano ikaeleweka kwamba lazima sisi (watoto) turudi kwenye chimbuko letu (TANZANIA) ukizingatia wote ni wakiume. Basi mama akarudi na kutupa habari yote, ilikuwa vingumu kuamini na kuelewa eti baada ya miaka Ishirini na Miwili tungeweza kuondoka na kuacha kila kitu lakini kutokana na kuweka furaha ya mama mbele ikabidi tukubaliane nalo.

      BABA ANARUDI
      Baada ya mwezi mmoja toka mama arudi toka Dar es salaam. Baba akawasili, lakini tofauti na mategemeo yetu alikuwa hafanani na mafanikio ambayo tulidhani angekuwa nayo baada ya miaka yote hiyo. Tukampokea na kuamini huu ndo mwanzo mpya wa maisha na familia kwa ujumla. Cha kushangaza wote wawili waliamua kuuza kila kitu ambacho mama yangu alikuwa nacho ilikuja Tanzania waanze upya. Hiyo kwangu ilikuwa dalili ya baba hayupo hali njema ki fedha. Tukauza kila kitu na kuhamia Tanzania. Fedha iliyopatikana ndiyo ikawa kianzio, ikumbukwe mama hajastaafu hivyo ukasukwa mpango ahamishiwe shule jirani na mpaka wa TARIME na KENYA ili aweze kumalizia miaka yake na kupata pension yake. Mama akawa anakwenda asubuhi Kenya anafundisha na jioni anarejea Tanzania. Mshahara wake ukawa unalisha familia kwa sababu Baba hana kazi, mshahara huo huo ukawa unatumika kuwalipia wadogo zangu shule za sekondari hapa Tanzania. Baada ya miaka miwili mama akaja na idea ya kuanzisha shule, ikabidi baba atumie uwenyeji wake na wakapata eneo, mama akatoa hela ikawa kodi ya jengo na baby care class ikaanzishwa. Mama akalazimika kupata mkopo ilikuwezesha Baby Class itabuke ikiwa pamoja na huduma zake, waalimu wawili, uji na chakula cha mchana vikawa vivutio vvya vya wanafunzi kuongezeka. Pakawa na ongezeko kubwa la wanafunzi hadi wazo likawa kuanzisha shule kubwa. Basi Mama aakarudi benki tena na kuchukua mkopo mkubwa zaidi, likapatikana eneo kubwa na majengo matatu yakajengwa.

      Wazazi wangu walienda hatua moja mbele wakafunga ndoa kanisani, hili lilitokea baada ya kubaini baba anawatoto wengine hapa Dar es salaam. (3 watatu wakike 1 dume) baba alibisha sana na kumshawishi mama kwamba ili aamini yupo naye tu na hana mpango wa kado basi wafunge ndoa.. Mama alipostaafu pension yake ilikuwa nzuri sana kiasi kwamba Baba akawa anaitamani. Akaanza visa kwamba haheshimiki kwenye familia kwa sababu hana kazi maalum, akaanza kumlaumu mama eti ndiye anayeharibu familia, eti anatushawishi sisi watoto tudharau baba. Haya yote kwa sababu baba anapenda sana pombe, mara kadhaa amekutwa na vimwana akijirusha, hadi disko, aibu kweli kwa mama na familia kwani wote ni watu wazima na mama ni mzee wa kanisa. Sasa sisi hatukulelewa katika misingi ya ulevi na kujirusha kiasi hicho lazim tutofautiane naye. Lakini hili likawa chanzop cha kuleta vurugu za kumnyima mama usingizi. Ili kumtuliza mama akamnunulia Canter ambayo angeweza kufanyia biashara ya kusafirisha samaki na mazao, yeye akawa akipata hela haonekani nyumbani analewa hadi mtaji, zikiisha analianzisha nyumbani ili apate hela na kuendelea na ufuska wake. Upande wa pili shule imehsakuwa ngumzo katika wilaya ya MARA, kwani hivi sasa ina Boarding na DAY hadi darasa la SABA, ina magari matatu ya kusafirisha watoto na zaidi ya yote matokeo yake yamekuwa ngumzo MARA nzima. Kwa miaka miwili mfululizo imekuwa imeshikilia nafasi ya kwanza wilayani na kufaulisha wanafunzi asilimia 85%. Credit zote ni kwa mama kwa sababu she has been behind the steering all the way. Baba kazi kubwa bi kunywa na kuspend. Anaiba hadi ATM kadi ya account ya shule na ku draw hela bila ridhaa ya mtu yeyote an kuspend anavyotaka.

      Sasa ametangaza kwamba vyote ni vyake, nyumba, magari shule kila kitu ni chake. Anauwezo wa kufanya chochote awezalo bila ushauri wa yeyote yule. Mimi nimeoa na nina motto mmoja hapa DAR, mdogo wangu ameoa ni mwalimu na ana mtoto mmoja anaishi nyumbani tarime, mdogo wetu wa mwisho yupo SAUT Mwanza mwaka wa tatu. Kwangu na wote tunaamini huku nikumuonea mama kwani jasho lote ni lake.


      SWALI LANGU NI JINSI GANI NITAMUOKOA MAMA ILI?

      Kumuajibisha baba kwani ni dhahili siyo responsible but in human?

      Mali ziwe salama?

      Baba asiweze kuuza au kuingia mkataba wowote bila kuhusisha familia yote.?

      Kumdhibiti baba asifanye vurugu?

      Kuhakikisha nia ya mama kwamba vyote vifaidi watoto wa tumbo lake tu litimie.?


    2. #2
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 16,973
      Rep Power : 7708
      Likes Received
      4056
      Likes Given
      11108

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      very interesting and so sad
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    3. #3
      bucho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th July 2010
      Location : kandahar
      Posts : 2,298
      Rep Power : 4123
      Likes Received
      354
      Likes Given
      352

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Duh embu ngoja wataalam wafike.

    4. #4
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 6,231
      Rep Power : 1788
      Likes Received
      862
      Likes Given
      631

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Sisi tumezaliwa watatu wote wakiwa ni wannaume (1978,1980,1985).....kwa sasa mtakuwa 34,32 na 27....nyie ni watu wazima na mko huru kujiamulia kwa manufaa ya mama yenu

      Mamndenyi likes this.

    5. #5
      Mlavumbi Orijino's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 12th February 2012
      Posts : 6
      Rep Power : 316
      Likes Received
      2
      Likes Given
      3

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Nimepata hasira mpaka nakosa uwezo wa kufikiri ngoja nipoe kwanza, poleni sana kwa mliyopitia, story yako inatufundisha vitu kadhaa katika maisha. Pole bro
      Mamndenyi likes this.

    6. #6
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Ndugu yangu pole kwa matatizo yanayoikumba ndoa ya wazazi wako. Umejieleza vizuri, ila hujatuambia kama walioana ndoa ya kanisani, msikitini, kimila au waliamua kuishi tu kinyumba.
      Kiufupi wakati baba yako anawaletea vitimbi kule Kenya, mama yako alikuwa na nafasi nzuri ya kuomba talaka wakati ule kwani angeweza kuleta ushahidi wa cruelity anayowafanyia ila hakufanya hivyo kwa hiyo haitakuwa sabcu nzito mahakamani ila itakuwa kama kuelezea tabia ya huyo baba yenu.
      Pili, alipowaacha kenya na kuja TZ kwa muda wote huo mama aliweza kuomba talaka pia kwa kuwatelekeza au presumption of death ila hakufanya hivyo napo pana tatizo.
      Alipoamua kumfata mdingi hapo ndo inadhihirisha kukubaliana na mambo ya mumewe pamoja na vitimbi vyote akamtafuta mwenyewe tena sio baba kamtafuta. Hiyo inaweza kuwa kitu tunaita CONNIVANCE kisheria.
      BUT:
      Mama amefahamu baba anawatoto wengine inamaana alifanya uzinzi, hapa ndipo mama anaweza kuleta ushahidi kama anataka kupeleka petition ya DIVORCE. Huo ni ushahidi tosha na mkiunganisha na CRUELITY na ulevi na utumiaji wa mali za familia hovyo bila manufaa. Ila kumbuka ni kama mama anataka divorce kama walioana kisheria.
      Mamndenyi likes this.

    7. #7
      happiness win's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Posts : 431
      Rep Power : 424
      Likes Received
      115
      Likes Given
      29

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Pole. Nimepata fundisho fulani kupitia stori yako. Nami nasubiri kwa hamu wataalam wanasema nini katika hili.
      Mamndenyi likes this.

    8. #8
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Ila kumbuka unasema kiwanja baba yenu alisaidia katika kuwashauri wanakijiji wawauzie, pamoja hela anaweza kuwa alitoa mama ila hiyo tayari ni joint effort towards that property, mama akiomba divorce na ikakubalika, wanapokuja kugawa mali baba anaweza kupewa sehemu ya mali.
      Wale watoto waliopatikana kwenye uzinzi hawahusiki na mgawanyo hapa.
      Otherwise inaonekana nyie hamumpendi huyo mzee kutokana na vitimbi vyake ila mama anamchukulia poa kama mzazi mwenzie kwani yeye ndiye mwenye uamuzi na sio nyinyi hamuwezi kufanya kitu ukichukulianyie ni wakubwa kabisa itakuwa ngumu kwenu. Mama anatakiwa afahamu ana uwezo wa kukusanya ushahidi tosha wa hiyo CRUELITY, ADULTERY na pia mengineyo kama ulevi wake, na ufujaji wa mali ya familia nk.
      Kumbukeni, baba atapata sehemu ya mgao wamali kama wataachana, maana amecheza karata dume, unajua alijua akibaki kenya ile mali asingepata mgao ndo maana akamsolicit mama auze waanze upya.
      Katika kuanza upya mama akajikuta anamtumha mzee katika ujenzi wa hiyo shule na mali nyinginezo so hiyo ni JOINT EFFORTS TOWARDS THE ACQUIRING THE MATRIMONIAL PROPERTY.
      Mama anasababu zote za kuomba na kupata divorce ila akumbuke kuna sehemu ya mali baba atakuwa entitled. Otherwise nitafuteni for further consultation and representation in the court.
      Mamndenyi and 19don like this.

    9. #9
      LISAH's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th January 2012
      Posts : 81
      Rep Power : 393
      Likes Received
      15
      Likes Given
      21

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Pole bro inatia hasira sana.
      Hawa na mfumo wao dume ndio maana wanawake wa kenya wameamua kuwatwanga mingumi!

      Hebu wanasheria na akina anania Nkya msaada wenu hapa unahitajika kumkomboa huyu mama.

    10. #10
      Elli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 5,276
      Rep Power : 1582
      Likes Received
      715
      Likes Given
      604

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Kabla ya kufanya maamuzi hebu mhusishe na MUNGU pia, sijui unaonaje wazo langu maana binadamu wataishia kuku-confuse zaidi na MUNGU huyu usimtafute wala kumshirikisha kwa kubadili dhehebu wala usifikirie kulipa kisasi. Asante
      Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, Watu aliowachagua kuwa urithi wake. Zaburi 33:12

    11. #11
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Kama hawakuoana ila waliishi tu kama mke na mume hapo kuna suala la mahakama ifanye PRESUMPTION OF MARRIAGE kama itatimiza vigezo vyote ambavyo nadhani vipo. Then mahakama itapresume kulikuwa na marriage ili kumsaidia mama apate haki yake although kumbuka baba atapewa mgao katika mali.
      Mama afanye maamuzi na wala msimuingilie.


    12. #12
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By LISAH View Post
      Pole bro inatia hasira sana.
      Hawa na mfumo wao dume ndio maana wanawake wa kenya wameamua kuwatwanga mingumi!

      Hebu wanasheria na akina anania Nkya msaada wenu hapa unahitajika kumkomboa huyu mama.
      Punguza hasira, hata wanaume wanapata matatizo makubwa kutokana na wanawake.
      Sheria ya ndoa ipo wazi katika kutoa haki kwa wanaume na wanawake, na kutokana na story ya huyu mwenzetu sioni kama huyo mama yake baada ya mateso yote kama alilazimishwa kukaa na huyo mwanaume.
      Alikuwa na uwezo wa kutomtafuta, lakini out of love aliamua mwenyewe so hapa hakuna mahusiano na mambo ya mfumo dume.
      Mianya ya kisheria ipo wazi tena kwa mama msomi na mwenye uelewa kama huyu, its her love to the husband hapo ndo tatizo, watoto wake ni wakubwa na wasomi nao wanashindwa kuingilia sababu hiyo ni ishu ya wao wazazi na huyo mama kuamua.
      Ona jinsi anavyomlea huyo baba hadi kumnunulia gari, hapo kuna mfumo dume upi? Nadhani huyo mama anamapenzi kwa mumewe sema tu amepata bahath mbaya.
      Tuelewe, sheria ipo wazi na mahakama zinawasubiri watu wa jinsia zote, tatizo ni kwamba, marriage conflict ni private matter so anatakiwa aamue na hapo hakuna mfumo dume.

    13. #13
      sweetlady's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 8,385
      Rep Power : 4450
      Likes Received
      2537
      Likes Given
      934

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Pole sana! Tusubiri wanaojua sheria..

    14. #14
      BelindaJacob's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 24th November 2008
      Location : Санкт-Петербург
      Posts : 4,056
      Rep Power : 1318
      Likes Received
      1050
      Likes Given
      754

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Du! Pole sana mkuu kwa yote mliyopitia. Naamini wadau wengine watakusaidia zaidi. imenisikitisha sana hii issue.
      Thy word is a lamp unto my feet, and a light unto my path!..(Psalm 119:105)

    15. #15
      nitonye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th December 2011
      Posts : 2,964
      Rep Power : 915
      Likes Received
      702
      Likes Given
      24

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Mkuu pole sana kwa hilo tatizo mimi sio mtaalamu wa sheria ila mawzo yangu yanaweza kuwa msaada kwako
      Linapokuja suala la kugombea mali kati ya wanandoa linakuwa ngumu kwenu nyie watoto kulitatua kawa sababu hizi zifuatazo:-
      1. Wakati wanaanzisha hiyo miradi waliiandika kwa majina yapi ya mume au mke? Kinachowaponza wanawake ni kuandikisha miradi yao kwa jina la waume zao kitu ambacho ni hatari kwao.
      2.Pili mama yenu kama hatakuwa willing kwa ajili ya kuitetea mali yake nyie watoto mtaishia kupigana bastola. Muulize mama yenu kama yuko tayari kuachana na baba yenu maana wewe unaweza ukawa unahangaika huku jf kumbe mama bado anamuhitaji mme wake.
      mama D and Mamndenyi like this.

    16. #16
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By nitonye View Post
      Mkuu pole sana kwa hilo tatizo mimi sio mtaalamu wa sheria ila mawzo yangu yanaweza kuwa msaada kwako
      Linapokuja suala la kugombea mali kati ya wanandoa linakuwa ngumu kwenu nyie watoto kulitatua kawa sababu hizi zifuatazo:-
      1. Wakati wanaanzisha hiyo miradi waliiandika kwa majina yapi ya mume au mke? Kinachowaponza wanawake ni kuandikisha miradi yao kwa jina la waume zao kitu ambacho ni hatari kwao.
      2.Pili mama yenu kama hatakuwa willing kwa ajili ya kuitetea mali yake nyie watoto mtaishia kupigana bastola. Muulize mama yenu kama yuko tayari kuachana na baba yenu maana wewe unaweza ukawa unahangaika huku jf kumbe mama bado anamuhitaji mme wake.
      Hilo la kwanza uliloliongea kisheria halitambuliki, jitahidi usome post zangu hapo juu utaelewa, usijaribu kutoa ushauri wa kisheria wakati tupo wenye fani hapa.
      Kuandika majina hakuna uhusiano wakati wa mgawanyo wa mali, soma post zangu vizuri itakufumbua ufahamu nawe pia.
      Usitie uvivu kusoma mkuu au wewe ni mathematician? Wao ndo wanapata tabu kusoma maandishi mengi.
      I urge you to please read the posts nilizoweka hapo ili usie ukatoa ushauri mwingine wa namna hii although umesdma hujui sheria so pitia upate ufahamu tupo kwa ajili yenu kuwapa kaufahamu.

    17. #17
      19don's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 13th May 2011
      Posts : 230
      Rep Power : 400
      Likes Received
      27
      Likes Given
      108

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      pole sana ndugu mtangulizeni mungu kitikakulitatua jambo hili,

    18. #18
      nitonye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th December 2011
      Posts : 2,964
      Rep Power : 915
      Likes Received
      702
      Likes Given
      24

      Default

      Quote By Bondpost View Post
      Hilo la kwanza uliloliongea kisheria halitambuliki, jitahidi usome post zangu hapo juu utaelewa, usijaribu kutoa ushauri wa kisheria wakati tupo wenye fani hapa.
      Kuandika majina hakuna uhusiano wakati wa mgawanyo wa mali, soma post zangu vizuri itakufumbua ufahamu nawe pia.
      Usitie uvivu kusoma mkuu au wewe ni mathematician? Wao ndo wanapata tabu kusoma maandishi mengi.
      I urge you to please read the posts nilizoweka hapo ili usie ukatoa ushauri mwingine wa namna hii although umesdma hujui sheria so pitia upate ufahamu tupo kwa ajili yenu kuwapa kaufahamu.
      Nimekuelewa mkuu ndio nikadeclare interest mwanzoni kuwa mimi sio mtaalamu wa sheria ila majina ya umiliki yanaletaga taabu, ikiwa pale mwenye dhamiri ya kukudhulumu anapojua udhaifu wako uko wapi.
      Hofstede likes this.

    19. #19
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By nitonye View Post
      Nimekuelewa mkuu ndio nikadeclare interest mwanzoni kuwa mimi sio mtaalamu wa sheria ila majina ya umiliki yanaletaga taabu, ikiwa pale mwenye dhamiri ya kukudhulumu anapojua udhaifu wako uko wapi.
      Hiyo labda ni kwenye mashauri mengine yanayohusu mikataba ya kibiashara ndipo umiliki huwa unaleta tabu, yani mkataba wa ndoa ni kitu kingine, una taratibu zake wakati wa mgawanyo wa mali, ukisoma kesi ya BI Hawa d/o Mohammed.V. Ally s/o Seif, imeelezea mgawanyo wa mali na mambo mengine mengi tu. Suala la kuandika jina halinauzito wakati wa kugawana kinachoangaliwa ipi mali ilipatikana wakati wa ndoa period.

    20. #20
      Mazeejoh's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th January 2011
      Posts : 8
      Rep Power : 372
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      No prob

    21. #21
      Navoyne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th December 2010
      Location : Tandahimba
      Posts : 588
      Rep Power : 493
      Likes Received
      112
      Likes Given
      70

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Hapo haitajiki sheria grey area kubwa sana cha msingi ni maarifa, na ni rahisi kabisa kwa sababu baba ni mlevi. Ngoja nifikirie linchpin ili dominoes zianze kufall.
      IMMITATIONS are LIMITATIONS

    22. #22
      Mazeejoh's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th January 2011
      Posts : 8
      Rep Power : 372
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      @ Bondpost, sina cha kukulipa ndugu yangu, from your post i have learnt alot, kikubwa kuondokana na hofu ya hatma ya jasho la mama. Labda niongeze kwamba kesho mungu akijalia nasafiri kwenda nyumbani kwani mama kanipigia kuniambia mdingi kaliwasha toka last week. I believe am going home like a first born thanks to you. Ombi langu ni kukuomba upokee updates zangu on the situation na mungu akuongeze nguvu na maarifa katika kunishauri. May god bless you

    23. #23
      Mazeejoh's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th January 2011
      Posts : 8
      Rep Power : 372
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      On second thought, given that the school is under his name and some of the properties too, can he sell them and if so how can we stop that from happening? And with the constant emotional torture akilewa na kumsumbua mother kwa mikwala, how can that be tamed?

    24. #24
      Mazeejoh's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th January 2011
      Posts : 8
      Rep Power : 372
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Baba namjua sana, ni mjanja sana katika kesi kesi, naimani nikimuomba tukae tuongee kifamilia ataleta hoja kwamba wote tupo against him, kibaya zaidi atapata point ya kumsingizia maza kwamba kapanga njama na wanae. SWALI: Approach gani effective itakayomfanya aheshimu wito at the same isimnyime mama usingizi?

    25. #25
      Mazeejoh's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 15th January 2011
      Posts : 8
      Rep Power : 372
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      At this point naomba niwashukuru wote mliopata mda kushare ma experience and pain regardless of who and what he or she said, making a point to read my post was encouraging enough may you all be blessed na mungu awaepushia yalionifika mwenzenu

    26. #26
      Mamndenyi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 5,521
      Rep Power : 1548
      Likes Received
      1307
      Likes Given
      4410

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Poleni sana,
      Hata hivyo mshukuru Mungu kuwa mama yenu alipona kuambulia
      marazi.
      SIYO WOTE WANAOTANGATANGA WAMEPOTEA

    27. #27
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Nenda na huo ushauri niliokupatia kamuelezee mama, msikilize kwanza yeye anachokitaka haswa ni nini ndipo tutaweza kushauriana zaidi.
      Suala la baba kujimilikisha mali sio tatizo, mahakama inaangalia ushahidi ndugu, wala haiangalii mambo atakayoyazua tu, kumbuka mahakama ndio sehemu pekee mtakayopata suluhisho la kudumu.
      Ila soma vizuri yote niliyokushauri. Nashindwa ku-quote vifungu maana vitakuchanganya tu since wewe sio mtaalamu wa sheria but otherwise hayo yote ni msimamo wa sheria.
      Kumbuka mahakama inamaamuzi yake na sio kila unachotaka utapata but at least mtakuwa na msimamo wa kueleweka na kumuweka baba yenu katika utaratibu madhubuti kwenye mambo kadhaa mnayoyalalamikia.
      Cha muhimu ni mama afanye maamuzi, otherwise there is nothing you can do mtabaki kulalama na kuaibisha familia yenu.
      Thats all. Ukitaka ushauri zaidi, tafuta mwanasheria mzuri wa mambo ya ndoa awasaidie, am ready to be of any assistance at fee mkuu hapa nimesaidia kukupa mwangaza wa mambo yalivyo, its more than enough my friend if you happen to read between lines.
      Pia waweza kumshauri mama aende nanyi TAMWA, LHRC na kwingine wanatoa msaada wa kisheria bure au kwa gharama ndogo sana ila ndio mfahamu kuwa wao wako busy kwa kesi nyingi.

    28. #28
      mama D's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2010
      Posts : 881
      Rep Power : 559
      Likes Received
      207
      Likes Given
      963

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      ikifikia hapa ndo pale familia inamwomba Mungu amchukue huyo baba mapeeema!
      Amri mpya nawapa - Pendaneni kama nilivyowapenda!!!!

    29. #29
      Bondpost's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 16th October 2011
      Posts : 569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      108
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By mama D View Post
      ikifikia hapa ndo pale familia inamwomba Mungu amchukue huyo baba mapeeema!
      Ha ha ha haaa! Mnaanza kuingia ubia na ziraili aondoke na huyo kiumbe wake! Duh! Hiyo ni stage mbaya sana.
      Ila kuna watu wanaombewa wafe maana ni majanga katika familia. Ila suluhisho ni kumtanguliza mungu tu na kufahamu njia sahihi ya kudai haki yako.

    30. #30
      L'AMOUR's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th March 2011
      Posts : 102
      Rep Power : 383
      Likes Received
      15
      Likes Given
      9

      Default Re: Muokoeni mama yangu

      Mmhh tunakoelekea hapa TZ kuna haja ya kuanzisha family Courts

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...