Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mwenziyo unanikosha!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 25
    1. #1
      Choveki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2006
      Posts : 477
      Rep Power : 766
      Likes Received
      88
      Likes Given
      163

      Default Mwenziyo unanikosha!

      Mpendwa,

      Salamu natuma kwako, naomba uzipokee
      Nauliza hali yako, nataka nikujulie
      Barua hii ni yako, ujumbe uusikie
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Binti Msemaovyo, mwenziyo unanikosha
      Siropoki hovyohovyo, na hilo nakujulisha
      Nasema ujue hivyo, sikwamba nimechemsha
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Kwa maumbile na pozi, kiroho chaniripuka
      Nashindwa kufanya kazi, kichwani wanizunguka
      Nauomba ukimbizi, kwa weye uloumbika
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Ningali bado kijana, m-bichi nisiyeoa
      Tuli nimetulizana, ni mwenza natafutia
      Usiku pia mchana, nikweli nakuwazia
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Pia tena mcha mungu, huyo huyo wako wewe
      Naomba tena kwa mungu, niweze kupata wewe
      Dini yako ndiyo yangu, nasema bila kiwewe!
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Msomi ki kweli kweli, kijana miye nasema
      Shahada ya uzamili, nimemaliza si zama
      Ki pesa nipo kamili, nimejaliwa karama
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Nitawacha ukapera, na hilo nasisitiza
      Kijana sina papara, nashinda nikikuwaza
      Nitakufanya kinara, uweze kuniongoza
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Nane nasema tamati, kwako uliye umbika
      Hakuna ambayo nyeti, kwangu yaliyofichika
      Ni mimi mtanashati, nakuagia waraka
      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha!

      Wakatabahu waraka,

      Kijana Bin Mbichi .
      Mrimu, chama, Yakuonea and 3 others like this.
      -------choveki

    2. Miaka 50

    3. #2
      Suki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2007
      Posts : 375
      Rep Power : 667
      Likes Received
      14
      Likes Given
      2

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Amazing choice of words
      Outstanding flow of ''emotions''
      Too bad I hadn't read it while fresh
      Good work!
      Choveki and Yakuonea like this.

    4. #3
      Choveki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2006
      Posts : 477
      Rep Power : 766
      Likes Received
      88
      Likes Given
      163

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Mpendwa;

      Yapata mwezi wa pili, ningali nikisubiri
      Nahisi kama ni zali, kwanini hunifikiri
      Sichezi miye kidali, mwenziyo hapo nakiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Nauliza yako hali, pia jibu nasubiri
      Itume japo mahali, barua ulo hariri
      Nakesha nikiwa chali, usiku nikifikiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Barua hii ya pili, na wala sifanyi siri
      Nambie huo ukweli, pitia wako msiri
      Nijibu hata makali, majibu yalo mahiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Niandikayo ni kweli, bila yake kachumbari
      Namtafuta dalali, aweze kukuhubiri
      Uweze kunikubali, halafu tujivinjari
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Ninayapata makali, kichwani nikifiri
      Nahisi kama kabali, ya mtu mwenye jeuri!
      Dhoofu nisiye hali, nashindwa kuwa ngangari!
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Barua siyo batili, na wala siyo stori
      Najua siyo katili, ni yepi yalo kujiri?
      Yamenijaa maswali, nasaka yako nambari!
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Saba zilizo kamili, ni mwisho wangu jasiri
      Zaidi ya pilipili, moyoni mwangu nakiri
      Uchungu huo mkali, naomba uufikiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Wasalam.

      Daima akupendaye,

      Kijana Bin Mbichi
      Mrimu, chama, Yakuonea and 2 others like this.
      -------choveki

    5. #4
      Mtu wa Pwani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th December 2006
      Posts : 4,250
      Rep Power : 1491
      Likes Received
      159
      Likes Given
      147

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Quote By choveki
      Mpendwa;

      Yapata mwezi wa pili, ningali nikisubiri
      Nahisi kama ni zali, kwanini hunifikiri
      Sichezi miye kidali, mwenziyo hapo nakiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Nauliza yako hali, pia jibu nasubiri
      Itume japo mahali, barua ulo hariri
      Nakesha nikiwa chali, usiku nikifikiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Barua hii ya pili, na wala sifanyi siri
      Nambie huo ukweli, pitia wako msiri
      Nijibu hata makali, majibu yalo mahiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Niandikayo ni kweli, bila yake kachumbari
      Namtafuta dalali, aweze kukuhubiri
      Uweze kunikubali, halafu tujivinjari
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Ninayapata makali, kichwani nikifiri
      Nahisi kama kabali, ya mtu mwenye jeuri!
      Dhoofu nisiye hali, nashindwa kuwa ngangari!
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Barua siyo batili, na wala siyo stori
      Najua siyo katili, ni yepi yalo kujiri?
      Yamenijaa maswali, nasaka yako nambari!
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Saba zilizo kamili, ni mwisho wangu jasiri
      Zaidi ya pilipili, moyoni mwangu nakiri
      Uchungu huo mkali, naomba uufikiri
      Ningali nikisubiri, mwenziyo kwangu ni zali!

      Wasalam.

      Daima akupendaye,

      Kijana Bin Mbichi
      duh swahiba mashairi makali kinoma kama ningekuwa mie ningeingia kichwa kichwa bila hata ya kuangalia mlango wa kutokea


      ila ikifika mwezi wa tatu na ukahakikisha hajakujibu ujue hakutaki sasa ni juu yako kusuka au kunyowa
      Choveki and Yakuonea like this.
      Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown

    6. #5
      YournameisMINE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2007
      Location : Peramiho
      Posts : 3,794
      Rep Power : 1155
      Likes Received
      16
      Likes Given
      0

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      swadaktaa bin mash'allah, kijana unajitahidi na tenzi hizooooo!! ila ka'asemavyo mkuu hapo juu ukifika mwezi watatu hujajibiwa basi kipepeo hicho si chako!!. itabidi utafuta ghuba nyingine ilo tulii.

      goodluck.
      Choveki and Yakuonea like this.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Choveki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2006
      Posts : 477
      Rep Power : 766
      Likes Received
      88
      Likes Given
      163

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Quote By Mtu wa Pwani
      ....kama ningekuwa mie ningeingia kichwa kichwa bila hata ya kuangalia mlango wa kutokea"ila ikifika mwezi wa tatu na ukahakikisha hajakujibu ujue hakutaki....."
      Quote By YournameisMINE
      ......ka'asemavyo mkuu hapo juu ukifika mwezi watatu hujajibiwa basi kipepeo hicho si chako!! itabidi utafuta ghuba nyingine ilo tulii.goodluck.

      Wapendwa
      ndugu, jamaa na marafiki;


      Hiyo tamaa sikati, ninawajuza wengine
      Nimpendaye kwa dhati, ni huyu siyo mwengine
      Nitasubiri wakati, miezi hata minane
      Mitatu ama minane, nitasubiri kwa dhati!

      Nitasubiri kwa dhati, mitatu hata minane
      Na bado tampa chati, hata akiwa mjane
      Ni huyu huyu binti, sitaki hao wengine
      Mitatu ama minane, sitojalia wakati

      Nasema kweli sikati, kwa huyu siyo wengine
      Ingawa jibu sipati, upite mwezi wa nane
      Mwengine simtafuti, na wala sendi pengine
      Mitatu ama minane, tamaa miye sikati

      Dhamira yangu ya dhati, kutozengea wengine
      Sitotumia visheti, wala vitamu vingine!
      Mitego ama manoti, kuwinda hao wengine!
      Mitatu ama minane, hiyo tamaa sikati

      Maneno mengi siteti, bali barua nyengine
      Najua ni vizingiti, muvisemavyo wengine
      Ni miye mtanashati, ambaye sina mwingine
      Mitatu ama minane, kamwe tamaa sikati

      Undeni hata kamati, nakadhalika nyingine
      Kuwacha kweli siwati, wala silongi mengine
      Majibu kwenu ya dhati, ni huyu siyo mwingine
      Mitatu ama minane, nitasubiri wakati

      Nasema hapa tamati, sitoongeza mengine
      Nawajulisha umati, pamoja nanyi wengine
      Ingawa kuwa sipati, sitompenda mwengine
      Mitatu ama minane, tamaa hiyo sikati!!

      Wakatabahu waraka,

      Kijana Bin M'bichi
      Mrimu, chama, Yakuonea and 1 others like this.
      -------choveki

    9. #7
      AmaniGK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th January 2008
      Location : MAHALI FLANI
      Posts : 826
      Rep Power : 745
      Likes Received
      64
      Likes Given
      150

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Tamati iso na jibu,sitokubali asilani
      Utampata tabibu,ukitazama kwa ndani
      Kuna akina mwajabu,dadae na hamdani
      Aweza kuwa tabibu,akutoe mashakani.

      Usijikune sharubu,Kwa mawazo ya moyoni
      Mtume hata habibu,akuletee mwandani
      Uliza wa kina babu,walifanyaje zamani
      Moyoni sipate tabu,Kumtafuta mwandani

      Mbona wajipa sulubu,na kuumia moyoni
      Nenda hata bububu,takwambia kwa shani
      Utoe hata dhahabu,Maneno ndio sumuni
      Upole pia adabu,Vitakushindia mwandani
      Choveki, chama and Yakuonea like this.

    10. #8
      Choveki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2006
      Posts : 477
      Rep Power : 766
      Likes Received
      88
      Likes Given
      163

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Mpendwa

      Mwenziyo ninarejea, kukujulisha kiumbe
      Barua nasubiria, ya kwako yenye ujumbe
      Kimwana weye sikia, sikwiti wala mzembe
      Uloumbika kiumbe, ni miye nakumbushia

      Ni miye nakumbushia, ambaye nitaabani
      Mshenga nilitumia, na humu mtandaoni
      Naomba yako barua, ibwage hata njiani
      Uloumbika kiumbe, ni miye nakumbushia

      Imeshapita kadhaa, niisemayo miezi
      Nisijepata kichaa, ama uchizi uchizi
      Kuhepa hilo balaa, kwako miye mkimbizi
      Uloumbika kiumbe, ni miye nakumbushia

      Sikiya kweli sikia, na wala si longolongo
      Mapenzi yanitesea, pia yavunja mgongo
      Ukweli nakuambia, tena sisemi uongo
      Uloumbika kiumbe, ni miye nakumbushia

      Mwenziyo yanizidia, mashaka nikifikiri
      Kichwani ninahisia, ni mengi natafakari
      Kitanda nikilalia, nahisi ni misumari
      Uloumbika kiumbe, ni miye nakumbushia

      Tamati ninaishia, ewe unayenikosha
      Ningali nasuburia, na huku wanikondesha
      Charanga hiyo barua, uweze kuniponyesha!
      Uloumbika kiumbe, ni miye naku agia!

      Wasalaam,
      “Umkondeshaye”
      Mrimu, chama, Yakuonea and 1 others like this.
      -------choveki

    11. #9
      Choveki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2006
      Posts : 477
      Rep Power : 766
      Likes Received
      88
      Likes Given
      163

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Mpendwa,

      Ni mingi imetimia, niisemayo miaka

      Na bado nasubiria, kwa dhati ninatamka

      Moyoni naugulia, kwa kweli hilo kumbuka

      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha


      Sikia mwenza sikia, ningali nataabika

      Naliya miye nalia, kichwani nikisumbuka

      Moyoni nakulilia, ni lini utakumbuka?

      Kwa pozi na maumbile, mwenziyo unanikosha


      Waraka wangu pokea, usome nimeandika

      Zamani hizo tangia, kichwani hujanitoka

      Kwa kweli ninaumia, machozi yanidondoka

      Ningali nikisubiri, wajua kwangu ni zali?


      Mshenga natafutia, ambaye hatajachoka

      Wa kwanza, wa pili pia, wasema walishachoka

      Wahisi nitajifia, wasema kwa uhakika

      Ningali nikisubiri, wajua kwangu ni zali?


      Wazee wanizengua, wasema ninazeeka

      Kwa hamu wanangojea, harusi ije sikika

      Wameikata tamaa, harusi yetu kufika

      Mitatu ama mine, tamaa hiyo sikati!


      Sitaikata tamaa, kichwani mwako kumbuka

      Kwa ndugu pia jamaa, ukweli unajulika

      Wasisitiza komaa!, wajua utanasika

      Mitatu ama minane, tamaa hiyo sikati


      Mwenziyo nakuitia, itika kwanza itika

      Nahisi umesinzia, ni lini utaamka?

      Najua hujasikia, sauti yanikauka

      Uloumbika kiumbe, ndo miye nakumbushia


      Kapera na sijaoa, ni wewe wasubirika

      Tulia kwangu tulia, najuwa umetukuka

      Ni wangu wewe najua, mwengine sijamtaka

      Uloumbika kiumbe, ndo miye nakumbushia


      Kikomo nakomelea, wakatabahu waraka

      Nahisi umejulia, ni wewe uloumbika

      Mwengine sijapatia, na wala sitomtaka

      Ningali nasubiria, majibu yako mwanana


      Wakatababu,

      Kijana Bin Mbichi
      Mrimu, chama, Roulette and 2 others like this.
      -------choveki

    12. #10
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,317
      Rep Power : 18677
      Likes Received
      1098
      Likes Given
      1049

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Hu'z that shit Choveky?
      Mlipue...
      Choveki and Yakuonea like this.

    13. #11
      Mwali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2011
      Location : Ushongo Mabaoni
      Posts : 5,867
      Rep Power : 26882
      Likes Received
      4366
      Likes Given
      4647

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Nakusalimu kaka yangu, nakutakia Amani
      Nahisi wako uchungu, umeanza ni zamani
      Leo ni mwaka wa tatu, mpenziwe wamtaman
      iElewa huyo mwenzangu,hakutaki asilani

      Mara ya kwanza tunaona, kwa shahiri ulinena
      Sifa zako twakumbuka, hapa ndani ulimwaga
      Akajibu kwa dharau, msichana ulie mlenga
      Elewa huyo mwenzangu, hakutaki asilani

      Barua yako ya pili, ukakusudia kukiri
      Kilokua chasumbua, humo mwako kifuani
      Msichana akazidi kukuona mpuuzi
      Elewa huyo mwenzangu, hakutaki asilani

      Mara ya tatu ukaja, kwa dhiki na hasama
      Jibu lako kulitaka, na bado hukupata
      Mwanadada kama kawa, akapiga kimya kimya
      Elewa huyo mwenzangu, hakutaki asilani

      Hatimae ukasema kua shaka laingia
      Ukakosa uhakika, maana kimya cha sumbua
      Ila tamaa hukukata, ingawa hukujibiwa
      Elewa huyo mwenzangu, hakutaki asilani

      Ndoto yako hujatimiza, huku muda unasonga
      Wazee wanauliza: Bin Mbichi kaoa?
      Walazimisha kumngoja, yako ndoa hujafunga
      Elewa huyo mwenzangu, hakutaki asilani.

      Unaumwa, wateseka…Na moyo wasononeka
      Nakuonea huruma, ndugu yangu wahathirika
      Tafuta pakufarijika, ingawaje kwa dakika
      Elewa huyo mwenzangu, hakutaki asilani
      Great spirits have always encountered violent opposition from mediocre minds
      Albert Einstein


    14. #12
      Choveki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2006
      Posts : 477
      Rep Power : 766
      Likes Received
      88
      Likes Given
      163

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Quote By Mwali
      Nakusalimu kaka yangu, nakutakia Amani
      Nahisi wako uchungu, umeanza ni zamani
      Leo ni mwaka wa tatu, mpenziwe wamtaman
      iElewa huyo mwenzangu,hakutaki asilani
      ............................
      Unaumwa, wateseka…Na moyo wasononeka
      Nakuonea huruma, ndugu yangu wahathirika
      Tafuta pakufarijika, ingawaje kwa dakika
      Elewa huyo mwenzangu, hakutaki asilani
      Nilishajibu zamani, kwa ndugu pia jamaa
      Marafiki na watani, ukweli wakajulia
      Walijikuna vichwani, wakati wakishangaa
      Kwa ndugu pia jamaa, nilishajibu zamani

      Nasema kweli zamani, mwenzenu nilijulia
      Mwengine sitotamani, ingawa anizengua
      Walisema utotoni, kichwani wanisumbua
      Kwa ndugu pia jamaa, nilishajibu zamani

      Hamsa wa ishirini, miezi ikapitia
      Sikuwacha asilani, kichwani kufikiria

      Ni huyu wangu mwandani, ingawa asua sua
      Kwa ndugu pia jamaa, nilishajibu zamani

      Kijana Bin Mbichi
      Last edited by Choveki; 21st December 2011 at 23:42.
      chama, Yakuonea and Mwali like this.
      -------choveki

    15. #13
      obsesd's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd November 2011
      Posts : 1,002
      Rep Power : 631
      Likes Received
      381
      Likes Given
      627

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Quote By Choveki
      Wapendwa
      ndugu, jamaa na marafiki;


      Hiyo tamaa sikati, ninawajuza wengine
      Nimpendaye kwa dhati, ni huyu siyo mwengine
      Nitasubiri wakati, miezi hata minane
      Mitatu ama minane, nitasubiri kwa dhati!

      Nitasubiri kwa dhati, mitatu hata minane
      Na bado tampa chati, hata akiwa mjane
      Ni huyu huyu binti, sitaki hao wengine
      Mitatu ama minane, sitojalia wakati

      Nasema kweli sikati, kwa huyu siyo wengine
      Ingawa jibu sipati, upite mwezi wa nane
      Mwengine simtafuti, na wala sendi pengine
      Mitatu ama minane, tamaa miye sikati

      Dhamira yangu ya dhati, kutozengea wengine
      Sitotumia visheti, wala vitamu vingine!
      Mitego ama manoti, kuwinda hao wengine!
      Mitatu ama minane, hiyo tamaa sikati

      Maneno mengi siteti, bali barua nyengine
      Najua ni vizingiti, muvisemavyo wengine
      Ni miye mtanashati, ambaye sina mwingine
      Mitatu ama minane, kamwe tamaa sikati

      Undeni hata kamati, nakadhalika nyingine
      Kuwacha kweli siwati, wala silongi mengine
      Majibu kwenu ya dhati, ni huyu siyo mwingine
      Mitatu ama minane, nitasubiri wakati

      Nasema hapa tamati, sitoongeza mengine
      Nawajulisha umati, pamoja nanyi wengine
      Ingawa kuwa sipati, sitompenda mwengine
      Mitatu ama minane, tamaa hiyo sikati!!

      Wakatabahu waraka,

      Kijana Bin M'bichi
      mmh mshair mzur weye had raha na majib ya hapo kwa hapo jaman mmh
      Choveki and Yakuonea like this.

    16. #14
      Yakuonea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : IMEZUILIWA
      Posts : 575
      Rep Power : 526
      Likes Received
      230
      Likes Given
      259

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      UNGALI WASUBIRIA?

      Heri ya mwaka mpya, pokea zangu salamu
      vipi ya kwako afya, maisha na majukumu
      Ni muda upo kimya, sina ninachofahamu
      Je vipi yule mwandani, ungali wasubiria?

      Ni muda tena kitambo, walia na penzi lake
      Nadhani kunalo jambo, hauna haiba kwake
      Au akuona shombo, wewe si mapigo yake
      Je vipi yule mwandani, ungali wasubiria?

      Wasubiri hadi lini, bora upya ujipange
      Tafute alo makini, yule nadhani mtenge
      Madhila hutobaini, mtani wacha unyonge
      Je vipi yule mwandani, ungali wasubiria?

      Subira ina kikomo, siku nazo hazigandi
      wavutwa na chake kimo, kifua nao mtindi
      Hiki kipimo dhaifu, kama hanao ufundi
      Je vipi yule mwandani, ungali wasubiria?

      Na penda unapopendwa, usipopendwa achia
      Ni wengi tumeshatendwa, ndo maana nakwambia
      Si wote waliofundwa, wachache wathaminia
      Je vipi yule mwandani, ungali wasubiria?


      SINDANO MWANA WA GANZI (SMG)
      Choveki, Mrimu, chama and 1 others like this.
      "And do not let the hatred of a people prevent you from being just, be just; that is nearer to righteneous" [Qur'an 5:8]

    17. #15
      Choveki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2006
      Posts : 477
      Rep Power : 766
      Likes Received
      88
      Likes Given
      163

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Quote By Yakuonea
      UNGALI WASUBIRIA?
      .............................. ....................
      Na penda unapopendwa, usipopendwa achia
      Ni wengi tumeshatendwa, ndo maana nakwambia
      Si wote waliofundwa, wachache wathaminia
      Je vipi yule mwandani, ungali wasubiria?

      SINDANO MWANA WA GANZI (SMG)

      Wapendwa
      Ndugu ,Jamaa na Marafiki,

      Nakukumbusha mtani, tamaa kweli sikati
      Nilishasema zamani, kuwacha kweli siwati
      Na wala siyo utani, nina mpenda kwa dhati
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Mwengine sitotamani, ingawa nakula buti
      Ni huyu kwangu mwandani, juweni wana kamati
      Asiye na mshindani, kwa kweli nampa chati
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Majungu pia pigeni, moyoni mwangu hatoki
      Semeni mengi semeni, mseme ana nishiti
      Ni huyu kwangu moyoni, siwezi kum saliti
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Nafikiria kichwani, kupenda kama mauti
      Yaingiapo mwilini, huwezi pata zingiti
      Utabaki mtu duni, wakati u mahututi
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Nakomelea mwishoni, na tena hapa tamati
      Mwenzenu nipo penzini, nasubiria wakati
      Nasema wangu mwandani, tamaa kwake sikati
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Kijana Bin M’bichi
      Mrimu, chama, Yakuonea and 1 others like this.
      -------choveki

    18. #16
      Yakuonea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : IMEZUILIWA
      Posts : 575
      Rep Power : 526
      Likes Received
      230
      Likes Given
      259

      Default

      Quote By Choveki
      Wapendwa
      Ndugu ,Jamaa na Marafiki,

      Nakukumbusha mtani, tamaa kweli sikati
      Nilishasema zamani, kuwacha kweli siwati
      Na wala siyo utani, nina mpenda kwa dhati
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Mwengine sitotamani, ingawa nakula buti
      Ni huyu kwangu mwandani, juweni wana kamati
      Asiye na mshindani, kwa kweli nampa chati
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Majungu pia pigeni, moyoni mwangu hatoki
      Semeni mengi semeni, mseme ana nishiti
      Ni huyu kwangu moyoni, siwezi kum saliti
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Nafikiria kichwani, kupenda kama mauti
      Yaingiapo mwilini, huwezi pata zingiti
      Utabaki mtu duni, wakati u mahututi
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Nakomelea mwishoni, na tena hapa tamati
      Mwenzenu nipo penzini, nasubiria wakati
      Nasema wangu mwandani, tamaa kwake sikati
      Tamaa kweli sikati, juweni ndugu juweni!

      Kijana Bin M’bichi

      SHAURI SASA UKATE

      Mapenzi si kama ufu, Mfu hajui kupenda
      Ni jambo lilo tukufu, si vyema kuwa na inda
      Amelisifu Latifu, na nyoyo yanazilinda
      Tasubiri hadi lini, shauri sasa ukate

      Miaka inakatika, ni nini wasubiria
      Mvi zitaja kufika, bila lengo kutimia
      Au waweza zimika, huna ulicho twachia
      Tasubiri hadi lini, shauri sasa ukate

      Wajipa nyingi adhabu, kweli wajiadhibia
      Moyo waupa na tabu, mapenzi waunyimia
      Tafuta mwenye adabu, huwezi kuja jutia
      Tasubiri hadi lini, shauri sasa ukate

      Kibuti alikupatia, ni wewe umetwambia
      Binti kaonyesha nia, njema hajakusudia
      Mbona wapapatikia, wadai kuvumilia
      Tasubiri hadi lini, shauri sasa ukate

      Hakuna alo majungu, huruma twakuonea
      Ondoa huo ukungu, kaumu yakuzomea
      Jipatie mcha mungu, mpole aso gomea
      Tasubiri hadi lini, shauri sasa ukate

      Sipendi uwe wa duni, sababu eti mapenzi
      Hofu na shida mwilini, kwa asiyejua kuenzi
      Tabu wajipia nini, kupenda huyo hawezi
      Tasubiri hadi lini, shauri sasa ukate

      Sindano Mwana wa Ganzi (SMG)
      Safarini Tongoleani




      LA KWAKO LA PANDE MOJA

      Yailahi yarabana, Mola mtangu na tangu
      waja twakimbizana, Mapenzi nayo machungu
      Kila leo danadana, Tusaidie e Mungu
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      Choveki u mahututi, Kwa penzi usilopata
      Nimefanya utafiti, na pia ninazo 'data'
      Ulisha pigwa kibuti, yanini sasa kufata
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      Mapenzi jambo swadifu, wawili mkipeana
      Na wala hayana kifu, mwaruka mwatekenyana
      Yataka na utwiifu, hakuna cha kunyimana
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      Mapenzi ni ya wawili, la mmoja sijaona
      Haitakiwi bahili, vyote vyote mwapeana
      Utanawiri na mwili, kwa penzi lisilo bana
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      Na hili la pande moja, si pendo ni ukatili
      Huwezi kuwa na hoja, limefungwa ka pingili
      Hata useme wangoja, haliwezi kuwa 'dili'
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      Kwa kweli pendo sioni, yako ni mataabiko
      Iweje wewe huoni, pasipo na furahiko
      Au tupulize honi, waweza pata zinduko
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      Na pendo ni kuwa nalo, si kama wafikiria
      Ukiona hilo silo, ni bora kujiachia
      Utafute lile ndilo, moyoni utatulia
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      Yatosha kubembeleza, fanya tafuta mwingine
      kuna miji ya Arusha, Tanga Pwani na kwingine
      Waweza kubahatisha, ujitoe kivingine
      Mapenzi hapo sioni, la kwako la pande moja

      SINDANO MWANA WA GANZI (SMG)
      KIJIJINI TONGOLEANI
      Last edited by Yakuonea; 15th February 2012 at 21:42.
      Choveki, Mrimu, chama and 1 others like this.

    19. #17
      AmaniGK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th January 2008
      Location : MAHALI FLANI
      Posts : 826
      Rep Power : 745
      Likes Received
      64
      Likes Given
      150

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Kumbe huu uzi bado uko? nitarudi
      Choveki and Yakuonea like this.
      He who wants to keep his garden tidy doesn't reserve a plot for weeds

    20. #18
      Excellent's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th December 2009
      Posts : 5,552
      Rep Power : 2283
      Likes Received
      2346
      Likes Given
      4030

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Guys that's really good job
      Choveki and Yakuonea like this.

    21. #19
      Omonto wa-hene's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 150
      Rep Power : 390
      Likes Received
      39
      Likes Given
      37

      Default Re: Mwenziyo unanikosha!

      Huyu binti anaelekea kufa kwa umri. Ningojeni kidogo nikushushieni beti za tanzia!
      Choveki and Yakuonea like this.

    22. #20
      Yakuonea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : IMEZUILIWA
      Posts : 575
      Rep Power : 526
      Likes Received
      230
      Likes Given
      259

      Default

      Quote By AmaniGK
      Kumbe huu uzi bado uko? nitarudi

      Amani fanya urudi, muase ndugu choveki
      Afanye jambo la budi, amuache yule feki
      Na raha atafaidi, asijue nini dhiki
      CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA

      Beti nilimtumia, kumpa yeye nasaha
      Hekima nikajazia, aepuke ya karaha
      Awache kung'ang'ania, ajenge yake staha
      CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA

      Beti zangu hakujibu, sijui hata kwa nini
      Labda ni zake ghadhabu, kwa vile bado kuwini
      Au kashikwa aibu, binti kutomthamini
      CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA

      Na hataki shaurika, eti mrembo ni wake
      siku nazo zakatika, aishi kivyake vyake
      uzee utamfika, bila hata ya mwenzake
      CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA

      Amani mpe shauri, atafute yeye mwenzi
      Kuna wadada wazuri, mahodari wa mapenzi
      Tena hawana viburi, kwa mema yao malezi
      CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA

      SINDANO MWANA WA GANZI (SMG)
      KIJIJINI TONGOLEANI
      Choveki and AmaniGK like this.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...