Nimekuwa nasikia maneno haya lakini yananichanganya kujua matumizi yake sahihi.
Vukiza au fukiza?
Vundika au vumbika?
Compyuta?
Mtandao
ila
ingawa
msanii
puchu
mkwara
mwake
chuna
mbongo
Ninayo maneno lukuki lakini nashindwa kuyaainisha yote hapa. Naomba wataalam wa lugha hii adhimu mnisaidie nitoke niliko walau hatua moja mbele katika kujifunza Kiswahili.
Ahsanteni
__________________ Welcome to JF Phase II...
Contact me:
Mobile: +255713444649
Email: maxence@maxence.co.tz
Pls DO NOT send me Job applications... Read adverts carefully!
...hii thread members wengine mme-iundermine sana kwa kutoisoma mapema!!!
tafsiri ya: 'members should not undermine the efforts of the administration'
"wanachama wasidhoofishe ((kwa)makusudi) jitihada za uongozi"
__________________
Jamii ijuayo uwiano thabiti kati ya dharau, ubinafsi, chuki na ustaarab dhidi ya jamii nyingine na baina ya watu wake ni jamii yenye maendeleo. Isiyojua ni dumazi. SD1-09.
Fikra ni nyenzo endelezi au potofu. Changamoto tuliyonayo ni kuchanganua na kutenganisha kati ya fikra endelevu na fikra potofu, kwani mwisho wa fikra ni matendo pale fikra hazibakii kuwa fikra. SD6-07Rev.2-09.
Mzee Mwanakijiji
anawashangaa wanaoitetea sheria mbovu
JF Premium Member
Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 18,469
Thanks: 8,494
Thanked 4,671 Times in 1,312 Posts
Rep Power: 44
Re: Maana ya 'undermine'
sasa neno kudhoofisha ni sawa na kupunguza nguvu (to weaken). Mtu ambaye ni dhaifu (which is the root word ya neno dhoofu) inahusiana na hali ya kuchoka nguvu, kupungua nguvu n.k
Nilitaka tutumie lile neno "tekua" alilolisema memba hapo nyuma.
__________________ Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
sasa neno kudhoofisha ni sawa na kupunguza nguvu (to weaken). Mtu ambaye ni dhaifu (which is the root word ya neno dhoofu) inahusiana na hali ya kuchoka nguvu, kupungua nguvu n.k
Nilitaka tutumie lile neno "tekua" alilolisema memba hapo nyuma.
Weaken ni katika synonyms za undermine. Tekua ni neno zuri lenye maana halisi ya undermine, ila nahofia hadhira yako kuweza kuling'amua mara moja. Kama unaandaa sheria ndogo ndogo tumia lugha rahisi iwezekanavyo.
tafsiri ya msemo huo wa mwanakijiji ni
"wanachama wasitweze juhudi za mamlaka"
__________________ Ni haki yangu kuukataa uwongo kama ilivyo wajibu wangu kuukubali ukweli ,itakuwa ni makosa makubwa kuukataa ukweli eti kwa vile siupendi-gamba la nyoka.
mpaka sasa neno "komputer" ni msamiati sahihi wa kiswahili. ni neno ambalo limetoholewa/ kukopwa kutoka katika kiingereza kama maneno mengine kama vile shati-(shirt), trekta-(tractor). kutohoa au kukopa maneno kutoka lugha nyingine, ni jambo la kawaida na katika lugha zilizo nyingi duniani zimetumia njia hii kujiongezea msamiati wake.
Nitasaidia kama ninavyoweza kama ifuatavyo:
*Vukiza/Fukiza ni maneno yenye maana sawa,yaani kuweka kwenye mazingira ya moshi,iwe wa kuni au maVumba kwa nia ya kukausha kwa maana ya kuhifadhi au kufanya takatifu.
*Vundika au Vumbika:Haya ni maneno yenye maana sawa.Yaani kufanya ive au ioze:
*Compyuta:Hili sio neno la kiswahili,ila ni neno lililoazimwa kutoka kwenye kiingereza.
*Ingawa:Hili ni neno linalo halalisha udhuru.Kwa mfano,'ingawa sikwenda lakini mambo yatakwenda vizuri.'
*Msanii:Maana halisi ya msanii ni mstareheshaji,ingawa siku hizi msanii anaelezwa pia kama mtu asiye mkweli.
*Puchu:Hali ya kutokuwa na manyoya.
*Mkwara:kumkosoa mtu katika hali ya kukasirika.
*mwake:mazingira yanayomilikiwa na mtu husika.
Chuna:Toa ngozi.
Mbongo:Sina hakika sana ya neno hili,lakini nimesikia watu wengine wakilitumia wakimaanisha akili nyingi.
Fukiza ni kwa Moshi, Vukiza ni kwa Mvuke hivyo ukisema yana maana sawa si kweli ila yanakaribiana kimaana kwa kiasi.
Vundika ni neno mnyumbuliko wa Neno VUNDA
Vumbika linatokana na mnyumbulisho wa VUMBA/VUMBI
kwa hayo mengine sitofautiani sana nawe.
Shukrani kwa wote waliochangia katika kudadavua maneno yaliyoulizwa. Ningependa kuongeza tu kwamba Baraza la Kiswahili la Taifa (Tanzania) limeridhia kutohoa neno "Computer" na kuwa kiswahili bali linaandikwa kwa silabi za kiswahili yaani "Kompyuta".
Mzee Mwanakijiji
anawashangaa wanaoitetea sheria mbovu
JF Premium Member
Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 18,469
Thanks: 8,494
Thanked 4,671 Times in 1,312 Posts
Rep Power: 44
Maana ya neno "Venture"
HIvi neno "venture" tunaweza kulitafsiri vipi katika Kiswahili.?
a. He ventured into new mission
b. He was a venture capitalist
__________________ Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"