| Find/Invite Friends | Register | Calendar | Search | Today's Posts | Mark Forums Read |
| FAQ | Members List | Bongo Flava | Zilipendwa | Taarab | Injili |
|
|
#1 | |||||||||||
|
||||||||||||
|
Views: 239
|
||||||||||||
|
#2
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Hoja yako ni kweli tupu na sababu zako pia zina ukweli, Watanzania tumelala, sijui ni ile sera ya Ujamaa enzi za shule bure, matibabu bure na kipindi cha njaa, chakula bure.
Miaka ya 60, Tanzania ndio ilikuwa nchi ya kwanza duniani kutangaza rasmi Kiswahili ndio lugha yake ya Taifa. Mataifa ya nje yalichukua watangazaji wa Redio Tanzania kuwa waanzilishi wa Idhaa za Kiswahili za redio hizo. Godfrey Mngodo alikwenda kuanzisha Idhaa ya Kiswahili ya Voice of America, Elli Mboto na David Wakati wakaenda kuanzisha BBC kule London, Erasto Mbwana akaenda Sauti ya Ujerumani, nchi nyingine nyingi zikafuatia ikiwemo Japan-Florian Kaiza, India, Radio Moscow, Sauti ya China, Abdala Mbamba wa Sauti ya Umoja wa Mataifa, New-York, hata nchi kama Afrika Kusini na Rwanda walichukua watangazaji toka Tanzania kuanzisha idhaa za Kiswahili. Jirani zetu Kenya walikuwa na Kiswahili kibovu. Tido Mhando alipoondoka RTD na kujiunga na Sauti ya Kenya, ndiye alikuwa super star wao kabla ya kuhamia BBC. Sasa Kiswahili kinatawaliwa na Kenya, idadi ya watangazaji wa Kiswahili kutoka Kenya, wametupiku vibaya!.Nairobi ndio makao makuu ya BBC Swahili kanda ya Afrika. Mabosi karibu wa redio zote za kimataifa za Kiswahili sasa ni Wakenya, ukiondoa Sauti ya Ujerumani ambako bado ni Mtanzania. Nilitembelea chuo kikuu cha Sweeden, kinafundisha Kiswahili, malecture Wakenya!. Nikiwa Uswisi, kuna jamii kubwa ya Watanzania na demandi ya wanaotaka kujua lugha ya Kiswahili ni kubwa, karibu tuition zote za Kiswahili, zinafundishwa na Wakenya!. Kulala kwetu sio kwenye Lugha tuu, hata katika ajira za kimataifa, Tanzania hatuna sera yoyote ya job-export, ukifika Makao Makuu ya UN pale New York, waswahili kibao ila wengi ni Wakenya, Waganda na Wasomali, nilipomuuliza ofisa mmoja akasema nafasi zinatangazwa mtandaoni, Watanzania hatuziombi, Wakenya wao wanazichukua na kuzitangaza nchini mwao ikiwemo juhudi mahsusi kuwasaidia Wakenya wenye sifa, kuziomba nafasi hizo, Watanzania kimya. Mipaka ya soko la ajira ikishafunguliwa na kuwa huru, kama serikali yetu haitafanya juhudi za makusudi za kulinda ajira za sekta binafsi, kazi zote za wajanja (decent jobs) na zile za akili, zitachukuliwa na Wakenya, na sisi tutabakia na kazi za wajinga wajinga na zile manual. Baadhi ya Watanzania sijui tuna nini!?, kama vile tumelogwa!. Mimi binafsi ni miongoni mwa waliojaribu life, Uk, US na nchi kibao ughaibuni lakini niliambulia patupu na kujirudia bongo kuendelea na kukurukushana na kukurukakara za kazi za kijungu jiko katika lindi la umasikini uliotopea. |
|
#3
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
asanteni kwa kuleta hiii mada jukwaaani yaaani huo ndio ukweli wenyewe ,umefika wakati watanzania tujikwamue kiamawazo kwanza maana wengi wetu tuko busy kujikwamua kimaisha huku hatujui kwamba unatakiwa uanze kujikwamua kimawazo ili ujikwamue kimaisha.
|
|
#4
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Kinetiq01 na pasco katika hoja mlizowahi toa hapa jamvini wakuu hapa mmegusa penyewe....saa ingine sisi wa tz tuko kama sikio la kufa...sijui dawa itatoka wapi tunalala sana, hizi post zenu almanusura zinitoe chozi
__________________
Women will never be as successful as men because they have no wives to advise them. Dick Van Dyke
«
Previous Thread
|
Next Thread
»
Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako! All times are GMT +3. The time now is 12:00 PM.
Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||