Je tunajua Kenya inanufaika zaidi na Kiswahili? - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Education, Science & Technology Forums > Jukwaa la Lugha


Jukwaa la Lugha Swahili, English languages special forum.


Reply
 
LinkBack Thread Tools Display Modes
Old 10th June 2009, 02:21 AM   #1
Je tunajua Kenya inanufaika zaidi na Kiswahili?
kinetiq01 kinetiq01 is offline 10th June 2009, 02:21 AM

Huenda si hoja mpya, lakini najiuliza endapo tunajua kwamba Kenya inanufaika zaidi na Kiswahili licha ya kuwa na wazungumzaji wachache kuliko Tanzania?

Nasema hayo kwasababu kibiashara au kiteknolojia inaonyesha Kenya inapata miradi mingi na mikubwa zaidi kuliko Tanzania kwa kigezo cha lugha ya Kiswahili.Nitatoa mfano:-

1. Jumapili ijayo Facebook watafanya sherehe Nairobi ya kuzindua mradi wa Facebook kwa lugha ya Kiswahili. CEO na founder Mark Zuckerberg ndiye atakuwa mgeni rasmi.

2. Microsoft wamekuwa na ofisi kubwa Nairobi kwa muda mrefu, ambapo project yao ya OS localisation imepata mafanikio makubwa.

3. Google wana ofisi ya kanda Nairobi, wanafanya shughuli mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuunda translation tool ya Kiswahili.

Mashirika yote haya yanaajiri wataalam wa Kiswahili ambapo kwa asilimia kubwa ni wakenya. Sisi wa kwetu wanaishia kulalamika kuwa Kiswahili kinachotumika siyo fasaha, lakini hawachukui hatua kuwavutia hao wenye miradi kuiendeleza ndani ya Tanzania.

Nimetoa mifano hiyo michache, lakini yako mambo mengi ambayo naona hatuyachangamkii. Kama kuna kitu watanzania tungeweza kufanikiwa kwa urahisi ni ku-export Kiswahili kama product, hakuna wa kutubabaisha. Lakini wapi bwana. Najiuliza tatizo ni nini? Zifuatazo zaweza kuwa baadhi ya sababu.

- Hatuna sera ya kitaifa kujenga na kutumia Kiswahili kama biashara
- Huenda ikawa sisi hatujui kutumia fursa zinazojitokeza.
- Huenda jamaa wakiwasilisha mawazo ya kufanya kazi zao kwetu hawapati ushirikiano.
- Huenda mawasiliano duni ya teknolojia yanawakatisha tamaa
- Hatuna wataalam wa Kiswahili ingawa tuna wazungumzaji wa Kiswahili
__________________
FACT: A democracy requires accountability, and accountability requires transparency.

 
kinetiq01's Avatar
kinetiq01
Member
Points: 126,824, Level: 100 Points: 126,824, Level: 100 Points: 126,824, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
Join Date: Fri Aug 2006
Location: cyberspace
Posts: 49
Thanks: 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Views: 239
Reply With Quote
  #2  
Old 10th June 2009, 07:15 AM
Pasco Pasco is offline
Pasco has no status.
JF Premium Member
Points: 800,358, Level: 100 Points: 800,358, Level: 100 Points: 800,358, Level: 100
Activity: 11% Activity: 11% Activity: 11%
 
Join Date: Mon Sep 2008
Posts: 2,107
Thanks: 1,725
Thanked 1,217 Times in 468 Posts
Rep Power: 66
Pasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the rough
Default Re: Je tunajua Kenya inanufaika zaidi na Kiswahili?

Hoja yako ni kweli tupu na sababu zako pia zina ukweli, Watanzania tumelala, sijui ni ile sera ya Ujamaa enzi za shule bure, matibabu bure na kipindi cha njaa, chakula bure.
Miaka ya 60, Tanzania ndio ilikuwa nchi ya kwanza duniani kutangaza rasmi Kiswahili ndio lugha yake ya Taifa. Mataifa ya nje yalichukua watangazaji wa Redio Tanzania kuwa waanzilishi wa Idhaa za Kiswahili za redio hizo. Godfrey Mngodo alikwenda kuanzisha Idhaa ya Kiswahili ya Voice of America, Elli Mboto na David Wakati wakaenda kuanzisha BBC kule London, Erasto Mbwana akaenda Sauti ya Ujerumani, nchi nyingine nyingi zikafuatia ikiwemo Japan-Florian Kaiza, India, Radio Moscow, Sauti ya China, Abdala Mbamba wa Sauti ya Umoja wa Mataifa, New-York, hata nchi kama Afrika Kusini na Rwanda walichukua watangazaji toka Tanzania kuanzisha idhaa za Kiswahili.
Jirani zetu Kenya walikuwa na Kiswahili kibovu. Tido Mhando alipoondoka RTD na kujiunga na Sauti ya Kenya, ndiye alikuwa super star wao kabla ya kuhamia BBC.
Sasa Kiswahili kinatawaliwa na Kenya, idadi ya watangazaji wa Kiswahili kutoka Kenya, wametupiku vibaya!.Nairobi ndio makao makuu ya BBC Swahili kanda ya Afrika. Mabosi karibu wa redio zote za kimataifa za Kiswahili sasa ni Wakenya, ukiondoa Sauti ya Ujerumani ambako bado ni Mtanzania.
Nilitembelea chuo kikuu cha Sweeden, kinafundisha Kiswahili, malecture Wakenya!.
Nikiwa Uswisi, kuna jamii kubwa ya Watanzania na demandi ya wanaotaka kujua lugha ya Kiswahili ni kubwa, karibu tuition zote za Kiswahili, zinafundishwa na Wakenya!.

Kulala kwetu sio kwenye Lugha tuu, hata katika ajira za kimataifa, Tanzania hatuna sera yoyote ya job-export, ukifika Makao Makuu ya UN pale New York, waswahili kibao ila wengi ni Wakenya, Waganda na Wasomali, nilipomuuliza ofisa mmoja akasema nafasi zinatangazwa mtandaoni, Watanzania hatuziombi, Wakenya wao wanazichukua na kuzitangaza nchini mwao ikiwemo juhudi mahsusi kuwasaidia Wakenya wenye sifa, kuziomba nafasi hizo, Watanzania kimya.

Mipaka ya soko la ajira ikishafunguliwa na kuwa huru, kama serikali yetu haitafanya juhudi za makusudi za kulinda ajira za sekta binafsi, kazi zote za wajanja (decent jobs) na zile za akili, zitachukuliwa na Wakenya, na sisi tutabakia na kazi za wajinga wajinga na zile manual.
Baadhi ya Watanzania sijui tuna nini!?, kama vile tumelogwa!. Mimi binafsi ni miongoni mwa waliojaribu life, Uk, US na nchi kibao ughaibuni lakini niliambulia patupu na kujirudia bongo kuendelea na kukurukushana na kukurukakara za kazi za kijungu jiko katika lindi la umasikini uliotopea.
Reply With Quote
  #3  
Old 10th June 2009, 10:33 AM
agika agika is offline
agika has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 77,337, Level: 100 Points: 77,337, Level: 100 Points: 77,337, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Fri Jun 2009
Posts: 385
Thanks: 3
Thanked 4 Times in 3 Posts
Rep Power: 21
agika will become famous soon enoughagika will become famous soon enoughagika will become famous soon enoughagika will become famous soon enoughagika will become famous soon enoughagika will become famous soon enoughagika will become famous soon enoughagika will become famous soon enough
Default Re: Je tunajua Kenya inanufaika zaidi na Kiswahili?

asanteni kwa kuleta hiii mada jukwaaani yaaani huo ndio ukweli wenyewe ,umefika wakati watanzania tujikwamue kiamawazo kwanza maana wengi wetu tuko busy kujikwamua kimaisha huku hatujui kwamba unatakiwa uanze kujikwamua kimawazo ili ujikwamue kimaisha.
Reply With Quote
  #4  
Old 10th June 2009, 10:50 AM
Nguli's Avatar
Nguli Nguli is offline
Nguli is a God fearing Man
JF Premium Member
Points: 817,313, Level: 100 Points: 817,313, Level: 100 Points: 817,313, Level: 100
Activity: 22% Activity: 22% Activity: 22%
 
Join Date: Mon Mar 2008
Location: HOME
Posts: 2,520
Thanks: 601
Thanked 1,029 Times in 541 Posts
Rep Power: 27
Nguli will become famous soon enoughNguli will become famous soon enoughNguli will become famous soon enoughNguli will become famous soon enoughNguli will become famous soon enoughNguli will become famous soon enoughNguli will become famous soon enoughNguli will become famous soon enough
Default Re: Je tunajua Kenya inanufaika zaidi na Kiswahili?

Kinetiq01 na pasco katika hoja mlizowahi toa hapa jamvini wakuu hapa mmegusa penyewe....saa ingine sisi wa tz tuko kama sikio la kufa...sijui dawa itatoka wapi tunalala sana, hizi post zenu almanusura zinitoe chozi
__________________
Women will never be as successful as men because they have no wives to advise them. Dick Van Dyke
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
inanufaika, je, kenya, kiswahili, tunajua, zaidi


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Proudly Kenyan Nyaralego International Forum 5 12th May 2009 08:36 PM
Proudly Kenyan Shy Jukwaa la Elimu (Education Forum) 0 5th March 2008 03:25 PM
Kenya sasa wananyoana, Watanzania tutie maji Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 0 30th January 2008 02:15 AM
Maandamamano ya Kenya kuhamia Tanzania? Asha Abdala Habari na Hoja mchanganyiko 62 7th January 2008 12:14 PM
Kenya Waamua Kuwa Na Ccm Yao Ole Habari na Hoja mchanganyiko 4 25th January 2007 07:46 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 12:00 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com