Re: Ugali kweli mtamu?
Ugali mtamu ee! Hongera kwa kuusifia ugali.
10th June 2009, 10:09 PM
Mtu wa Kawaida
has no status.
JF Premium Member
Join Date: Fri May 2008
Posts: 182
Thanks: 1
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power:
22
Re: Ugali kweli mtamu?
Quote:
Wote nimewashangaa, mlosifia ugali,
Mmefanya ukang’aa, kwa sifa zisizo kweli,
Wengine mwagaagaa, kushangilia ugali,
Utamu ni wa ugali, au chake kitoweo?
Kila palipo ugali, hapakosi kitoweo,
Kumeza tonge muhali, bila chake kimezeo,
Na huo ndio ukweli, mawio hadi machweo,
Utamu ni wa ugali, au chake kitoweo?
Mnasifia ugali, pembeni mwataja mboga,
Hebu semeni ukweli, mboga ndio inanoga,
Acheni kututapeli, kutugeuza mizoga,
Utamu ni wa ugali, au chake kitoweo?
Mzee Mwanakijiji, ndugu yangu wa daima,
Ugali si kama uji, bila mboga utatema,
Bora wali wa Ujiji, usiokuwa na nyama,
Utamu ni wa ugali, au chake kitoweo?
Yametajwa matembele, mlenda pia kisamvu,
Pweza, dagaa mchele, kachumbari na mnavu,
Nyama nayo vilevile, ya mchuzi ama kavu,
Utamu ni wa ugali, au chake kitoweo?
Ugali huli mkavu, kama ubwabwa wa Kyela,
Yatakuvimba mashavu, tonge huwezi kulila,
Yataka uwe shupavu, vinginevyo ni madhila,
Utamu si wa ugali, bali chake kitoweo!
Msinione mbishi, bali ni yangu maoni,
Wala msinishawishi, niyakubali ya nani,
Maswali siyajalishi, kuweni uhuru moyoni,
Utamu si wa ugali, bali chake kitoweo!
Maamuma nimekubali, yako mapungufu ugali
Ni kweli umeona mbali, kwa sifa iliyopata ugali
Hata mie sikubali, kwa hayayote ya ugali
Kitoweo unogesha ugali, mie pia nimekubali
Bila kitoweo chochote, huwezi kula ugali
Ili waulize wote, hata wapenzi wa wali
Weye pitia kokote, na tia hilo swali
Kitoweo unogesha ugali,mie pia nimekubali
__________________
Tabia ni kama ngozi hauwezi kuibadili....
12th June 2009, 02:29 PM
JosM
where do we go? what do we know?
JF Senior Expert Member
Join Date: Sat Oct 2008
Location: Dar es salaam/Kampala/lam
Posts: 638
Thanks: 8
Thanked 6 Times in 6 Posts
Rep Power:
23
Re: Ugali kweli mtamu?
Quote:
Ugali kweli mtamu,
Kwa huo ninayo hamu,
Kwa mboga yenye saumu!
Ugali tangu shuleni
Jamani hadi jeshini
Nikaula na chuoni
Ugali iwe mchana
Kwenye upepo mwanana
Mwenzenu ninajichana
Ugali hata jioni,
Mezani au jikoni
Nikishatoka kazini
Ugali iwe kwa mboga
Sima kwa kweli yanoga
Kwa tembele na maboga!
Ugali kwa kurumagia
Vidole kujilambia
Na nyama inanukia!
Ugali ule kwa mchuzi
Wa samaki hata mbuzi,
Mwanawane kama kazi!
Ugali msosi wa nguvu
Haupikwi kwa wavivu,
Au walio wachovu
Ugali uwe kiporo
Alfajiri na mmajoro
Kwa mapanki ya Nyamanoro!
Ugali nimesifia
Wali ninautungia
Beti nitaupangia,
Ugali nafakamia
Matonge navingiria
Nakula nafikiria
UGALI KWELI MTAMU!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
lunch time jamani karibuni tupate ugali.
http:// ugali.jpg tanzania_food.jpg DSC00066.JPG makande.jpg DSC01837.JPG
__________________
Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki,na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu .
Last edited by JosM; 19th June 2009 at 02:43 PM ..
13th June 2009, 03:01 PM
Kingi
is down to earth
JF Senior Expert Member
Join Date: Thu Mar 2009
Posts: 1,612
Thanks: 165
Thanked 215 Times in 169 Posts
Rep Power:
25
Re: Ugali kweli mtamu?
Quote:
Ugali kweli mtamu,
Kwa huo ninayo hamu,
Kwa mboga yenye saumu!
Ugali tangu shuleni
Jamani hadi jeshini
Nikaula na chuoni
Ugali iwe mchana
Kwenye upepo mwanana
Mwenzenu ninajichana
Ugali hata jioni,
Mezani au jikoni
Nikishatoka kazini
Ugali iwe kwa mboga
Sima kwa kweli yanoga
Kwa tembele na maboga!
Ugali kwa kurumagia
Vidole kujilambia
Na nyama inanukia!
Ugali ule kwa mchuzi
Wa samaki hata mbuzi,
Mwanawane kama kazi!
Ugali msosi wa nguvu
Haupikwi kwa wavivu,
Au walio wachovu
Ugali uwe kiporo
Alfajiri na mmajoro
Kwa mapanki ya Nyamanoro!
Ugali nimesifia
Wali ninautungia
Beti nitaupangia,
Ugali nafakamia
Matonge navingiria
Nakula nafikiria
UGALI KWELI MTAMU!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
raha ya ugali dona
sio sembe hapana
dona ile mchana
mwili takingwa maradhi
utajenga stamili na hadhi
hakika hutamhitaji 'kadhi'
__________________
"The only problem with Africans is implementation and maintenance"- Kingi .
15th June 2009, 02:24 PM
AbbyBonge
has no status.
Member
Join Date: Thu Apr 2009
Posts: 41
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power:
0
Re: Ugali kweli mtamu?
Nashindwa kustahimili,
Na kuusifia Ugali,
Hata upikwe na mwali,
Kamwe sijuvunii Ugali,
Ni chakula cha mifugo,
Wanakiweza wagogo,,
Nipe wali na Pongo,
Hapo Napata usongo,
Wali si lazima na nyama,
Japo umevikwa heshima,
Na kama utaupa nyama,
Basi ndoa himahima.
Vigori wetu mkoleni,
Tuwafunde kishuleni,
Nao wakiwa nyumbani,
Wali wapike jikoni,
Wali ukitiwa nazi,
Kama uchi wenye vuzi,
Hata kama mwanafunzi,
Utadinda kama tozi.
15th June 2009, 03:34 PM
AbbyBonge
has no status.
Member
Join Date: Thu Apr 2009
Posts: 41
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power:
0
Re: Ugali kweli mtamu?
Quote:
Wali ukitiwa nazi,
Kama uchi wenye vuzi,
Hata kama mwanafunzi,
Utadinda kama tozi.
Hodihodi Jamvini, naomba nipokeeni,
Mja wenu najirudi, mwenzenu nisameheni,
Nimechanganya maneno, niliyotoa jamvini,
Sikutumia busara, matusi kuyathamini,
Nikaanika jamvini, maneno yasoakili,
Nikasahau watoto, eti napinga ugali,
Huyu shetani gani, nimtafutie nauli,
Aende zake mwituni, akale wake ugali,
Naapa kutorudia, nikichangia mawazo,
Nitaheshimu maneno, sio kama vile mwanzo,
Niacheni nikalale, nipate tuliza mawazo,
Abbybonge ni mnyonge, msiniwekee vikwazo.
19th June 2009, 01:52 PM
Choveki
has no status.
JF Senior Expert Member
Join Date: Sun Apr 2006
Posts: 381
Thanks: 47
Thanked 18 Times in 9 Posts
Rep Power:
24
Re: Ugali kweli mtamu?
Quote:
Ugali kweli mtamu,
Kwa huo ninayo hamu,
Kwa mboga yenye saumu!
........UGALI KWELI MTAMU!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Choveki ninarejea
Ilani kuwatolea
Ugali kuusifia
Uchuro mwajitakia?
Duniani kuna mambo
Ambayo yaleta shombo
Ugali kama makombo
Na hepa na lake shombo!
Mnaliita ugali
Lifananie na wali
Dona kamwe siyo wali
Pia hata kwa asili
Dona lapigiwa debe
Na kelele kebekebe
Nashangaa wenye ngebe
Tatizo lenu ni shibe!
Jina halisi ni dona
Tangia juzi na jana
Wazee pia vijana
Wajua jina ni dona!
Pia bondo ni jengine
Amekumbusha mwingine
Majina mengi mengine
Zaidi yake manne
Chakula hicho cha jela
Napata shida kukila
Sababu miye kabwela
Ndiyo maana nakila!
Dona kwangu la ugwadu
Na tena sili husudu
Lafanania kibudu
Nawaachia wa Ngudu!
__________________
-------choveki
Last edited by Choveki; 21st June 2009 at 04:16 PM ..
Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
Thread Tools
Display Modes
Linear Mode
Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts
HTML code is Off
Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako !
All times are GMT +3. The time now is 08:28 AM .
Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com