Zabibu langu li tamu,
Pekee lanipa hamu,
Ni tamu tunda adhimu,
La kale kama ya Shamu!
Linaendelea...
__________________ Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
Njoo uje huku kwa energy needs bana.
Tusiishie tunda tunda...huku mabazazi wanakata mti.
duh.. wapi tena usije kukuta mti wa tunda wenyewe umekatwa!!
__________________ Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
__________________ Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
Mimi nina swali moja
Mara kichwani huja
Sitegemei vioja
Bali jibu lenye hoja
Mimi nataka kujua
Linahisije kuliwa
Tunda linalosifiwa
Au halina hisia?
Zabibu, nanasi, embe
Hivyo vyote ni viumbe
Vipi navyo visitambe
Atambe mshika jembe?
Mwenye ujuzi fumbua
Linahisije kuliwa
Tunda mnalochukua
Ganda lake kulivua?
Swali lako ni makini
Ila ndani ni mtego
Umetegwa kilaini
kunasa wenye magego!
Siri nitaifichua
Hisia zake matunda,
Hili ukishalijua
Na mti utaupanda!
Tunda lapenda kuliwa,
Linapenda kutafunwa,
Langoja kutunguliwa,
Pole pole likamenywa!
Kisu kikapenya kati,
Mchuzi ukamwagika,
Bila hata varangati,
Meza tukaziandika.
Ndiyo maana yaiva,
Ili baadaye yaliwe,
Mengine yasiyoiva,
Kwanini yatunguliwe?
Raha yake ni kung'atwa
Au kisu kuchomekwa,
Na kisha hata kupikwa,
Jikoni yakabandikwa!
Yanajitoa mhanga,
Matunda nayasifia
Na yale yanayoringa,
Watu wanayachukia!
Raha ya tunda kuliwa
Mbinguni wameandika
Na mbegu zapunjuliwa
Wa kijiji naandika.
Kalamu naweka chini,
Tunda langu limeiva,
Kisu kiko mkononi
Tunda kalileta Eva!!
__________________ Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"