Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Usiku Wa Giza

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. Shy
      #1
      Shy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2006
      Posts : 4,922
      Rep Power : 0
      Likes Received
      75
      Likes Given
      0

      Default Usiku Wa Giza

      Wewe usiku wako labda unautumia kwa ajili ya kulala tu usiku unakaa unaota ndoto nzuri wakati mwingine za kutisha na kuchekesha ndoto hizo wakati mwingine ni kama zinakuhabarisha mambo unayokuja kukutana nayo siku za mbeleni kama prophecy wengine husema , ndio wewe unaona na kushangilia usiku wako , wengine usiku huu huutumia kwa kazi zao mfano polisi na walinzi wao hutumia saa za usiku kulinda watu wao na taifa kwa ujumla , wengine kama Malaya huutumia usiku huu kwa kujiuza na kufanya biashara za miili yao , wengine kazi yao ni kucheza muziki kwahiyo saa za usiku kwao ni kucheza muziki kuburudisha wengine na wengine ni majambazi usiku wa giza wao huutumia kurubuni watu , kuuwa watu ili wajipatie chochote kile kwa maisha yao ya kila siku , wengine wa wanga na wachawi hutumia usiku kama wakati wao wa kufanya mambo yao ya kishirikina bila kuonekana na roho za kawaida kwahiyo kila mtu ana mambo yake wakati wa usiku .

      Basi bwana nyumbani kwetu tulikuwa na ngombe kama 3 hivi huko moshi vijijini , hawa ngombe wote ni wakike , walivyokuwa wakubwa babu yetu akaamua kuwapeleka kwa dume awapande ili waweze kuzaa watoto na tupate ndama , maziwa na maziwa mengine yawe ni ya kuuza kwa watu wengine katika mtaa huo huko vijijini .

      Haya ngombe walipandwa , mmoja akazaa lakini ndama wake akafa huyu mwingine ndama wake hakufa lakini yule ndama alikufa katika mazingira ya kutatanisha daktari wa kujiji alivyokuja kuangalia hakukuta alama yoyote ya sumu au kama amekula chakula chochote kile kibaya basi tukamwachia mola.

      Ngombe bwana wakawa wanatoa lita 20 mpaka 30 kwa siku moja babu yetu alifurahi sana , lakini baada ya wiki 2 hivi hali ikaanza kuwa tofauti sana , yaani yule ngombe hatowi maziwa yanakuwa kama vile yamekamuliwa usiku kutwa .

      Siku moja tumakaa kibarazani babu yetu akawa anatupa hadithi za hapa na pale jirani yetu akaja alipofika pale akamwambia babu kuhusu yule mzee wa mtaa wa pili anavyokuja kuiba maziwa usiku kwa njia za kishirikina akamweleza kila kitu .

      Lakini babu hakuwa na nguvu zozote basi bwana ikabidi yule mzee atupe dawa mimi na kaka yangu mmoja ili yule mzee akija usiku tuweze kumkamata na kumwadhibu usiku unaofuatia akatuelekeza cha kufanya kila kitu .

      Usiku ukafika , tukajipaka zile dawa tukakaa sehemu karibu na banda la ngombe tukasikia kengele zinalia kutokea mbali ngrii ngrii ngrii , tukakaa kimya , ndio tukaona mzee mmoja anakuja miguu yake ikiwa juu na mikono chini yaani anatembea kwa mikono badala ya kutembea kwa miguu huku akiruka ruka na kuimba nyimbo zake .

      Yule mzee akufika pale ngombe alipo akatowa ndoo yake nyuma ya mgongo wakati anakuja hakuwa na ndoo wala hakubeba chochote hiyo ndoo ilikuwa hewani tu , akaitowa pale akaweka akaanza kuchukuwa maziwa toka kwa ngombe haraka haraka akavamia ngombe wa pili , basi kabla hajafika mbali sisi tukafika pale nyuma yake na kumkamata .

      Mimi nilimkamata , lakini kaka yangu alikuwa na hasira sana , ndio yeye akaanz akumpiga kichwani mzee wa watu akaanza kuomba msamaha akasema hatorudia tena , basi tulioijisahau tu , fyuuu yule mzee aligeuka moto , kaka yangu alishituka ameshika moto lakini alikuwa ameshajisahau ule moto ulimchoma karibu mwili mzima .

      Kaka yangu alimwachia moto ukaendelea kuwaka tu mimi nikakimbilia ndani lakini ghafla moto ule ukaisha kimaajabu , nikatoka tena nje nikakuta kaka yangu ameungua sana hajiwezi , nikasikia sauti kali inaniambia na mukome mimi sio saizi yenu halafu mvua ya mawe ikaanza kunyesha .

      Nilikimbia sikuweza kumsaidia kaka yangu kwa sababu mawe yalikuwa makubwa yamenidondokea yananiumiza nikamwacha pale kuridi nyumbani kuja kulala , basi kesho yake asubuhi tunaamka , ndio hivyo kaka akawa chizi tuseme kichaa hakuweza tena kuwa na akili timamu .

      Sikuamini hali hiyo mpaka leo hii , nikaendelea tu kuishi kwa nguvu za maulana , siku moja tukaamua kumpeleka kaka yetu kwa kakobe akaombewe aweze kupona ugonjwa wake , basi tulipofika pale ubungo tu gari yetu ilipata ajali mbaya lakini wote tulisalimika .

      Tulishindwa kumpeleka kaka kwa kakobe , siku ingine ikabidi tumpeleke kwa waganga huko mkoani tanga kwa wataalamu tuone kama watamponya au la , kabla ya kufika kwa yule mganga , tulisikia sauti inatuamrisha kugeuza njia tusielekee kule tunapoenda .

      Dereva alipoendeleza mwendo ili tufike basi gari ilikumbana na upepo mkubwa sana ghafla gari ile ilisimama tairi zikapata pancha , dakika 5 baadaye nilipoangalia katika kiti cha dereva nikakuta simba amesimama pale yaani ndio ameshikiria ile usikanio wa gari .

      Tulipiga sana kelele , tukaliacha lile gari pale tukapanda basi kuelekea kule tunapotaka kwenda , basi bwana tulivyopita vituo 2 vya mwanzo kondakta akapotea ghafla , kukawa na dereva tu .

      Nyuma yetu jamaa mmoja akawa anasema ashushwe , kufika kituo cha 3 dereva akaangalia nyuma nani anataka kushuka hakuona mtu yaaani alikuwa ni mtu hewa , tuligopa sana basi dereva alikimbiza gari tu .

      Mwishowe tukafika pale kwa mganga , tukamweleza shida zetu basi tukawa tunalala nyumbani kwake kwa siku kama 4 hivi hizo siku zilikuwa za balaa sana mimi nilikuwa nimempeleka kaka yangu nilikuwa na akili timamu nikajionea mwenyewe mambo yalivyo katika usiku huo wa giza .
      Siku ya kwanza wakati niko pale nimelala kitandani usiku wa manane nilishituka ghafla nikamwona babu yangu mzaa babu amekaa kitandani amevaa nguo nyeupe kabisa ananiangalia huku machozi yakimtoka , sikuelewa kwa nini analia vile mimi sikuweza kufungua mdomo kusema chochote .

      Siku iliyofuatia basi bwana nikachukuwa zangu ndoano nikaenda kuvua samaki mtoni na vijana wengine wa pale , nikaanza kuvua na kuvua , mpaka jioni kikafikia kigiza kidogo hivi wale jamaa waliniacha mwenyewe .

      Kila nikivuta ndoani naona ni nzito sana nikafurahi nimeona samaki mkubwa lakini huyu anatisha zaidi yaani mzito sana sikuamini nikaendelea kuvuta tu ile kamba kuvuta kuvuta mpaka mwisho kuangalia vizuri kumbe nilikuwa namvuta mama yangu mzazi na ndoani toka mtoni .

      Kweli alifika pale nikamburuta kwenda kumwangalia ni kweli yeye hana tofauti , kwenda kumuuliza kunani akawa analalamika tu yoo yoona mwanangu unaniuwa , mwanangu unaniuwa hivi hivi , huyooo akakata roho , ghafla tu akadondoka chini na huo ukawa mwisho wake .

      Asubuhi naamka napigiwa simu toka nyumbani kuambiwa kwamba mama yangu amefariki dunia nyumbani , kwahiyo niende haraka , nikamwacha kaka yangu kwa mganga mimi nikaelekea zangu nyumbani kwenda kufanya mambo mengine ya msiba .

      Msiba ulikuwa mkubwa sana watu wengi wakubwa kwa wadogo , ukafika wakati wa kumzika , kwenda kuliingiza kaburini tukamfukia na kumfunika kabisa wakati watu tunaanza kutoka makaburini ghalfa lile kaburi likafunuka likatoka nyoka kubwa sana mule kaburini .

      Watu walianza kulishambulia kwa mapanga na majembe mpaka wakaliuwa pale pale , bado katika mawazo yangu siamini nini kinachoendelea katika maisha yangu , tulimaliza msiba ule , kesho yake jumapili nikaamka kuelekea kanisani .

      Wakati napanda mitaani kwenda kanisani nikamwona mama yangu anatembea na mimii pembeni yangu lakini hasemi kitu , nikijaribu kumkimbia yeye ananishika , lakini nikimwangalia sioni kichwa chake ila anaonekana ni yeye kila nikijaribu kugeuka sioni kitu .

      Nikawahi kanisani bwana kwenda katika misa ya asubuhi ili nikitoka pale niwahii kuchukuwa gari nirudi zangu tanga kwa ajili ya kumcheki kaka yangu na mambo yake ya kulogwa .

      Kweli nikafanikiwa kwenda mpaka tanga , kufika kule nikamwona kaka yangu lakini yule mganga hakwepo basi niaanza kucheki katika vyumba vyake vitu anavyotumia mambo kama hayo .

      Nikafika chumba kimoja kuangalia mule ndani nikaona kichwa cha mama yangu , na mikono yake amekatwa katwa kama mbuzi , nikaona pia kichwa cha babu yangu kinavuja damu na kimakatwa na panga moja .

      Nikafunga ule mlango nikatoka nje , basi ndio nikashtuka toka usingizini kumbe nilikuwa naota ndoto za ajabu hivi , lakini imenifunza mambo

      Woooow

    2. Miaka 50

    3. #2
      Kasana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2007
      Posts : 552
      Rep Power : 731
      Likes Received
      2
      Likes Given
      2

      Default

      Ni ndoto nzuri ambayo inamtiririko, tegemea jambo fulani, kawaida ndoto nyngi hazina mtiririko unaoleweka

    4. Shy
      #3
      Shy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2006
      Posts : 4,922
      Rep Power : 0
      Likes Received
      75
      Likes Given
      0

      Default

      Ahsante Sana Kasana

      Nyingine Inakuja

    5. #4
      Apolonary's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Location : SAN DIEGO COMMUNITY
      Posts : 1,456
      Rep Power : 682
      Likes Received
      249
      Likes Given
      30

      Default Re: Usiku Wa Giza

      Duh nimeogopa kweli kemea katika jina lipitalo majina yote YESU KRISTO WA NAZARETHI. AMEN.

    6. #5
      Asulo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 629
      Rep Power : 473
      Likes Received
      224
      Likes Given
      38

      Default Re: Usiku Wa Giza

      Daah asee Shy nenda kaombe kazi kwa Shigongo kwa hicho kisa ni lazima akupe.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Rubi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2009
      Posts : 1,239
      Rep Power : 737
      Likes Received
      154
      Likes Given
      133

      Default Re: Usiku Wa Giza

      ukiota ndoto ya aina hii ukishituka tu sali na kemea katika jina la Yesu mana hayo ni mapepo.
      Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.

    Similar Topics

    1. ... .chakula cha usiku kwenye GIZA..
      By NG'ADA in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 42
      Last Post: 27th September 2011, 20:20
    2. Ngeleja ameamua kutuoenyesha akiamua watu mlale giza, mtalala giza
      By makandokando in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 10th August 2011, 11:19
    3. Viongozi CHADEMA waivuruga CCM Iringa na kuondoka usiku usiku
      By Mzito Kabwela in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 39
      Last Post: 21st May 2011, 00:01
    4. Replies: 5
      Last Post: 25th December 2010, 01:00
    5. Kimya kingi ni usiku wa giza
      By Lekanjobe Kubinika in forum Celebrities Forum
      Replies: 1
      Last Post: 2nd June 2010, 08:48

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...