Wewe usiku wako labda unautumia kwa ajili ya kulala tu usiku unakaa unaota ndoto nzuri wakati mwingine za kutisha na kuchekesha ndoto hizo wakati mwingine ni kama zinakuhabarisha mambo unayokuja kukutana nayo siku za mbeleni kama prophecy wengine husema , ndio wewe unaona na kushangilia usiku wako , wengine usiku huu huutumia kwa kazi zao mfano polisi na walinzi wao hutumia saa za usiku kulinda watu wao na taifa kwa ujumla , wengine kama Malaya huutumia usiku huu kwa kujiuza na kufanya biashara za miili yao , wengine kazi yao ni kucheza muziki kwahiyo saa za usiku kwao ni kucheza muziki kuburudisha wengine na wengine ni majambazi usiku wa giza wao huutumia kurubuni watu , kuuwa watu ili wajipatie chochote kile kwa maisha yao ya kila siku , wengine wa wanga na wachawi hutumia usiku kama wakati wao wa kufanya mambo yao ya kishirikina bila kuonekana na roho za kawaida kwahiyo kila mtu ana mambo yake wakati wa usiku .
Basi bwana nyumbani kwetu tulikuwa na ngombe kama 3 hivi huko moshi vijijini , hawa ngombe wote ni wakike , walivyokuwa wakubwa babu yetu akaamua kuwapeleka kwa dume awapande ili waweze kuzaa watoto na tupate ndama , maziwa na maziwa mengine yawe ni ya kuuza kwa watu wengine katika mtaa huo huko vijijini .
Haya ngombe walipandwa , mmoja akazaa lakini ndama wake akafa huyu mwingine ndama wake hakufa lakini yule ndama alikufa katika mazingira ya kutatanisha daktari wa kujiji alivyokuja kuangalia hakukuta alama yoyote ya sumu au kama amekula chakula chochote kile kibaya basi tukamwachia mola.
Ngombe bwana wakawa wanatoa lita 20 mpaka 30 kwa siku moja babu yetu alifurahi sana , lakini baada ya wiki 2 hivi hali ikaanza kuwa tofauti sana , yaani yule ngombe hatowi maziwa yanakuwa kama vile yamekamuliwa usiku kutwa .
Siku moja tumakaa kibarazani babu yetu akawa anatupa hadithi za hapa na pale jirani yetu akaja alipofika pale akamwambia babu kuhusu yule mzee wa mtaa wa pili anavyokuja kuiba maziwa usiku kwa njia za kishirikina akamweleza kila kitu .
Lakini babu hakuwa na nguvu zozote basi bwana ikabidi yule mzee atupe dawa mimi na kaka yangu mmoja ili yule mzee akija usiku tuweze kumkamata na kumwadhibu usiku unaofuatia akatuelekeza cha kufanya kila kitu .
Usiku ukafika , tukajipaka zile dawa tukakaa sehemu karibu na banda la ngombe tukasikia kengele zinalia kutokea mbali ngrii ngrii ngrii , tukakaa kimya , ndio tukaona mzee mmoja anakuja miguu yake ikiwa juu na mikono chini yaani anatembea kwa mikono badala ya kutembea kwa miguu huku akiruka ruka na kuimba nyimbo zake .
Yule mzee akufika pale ngombe alipo akatowa ndoo yake nyuma ya mgongo wakati anakuja hakuwa na ndoo wala hakubeba chochote hiyo ndoo ilikuwa hewani tu , akaitowa pale akaweka akaanza kuchukuwa maziwa toka kwa ngombe haraka haraka akavamia ngombe wa pili , basi kabla hajafika mbali sisi tukafika pale nyuma yake na kumkamata .
Mimi nilimkamata , lakini kaka yangu alikuwa na hasira sana , ndio yeye akaanz akumpiga kichwani mzee wa watu akaanza kuomba msamaha akasema hatorudia tena , basi tulioijisahau tu , fyuuu yule mzee aligeuka moto , kaka yangu alishituka ameshika moto lakini alikuwa ameshajisahau ule moto ulimchoma karibu mwili mzima .
Kaka yangu alimwachia moto ukaendelea kuwaka tu mimi nikakimbilia ndani lakini ghafla moto ule ukaisha kimaajabu , nikatoka tena nje nikakuta kaka yangu ameungua sana hajiwezi , nikasikia sauti kali inaniambia na mukome mimi sio saizi yenu halafu mvua ya mawe ikaanza kunyesha .
Nilikimbia sikuweza kumsaidia kaka yangu kwa sababu mawe yalikuwa makubwa yamenidondokea yananiumiza nikamwacha pale kuridi nyumbani kuja kulala , basi kesho yake asubuhi tunaamka , ndio hivyo kaka akawa chizi tuseme kichaa hakuweza tena kuwa na akili timamu .
Sikuamini hali hiyo mpaka leo hii , nikaendelea tu kuishi kwa nguvu za maulana , siku moja tukaamua kumpeleka kaka yetu kwa kakobe akaombewe aweze kupona ugonjwa wake , basi tulipofika pale ubungo tu gari yetu ilipata ajali mbaya lakini wote tulisalimika .
Tulishindwa kumpeleka kaka kwa kakobe , siku ingine ikabidi tumpeleke kwa waganga huko mkoani tanga kwa wataalamu tuone kama watamponya au la , kabla ya kufika kwa yule mganga , tulisikia sauti inatuamrisha kugeuza njia tusielekee kule tunapoenda .
Dereva alipoendeleza mwendo ili tufike basi gari ilikumbana na upepo mkubwa sana ghafla gari ile ilisimama tairi zikapata pancha , dakika 5 baadaye nilipoangalia katika kiti cha dereva nikakuta simba amesimama pale yaani ndio ameshikiria ile usikanio wa gari .
Tulipiga sana kelele , tukaliacha lile gari pale tukapanda basi kuelekea kule tunapotaka kwenda , basi bwana tulivyopita vituo 2 vya mwanzo kondakta akapotea ghafla , kukawa na dereva tu .
Nyuma yetu jamaa mmoja akawa anasema ashushwe , kufika kituo cha 3 dereva akaangalia nyuma nani anataka kushuka hakuona mtu yaaani alikuwa ni mtu hewa , tuligopa sana basi dereva alikimbiza gari tu .
Mwishowe tukafika pale kwa mganga , tukamweleza shida zetu basi tukawa tunalala nyumbani kwake kwa siku kama 4 hivi hizo siku zilikuwa za balaa sana mimi nilikuwa nimempeleka kaka yangu nilikuwa na akili timamu nikajionea mwenyewe mambo yalivyo katika usiku huo wa giza .
Siku ya kwanza wakati niko pale nimelala kitandani usiku wa manane nilishituka ghafla nikamwona babu yangu mzaa babu amekaa kitandani amevaa nguo nyeupe kabisa ananiangalia huku machozi yakimtoka , sikuelewa kwa nini analia vile mimi sikuweza kufungua mdomo kusema chochote .
Siku iliyofuatia basi bwana nikachukuwa zangu ndoano nikaenda kuvua samaki mtoni na vijana wengine wa pale , nikaanza kuvua na kuvua , mpaka jioni kikafikia kigiza kidogo hivi wale jamaa waliniacha mwenyewe .
Kila nikivuta ndoani naona ni nzito sana nikafurahi nimeona samaki mkubwa lakini huyu anatisha zaidi yaani mzito sana sikuamini nikaendelea kuvuta tu ile kamba kuvuta kuvuta mpaka mwisho kuangalia vizuri kumbe nilikuwa namvuta mama yangu mzazi na ndoani toka mtoni .
Kweli alifika pale nikamburuta kwenda kumwangalia ni kweli yeye hana tofauti , kwenda kumuuliza kunani akawa analalamika tu yoo yoona mwanangu unaniuwa , mwanangu unaniuwa hivi hivi , huyooo akakata roho , ghafla tu akadondoka chini na huo ukawa mwisho wake .
Asubuhi naamka napigiwa simu toka nyumbani kuambiwa kwamba mama yangu amefariki dunia nyumbani , kwahiyo niende haraka , nikamwacha kaka yangu kwa mganga mimi nikaelekea zangu nyumbani kwenda kufanya mambo mengine ya msiba .
Msiba ulikuwa mkubwa sana watu wengi wakubwa kwa wadogo , ukafika wakati wa kumzika , kwenda kuliingiza kaburini tukamfukia na kumfunika kabisa wakati watu tunaanza kutoka makaburini ghalfa lile kaburi likafunuka likatoka nyoka kubwa sana mule kaburini .
Watu walianza kulishambulia kwa mapanga na majembe mpaka wakaliuwa pale pale , bado katika mawazo yangu siamini nini kinachoendelea katika maisha yangu , tulimaliza msiba ule , kesho yake jumapili nikaamka kuelekea kanisani .
Wakati napanda mitaani kwenda kanisani nikamwona mama yangu anatembea na mimii pembeni yangu lakini hasemi kitu , nikijaribu kumkimbia yeye ananishika , lakini nikimwangalia sioni kichwa chake ila anaonekana ni yeye kila nikijaribu kugeuka sioni kitu .
Nikawahi kanisani bwana kwenda katika misa ya asubuhi ili nikitoka pale niwahii kuchukuwa gari nirudi zangu tanga kwa ajili ya kumcheki kaka yangu na mambo yake ya kulogwa .
Kweli nikafanikiwa kwenda mpaka tanga , kufika kule nikamwona kaka yangu lakini yule mganga hakwepo basi niaanza kucheki katika vyumba vyake vitu anavyotumia mambo kama hayo .
Nikafika chumba kimoja kuangalia mule ndani nikaona kichwa cha mama yangu , na mikono yake amekatwa katwa kama mbuzi , nikaona pia kichwa cha babu yangu kinavuja damu na kimakatwa na panga moja .
Nikafunga ule mlango nikatoka nje , basi ndio nikashtuka toka usingizini kumbe nilikuwa naota ndoto za ajabu hivi , lakini imenifunza mambo
Woooow

Reply With Quote


Follow Us Here