WanaJF,
Jana kuna MwanaJF alianzisha thread akilalamika kuwa mbunge wake wa Arumeru Mashariki ni mgonjwa sana na hivyo hawana mwakilishi jimboni kwao. Alitaka kujua serikali inaonaje kama Wana-Arumeru wakifanya uchaguzi mwingine ili wapate muwakilishi mwingine. Kwenye ile thread wapo waliosema kuwa “wakati mwingine tuweke utu mbele, thamani ya mtu ni utu, ubinaadamu ndio unatangulia na mengine yote yanafuatia..” Wengine wakasema kuwa “suala sio kubeza ugonjwa wa mbunge bali ni uwakilishi wa wanajimbo la Arumeru Mashariki full stop.”
Pia jana hiyo hiyo, Faiza Foxy alipewa ban ya miaka miwili kwa kwa kutenda “kosa dhidi ya UTU” ikiwa na maana ya “Kukejeli na kubeza marehemu na sababu zilizopelekea kifo chake ni kosa tena kukosa Heshima.”
Swali langu ni nini hasa maana ya utu? Ni utu kuendelea kumwacha madarakani kiongozi ambaye ni mgongwa sana to the extent kuwa hawezi hata kuwawakilisha tena waliomchagua? Je, mtu unaweza kula ban hapa JF kwa kutokuwa na utu? Ni vigezo gani tunavyotumia kujua kama mtu hana utu au amefanya jambo ambalo halina utu?
Nim-quote Gaijin: “Utu ndio kitu gani? Utu unau define vipi? Kwa standards za nani? Tunaweza kusemaje nani ana utu zaidi kuliko mwingine kwa kufanya vitendo gani?”

Reply With Quote




Follow Us Here