Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kuandikwa au kufutwa kazi na sintofahamu hiyo

    Report Post
    Results 1 to 5 of 5
    1. #1
      L'AMOUR's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th March 2011
      Posts : 109
      Rep Power : 437
      Likes Received
      20
      Likes Given
      9

      Default Kuandikwa au kufutwa kazi na sintofahamu hiyo

      Imenishangaza kutumika kwa Tanzania maneno kama kuandikwa na kufutwa kazi pia hali ya sintofahamu. Sasa najiuliza yale maneno yetu ya kuajiriwa au kupata kazi na kufukuzwa kazi ni yepi hasa ndio tuyatumie? Haya maneno nimezoea kuwasikia wakenya kupitia TV zao na sasa yameingia Tanzania na tunakutana nayo magazetini. Je magazeti au vyombo vya habari vinaruhusiwa kutumia lugha yoyote hata kama inaweza kupotosha umma?
      Natangulisha shukurani za dhati kwa kunijengea kiswahili kizuri

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Crucifix's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 1,569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      430
      Likes Given
      321

      Default Re: Kuandikwa au kufutwa kazi na sintofahamu hiyo

      nimemsikia mkuu wa nchi akitumia neno 'sintofahamu', nalo hili sijui limetokea wapi na nini hasa maana yake.

    4. #3
      Senior Bachelor's Avatar
      Member Array
      Join Date : 22nd March 2011
      Location : Tanzania
      Posts : 86
      Rep Power : 431
      Likes Received
      29
      Likes Given
      10

      Default Re: Kuandikwa au kufutwa kazi na sintofahamu hiyo

      Quote By L'AMOUR
      Imenishangaza kutumika kwa Tanzania maneno kama kuandikwa na kufutwa kazi pia hali ya sintofahamu. Sasa najiuliza yale maneno yetu ya kuajiriwa au kupata kazi na kufukuzwa kazi ni yepi hasa ndio tuyatumie? Haya maneno nimezoea kuwasikia wakenya kupitia TV zao na sasa yameingia Tanzania na tunakutana nayo magazetini. Je magazeti au vyombo vya habari vinaruhusiwa kutumia lugha yoyote hata kama inaweza kupotosha umma?
      Natangulisha shukurani za dhati kwa kunijengea kiswahili kizuri
      Si wewe tu unayeshangaa. Unajua tatizo ni kupenda kuiga bila kufikiri sawa sawa. "Kuandikwa na kufutwa" sio maneno sahihi kwa maoni yangu. Inashangaza sana kuona kuwa watu wanaotakiwa wajifunze kiswahili kwetu (Wakenya) ndio tunaowaiga.
      Hilo la sintofahamu kwanza limeanzia redio za kimataifa (sana sana Sauti ya Ujerumani, na BBC). Halina maana pia. Wanaolitumia nadhani wanataka kumaanisha dhana inayobebwa na neno "CONTROVERSY" katika lugha ya kiingereza. Waseme tu "Utata".
      Mimi huwa nakasirika sana japo kitaluma sio mweledi wa lugha. Ni sawa na wanaotumia neno"nimeboreka" wakimaanisha "am bored". Sasa jamani kuboreka ni mnyambuliko wa mzizi wa neno "bora" ambao unamanisha kuwa bora zaidi. Kwa nini hao wasiseme "nimeudhika"? au "sijafurahia"?
      "You cannot clap with one hand"- Mahatma Gandhi

    5. #4
      mdau wetu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Location : Vatican
      Posts : 540
      Rep Power : 517
      Likes Received
      46
      Likes Given
      36

      Default Re: Kuandikwa au kufutwa kazi na sintofahamu hiyo

      ni suutafahamu na sio sintofahamu

    6. #5
      L'AMOUR's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th March 2011
      Posts : 109
      Rep Power : 437
      Likes Received
      20
      Likes Given
      9

      Default Re: Kuandikwa au kufutwa kazi na sintofahamu hiyo

      Kwa hiyo ni suutafahamu??? Nashukuru kama ni kiswahili sahihi na vipi hawa waandishi wa habari huwa wanasisitizwa kusomea lugha kama ilivyokuwa zamani kwenye kozi zao za HGL, HKL au KLF ili waweze kutufundisha sisi wasomaji,wasikilizaji au watazamaji wa TV? Kama ni hivyo basi kiswahili kinakuwa na kama si hivyo basi ni kwa nini wanaachia watu wachache wachafue fani yao bila sababu. Pia mkuu kama neno sahihi ni suutafahamu je si sahihi kulitumia kama kuna utata kama mdau alivyoeleza hapo juu?? Tafadhali tujulishe jinsi ya kutumia maana hii lugha inachezewa mpaka wageni wanatudharau kwa kuiga kiswahili chao kibovu kisicho na ladha ya matamshi. Naomba niwasilishe tena hoja hii kwa waliobobea. Ahsante

    7. Miaka 50

    Similar Topics

    1. Replies: 0
      Last Post: 20th July 2011, 15:59
    2. Polisi kufutwa kazi Misri
      By sulphadoxine in forum International Forum
      Replies: 4
      Last Post: 11th July 2011, 14:51
    3. kwa wanaopenda kufanya kazi un ingieni link hiyo hapo
      By kilimasera in forum Nafasi za Kazi na Tenda
      Replies: 28
      Last Post: 19th February 2011, 18:29
    4. 80 kufutwa kazi ATCL
      By Gudboy in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 29th October 2009, 08:32
    5. Mawaziri kufutwa kazi,asema Waziri Mkuu!
      By Ab-Titchaz in forum International Forum
      Replies: 16
      Last Post: 2nd April 2009, 11:10

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...