Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hii inasikitisha sana

    Report Post
    Results 1 to 8 of 8
    1. #1
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,751
      Rep Power : 3269
      Likes Received
      993
      Likes Given
      787

      Default Hii inasikitisha sana

      SHULE ya msingi Mazizi iliyoko kata ya Gwata, tarafa ya Mikese, wilaya ya Morogoro imefaulisha mwanafunzi mmoja katika kipindi cha miaka saba iliyopita ilipoanzishwa shule hiyo.


      Akizungumza katika mkutano na wanachama wa Umoja wa Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali mkoani Morogoro (UNGO) waliotembelea shule hiyo, mkuu wa shule hiyo Chalo Chalo alisema kuwa mwanafunzi aliyefaulu darasa la saba kwenda kidato cha kwanza alihitimu mwaka 2008.
      Alisema kuwa kitendo cha shule hiyo kushindwa kufaulisha wanafunzi kimetokana na changamoto nyingi zinazoikabili ikiwa ni pamoja na uhaba wa walimu, vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, huduma za kijamii na nyinginezo.


      Alisema kuwa kwa miaka mitano toka ilipoanzishwa shule hiyo kulikuwa na mwalimu mmoja ambaye alikuwa akilazimika kufundisha wanafunzi wote hali ambayo alidai kuwa isingewezesha watoto kuendelea kielimu.


      Chalo aliongeza kuwa kwa sasa shule hiyo inajumla ya walimu wanne huku wawili kati yao wakidaiwa kuondoka kwa ruhusa maalum katika kipindi kisicho julikana.
      “Mazingira ya kazi huku yanakatisha tamaa kwa walimu kuja kufundisha, kwa vile hakuna huduma muhimu ya kijamii huduma tunalazimika kuzifuata mbali, hakuna nyumba za walimu ndiyo maana walimu wanakuja na kuondoka,” alisema mwalimu mkuu huyo.


      Mwalimu huyo ameiomba serikali kuboresha mazingira ya kazi katika shule hiyo na kuongeza idadi ya walimu, kujenga nyumba za walimu, kuongeza vyumba vya madarasa, kuboresha miundombinu ili kuimalisha elimu katika shule hiyo.


      Nao wanachama wa UNGO waliotembelea shule hiyo na kukutana na kamati na walimu wa shule hiyo kama sehemu ya mafunzo yao kwa vitendo baada ya kujifundisha darasani juu ya utawala bora walisema bado yako mambo yanayohitajika kufanyika.


      Charles Mengere mkurugenzi wa taasisi ya Greenbelt Secondary school alisema kuwa kukosekana kwa ushirikishwaji miongoni mwa jamii ni kikwazo cha utawala bora.


      Alisema kuwa katika shule hiyo kamati ya shule na walimu wamekuwa hawashirikishwa sawia na halmshauri ya wilaya katika mipango mbalimbali ya maendeleo.
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.


    2. #2
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,203
      Rep Power : 12279
      Likes Received
      6062
      Likes Given
      6927

      Default Re: Hii inasikitisha sana

      tupeni ridhaa yenu, na tutafanya zaidi...

      tutafanya zaidi mkitupa ridhaa zaidi...
      tupeni ridhaa yenu na tutfanya zaidi
      tutafalakjso[a[ajaaaaa...a zaiidiama/....a

      tfvdklal [KISHINDO]

      KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
      ....Time is the wisest counselor !!!

    3. #3
      TUKUTUKU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Location : KIPALAPALA TU
      Posts : 8,679
      Rep Power : 2180
      Likes Received
      1927
      Likes Given
      748

      Default Re: Hii inasikitisha sana

      Hayo ndiyo matunda ya kazi za mikono ya CCM!!!!

    4. #4
      Taifa_Kwanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2010
      Posts : 443
      Rep Power : 534
      Likes Received
      75
      Likes Given
      36

      Default Re: Hii inasikitisha sana

      Inapendeza sana.

      Lakini tutafika, Imani yangu ni kwamba, Mungu hajatuacha watanzania kabisa kabisa.
      Ipo siku atatukumbuka, ipo siku Mungu ataingilia kati na kushiriki katika kuweka viongozi sahihi katika nchi yetu, Mungu atatupa nafasi Watanzania kufarijika japo kidogo. Atasitisha washirikina kutuchagulia viongozi

      Haya yote yanayofanywa na CCM, Mungu anayaona,Elimu ni ufunguo wa Maisha, Binaadamu asiyekuwa na ufahamu ni kama mnyama kabisa, CCM Hawajali hili, wanafurahia hali hii.kwao, hii inawapa fursa ya kututawala zaidi zaidi

      Watanzania tunapaswa kupiga kulele na kulia sana, tunapaswa kugalagala chini na kujipaka majivu, tumulilie Mungu, tumueleze Mungu Mbona ametuacha, Mbona sisi tu.

      Labda ni Sasa

    5. #5
      pmwasyoke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,514
      Rep Power : 986
      Likes Received
      338
      Likes Given
      438

      Default Re: Hii inasikitisha sana

      Usishangae wanakijiji hicho wengi kuipigia kura CCM - sijui watu wamelogwa huko vijijini?


    6. #6
      DR. Mlay's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 19
      Rep Power : 440
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Hii inasikitisha sana

      Si lolote si chochote hizi ni mbinu tu za kutaka watoto wao waendelee kututawala. nikiwa na maana kwamba watoto wao tu ndio watakao pata elimu bora na si vinginevyo. Ili kulithibitisha hili angali kama kwenye shule hiyo kuna mtoto hata mmja wa kigogo. Mmmmh!!!!!!!!! inauma sana lakini tusemenini ili hali wao ndio walioshikilia nchi. Yangu mi sala tu!!!!!!!!!!!!!!!!

    7. #7
      Wa Ndima's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th August 2010
      Posts : 1,388
      Rep Power : 735
      Likes Received
      223
      Likes Given
      645

      Default Re: Hii inasikitisha sana

      Kidumu Chama Cha Mapinduzi, Zidumu Fikra za Mwenyekiti.

      Mapinduzi Daima, Tutawapindua Tuendelee Kuwatawala.

      CCM OYEEE!!!


    8. #8
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,741
      Rep Power : 10184
      Likes Received
      5679
      Likes Given
      12666

      Default Re: Hii inasikitisha sana

      Quote By Wa Ndima View Post
      Kidumu Chama Cha Mapinduzi, Zidumu Fikra za Mwenyekiti.

      Mapinduzi Daima, Tutawapindua Tuendelee Kuwatawala.

      CCM OYEEE!!!
      oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee ccm na wao dam dam
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    Similar Topics

    1. inasikitisha sana baada ya mauaji
      By kilimasera in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 26th March 2011, 11:31
    2. Inasikitisha sana! Lakini ndio imetokea
      By MziziMkavu in forum Jamii Photos
      Replies: 13
      Last Post: 3rd October 2010, 14:43
    3. Picha hii inasikitisha sana
      By El Toro in forum Jamii Photos
      Replies: 9
      Last Post: 21st July 2010, 18:11
    4. CCM: Hero to Zero - inasikitisha sana
      By Bongolander in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 2nd April 2008, 13:26

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...