KUNDI la wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kujiunga na vyuo mbalimbali vya serikali na kupata alama za juu leo wamefurika nje ya Jengo la Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) lililopo Mikocheni jijini Dar es Salaam wakipinga uamuzi wa wenzao waliopata alama ndogo kupatiwa nafasi za kujiunga na vyuo vya serikali na wao kukosa nafasi na kudai uamuzi huo ni wa kuwaonea.
Askari wa jengo hilo akiinyoosha mkono kuwataka wanafunzi hao kukaa mbali na eneo hilo, amri waliyokataa kuitii.
Muuza “lamba-lamba” (ice cream) akiwa kwenye mkusanyiko huo kukata kiu ya ‘madenti’ hao.
PICHA: RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY
Last edited by SuperNgekewa; 29th September 2010 at 16:40.
Reason: Spelling
Ndio muelewe jinsi jamaa wanavyochakachua hata usaili.Huu ndio mfumo tuliouchagua sisi wenyewe msilalamike.Wakati jamaa walipokupa 5,000/= na tshirt ulifikiri nini.Hao ni wazee wetu waliposhindwa kujua na njaa yao wakauza haki yao.Wanafunzi msiondoke mpaka kieleweke
Follow Us Here