Jukwaa la Elimu (Education Forum)Educational discussions in here... If you have some College/School materials and you wanna give them to your fellows pls do that favour to them. Let them get educated here! Become a Member to enjoy more stuffs
Nimesikitishwa sana na matokeo ya kidato cha nne. Katika matokeo hayo zaidi ya 82% ya wanafunzi waliofanya mtihani, wamepata division zero au four!!!!!! Tunaenda wapi??? Ni lazima tujiulize credibility ya hawa wanaojiita mawaziri wanafanya nini ofisini??
Nilipata kusoma shule moja ya pale Kilimanjaro(Shule ya ufundi). Nilikuwa nasoma ufundi wa umeme (O'level). Kwa kweli nilikuwa nashangazwa sana na utaratibu wa shule hiyo, katika swala zima la ufundi na baadhi ya masomo mengine. Zamani mtu alikuwa akimaliza shule ya sekondari ya ufundi alikuwa anaweza kujiajiri mwenyewe.. Lakini katika kipindi hicho ufundi huo niliosoma mimi swala la masomo kwa vitendo lilikuwa halitiliwi maanani.. Walim walikuwa wakijisifu kwa matokeo mazuri(Theoretically) ambapo wanafunzi hawa katika real life hawana chochote. Wengi waliosoma shule hizo wanaweza kuwa mashahidi kuwa kwa sasa asilimia kubwa ya wanafunzi wanaomaliza shule za ufundi ni empty kabisa, hawana chochote.
Baada ya hapo nilipata kusoma shule moja, wanayoiita ya vipaji. Kiukweli sielewi maana ya huu msemo. Ila huenda wanamanisha shule ni ya vipaji kwa maana zinachukua wanafunzi waliofaulu sana. Walimu wengi katika shule hizo hawana uwezo, mpango-mkakati wa kumjenga mwanafunzi kuwa CREATIVE. Hawana utaalamu wa kisaikolojia wa kumjenga mwanafunzi ili nae aweze ku-reason mambo.. HAKUNA!!
Wanafunzi wengi wanaofanya vizuri, wanaotoka shule za serikali, wengi wao hujihangaikia wenyewe na kwa kusoma vitabu vya kutosha na twisheni ili waweze kuelewa mambo mbalimbali.. Kuna wakati mpaka wanafunzi wanaelewa mambo mpaka wanamzidi hadi mwalimu anaewafundisha ( Maana walimu wengi hawana vipaji vya kufundisha).
Tanzania ni moja ya nchi isiyojali wasomi kwa kuwaacha wakijihangaikia wenyewe bila angalau ya kuwapa sapoti ya aina yoyote. Kwa mtoto wa maskini, hawezi hata kununua vitabu vizuri wala ya kulipa twisheni, ili aweze kujisomea ili afikie malengo yake.. Na wala haina taim nao, kwa maana, serikali inaona kuwa usomi ni swala lisilo na tija kwa taifa hili, bali siasa za kifisadi ndizo zenye tija..
Naomba mwongozo:Kuna haja gani ya kuwa na majengo kibao ya shule, baadhi yaliyojengwa kwa kunyang'anya kuku na mbuzi wa wananchi, wakati walimu wa kutosha hakuna?? Ni bora kuwe na mwalimu makini anaewafundisha wanafunzi chini ya mti, kuliko kuwa na majengo ambayo wanafunzi wake wanafundishwa na ubao mweusi.
Ndg. Majembe asimame sasa, atueleze kwamba mwaka huu katuzawadia zero 65,700. Anatupeleka wapi?? Mipango iko wapi?? Je, ndo kusema wanaongeza wajinga ili watutawale milele?? KWA NINI SERIKALI YA TANZANIA HAMJALI ELIMU??? Ingekuwa ni nchi zenye adabu, waziri huyu angejiuzulu mara moja, au Rais angempa adabu yake! Ila kwa sababu bongo ni TAMBARARE, anapeta tu na kodi za wananchi na wala hana shida.. Inasikitisha!!
Wenzetu wa amerika na ulaya wanawaza jinsi ya kugundua vitu vizito na vyenye technolojia ya hali ya juu, SISI TUNAKAA KUJADILI JINSI YA KUPUNGUZA ZERO, Mmmh!! Huu ni upuuzi.. Haya mambo ya ajabu kabisa.
Lazima watanzania tukae chini tujifikirie kuwa, Mfumo wetu huu wa elimu utatufikisha?? Wasomi wa Tanzania wanatapatapa tu huko duniani wanatafuta elimu, ingawa cha kusikitisha serikali yao haiwajali! Kama hatutakaa chini na kujipanga upya juu ya swala la elimu, basi hakuna sababu ya akina MKURABITA wala MKUKUTA, Maana yatupasa kuandika maumivu kuwa, sisi ni MASKINI MILELE..
Inakatisha tamaa kwa kweli. Serikali ilitilia nguvu ujenzi wa shule za kata na kusahau walimu wenye taaluma watatoka wapi, sasa mijengo ipo pasipo walimu wenye taaluma. Ni bora kabisa kuwepo na walimu wenye taaluma na kufundishia chini mbuyu kuliko walimu wa UPE kufundishia mijengoni.... tunaenda wapiiiiiiiii TZzzzzzzz !!!!
Tatizo ni wale wenye kutoa maamuzi ya msingi kuhusu mwelekeo wa elimu,ni wazi katika karne hii ya sci& tech lazima kuwe na watu wenye mitizamo na muelekeo huo,jinsi ya kufundisha,vifaa vya kufundisha,ni nini unafundisha,watu unaowafundisha,walimu wenyewe,mazingira yao,kipato chao,vyuo etc.Kwa sasa ni kama hamna direction kiukweli.kibinafsi sijawahi sikia katika historia shule kama ilboru inakuwa na zero na div nyingi kama this time
.....ukipitia ile website ya NECTA then ukajaribu kuangalia randomly matokeo....unaweza ukalia kama kweli ni mzalindo wa TZ.......! mi nadhani ni more than 82% wamepata div zero na four! hata wachache waliopata div 3 combinations za waliowengi zinagoma?
What are we doing to end this? kwa nini hawa mawaziri bado tunawachekea tuuuuuu.....? can't we do something for our young brothers' future?
__________________ “Without leaps of imagination, or dreaming, we lose the excitement of possibilities. Dreaming, after all, is a form of planning - GLORIA STEINEM.
Sasa ndo tumeelewa kwa nini ex-dc mnali na Makweta walikuwa sahihi!
Wakati fulani waziri makweta alishauri watoto wanaopata div zero wafikishwe mahakamani kwa uzembe na kuisababishia hasara serikali, nadhani niwakati mwafaka kulifanyia kazi hili wazo.
Kwaupande wa walimu nashauri uanzishwe mpango wa "performance contract" mwalimu atakaefelisha afutwe kazi na ikiwezekana apandishwe kizimbani kwa kuisababishia serikali hasara kwani kalipwa mshahara ili afundishe kazi ambayo hakuitimiza. Walimu wengi vijijini wanachukua mikopo NMB na kununua pikipiki then wanaanza kazi ya kubeba abiria na kusahau majukumu yao.
Madc wapewe jukumu la kufatilia mahudhuio ya walimu na wapewe mamlaka ya kuwafuta kazi watumishi wa umma walevi wazururaji na watoro.
Uwekwe mpango wa kutenganisha majukumu ya utawala na taaluma kwani walimu wakuu sasa wamekuwa "supplies officers" kutwa nzima wako na Quotation kwenye mikoba watasimamia taaluma saa ngapi?
The Following User Says Thank You to eddy For This Useful Post:
Hii batch ndio wale wa darasa la saba 2005. Mwaka huo asilimia 62 (kama 400,000) kati ya watihaniwa 700,000 walifaulu. Kwahiyo mwaka huo kuna kama vijana 300,000 walioachwa nyuma (walifeli). Sasa basi, wale 400,000 waliofaulu na kuendelea na O level, ndio matokeo yao tumeyaona majuzi na kati yao wengine ndio wameachwa nyuma. Walioachwa ni 200,000 ambao wamepata daraja la 4 na 0. Ukijumlisha hawa wa kidato cha nne mwaka 2009, na wenzao kiumri ambao walifeli darasa la saba 2005, jumla tuna kama vijana laki 700,000 nchini kwa sasa ambao system ya elimu ya Tanzania imewashinda.
Hypothetically, tunaweza kusema kuna vijana kama Laki Saba wenye umri kati ya 16-19 ambao academically ni failures. This is easily 2% of Tanzania's population.
Sasa, kila mwaka tukiwa tunafelisha wanafunzi, baada ya miaka kumi nchi yetu itakuwa inazidi kuwa ni nchi ya wasio na elimu ya kutosha. Imagine tukiendelea na rate hii hii ya vijana kufeli mitihani, huko mbele tutapata kweli nguvu kazi ya kutusaidia kusonga?
The Following 2 Users Say Thank You to mtatifikolo For This Useful Post:
Sasa ndo tumeelewa kwa nini ex-dc mnali na Makweta walikuwa sahihi!
Wakati fulani waziri makweta alishauri watoto wanaopata div zero wafikishwe mahakamani kwa uzembe na kuisababishia hasara serikali, nadhani niwakati mwafaka kulifanyia kazi hili wazo.
Kwaupande wa walimu nashauri uanzishwe mpango wa "performance contract" mwalimu atakaefelisha afutwe kazi na ikiwezekana apandishwe kizimbani kwa kuisababishia serikali hasara kwani kalipwa mshahara ili afundishe kazi ambayo hakuitimiza. Walimu wengi vijijini wanachukua mikopo NMB na kununua pikipiki then wanaanza kazi ya kubeba abiria na kusahau majukumu yao.
Madc wapewe jukumu la kufatilia mahudhuio ya walimu na wapewe mamlaka ya kuwafuta kazi watumishi wa umma walevi wazururaji na watoro.
Uwekwe mpango wa kutenganisha majukumu ya utawala na taaluma kwani walimu wakuu sasa wamekuwa "supplies officers" kutwa nzima wako na Quotation kwenye mikoba watasimamia taaluma saa ngapi?
Hiyo pointi ya wanaofeli kupelekwa mahakamani imenichekesha.
Mi sielewi tatizo ni nini. Mbona fom foo mtihani ni mrahisi? Yaani mtu unashindwa kupata zaidi ya 35% kati ya masomo 7?