Jukwaa la Elimu (Education Forum)Educational discussions in here... If you have some College/School materials and you wanna give them to your fellows pls do that favour to them. Let them get educated here! Become a Member to enjoy more stuffs
Nimesikitishwa sana na matokeo ya kidato cha nne. Katika matokeo hayo zaidi ya 82% ya wanafunzi waliofanya mtihani, wamepata division zero au four!!!!!! Tunaenda wapi??? Ni lazima tujiulize credibility ya hawa wanaojiita mawaziri wanafanya nini ofisini??
Nilipata kusoma shule moja ya pale Kilimanjaro(Shule ya ufundi). Nilikuwa nasoma ufundi wa umeme (O'level). Kwa kweli nilikuwa nashangazwa sana na utaratibu wa shule hiyo, katika swala zima la ufundi na baadhi ya masomo mengine. Zamani mtu alikuwa akimaliza shule ya sekondari ya ufundi alikuwa anaweza kujiajiri mwenyewe.. Lakini katika kipindi hicho ufundi huo niliosoma mimi swala la masomo kwa vitendo lilikuwa halitiliwi maanani.. Walim walikuwa wakijisifu kwa matokeo mazuri(Theoretically) ambapo wanafunzi hawa katika real life hawana chochote. Wengi waliosoma shule hizo wanaweza kuwa mashahidi kuwa kwa sasa asilimia kubwa ya wanafunzi wanaomaliza shule za ufundi ni empty kabisa, hawana chochote.
Baada ya hapo nilipata kusoma shule moja, wanayoiita ya vipaji. Kiukweli sielewi maana ya huu msemo. Ila huenda wanamanisha shule ni ya vipaji kwa maana zinachukua wanafunzi waliofaulu sana. Walimu wengi katika shule hizo hawana uwezo, mpango-mkakati wa kumjenga mwanafunzi kuwa CREATIVE. Hawana utaalamu wa kisaikolojia wa kumjenga mwanafunzi ili nae aweze ku-reason mambo.. HAKUNA!!
Wanafunzi wengi wanaofanya vizuri, wanaotoka shule za serikali, wengi wao hujihangaikia wenyewe na kwa kusoma vitabu vya kutosha na twisheni ili waweze kuelewa mambo mbalimbali.. Kuna wakati mpaka wanafunzi wanaelewa mambo mpaka wanamzidi hadi mwalimu anaewafundisha ( Maana walimu wengi hawana vipaji vya kufundisha).
Tanzania ni moja ya nchi isiyojali wasomi kwa kuwaacha wakijihangaikia wenyewe bila angalau ya kuwapa sapoti ya aina yoyote. Kwa mtoto wa maskini, hawezi hata kununua vitabu vizuri wala ya kulipa twisheni, ili aweze kujisomea ili afikie malengo yake.. Na wala haina taim nao, kwa maana, serikali inaona kuwa usomi ni swala lisilo na tija kwa taifa hili, bali siasa za kifisadi ndizo zenye tija..
Naomba mwongozo:Kuna haja gani ya kuwa na majengo kibao ya shule, baadhi yaliyojengwa kwa kunyang'anya kuku na mbuzi wa wananchi, wakati walimu wa kutosha hakuna?? Ni bora kuwe na mwalimu makini anaewafundisha wanafunzi chini ya mti, kuliko kuwa na majengo ambayo wanafunzi wake wanafundishwa na ubao mweusi.
Ndg. Majembe asimame sasa, atueleze kwamba mwaka huu katuzawadia zero 65,700. Anatupeleka wapi?? Mipango iko wapi?? Je, ndo kusema wanaongeza wajinga ili watutawale milele?? KWA NINI SERIKALI YA TANZANIA HAMJALI ELIMU??? Ingekuwa ni nchi zenye adabu, waziri huyu angejiuzulu mara moja, au Rais angempa adabu yake! Ila kwa sababu bongo ni TAMBARARE, anapeta tu na kodi za wananchi na wala hana shida.. Inasikitisha!!
Wenzetu wa amerika na ulaya wanawaza jinsi ya kugundua vitu vizito na vyenye technolojia ya hali ya juu, SISI TUNAKAA KUJADILI JINSI YA KUPUNGUZA ZERO, Mmmh!! Huu ni upuuzi.. Haya mambo ya ajabu kabisa.
Lazima watanzania tukae chini tujifikirie kuwa, Mfumo wetu huu wa elimu utatufikisha?? Wasomi wa Tanzania wanatapatapa tu huko duniani wanatafuta elimu, ingawa cha kusikitisha serikali yao haiwajali! Kama hatutakaa chini na kujipanga upya juu ya swala la elimu, basi hakuna sababu ya akina MKURABITA wala MKUKUTA, Maana yatupasa kuandika maumivu kuwa, sisi ni MASKINI MILELE..
nguvumali
uzuri kipimo cha ubaya, hakuna haki isio ambatana
na wajibu
JF Senior Expert Member
Join Date: Thu Sep 2009
Location: Mwanza
Posts: 1,240
Thanks: 540
Thanked 687 Times in 376 Posts
Rep Power: 23
Re: Zero 65,000.. Maghembe unatupeleka wapi?
kwakweli akili ni nywele na kila mmoja anazake ila akili za Maghembe hazilingani na nafasi ya waziri mwenye dhamana na elimu yetu, hastuki wala kuogopa , yeye kwake ni faraja kwasababu mshahara na posho zake ziko constant, ameshindwa kuifanya elimu ya vijana wetu ing'are kwenye mwanga uliobora, watu tulisema sana wakati wanaanza kutumia waalimu wa Voda faster kua ni bomu lingine linategwa kwenye mfumo wa elimu ya TZ...wakazibz masikio, wakatenda walioona yanafaa sasa leo tunawataka wawajibike na matendo yao.
__________________ The most potent weapon of the oppressor is the mind of the oppressed
Shule za kata zilianzihwa na Kikwete and Co hapo 2006 kwa hivo
2006(FI)... no indicators than pomp and plumb
2007(FII)...no indicators again,more political bashfulness
2008(FIII)...teachers misbehaves,Col Mnali whips them and got fired
2009(IV)...teacher got back to the old game...resulting with 65,000 failures!
Napendekeza hizo pesa zitakazorudishwa na Waingereza kutokana na kashfa ya rushwa ya radar, yaani "vijisenti" kutoka BAE Systems, zielekezwe kwenye elimu. (Ila tuna uhakika kama zitafikishwa huko?). Bila kujali hilo, kwanza walipwe waalimu madeni ya haki zao zote bila ya visingizio vya "kuhakiki" kila mwaka. Pili wachukuliwe vijana wanafunzi waliofaulu vizuri masomo yao ya kidato cha sita wajiunge na vyuo vya ualimu kwa ajili ya kusomea stashahada za ualimu. Ualimu ngazi ya cheti ufutwe kama walivyofanya jirani zetu wa Zambia. Walimu wote kuanzia shule ya msingi wawe angalau na stashahada. Sifa ya mtu kujiunga na chuo cha ualimu iwe ni kuwa na angalao ufaulu wa division 3. Walimu wa vodafasta (miezi miwili) waondolewe mashuleni taratibu mpaka waishe kama hawatajiendeleza na kupata sifa zinazohitajika ndani ya miaka miwili. Na vile vile mimi nafikiri ni wakati muafaka wa kukubali kuanza kufundisha masomo katika sekondari kwa Kiswahili. Tunaweza kuwa na njia mbili zinazokubalika wale wanaopenda kufundisha kwa Kiingereza, hasa shule binafsi, waruhusiwe kuendelea. Lakini kwa hizi shule za kata Kiingereza ni mzigo. Waalimu wenyewe hawakijui na wanafunzi wenyewe hawana msingi mzuri na hiyo lugha kutoka huko kwenye shule za msingi. Sasa hii lugha mtu atajielezaje kweli ashinde mtihani wakati hata sentensi moja ya kuombea maji hawezi? Nimewaona vijana wajanja sana (waendesha taxi) wakikimbia wateja wazungu au wageni kwa sababu hawawezi kuongea nao. Hivi nini kinatufanya tufikiri kwamba kwa mwendo huu ipo siku tutakuja ku-master Kiingreza? Tutaanzia wapi? Halafu hili pendekezo (au tusemwe mwongozp wa JK) wa kitabu kimoja kwa kila somo kama utatekekezwa nao utakuwa janga jipya kwa elimu ya Tanzania. Tunaiiga nchi gani inayotumia mfumo huo? Tuache experiment zisizo na maana.
__________________
Loosing is a starting point to success
Ukiangalia kwa makini utagundua kuwa zile shule nyingi maarufu ka jina la shule za kata zalizoanzishwa kwa kasi miaka ileeeeee minne iliyopita wakati mheshimiwa na yule mwenzie mwenye mvi nyingi walipokuwa wanaingia madarakani ndiyo zimetoa form four wa kwanza sasa, kama kiongozi anafikiria kwa makini ni lazima atagundua haya ni matokeo ya upotofu wa sera ile, haina maana kujisifu kwa kuwa narundo la madarasa na malaki ya wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza wakati hakuna walimu wa kuwafundisha.,hakuna vitabu wala maabara nk, serikali ni lazima ijichunguze na kama hawaoni tatizo wajiunge hapa JF sie tutawaelewesha tatizo ni nini kuliko kupiga kelele majukwaani tu na kujisifu eti idadi ya wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza imeongezeka..,upuuzi mtupu, waziri husika alipaswa kuona aibu hii na kuamua kuwajibika lakini utamu wa madaraka ndio unaomziba masikio.
__________________ Every generation revolts against its fathers and makes friends with its grandfathers
KILIMO KWANZA!
WE ARE NOT INTERESTED IN EDUCATION ANY MORE!!
hahahaha, hahahah
kaaaaazi kweli kweli!
LAKINI HAO WALIOPATA ZERO (65,000) SI WANA ULE UWEZO WA KUANDIKA KWENYE ILE KARATASI YA KUPIGIA KURA NA KUPIGA KURA? fyi: SERIKALI INATENGENEZA WASOMI WAPIGA KURA TU!!! hiyo ndio ilani ya ccm; zaidi ya hayo yanatoka kwa yule mwovu!!!
my take: "TZ U BETTER WAKE UP AND CHANGE THINGS..OTHERWISE ITS GONNA BE DIVERSTATING"
__________________ MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA=POLITICAL SLOGAN=NOON DREAM!!
WE TALK TOO MUCH....!
SI NDO TUNATAKA WANAFUNZI WAWE WANAENDA NA SIMU SHULENI? WAWE WANATUNGA MISTARI SHULENI NA KUTOA SINGO ZAO? SI HATUTAKI WANAFUNZI WAADHIBIWE PINDI WANAPOKIUKA?
MWALIMU HAPEWI NAFASI YA KUONYESHA UWEZO WAKE NDANI YA DARASA NA NJE YA DARASA.....!
TUNAWAINGILIA NJE YA DARASA NA NDANI PIA...MATOKEO YAKIJA HOVYO TWALALAMA....!
SHAME ON US......!
Tuwape nafasi, wanetu wakishindwa tuwawajibishe....!
__________________ TURUDISHE JKT KWA MUJIBU WA SHERIA, NA AJIRA ZOTE ZIPITIE J.K.T
The Following User Says Thank You to Mahesabu For This Useful Post:
imebidi nikatafute kitambaa cha kufutia machozi maana hali hii inaumiza sana.
Huyu Maghembe mimi nawasi wasi naye sana maana hata elumu yake inatia shaka, anaweza kuwa kama ngugu yake mmoja alikuwa anaitwa Prof Saburi, alishakuwa mkuu VC wa ARDHI (wakati ule ni College).Huyu amegundulika kuwa hakuwa na PHD halali. sasa na huyu jamaa na strategies zake zinanitia shaka sana
__________________
Humble One
The Following User Says Thank You to Joel For This Useful Post:
Hii inatisha sana kuna haja ya wadau wa elimu kukaa chini na kulitafakari hili vinginevyo, tutaisha.65700 siyo number ya kupuuza hata kidogo, hii ni status ya wilaya nzima hapa Tanzania, swali la msingi Je hawa wataenda wapi???????????
__________________
Greatness is difficult to appreciate from close up. The great mountain on the horizon is only the ground when you are standing on it.
..........Tatizo mfumo wa elimu yetu ni mbovu na isitoshe zero nyingi hapa zimetoka shule za kata.
Mtu ukitaka kufanya mtihani wa form 4 inabidi usome mambo yote uliyofundishwa tokea form 1 hadi hiyo form 4, na wakati form two ulishafanya mtihani ukaenda form 3 lakini bado tu usome vitu vyote.
Ingekuwa bora ungekuwa unafanyika mtihani wa annual kwa kila kidato, baada ya hapo hakuna tena kurudia topic mlizozifanyia mtihani huko nyuma.Hii ingewasaidia wanafunzi kuwa makini kipindi wanaposoma na sio kukariri........huu mtindo wa kutoa mtihani topic zote za form 1 hadi 4 wala sio mzuri.
..........Kuna nchi huko magharibi wana system nzuri ya elimu, kama mtu upo grade 8 baada ya muhula kuisha mnatungiwa mtihani ambao una topic ya ile grade tu.......hawawezi kutunga mtihani wa grade 8 halafu kuna topic za tokea grade 1.
Hivyo elimu yetu bado ipo ya kikoloni sana ya kuwapata watu wachache wa kufanya kazi badala ya wengi. Kwa mtindo huu we have a long way to go.
__________________ "The great pleasure in life is doing what people say you cannot do."
imebidi nikatafute kitambaa cha kufutia machozi maana hali hii inaumiza sana.
Huyu Maghembe mimi nawasi wasi naye sana maana hata elumu yake inatia shaka, anaweza kuwa kama ngugu yake mmoja alikuwa anaitwa Prof Saburi, alishakuwa mkuu VC wa ARDHI (wakati ule ni College).Huyu amegundulika kuwa hakuwa na PHD halali. sasa na huyu jamaa na strategies zake zinanitia shaka sana
Prof saburi na Prof Mbyopyo; enzi zile ardhi ni college hawa walikuwa watu wakubwa sana Miungu watu; na si hawa tu kulikuwa na wengi pale nashukuru msimamo uliowekwa na Chuo Kikuu cha sasa walau sasa watu wanauona mwanga bora.
__________________ "No matter how far down the wrong road you've gone, TURN BACK."