Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 23
    1. #1
      Kamundu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2006
      Posts : 1,371
      Rep Power : 914
      Likes Received
      296
      Likes Given
      9

      Default Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Tanzania kwa sasa inatatizo la walimu na kitu cha kushangaza serikali inasomesha wanafunzi wengi kwenye vyuo vikuu ambao hawatalipa mikopo yao. Mimi ningeshauri serikali kwa wakati huu wa uhaba wa walimu wange weka ulazima wa wanafunzi wa vyuo wa mwaka wa mwisho kufundisha kwa miezi sita tu kabla ya kupewa vyeti vyao. Inashangaza watanzania tunafikiria kila kitu serikali ifanye, lakini serikali inatakiwa kuweka sera kwa Watanzania kusaidiana wenyewe sioni sababu ya wanafunzi wa vyuo vikuu ni kwanini wasifundishe kwa sasa wakati serikali inafanya mikakati ya kusomesha walimu.

      Tutapiga siasa lakini kama kizazi kijacho hakina elimu Tanzania itatawaliwa na vijana wa nje.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Waberoya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd August 2008
      Location : Busia-Uganda
      Posts : 5,948
      Rep Power : 1742
      Likes Received
      1518
      Likes Given
      2835

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Mkuu, uamuzi na mawazo mazuri sana.
      Ila kufundisha kwa 'emergency' sitation kama hii, haihitaji walimu tu.
      Mtu yeyote mwenye elimu anaweza kujitolea kwenda shule yoyote ile na akafundisha bure, na hii inabidi tuanze na wewe.

      Huwa sipati picha ya nini wasomi tunaifanyia nchi hii, ila Kamundu, ujue ubnafsi wetu na roho za umimi ndio zinatufikisha hapa. Ubinafsi huu unaweza kutokana na matabaka tuliyo nayo na aina ya siasa tunayoipitia.

      Ukisemacho kingeweza kutekelezeka kirahisi kama nchi ingekuwa ya kijamaa.Ubepari hauruhusu hivyo, maana ubepari unaanzia ndani ya moyo (no free lunch)

      Nchi ina system mbili za elimu International school-matajiri
      English academ-kipato cha kati
      Kiswahili(kayumba)- maskini
      Kila mtu anawaza kuwa group la pili au la kwanza, watu wanapigana na kuhsindana hili wawe na maisha mazuri, ya kushindana na kuhodhi mali na utajiri.

      Ikifikia hapo, hakuna atakayeweza kufundisha bure, hata kama watalipwa na serikali ni sh. ngapi??

      we have challenge mkuu, kutokana na culture yetu, ndiyo maana huwa nasisitiza kiongozi mzuri ni yule anayejua haya matatizo na kutafuta mbinu ya kuyatatua
      You are not supposed to be so blind with patrotism that you cant face reality. Wrong is wrong no matter who says it. Malcom X

    4. #3
      Kamundu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2006
      Posts : 1,371
      Rep Power : 914
      Likes Received
      296
      Likes Given
      9

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Waperoya,
      Nahukuru Mtanzania mwenzangu umeona hili mimi sidhani kama ubepari ni tatizo sijawahi kuona watu wanaojitolea kama wamarekani na ni "wabepari". Kuna watu wengi sana wa Kimarekani wanachukua likizo na kwenda kufundisha nchi zinazoendelea kuanzia wafanyakazi hadi ma professor. Nakumbuka nilivyokuwa Ilboru tulikuwa na walimu wengi wa nje. Mimi natakiwa nilitolee lakini ningependa Serikali ianzishe kitu kama peace corp. Lakini pamoja na yote haya tulikuwa na JKT ni kwanini tusiwe na hili swala la muhimu kwa karne hii.

    5. #4
      Magezi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2008
      Posts : 2,654
      Rep Power : 1073
      Likes Received
      33
      Likes Given
      50

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Nadhani hii kitu si kwa wanafunzi peke yao tupo wengi na tunaweza kusaidia sana kuijenga nchi yetu ambayo mafisadi wanaimaliza. Mimi najipanga na mwezi januari lazima niombe kibali wizara ya elimu ili nifundishe sekondari itakayokuwa karibu na ofisini kwangu. Nawaomba watanzania kila mtu kwa fani yake tuvamie hii sekta ya elimu na kutoa ujuzi wetu, baada ya miaka kumi mabadiliko tutayaona.

    6. #5
      MkamaP's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2007
      Posts : 4,675
      Rep Power : 1569
      Likes Received
      310
      Likes Given
      93

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By Kamundu
      Waperoya,
      Nahukuru Mtanzania mwenzangu umeona hili mimi sidhani kama ubepari ni tatizo sijawahi kuona watu wanaojitolea kama wamarekani na ni "wabepari". Kuna watu wengi sana wa Kimarekani wanachukua likizo na kwenda kufundisha nchi zinazoendelea kuanzia wafanyakazi hadi ma professor. Nakumbuka nilivyokuwa Ilboru tulikuwa na walimu wengi wa nje. Mimi natakiwa nilitolee lakini ningependa Serikali ianzishe kitu kama peace corp. Lakini pamoja na yote haya tulikuwa na JKT ni kwanini tusiwe na hili swala la muhimu kwa karne hii.
      Mkuu
      Wazo lako zuri sana tena sana ,ila mie kwa kuongezea juu ya wazo lako ningependelea iwe hivi-
      Badala ya mhitimu kulipa mkopo inabidi mhitimu kokote anakoajiliwa awe na masaa ya ziada ya kufundisha shule yoyote kwa mda ambao atakamilisha deni la mkopo.

      Nafikiri si lazima kulipa mkopo kama serikali ilivyojipanga ila kuulipa mkopo kwa staili ya kufundisha nafikiri utakuwa ulipaji wenye efficiency nzuri zaidi.

    7. Miaka 50

    8. #6
      smalnama's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th October 2009
      Posts : 13
      Rep Power : 492
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      WAZO zuri. Ila tusisahau kufundisha ni fani. You need to be trained to teach. Labda vyuo viongeze kozi ya muda kwa wahitimu, kama mwezi ili wahitimu wajue basics za kufundisha. vinginevyo itakuwa chaos mashuleni.

    9. #7
      MkamaP's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2007
      Posts : 4,675
      Rep Power : 1569
      Likes Received
      310
      Likes Given
      93

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By smalnama
      WAZO zuri. Ila tusisahau kufundisha ni fani. You need to be trained to teach. Labda vyuo viongeze kozi ya muda kwa wahitimu, kama mwezi ili wahitimu wajue basics za kufundisha. vinginevyo itakuwa chaos mashuleni.
      Pamoja kufundisha ni fani lakini kwa asilimia kubwa mhitimu wa chuo kikuu ataweza kufundisha bila kuhitaji kozi nyingine.Ni wazo

    10. #8
      Pretty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th March 2009
      Location : Chumbani.
      Posts : 2,287
      Rep Power : 1119
      Likes Received
      188
      Likes Given
      84

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Hii ya wanafunzi wa vyuo kufundisha kwa muda na watu kujitolea sijui kama itawezekana, ni wazalendo wachache watakaokubaliana na hili.


      Nafikiri ni vizuri serikali kuboresha hii sector ya ualimu, ili watu wakimbilie huko. Wapange mishahara mizuri kwa walimu.Watu wengi tu wanasomea ualimu, ila wanaobaki kwenye hii kazi ni wachache wengi wanakimbia na kwenda kufanya kazi nyingine.

      Walimu wengine wanaamua kukimbilia International/academy school maana huko angalau pato lao zuri.Kwa mtindo huu kama serikali haitaki kuboresha hii sector ya ualimu, kila siku watakuwa wanapiga kelele kwa ukosefu wa waalimu.
      Serikali yetu ina pesa na inaweza kuboresha hii sector badala ya hizo pesa kwenda kwa mafisadi.
      A mother who is really a mother is never free.

    11. #9
      MkamaP's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2007
      Posts : 4,675
      Rep Power : 1569
      Likes Received
      310
      Likes Given
      93

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By Pretty
      Hii ya wanafunzi wa vyuo kufundisha kwa muda na watu kujitolea sijui kama itawezekana, ni wazalendo wachache watakaokubaliana na hili.


      Nafikiri ni vizuri serikali kuboresha hii sector ya ualimu, ili watu wakimbilie huko. Wapange mishahara mizuri kwa walimu.Watu wengi tu wanasomea ualimu, ila wanaobaki kwenye hii kazi ni wachache wengi wanakimbia na kwenda kufanya kazi nyingine.

      Walimu wengine wanaamua kukimbilia International/academy school maana huko angalau pato lao zuri.Kwa mtindo huu kama serikali haitaki kuboresha hii sector ya ualimu, kila siku watakuwa wanapiga kelele kwa ukosefu wa waalimu.
      Serikali yetu ina pesa na inaweza kuboresha hii sector badala ya hizo pesa kwenda kwa mafisadi.
      Kweli mkuu kujitolea ni kazi ngumu hasa ukizingatia asili yetu.Lakini mimi nashauri kuhusu mkopo badala ya kulipa mkopo watu wafundishe hata kama ameajiliwa kwingine awe na kipindi shuleni.

      Kama hataki kufundisha basi alipe mkopo strictly.

    12. #10
      Kamundu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2006
      Posts : 1,371
      Rep Power : 914
      Likes Received
      296
      Likes Given
      9

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Kama umepata mkopo wa serikali na hutaki kufundisha kwa miezi sita basi hupewi cheti mbona tulilazimisha watu waende JKT tumepata nini? Watoto hawana walimu na serikali inatumia pesa kusomesha wanafunzi wengi ambao hawalipi madeni na kukimbilia nje, kuna madactari wengi tu wako Botswana na USA na wamesoma bure kwa gharama zaidi ya $20,000 siwangeweza kufundisha Biology!. Mimi sioni ubaya wa serikali kuzuia vyeti kwani hii ni kama vita sasa nchi nyetu haitaweza kuendelea kwa madini au gas pekee inahitaji Human Resources.

    13. #11
      Ogah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Posts : 5,669
      Rep Power : 21814
      Likes Received
      735
      Likes Given
      3190

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Hili suala la kujitolea ni muhimu sana.......JF Foundation?

    14. #12
      Gudboy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th August 2009
      Location : DSM
      Posts : 805
      Rep Power : 658
      Likes Received
      9
      Likes Given
      10

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Jamani nashauri tuanze na hapa wana JF itajenga sana heshima na pia hata mafisadi wataipenda hii JF maana itakua ni mfano wa kuigwa na yenye tija kwa jamaii na sio yenye kusema huku haionyeshi mfano, charity begins at home, JF is our home and TZ is our country mazee
      Kuwa na Mashori wengi si kipimo cha Urijali, kama mwanaume wa kweli, nyumbani wapate Ugali

    15. #13
      Pretty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th March 2009
      Location : Chumbani.
      Posts : 2,287
      Rep Power : 1119
      Likes Received
      188
      Likes Given
      84

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By Gudboy
      Jamani nashauri tuanze na hapa wana JF itajenga sana heshima na pia hata mafisadi wataipenda hii JF maana itakua ni mfano wa kuigwa na yenye tija kwa jamaii na sio yenye kusema huku haionyeshi mfano, charity begins at home, JF is our home and TZ is our country mazee
      Basi mfanye kweli wazalendo, isiwe typing tu kwenye keyboard halafu matendo zero.
      A mother who is really a mother is never free.

    16. #14
      Ilongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2007
      Posts : 431
      Rep Power : 712
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By Kamundu
      Tanzania kwa sasa inatatizo la walimu na kitu cha kushangaza serikali inasomesha wanafunzi wengi kwenye vyuo vikuu ambao hawatalipa mikopo yao. Mimi ningeshauri serikali kwa wakati huu wa uhaba wa walimu wange weka ulazima wa wanafunzi wa vyuo wa mwaka wa mwisho kufundisha kwa miezi sita tu kabla ya kupewa vyeti vyao. Inashangaza watanzania tunafikiria kila kitu serikali ifanye, lakini serikali inatakiwa kuweka sera kwa Watanzania kusaidiana wenyewe sioni sababu ya wanafunzi wa vyuo vikuu ni kwanini wasifundishe kwa sasa wakati serikali inafanya mikakati ya kusomesha walimu.

      Tutapiga siasa lakini kama kizazi kijacho hakina elimu Tanzania itatawaliwa na vijana wa nje.

      What a thread!!!


      Asante sana Mzalendo Kamundu kwa thread hii; na wale wote waliochangia tayari. Kuna yule aliyezungumzia wamarekani pamoja na ubepari wao. Huu ni mfano mzuri sana. Community service kwao ni kitu wanachokipa kipaumbele cha hali ya juu. Haya ni mawazo ya kujenga kweli kweli kwa sababu yanalenga mwananchi wa kawaida kabisa.

      Nadhani kama kukiwa na utaratibu mzuri kama alivyosema Ogah (wazo la foundation), hii kitu inaweza kuanza taratibu na baadae lobbying ikafanyika serikalini ili iweze kusimamia uendeshaji wake.

      Inabidi pawepo na mtaala pia wa kufundishana uzalendo wa kuipenda nchi yetu pamoja na maendeleo yake (Tuwe na moyo wa kujitolea pale tunapopata fursa ya kufanya hivyo bila malipo). ... Ni kwa vile nchi kama Amerika zina vitu kama hivi, na kila mgeni anayeingia hataki kuondoka maana anahisi amefika nchi ya ahadi.

      Sasa hivi tunaongelea uhaba wa walimu katika taasisi mbalimbali za elimu ya msingi hadi ya vyuo vikuu; lakini je ni walimu wangapi wa vyuo vikuu wamekuwa wakilipiwa na serikali na kupata mishahara yao kila mwezi wakiwa masomoni, lakini wakishamaliza masomo yao wanaamua kujilipua huko huko ili waendelee kula neema zilizoasisiwa na wenyeji wao. Kuna haja ya kubadili system tuliyo nayo ili kila mmoja wetu atambue kwamba maisha mazuri hayako Amerika au Uropa tu.

      Ubinafsi ndiyo mwishowe unazaa ufisadi.
      Abstinence is the only key to no regrets!

    17. Tom
      #15
      Tom's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2007
      Posts : 504
      Rep Power : 715
      Likes Received
      17
      Likes Given
      30

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By Kamundu
      Kama umepata mkopo wa serikali na hutaki kufundisha kwa miezi sita basi hupewi cheti mbona tulilazimisha watu waende JKT tumepata nini? Watoto hawana walimu na serikali inatumia pesa kusomesha wanafunzi wengi ambao hawalipi madeni na kukimbilia nje, kuna madactari wengi tu wako Botswana na USA na wamesoma bure kwa gharama zaidi ya $20,000 siwangeweza kufundisha Biology!. Mimi sioni ubaya wa serikali kuzuia vyeti kwani hii ni kama vita sasa nchi nyetu haitaweza kuendelea kwa madini au gas pekee inahitaji Human Resources.
      Wanafunzi wanatakiwa kujilipia lakini kama wamekopa ada hamna sababu ya kumlazimisha mtu kwa kumyima cheti maana deni halifutwi.
      Hata kama wanavyuo watajitolea hamna faida yeyote kwa sababu tutasoma sana lakini bila uzalishaji hatufiki kokote, tutaendelea tu kushangilia misaada ya vyandarua vya (Bush) mbu toka USA.
      Matatizo yote haya ya kukosa waalimu na mengineyo, bila serikali ya CCM kubadilika na kujali uzalishaji ama kuacha ufisadi hatutafika popote. Tutajitolea sana lakini kama mafisadi na serikali yao ya CCM wanaendelea kufyonza basi haina maana yeyote. Dawa nyingine ni kuiondoa CCM madarakani, ili kuwazindua usingizini.

    18. #16
      Magezi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2008
      Posts : 2,654
      Rep Power : 1073
      Likes Received
      33
      Likes Given
      50

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Nadhani ni wazo zuri kuna mdau amesema tuwe na JF Foundation itakayo ratibu mipango ya wale wote watakao kuwa tayari kuanza kufundisha kwa kujitolea ktk shule ambazo ziko karibu na ofisi/biashara zao.

      Basi napendekeza tuanze kupata mawazo ya jinsi ya uanzishwaji wa JF Foundation na ningependa by January 2010 iwe tayari ili watakao kuwa tayari waanze kupiga chaki.

      Naomba JF Founder utusaidie jinsi ya kuunda JF Foundation ambayo haita athiri activities zingine za JF.

    19. #17
      Ilongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2007
      Posts : 431
      Rep Power : 712
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By Tom
      Wanafunzi wanatakiwa kujilipia lakini kama wamekopa ada hamna sababu ya kumlazimisha mtu kwa kumyima cheti maana deni halifutwi.
      Hata kama wanavyuo watajitolea hamna faida yeyote kwa sababu tutasoma sana lakini bila uzalishaji hatufiki kokote, tutaendelea tu kushangilia misaada ya vyandarua vya (Bush) mbu toka USA.
      Matatizo yote haya ya kukosa waalimu na mengineyo, bila serikali ya CCM kubadilika na kujali uzalishaji ama kuacha ufisadi hatutafika popote. Tutajitolea sana lakini kama mafisadi na serikali yao ya CCM wanaendelea kufyonza basi haina maana yeyote. Dawa nyingine ni kuiondoa CCM madarakani, ili kuwazindua usingizini.

      Well kuna watakaofaidika, angalau, badala ya kuendelea kuteseka kwa kukosa elimu na upeo wa kuchanganua mambo itawasaidia hata kuelewa madhila unayoyazungumzia. Wengine hiyo misaada ya mbu wala hatuihitaji sababu ya hii elimu tuliyo nayo inatusaidia kujimudu katika hali mbalimbali ... na kumbuka kwamba hivyo vyandarua vyenyewe (na misaada mingine) unavyovizungumzia siyo vyote vinawafikia walengwa. Hata wakipata hawatadumu navyo maisha yao yote. So, kinachotakiwa ni elimu ambayo pamoja na hayo itamkomboa kiakili kuweza kujua jinsi ya kupata chandarua chake mwenyewe badala ya kuendelea uwa mtumwa wa misaada.

      Wakati mwingine najiuliza kwamba kama si hii elimu niliyoipata, labda sasa hivi ningekuwa kijijini nabanana na ndugu zangu kwenye mali ya urithi (kwa maana ndiyo utamaduni wetu huo, aidha unakatiwa kipande chako na kujenga mji wako mwenyewe au unasubiri mzazi afariki ndipo ugawiwe kilicho chako). Ndicho kipimo cha uelewa katika level hiyo. Lakini mtu anapoelimika zaidi kuna faida zaidi zitokanazo na elimu hiyo ikiwa ni pamoja na kuyatambua mazingira yanayomzunguka na kuweza kupambana nayo.

      Kelele zitapigwa saaaana kuhusu ufisadi, sijui siasa, lakini kama walengwa wanakosa uelewa katika mambo ya msingi watabaki kukushangaa maana kupitia ufisadi wengine wanapata angalau pilau na fulana once in 5 years!
      Abstinence is the only key to no regrets!

    20. #18
      Magezi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th October 2008
      Posts : 2,654
      Rep Power : 1073
      Likes Received
      33
      Likes Given
      50

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Nafikiri hili wazo ni muhimu kama tulivyo kwisha sema hapoawali nadhani cha msingi sasa kila mmoja wetu ambaye yuko tayari ajiandae kwa kazi ikiwa ni pamoja na kushughulikia kibali cha kufundia hapo mwakani.

      Tujaribu tuone nadhani mambo yatakuwa mazuri tu, mimi niliwahi kufanya hivi miaka ya 1996 huko kagera sehemu fulani japo nilikuwa nawafundisha vijana wawili tu lakini nilifurahi kufanya hivyo.

    21. #19
      bm21's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2008
      Location : Britain
      Posts : 777
      Rep Power : 718
      Likes Received
      2
      Likes Given
      15

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Quote By MkamaP
      Kweli mkuu kujitolea ni kazi ngumu hasa ukizingatia asili yetu.Lakini mimi nashauri kuhusu mkopo badala ya kulipa mkopo watu wafundishe hata kama ameajiliwa kwingine awe na kipindi shuleni.

      Kama hataki kufundisha basi alipe mkopo strictly.
      Kujitolea siwazo sahihi sana kwa hali ya sasa na maisha ya Kitanzania. Suala lamsingi ni kuomba wasomi walioko maofficini wenye nafasi waombe kazi za part time teaching. Namaanisha walipwe pia. Hi ni approach ambayo inatumiwa sana na vyuo mfano Tumaini University inatumia sana part time lecturers. Kwa maana nyingine tuextend huu mfumo kwa shule zetu za secondary na colleges.

      Hatahivyo kuwa na waalimu wakutumu bado ni suala mhimu ili kuboresha elimu nchini.

    22. #20
      Mugo"The Great"'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th October 2007
      Posts : 257
      Rep Power : 645
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanafunzi wa Vyuo Wafundishe kwa muda!

      Wazo hili ni zuri sana. Kinachotakiwa ni coordination kama wenzangu walivyotangulia kutoa opinions zao. kama JF Foundation itaundwa then itatumika kuratibu Volunteers online na hii itawapatia muda wa kuapnga ratiba/likizo zao vizuri ili kuendana na mihula ya masomo huko Tanzania.
      Man can believe the impossible, but man can never believe the improbable -Oscar Wilde

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 11
      Last Post: 16th September 2011, 18:32
    2. Kwa wanafunzi wa vyuo.
      By tcoal9 in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 0
      Last Post: 27th December 2010, 08:24
    3. wanafunzi wa vyuo vikuu (wanawake)
      By Kimbweka in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 40
      Last Post: 20th December 2010, 14:47
    4. Kwa Wanafunzi wa Vyuo Tu
      By Elli in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 9
      Last Post: 15th December 2010, 17:15

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...