Utakiona cha mtema kuni! - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Education, Science & Technology Forums > Jukwaa la Elimu (Education Forum)


Jukwaa la Elimu (Education Forum) Educational discussions in here... If you have some College/School materials and you wanna give them to your fellows pls do that favour to them. Let them get educated here! Become a Member to enjoy more stuffs


Reply
 
LinkBack Thread Tools Display Modes
Old 12th June 2009, 09:49 AM   #1
Utakiona cha mtema kuni!
Mzizi wa Mbuyu Mzizi wa Mbuyu is offline 12th June 2009, 09:49 AM

Nimekuwa nalitumia, kusikia sana msemo huu "CHAMTEMA KUNI" kwa muda mrefu sasa katika maisha yangu ya kila siku. Najua kuna maneno yanatumika kwa maana hiyo hiyo kama vile; kilichomtoa kanga manyoya ya shingo, kijinga cha moto, kilicho mfanya chura ashinde mtoni n.k haya maelezo yake yako wazi.

Ila ukweli ndugu zanguni nimejaribu kuulizia chanzo cha matumizi ya neno hili, nimeishawahi kusikia kuwa ni msemo wa wahenga tu..., wengine wanasema ni hadithi ya kimapokeo, wengine wanasema ni hadithi ya kwenye kitabu. Lakinipamoja na yoote hayo sina uhakia hasa nini chanzo cha neno.
Please, naomba ufafanuzi, kwa yeyote anaejua msemo huu "CHAMTEMA KUNI" ulitokana na nini. Cha mtema kuni! kipi! kiatu?, kisa?! ,kiuno?! nk kilifanya nini hadi kiogopwe namna hii??!!

Kama ni hadithi , ilikuwa kwenye kitabu gani? Mtunzi alikuwa nani...na mengineyo....
__________________
Heri kupendwa na mwenye akili mmoja, kuliko kupendwa wapumbavu maelfu!

Mzizi wa Mbuyu
JF Senior Expert Member
Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100
Activity: 16% Activity: 16% Activity: 16%
Join Date: Fri May 2009
Posts: 358
Thanks: 32
Thanked 59 Times in 32 Posts
Views: 502
Reply With Quote
  #2  
Old 13th June 2009, 11:16 AM
Kipala Kipala is offline
Kipala mzungu mtupu!
JF Senior Expert Member
Points: 84,107, Level: 100 Points: 84,107, Level: 100 Points: 84,107, Level: 100
Activity: 32% Activity: 32% Activity: 32%
 
Join Date: Sat Jan 2009
Posts: 656
Thanks: 32
Thanked 71 Times in 53 Posts
Rep Power: 23
Kipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Lugha ninayojua ni "akifanya hivyo atakiona cha mtemakuni". Ninaelewa ni kama tishio au onyo: akifanya kitu kisicho halali ataona matokeo yake yaani atapata adhabu.

Mtemakuni (pia: mtema-kuni au mtema kuni) ni mtu anayepasua miti kuwa kuni. Kwa hiyo ana kazi nzitonzito pia ni watu wenye nguvu ya kimwili. Maana neno "kutema" hupatikana kwa maana mawili moja ni "kutema mate" mengine ni "kupasua kitu" kama ubao, miwa n.k.

Sina uhakika juu ya asili ya usemi lakini nimeielewa hivyo:

Hawa watemakuni ni watu wenye nguvu wanajua kuadhibu. Ukitaka kuiba kwao utaona jinsi gani wanavyoweza kujitetea. -
au labda pia: Watemakuni ni watu wanaoishi katika mazingira magumu msituni wakifanya kazi hii nzito heri usijaribu kucheza nao...

Sijui wenzangu wanaonaje?
Reply With Quote
  #3  
Old 15th June 2009, 08:51 AM
Mzizi wa Mbuyu Mzizi wa Mbuyu is offline
Mzizi wa Mbuyu has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100
Activity: 16% Activity: 16% Activity: 16%
 
Join Date: Fri May 2009
Posts: 358
Thanks: 32
Thanked 59 Times in 32 Posts
Rep Power: 21
Mzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Nashukuru sana ndugu yangu, si haba, iatabidi niende BAKITA pia kujiridhisha.
Hapa inaoneka wengi wetu huwa tuna tumia misemo tusiyojua asili yake!
__________________
Heri kupendwa na mwenye akili mmoja, kuliko kupendwa wapumbavu maelfu!
Reply With Quote
  #4  
Old 15th June 2009, 03:43 PM
Kipala Kipala is offline
Kipala mzungu mtupu!
JF Senior Expert Member
Points: 84,107, Level: 100 Points: 84,107, Level: 100 Points: 84,107, Level: 100
Activity: 32% Activity: 32% Activity: 32%
 
Join Date: Sat Jan 2009
Posts: 656
Thanks: 32
Thanked 71 Times in 53 Posts
Rep Power: 23
Kipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enoughKipala will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

BAKITA unataka kuuliza namna gani? Je wanao ukurasa mtandaoni unapoandika maswali?
Reply With Quote
  #5  
Old 15th June 2009, 03:51 PM
Mzizi wa Mbuyu Mzizi wa Mbuyu is offline
Mzizi wa Mbuyu has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100
Activity: 16% Activity: 16% Activity: 16%
 
Join Date: Fri May 2009
Posts: 358
Thanks: 32
Thanked 59 Times in 32 Posts
Rep Power: 21
Mzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Quote:
View Post
BAKITA unataka kuuliza namna gani? Je wanao ukurasa mtandaoni unapoandika maswali?
Ntakwenda mzimamzima ofisini kwao, ninashida sana na hii kitu ndugu yangu nina kazi nayo. Sidhani kama watakosa ufafanuzi juu ya msemo huu. Kama unakingine cha kunisaidia, sema ndugu yangu.
__________________
Heri kupendwa na mwenye akili mmoja, kuliko kupendwa wapumbavu maelfu!
Reply With Quote
  #6  
Old 17th June 2009, 10:26 PM
Kwetunikwetu's Avatar
Kwetunikwetu Kwetunikwetu is offline
Kwetunikwetu is doing fine
JF Senior Expert Member
Points: 365,887, Level: 100 Points: 365,887, Level: 100 Points: 365,887, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Sun Dec 2007
Location: Kwetu uswahilini
Posts: 797
Thanks: 1
Thanked 71 Times in 55 Posts
Rep Power: 24
Kwetunikwetu will become famous soon enoughKwetunikwetu will become famous soon enoughKwetunikwetu will become famous soon enoughKwetunikwetu will become famous soon enoughKwetunikwetu will become famous soon enoughKwetunikwetu will become famous soon enoughKwetunikwetu will become famous soon enoughKwetunikwetu will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Mzizi wa Mbuyu nimekupata mkuu ngoja nichangie kidogo; Mimi hili nilipata simulizi toka kwa jamaa mmoja wa Kenya ambae anasema kuna mwalimu aliwasimulia shule ya msingi juu ya kisa cha mtema kuni. Hiyo hadithi inasema hivi:


Siku moja jamaa mtema (mkata) kuni alienda porini kukata kuni. Sasa akakuta mti mkubwa umeanguka na umekauka vizuri, ambao wenyeji wanaupenda sana kwa kutumia kwa vile kuni zake hazitoi moshi n.k. Sasa huyo mtema kuni akaanza kukata kuni na kurundika mzigo mkubwa tu.


Jua lilipozidi kuwa kali jamaa akavua nguo akabaki uchi (hakutarajia mtu kutokea maeneo hayo kwa vile ni mbali na makazi ya watu) huku akiendelea na kupasua kuni toka kwenye lile gogo. Ikatokea jamaa akawa amechoka na pia jua kali, kwa hivyo akaamua kukaa juu ya lile gogo kupumzika.


Sasa lile gogo lilikuwa lina ufa (kutokana na kutanuka kwa jua kali), kwa hivyo nyanya zikawa zimening'inia kwenye huo ufa. Baada ya kitambo kirefu kupita, jua nalo likawa linazama; kwa hivyo jamaa akaamua kunyanyuka ili ajitayarishe kuondoka. Sasa kumbe lile gogo lilikuwa limeshaanza ku-contract (kusinyaa); kwa hiyo nyanya zikashindwa kutoka.


Jamaa wakati anakukuruka, huku contraction ya gogo inaendelea taratibu; jamaa akajikuta immediate options zimekauka kwa vile hakuweza kujinasua na shoka lilikuwa mbali hivyo hawezi kuzikata nyanya ili atoke. So, jamaa ndio akafia pale juu ya gogo baada ya mateso ya muda mrefu, kwani hata kelele alizopiga hazikuweza kusikika kijijini ambako palikuwa mbali. Kwa hivyo, ndugu, jamaa na marafiki walipomtafuta ndio wakamkuta jamaa amejifia juu ya gogo na nyanya zimenasa ndani ya gogo....! Kwa hivyo ikaonekana ni mateso makubwa mno mtu anayoweza kuyapata, so watu wakawa wanafanya reference kwamba ukifanya jambo baya/ukaidi n.k then utakiona cha mtema kuni


Poa mkuu nipe thanks....
__________________
It's been long since I've lost all fears and concerns. I don't worry, I calculate

Last edited by Kwetunikwetu; 17th June 2009 at 10:36 PM.. Reason: Rephrasing
Reply With Quote
  #7  
Old 17th June 2009, 10:44 PM
Babuyao Babuyao is online now
Babuyao has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 83,775, Level: 100 Points: 83,775, Level: 100 Points: 83,775, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Sat Jun 2009
Posts: 507
Thanks: 32
Thanked 43 Times in 28 Posts
Rep Power: 22
Babuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enoughBabuyao will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Mtemakuni hakika ni mpasuaji au mkataji wa kuni kama wengine walivyosema. Hadithi ya mkatakuni wengine wanasema wakati akikata kuni alikosea mahesabu (umakini)shoka likatua kwenye mguu likampasua na kumjeruhi sana. Kwa hiyo, kukiona cha mtemakuni ina maana ya kujiingiza kwenye shida ya kujitakia, ni kukosa umakini katika kutenda jambo ambapo baadaye mtu anakuja kujuta kutokana na shida atakayoipata. Kumbe, ni msemo wa onyo, wa kumtaka mtu awe mwangalifu ili mabaya yasimkute. Ni msemo unaotaka seriousness ya mtu katika kutenda ili kujiepusha na matokeo mabaya.
Reply With Quote
  #8  
Old 18th June 2009, 11:26 AM
kela72 kela72 is offline
kela72 has no status.
Senior Member
Points: 68,710, Level: 100 Points: 68,710, Level: 100 Points: 68,710, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon May 2008
Posts: 171
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 22
kela72 will become famous soon enoughkela72 will become famous soon enoughkela72 will become famous soon enoughkela72 will become famous soon enoughkela72 will become famous soon enoughkela72 will become famous soon enoughkela72 will become famous soon enoughkela72 will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Bonge la elimu hii, tumeelimika wengi!
Reply With Quote
  #9  
Old 18th June 2009, 11:46 AM
Mzizi wa Mbuyu Mzizi wa Mbuyu is offline
Mzizi wa Mbuyu has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100 Points: 186,445, Level: 100
Activity: 16% Activity: 16% Activity: 16%
 
Join Date: Fri May 2009
Posts: 358
Thanks: 32
Thanked 59 Times in 32 Posts
Rep Power: 21
Mzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enoughMzizi wa Mbuyu will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Quote:
View Post
Mzizi wa Mbuyu nimekupata mkuu ngoja nichangie kidogo; Mimi hili nilipata simulizi toka kwa jamaa mmoja wa Kenya ambae anasema kuna mwalimu aliwasimulia shule ya msingi juu ya kisa cha mtema kuni. Hiyo hadithi inasema hivi:


Siku moja jamaa mtema (mkata) kuni alienda porini kukata kuni. Sasa akakuta mti mkubwa umeanguka na umekauka vizuri, ambao wenyeji wanaupenda sana kwa kutumia kwa vile kuni zake hazitoi moshi n.k. Sasa huyo mtema kuni akaanza kukata kuni na kurundika mzigo mkubwa tu.


Jua lilipozidi kuwa kali jamaa akavua nguo akabaki uchi (hakutarajia mtu kutokea maeneo hayo kwa vile ni mbali na makazi ya watu) huku akiendelea na kupasua kuni toka kwenye lile gogo. Ikatokea jamaa akawa amechoka na pia jua kali, kwa hivyo akaamua kukaa juu ya lile gogo kupumzika.


Sasa lile gogo lilikuwa lina ufa (kutokana na kutanuka kwa jua kali), kwa hivyo nyanya zikawa zimening'inia kwenye huo ufa. Baada ya kitambo kirefu kupita, jua nalo likawa linazama; kwa hivyo jamaa akaamua kunyanyuka ili ajitayarishe kuondoka. Sasa kumbe lile gogo lilikuwa limeshaanza ku-contract (kusinyaa); kwa hiyo nyanya zikashindwa kutoka.


Jamaa wakati anakukuruka, huku contraction ya gogo inaendelea taratibu; jamaa akajikuta immediate options zimekauka kwa vile hakuweza kujinasua na shoka lilikuwa mbali hivyo hawezi kuzikata nyanya ili atoke. So, jamaa ndio akafia pale juu ya gogo baada ya mateso ya muda mrefu, kwani hata kelele alizopiga hazikuweza kusikika kijijini ambako palikuwa mbali. Kwa hivyo, ndugu, jamaa na marafiki walipomtafuta ndio wakamkuta jamaa amejifia juu ya gogo na nyanya zimenasa ndani ya gogo....! Kwa hivyo ikaonekana ni mateso makubwa mno mtu anayoweza kuyapata, so watu wakawa wanafanya reference kwamba ukifanya jambo baya/ukaidi n.k then utakiona cha mtema kuni


Poa mkuu nipe thanks....
Mkuu, thanks umepata ila duh! kama ni kweli ilikuwa hivyo, mtema kuni aliteseka sanaa!! Yaani nanihii.. yake ilibanwa kwenye gogo!!
Poa, lakini kweli pia ntakwenda BAKITA, nikipata muda kuchunguza jambo hili.
__________________
Heri kupendwa na mwenye akili mmoja, kuliko kupendwa wapumbavu maelfu!
Reply With Quote
  #10  
Old 30th June 2009, 12:48 AM
Lilian's Avatar
Lilian Lilian is offline
Lilian has no status.
Member
Points: 57,486, Level: 100 Points: 57,486, Level: 100 Points: 57,486, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Feb 2009
Posts: 28
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
Lilian will become famous soon enoughLilian will become famous soon enoughLilian will become famous soon enoughLilian will become famous soon enoughLilian will become famous soon enoughLilian will become famous soon enoughLilian will become famous soon enoughLilian will become famous soon enough
Default Re: Utakiona cha mtema kuni!

Mi huwa nafahamu simulizi tofauti kuhusu ''kukiona cha mtemakuni'', sikuwahi kusikia pia hizo zilipoelezwa hapo juu.
Niliambiwa kuwa mtema kuni ni mtu anaekata kuni na alieenda kukata kuni porini na alipokuwa anataka kuzifunga kuni pamoja akawa anatafuta kamba, na bila kujua akamgusa nyoka akidhani ni kamba ili afungie kuni, loooo! kilichofuata ni mapambano... kwa hiyo hicho ndo kilikuwa ''cha mtemakuni'' nilichokifahamu.
It is so intresting kuwa kuna simulizi tofauti tofauti kuhusiana na msemo uleule. Na nafikiri mambo kama haya yangehifadhiwa vizuri (yangekuwa well documented) ingesaidia kwa vizazi vijavyo hasa ukizingatia kiswahili kinakua sana sasa hivi ktk nch nyingi za Afrika.
__________________
Happy, hopeful and confident in Christ
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
cha, kuni, mtema, utakiona


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Azimio la Arusha kuzaliwa upya? Mwanagenzi Jukwaa la Siasa 313 14th December 2009 08:17 AM
BoT Scandal: Tulikotoka, Tulipo, Tunakoelekea Maxence Melo Jamii Intelligence 3079 12th November 2009 08:12 AM
Budget Mbadala 2008/09 Kahangwa Jukwaa la Siasa 1 18th June 2009 03:09 PM
Kwanini watanzania wanamlaumu mwalimu Nyerere kwa kukosa elimu? popo Jukwaa la Siasa 304 6th April 2009 01:23 AM
Prof Msola Kawasilisha Bajeti Halisi Jukwaa la Siasa 5 22nd July 2007 02:09 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 01:34 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com