Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Acheni uvivu katika kutafuta elimu

    Report Post
    Results 1 to 5 of 5
    1. #1
      KiuyaJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2007
      Location : DSM
      Posts : 528
      Rep Power : 704
      Likes Received
      20
      Likes Given
      4

      Post Acheni uvivu katika kutafuta elimu

      Ninasema hivyo ni kiwa na maana kuwa uelewa wa mambo mengi ni kitu muhimu sana kwa binadamu tena katika zama hizi za utandawazi.Watanzania wenzako,naomba tuwe na jitihada za kujifunza mambo tofauti ili tuweze kupambana na maisha ya kila siku.
      Ukizingatia elimu ndiyo ufunguo wa maisha;basi ni vizuri tukawa na huo ufunguo ilituweze kutatua changamoto za kimaisha kama zinavyoibuka siku hadi siku hapa nchini na dunia kwa ujumla.
      Kitu kingi ambacho kinapelekea mimi kuandika hii habari;nimegundua kuwa watanzania wengi ni wavivu wa kujisomea/hawa utamaduni wa kujisomea.Mara nyingi utaonana mtu anajisomea kwaajili ya usahili/mtihani.
      Chukulia mfano mdogo tu ndani ya mbunge letu,ile sheria ya mafao ilipitishwa na wabunge katika bunge la mwezi March/April,2012.Taarifa zilipoanza kutolewa na SSRA(Social Security Regulatory Authority);baadhi ya watu wakagundua kuna kipengele cha umri wa miaka 55/60 ndiyo mtu anaruhusiwa kudai mafao yake.Wafanyakazi/wananchi wakaja juu kuona kuwa haiwatendei haki na wabunge wakaja juu pia na kuanza kuomba mwongozo baada ya kukiri kuwepo madhara hasi kwa wenye fedha zao.Jana Mr.Mbowe katika maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu akasema "mh.waziri mkuu sheria iliyotumika kulifungia gazeti la Mwana halisi kuwa ni sheria kandamiza na ulikwisha pigiwa kelele na vyombo vya habari kwasababu inavinyima uhuru vyombo vya habari pale vinapoandika habari zisizoifurahisha serikali na serikali inakuwa na nguvu za kukifungia chombo cha habari bila hata kukipa nafasi ya kujitetea;je,mh.waziri mkuu huoni kwamba ni sheria kandamiza katika nchi inayofuata demokrasia?Mh.akajibu kwa kusema,"sioni kama ina ubaya wowote katika utendaji wake,na kama mtu ameonewa anaruhusiwa kukata rufaa katika mahakama;na hata hivyo mh.spika sheria yenyewe imepitishwa na bunge lako tukufu na iataendelea kutumika mpaka pale mtakapo ileta hapa bungeni kwaajili ya marekebisho zaidi."
      Hii inaonyesha jinsi gani hata wabunge wetu wanapopewa makablasha kwenda kuyasoma inaonyesha hawasomi/hawayaelewi ndiyo maana utaona wanapitisha vitu halafu baadaye vinakuja ku-back fire ndiyo utasikia naomba mwongozo wakati wangeweza kuzuia hali kama hizi zisijitokeze mapema.
      Hebu angalia kiambatanisho hapa chini;kinaonyesha jinsi gani wenzetu walivyo serious katika kujifunza/kujua mambo.
      Attached Thumbnails  
      Tusiichukie Tanzania,bali tuwachukie viongozi wake

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Msafiri Kasian's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Posts : 1,119
      Rep Power : 612
      Likes Received
      113
      Likes Given
      72

      Default Re: Acheni uvivu katika kutafuta elimu

      Unachosema ni kweli,mimi binafsi nitaufanyia kazi ushauri wako.

    4. #3
      Awadh Mabaraza's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th August 2012
      Posts : 69
      Rep Power : 354
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: Acheni uvivu katika kutafuta elimu

      Naunga mkono na nitajitahidi kushare ujumbe huu na vijana wenzangu ambao hawajafanikiwa kujiung na JF

    5. #4
      EJay's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 161
      Rep Power : 385
      Likes Received
      36
      Likes Given
      18

      Default Re: Acheni uvivu katika kutafuta elimu

      Ni kweli Mkuu

    6. #5
      lutayega's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th February 2012
      Posts : 609
      Rep Power : 485
      Likes Received
      169
      Likes Given
      66

      Default Re: Acheni uvivu katika kutafuta elimu

      Unachosema nakiunga mkono ingawa na mimi ni mmoja ya watu wasopenda kusoma but umetushauri jambo jema

    7. Miaka 50

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...