Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

    Report Post
    Results 1 to 8 of 8
    1. #1
      kiogopeni's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th June 2012
      Posts : 31
      Rep Power : 354
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      Ulimboka ana damu tofuti na Waislamu waliouliwa Mwembechai?

      Sehemu ya mazungumo ya Mheshimiwa Kitwana Kondo (MB) mbele ya waandishi wa habari Mei 27, mwaka huu

      JUZI tarehe 21 ya mwezi huu, niliwaambia ya kwamba mimi ni mwanachama wa CCM, na kiongozi wa CCM, na nina wajibu mimi wa kufuata maagizo na maelekezo yote ya CCM. Niliwaambia pia ya kwamba nina wajibu mimi wa kutetea maamuzi ya serikali ya Chama Cha Mapinduzi.
      Lakini nilisema pia kwamba pia nina wajibu wa kuishauri serikali yangu pale ninapoona inafanya makosa. Wajibu huu mie ninao.
      Nililolisema na ninalisema tena leo ni kwamba serikali imekuwa Insensitive kwa mambo yanayowahusu Waislamu na mambo mengine. Na kwa kuwa serikali inakuwa insensitive Waislamu wanatafsiri ile insensivity ya serikali kuwa bila shaka serikali haiwapendi.
      Siku ile nilitoa mfano wa kuingia Msikitini Polisi wa serikali walikuwa hawana sababu ya kuingia Msikitini. Lakini lile limetokea na ghasia ambazo serikali yenyewe ili contribute (ilichangia). Kabla ya siku ile polisi wamekuwa wakiwakamata Masheikh majumbani kwao kimya kimya. Kama serikali ingekuwa inataka kumkamata Magezi wangeweza kumkamata Magezi nyumbani kwake.
      Lakini serikali katika busara zake iliona Magezi imkamate Msikitini baada ya swala ya Alasiri pale mahala pamejaa watu. Huku ikijua kwamba Magezi ana wafuasi wake. Kwanini isimkamate Magezi asubuhi nyumbani kwake? Kwanini isimkamate Magezi usiku nyumbani kwake?
      Wakaamua kumkamata pale. Kitendo kile ndicho kilicholeta rabsha ya tarehe 12.
      Watu walipozidiwa nguvu wakakimbilia ndani ya Msikiti. Msikiti ule una wanawake ambao hawakuwahi kutoka. Sasa mimi bado narudia kwamba kama serikali ingetaka ingeweza kuuzingira ule Msikiti wale wangetoka tu. Ni insensitivity yao ya kusema potelea mbali (kwanza) kwanini wangoje mpaka saa nane za usiku, wakavunja
      mlango ambao mpaka leo haujatengenezwa wakaingia ndani. Walishawakatia umeme na nini. Wakavunja Msikiti wakaingia ndani. Na si hivyo tu, wakawakamata, wakawapiga wale wanawake wakawapiga. Na wakawamwagia unga ambao unawasha. Mimi nilizungumza na wale wanawake wanaeleza mambo hayo. Sasa mimi nasema hilo linaonyesha insensivity ya serikali.
      Na imefanya kosa kuwashitaki wale Waislamu wa Mwembechai kwa kusema Yesu si Mungu. Au kusema Yesu si mwana wa Mungu au kusema Yesu hakusulubiwa. Imefanya kosa kubwa kuwashitaki wale. Kwa kusema maneno ambayo ndiyo anayoyaamini miaka yote. Kila mahali palipo na Uislamu maneno hayo yapo. Sasa naambiwa habari ya mahakama. Mimi sisemi habari ya mahakama. Nasema habari ya serikali. Mahakama inapelekewa kesi. Sasa kesi ya kusema Yesu si Mungu haikutoka kwenye mahakama.
      Haya yametoka nje, polisi ndio waliomshitaki mtu huyu kwa kusema Yesu si Mungu. Serikali ambayo haina dini!
      Mwaka 1996 walimamatwa vijana wawili Lushoto. Walikuwa Msikitini wanatoa mawaidha wakasema Yesu si Mungu. Wakangojewa nje walipokuwa wanakwenda sokoni wakakamatwa. Wakashitakiwa kwa kosa, kwa kashfa ya dini nyingine. Dini gani nyingine?
      Kashfa yenyewe ni nini wamesema Yesu si Mungu. Na hivi juzi juzi, mambo ndio hayo hayo. Sasa mimi nasema serikali inafanya kosa kubwa, serikali isiyokuwa na dini inafanya kosa kuwashitaki watu kwa sababu ya imani yao.
      Hivi karibuni Muadhama Kadinali Pengo amesema kwenye Kiti Moto ya kwamba kwa Muislamu kusema Yesu si Mungu si kashfa. Kwasababu ndio imani yake. Na amesema mimi yaani yeye Kadinali Pengo naamini ya kwamba Mtume Muhammad si Mtume wa mwisho. Hivyo ndivyo imani yangu. Si kashfa kwa dini yoyote.
      Si hivyo tu, juzi kwenye gazeti la Dar Leo ... kuna maneno Maaskofu wamuunga mkono K.K. Hawa ni Maaskofu wa Kanisa la Protestant, na wao wanasema kwa Muislamu kusema Yesu si Mungu si kashfa. Na kwa Mkristo kusema Yesu Mungu si kashfa.
      Haya ni maneno ambayo yamesemwa na Mabishops, sasa ikiwa dini yenyewe inayosemwa ni kashfa ni dini ya Kikristo, Wakristo wenyewe wanasema si kashfa. Sasa serikali inasema kashfa kwa dini nyingine, dini gani?
      Sasa mimi nilichowaomba mnisaidie siku ile ni kuiomba serikali ifute count hii. Serikali kusema lakini kesi iko
      mahakamani si kweli. Serikali bado ina uwezo wa kwenda mahakamani na kusema tunafuta count hii. Kuwashitaki kwa sababu wanasema maneno yaliyoko ndani ya Qur’an ndio kusema serikali inaona Qur’an ni kitabu cha uchochezi.
      Unapomshitaki mtu mahakamani kwa uchochezi kwa kusema maneno yaliyo ndani ya Qur’an, lazima useme na kitabu chenyewe ni kitabu cha uchochezi.
      Sasa ninachosema mimi kwa bahati mbaya hawa kina Bwana walioshtakiwa kwa count hii moja wamepata conviction maana yake, mahakama itakuwa inasema kitabu hiki ni kitabu cha uchochezi.
      Swali langu mimi, serikali itaifungia Qur’an? Serikali wataifungia dini ya Kiislamu? Huo ndio woga wangu mimi ... hiki kitabu ni kitabu cha uchochezi inabidi kifungiwe. Hawawezi kuwaambia Waislamu semeni yote lakini haya Yesi si Mungu msiseme. Sasa hii ndio hatari ninayoiona mimi.
      Kesi ikiwa mahakamani , pale mwenye uwezo ni hakimu. Lakini hakimu anapima ushahidi uliokuwa pale. Hawa
      watu wasema wanastahili kupata dhamana. Hawa watu wanaumwa, wagonjwa. Jana gazeti moja limesema Magezi kadhoofu kabisa. Yule Bwana Kamishna amesema Magezi anatibiwa jela. Na wengine.
      Kuna mzee moja Musa Katembo ana umri wa miaka themanini. Basi hata nyie watu wa magazeti hamna huruma, mtu wa miaka themanini! Siku hizi mahakama inasema hata mtu aliyeshitakiwa kwa kuua anaweza kupata dhamana. Itakuwa huyu mzee wa miaka themanini, atafanya nini huyu akipata dhamana.
      Sasa mie kuishauri serikali kwamba jamani hawa watu wamekaa zaidi ya miezi mitatu ndani. Ndani kule kuna adha wamekuwa wagonjwa. Mmoja kesha kufa.
      Sasa kusema aah alikuja ndani mgonjwa. Sasa kwanini msimpeleke hospitali! Sasa huenda akafa mmoja, mmoja mmoja na dhana ipo. Dhana ipo kwamba serikali inafurahia hivyo; kwamba wafe mmoja mmoja. Sasa dhana can be wrong. Na dhana usiitie kwenye sheria.
      Kesi ikiwa mahakamani , pale mwenye uwezo ni hakimu. Lakini hakimu anapima ushahidi uliokuwa pale. Hawa watu wasema wanastahili kupata dhamana. Hawa watu wanaumwa, wagonjwa. Jana gazeti moja limesema Magezi kadhoofu kabisa. Yule Bwana Kamishna amesema Magezi anatibiwa jela. Na wengine. Kuna mzee moja Musa Katembo ana umri wa miaka themanini. Basi hata nyie watu wa magazeti hamna huruma, mtu wa miaka themanini! Siku hizi mahakama inasema hata mtu aliyeshitakiwa kwa kuua anaweza kupata dhamana. Itakuwa huyu mzee wa miaka themanini, atafanya nini huyu akipata dhamana.
      Sasa mie kuishauri serikali kwamba jamani hawa watu wamekaa zaidi ya miezi mitatu ndani. Ndani kule kuna adha wamekuwa wagonjwa. Mmoja kesha kufa.
      Sasa kusema aah alikuja ndani mgonjwa. Sasa kwanini msimpeleke hospitali! Sasa huenda akafa mmoja, mmoja mmoja na dhana ipo. Dhana ipo kwamba serikali inafurahia hivyo; kwamba wafe mmoja mmoja. Sasa dhana can be wrong. Na dhana usiitie kwenye sheria.
      Sasa isisemwe maneno ya kwamba mahakama ndio inayowaweka. Si kweli. Mahakama inaamua baada ya kuambiwa. Waliokuwa wakipinga dhamana siku zote ni serikali. Sasa wakati ule walikuwa wazima afadhali, sasa wagonjwa. Kwahiyo, serikali isibabaishe hapa ikasema oh kesi ipo mahakamani.
      Viongozi wangu baadhi wanasema kuwa mimi natafuta umaarufu. Mimi sitafuti umaarufu. Mimi maarufu. Mimi sitafuti umaarufu. Mimi tayari maarufu. Kwahiyo, si kweli kwamba mimi natafuta umaarufu.Mimi nimeanza ubunge 1965. Na tokea nimeanza ubunge sijagombea nafasi yoyote mimi nikashindwa. Yoyote. Sasa umaarufu unakuaje.
      Nimegombea ubunge mara nne nimeshinda mara zote nne. Nimegombea udiwani mara tatu nimeshinda mara zote tatu. Nimegombea ubunge juzi juzi, nimeshinda. Nimegombea ujumbe wa kamati ya siasa ya mkoa juzi juzi nimeshinda. Sasa umaarufu unakuwaje. Mie sitafuti umaarufu.

    2. Miaka 50

    3. #2
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      593
      Likes Given
      76

      Default Re: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      Full rubbish!

    4. #3
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,459
      Rep Power : 1189
      Likes Received
      1435
      Likes Given
      939

      Default Re: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      Mimi nadhani yale mauaji ya Mwembe Chai kwa kila mpenda amani alitakiwa aishangilie Serikali na kuipongeza, huwezi kufananisha vitu walivyokuwa wanafanya na baadhi ya waliouawa pale Mwembechai na hili Suala la ulimboka. Sana sana tuwaulize Wanaharakati ni kwanini hawakuandamana kuipongeza Serikali kipindi kile hawaoni kwamba wapo Biased? kwasababu Serikali ikifanya jambo jema wanakaa kimya lakini ikifanya kitu kibaya wanaandamana kupinga.
      Mnang'oa meno ya Tembo ili mukayauze, mnang'oa meno na Kucha za Watanzania wasio na hatia ili iweje?

    5. #4
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,706
      Rep Power : 16252
      Likes Received
      3155
      Likes Given
      4076

      Default Re: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      ama kweli ukiyastaajabu ya mussa utayaona ya firahuni wewe unaakili timamu kweli wewe ,unajua ulichokiandika wewe,maana kuanzia tittle na msg ni vitu viwili tofauti,nyie ndio prof maji marefu nyie.umetumw na nani ????????????na ukirudia kumtajataja yesu utawekwa jela kabisa
      Kosea njia utaelekezwa,lakini usikosee mtu wakuoa /kuolewa naye,vinginevyo majuto yatakuwa sehemu ya maisha yako.tuliza kichwa unapochagua mwenzi wa maisha.

    6. #5
      Mboko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Location : Kwemunyu Muheza Tanga
      Posts : 599
      Rep Power : 557
      Likes Received
      108
      Likes Given
      1363

      Default Re: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      Idiot mkubwa


    7. #6
      Power G's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Location : Msoga Kijijini
      Posts : 2,414
      Rep Power : 993
      Likes Received
      776
      Likes Given
      261

      Default Re: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      Nimejaribu kulinganisha kichwa cha habari na habari yenyewe, sijaona uhusiano wowote kabisaaaa.
      TANZANIA ITAJENGWA NA WENYE MOYO NA KULIWA NA WENYE MENO KAMA AKINA EL, JK, EC na RA

    8. #7
      fidelis zul zorander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2012
      Posts : 450
      Rep Power : 454
      Likes Received
      52
      Likes Given
      9

      Default Re: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      duuuh!

    9. #8
      mariavictima's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th July 2010
      Posts : 180
      Rep Power : 487
      Likes Received
      38
      Likes Given
      15

      Default Re: WANAHARAKATI, Ulimboka MNAFANYA KAZI YA KANISA

      Mbona sielewi? Kwani nini kinazungumzwa hapo?

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...