Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

    Report Post
    Results 1 to 7 of 7
    1. #1
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,038
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      183
      Likes Given
      245

      Default Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

      Wanafunzi wagoma kufanya mtihani

      WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Kibaha iliyo mkoani Pwani wamegoma kwa siku nne kuendelea na mitahani ya ‘Mock’ kwa madai kuwa maswali mengi yaliyoulizwa yamerudiwa kwani yaliwahi kutoka katika mitihani ya mwaka 2008 na 2009.

      Wakizungumza na waandishi wa habari jana wameilalamikia bodi ya utungaji wa mitihani Kanda ya Mashariki na Pwani (EZEB) na kusema badala ya kutunga mitihani mipya wamenakili iliyopita wakati wao wamechanga fedha kuiwezesha bodi hiyo kutunga mitihani ya kuwapima vyema.

      Walisema hawawezi kuendelea na mitihani hiyo kwani haiwawezeshi kujiandaa vizuri na mtihani wao wa mwisho badala yake inawadidimiza kitaaluma kwani tayari mitihani hiyo walishaifanyia mazoezi.

      Walitolea mfano wa marudio ya maswali katika somo la Civics wakisema kuwa wameulizwa swali la mwenyekiti wa AU ambalo katika majibu yake ya kuchagua hakuna jibu hata moja kwani waliowekwa wote wameshamaliza muda wao kwa sasa.

      “Hatuwezi kuendelea kufanya mtihani kwani haitusaidii chochote katika maandalizi ya mtihani wetu wa mwisho, wakitaka watunge tena tufanye tujipime vizuri lakini hiki walichokifanya bodi ya mtihani hakitufurahishi ndio maana tumeamua kugoma kuendelea na mtihani huu,” alisema mmoja wa wanafunzi kwa niaba ya wengine.

      Aidha wanafunzi hao walidai kuwa wamekuwa wakichangia sh 12,000 kwa ajili ya mtihani huo jambo ambalo limewashangaza kwa bodi hiyo kurudia mitihani wakati ingeweza kutumia muda kwa ajili ya kutunga maswali tofauti na mitihani iliyopita.

      Mkuu wa shule hiyo Sekundi Kayenga alithibitisha kutokea kwa mgomo huo na kukiri kuwa baadhi ya mitihani ukiwemo wa somo la Baiolojia ilinakiliwa kutoka katika mitihani iliyopita.
      God doesn't require us to succeed; he only requires that you try

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Sizinga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th October 2007
      Location : Mars
      Posts : 3,942
      Rep Power : 1433
      Likes Received
      1510
      Likes Given
      1619

      Default Re: Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

      Good steps...hawa ndio vicha vilivyobakia!!sasa mitihani kama hii mtu ukikutana nayo,unapiga div 1 ya ajabu,..siku ya pepa ya mwisho..dah....zero ya ajabu!!
      GESI KWANZA KOROSHO BAADAE!!

    4. #3
      Jitihada's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th February 2011
      Posts : 155
      Rep Power : 451
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default Re: Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

      napita tu!

    5. #4
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,038
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      183
      Likes Given
      245

      Default Re: Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

      elimu inajifia yenyewe kila mtu kawa mchakachuaji!
      Quote By Sizinga
      Good steps...hawa ndio vicha vilivyobakia!!sasa mitihani kama hii mtu ukikutana nayo,unapiga div 1 ya ajabu,..siku ya pepa ya mwisho..dah....zero ya ajabu!!
      God doesn't require us to succeed; he only requires that you try

    6. #5
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,714
      Rep Power : 10174
      Likes Received
      5668
      Likes Given
      12666

      Default Re: Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

      wapo maofisini tu wanacopy na ku paste, hawa waalimu nao ni wa kata?
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    7. Miaka 50

    8. #6
      kilimasera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Posts : 3,038
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      183
      Likes Given
      245

      Default Re: Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

      na wamewachangisha pesa hawa watoto elfu kumi na tatu kila mmoja
      Quote By Ivuga
      wapo maofisini tu wanacopy na ku paste, hawa waalimu nao ni wa kata?
      God doesn't require us to succeed; he only requires that you try

    9. #7
      data's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th April 2011
      Posts : 2,095
      Rep Power : 854
      Likes Received
      363
      Likes Given
      316

      Default Re: Wizara ya Elimu fuatilieni hili Elimu inakufa

      Quote By kilimasera
      na wamewachangisha pesa hawa watoto elfu kumi na tatu kila mmoja
      Wanafunzi ndio wapuuzi.. wangefanya afu tuone kama wote wangepata one..... wapuuziiiii

    Similar Topics

    1. Wizara Ya Elimu
      By lowamond in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 4
      Last Post: 15th November 2011, 10:40
    2. Wizara ya Elimu
      By ACTIVCT in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 4
      Last Post: 26th July 2011, 21:37
    3. Wizara ya Elimu inanishangaza!
      By tatanyengo in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 0
      Last Post: 13th April 2011, 09:31
    4. Nina wasiwasi na wataalamu tulionao kwenye wizara ya Elimu kuhusu Elimu zao
      By kabila01 in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 5
      Last Post: 3rd June 2009, 17:31

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...