| Find/Invite Friends | Register | Calendar | Search | Today's Posts | Mark Forums Read |
| FAQ | Members List | Bongo Flava | Zilipendwa | Taarab | Injili |
|
|||||||
| Jukwaa la Elimu (Education Forum) Educational discussions in here... If you have some College/School materials and you wanna give them to your fellows pls do that favour to them. Let them get educated here! Become a Member to enjoy more stuffs |
|
|
#1 | |||||||||||
|
||||||||||||
|
Views: 16418
|
||||||||||||
|
#2
|
||||||||||||
|
||||||||||||
__________________
ONE OF THE STRONGEST WEAPONS IS DIALOGUE |
||||||||||||
|
#3
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Bodi ya mikopo hata ije na vigezo vya aina gani itakuwa ni vigumu kubadilika kama mambo ya msingi hayaguswi:
1. Wale waliosoma kwa mikopo kuna haja ya kuwekewa utaratibu warudishe. Ni rahisi bila hata hivyo vitambulisho vya taifa inawezekana. Kwa mfano ikiwekwa sheria/kanuni kwamba kila mwajiri wa Tanzania anaeajiri 'graduate' wa vyuo vikuu lazima afanye makato maalum kwa mfanyakazi huyo yatakayopelekwa TRA/MAMLAKA MPYA YA KUKUSANYA FEDHA HIZI ZA MALIPO YA MKOPO na mlipaji awe ametia saini kabisa kukubali kisheria kwamba analipa mkopo wake. Kiwe ni kiwango kidogo kinachoendana na mshahara wa mhusika. 2. Ikifanyika hivyo manake ni kuwa kutakuwa na hela toka kwa wananchi wenyewe waliowahi kuchukua mkopo, ambao watakuwa wanafadhili wanafunzi wengine. Kutakuwa na mzunguko maalum wa fedha zinazolipwa na kukopesha wanafunzi wengine. Hii ndio ilivyo kwa STUDENT LOANS COMPANY hapa Uingereza. 3. Nijuavyo ni kuwa tuna wanafunzi kidogo sana [tunahitaji vyuo vingi] ambao honestly ukiangalia kwa makini wangeweza kabisa kulipwa wote kwa asilimia mia moja bila kuathiri sekta nyingine. Kama tungekuwa tunazingatia kuwa hizi fedha ni mikopo sio misaada, niliwahi kuandika huko nyuma kuwa ukiangalia ni kama msaada kwa vile hamna utaratibu wa kurudisha. Kama wanafunzi japo elfu kumi waliowahi kupata mkopo wangekuwa wanarudisha kiasi cha shilingi elfu kumi tu kwa mwezi kila mmoja hii ingekuwa ni sawa na milioni mia moja kwa mwezi, bilioni moja nukta mbili kwa mwaka! Sasa hiki ni kiwango cha chini sana kuweka lakini tukiweka takwimu halisia ni kuwa tuna wanafunzi waliowahi kuchukua mkopo zaidi ya elfu kumi na wanaweza kulipa zaidi ya elfu kumi... 4. Kama shirika la mikopo ya wanafunzi lingefanya kazi kama mashirika ya NSSF,PSPF nk ingekuwa ni fursa nzuri kwao, wapewe mtaji kwa njia moja iweze kuwekeza na kuwakopesha wanafunzi kutoka matunda ya uwekezaji huo huku wakiendelea kukusanya malipo kwa upande mwingine. 5. Tukubali kwamba mambo ya mikopo yalipoanza hakukuwa na utaratibu mzuri wa kuchanganua nani alipwe nani asilipwe, nilipokuwa Dar miaka miwili iliyopita baadhi ya jamaa niliosoma nao Tambaza wakiwa wanafanya shahada ya pili walipewa mikopo! Kuna walakini katika mfumo huu. 6. Bado inawezekana kujipanga upya wakaweza kuanza vizuri in time for September. Vinginevyo tunaweza kuwa na vigezo vingiii lakini visisaidie... |
|
#4
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
idea nzuri lakini kuna maswal mengi yakuuuliza
|
|
#5
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Saidi uliyosema ni kweli acha hata UK bali Kenya wenyewe bodi ya mikopo ya vyuo vikuu inafanya kazi vizuri sana. Hapa waliparamia hii program bila ya maandalizi ya misingi both istitutional and legal aspects ili kuwaridhisha warold bank na IMF kwenye sera zao za cost sharing. Wanatakiwa wakae chini wapange zaidi, huu mfuko unaweza ukafanya kazi vizuri tuu kama mifuko mingine kama watarekebisha kasoro ambazo nadhani bado ni nyingi sana.
__________________
ONE OF THE STRONGEST WEAPONS IS DIALOGUE |
|
#6
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
mkuu Samvulachole hebu anika hayo maswali hapa nadhani hawa jamaa wa loan bord wakipita humu yanaweza kuwasaidia mkuu.
__________________
ONE OF THE STRONGEST WEAPONS IS DIALOGUE |
|
#7
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
kila siku mtasikia vigezo vya mikopo, hivi na hivi na vile. lakini mshawahi kusikia mtu yeyote mmoja tu unayemjua amepata huo mkopo ? mimi sijawahi
|
|
#8
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Hawa jamaa wanarudia makosa yaleyale. Unapotoa mashartia hayo leo karibia na mwezi wa June, uteuzi wa watakaopata mkopo utafanyika kwa muda gani na ni vipi wataweza kupitia na kuhakiki fomu zaidi ya elfu thelathini kama sio zaidi kwa muda huo.
Ushauri wangu masharti waliyoyatangaza sasa yatumike kwa watakaojiunga na vyuo 2008/2009 ambao watakiwe kuanza kufanya maombi ya awali mkopo tangia wakiwa kidato cha sita na baadae kuthibitisha maombi yao mara tu majibu ya kidato cha sita yatakapotoka. Hii itaipa bodi muda wa kutosha kufanya uchanganuzi wao kwa uhakika zaidi na utatoa nafasi kwa wanafunzi na wazazi kujipanga vizuri na majukumu yao. Tanzanianjema
__________________
NYENYERE ANAPO "MDHIBITI" SISIMIZI MBELE YA MSAFARA WA TEMBO |
|
#9
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Tatizo ni kuwa wengi wa hao wanaotakiwa kulipa walilazimishwa kujiunga na mpango huo wa mikopo katika hali fulani ya vitisho. Wengi walilazimishwa kujaza fomu hizo kama sharti la wao kurudi chuoni mara baada ya chuo haswa UDSM kufungwa kutokana na migomo mbalimbali inayohusiana na suala hilohilo la mikopo. Kitu ambacho kinabatilisha uwezo wa kisheria wa mikatba ya mikopo hiyo. Fomu zilizotumika zina makosa mengi kisheria na hata hiyo sheria inakiuka vifungu muhimu vya katiba. Yaani mikataba hiyo kwa kweli ni dhaifu sana kisheria na wala haihitaji mtikila kuipiga chini kabisa kisheria. Ni wazi tuna safari ndefu hapa...... Tanzanianjema
__________________
NYENYERE ANAPO "MDHIBITI" SISIMIZI MBELE YA MSAFARA WA TEMBO |
|
#10
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Bodi ya mikopo yenyewe ina mapungufu mengi mno.
Moja ni ukosefu wa watendanji waaminifu. Wengi wa watendaji wakuu ambao wamekuwa katika kazi hiyo kwa miaka mingi wanahusika na ulaji mkubwa wa mikopo na scholarship hewa kwa miaka mingi. Wale walioajiriwa karibuni wengi ni wajanjawajanja wa mjini na wengine wameingia humo kwa upendeleo kama kawaida yetu. Tunajuana maana tunatambiana sana mitaani. Sidhani kama wana uwezo wa kutenda majukumu yao kwa nidhamu inayohitajika ili kufanikisha zoezi hilo la uchambuzi wa waombaji wa mikopo hiyo. Vilevile bila ya watu binafsi kujitokeza na kusaidiwa na serikali kuanzisha mifuko binafsi ya kutoa mikopo kwa wanafunzi ni wazi Bodi ya Mikopo itakuwa inakinzwa na presha kubwa ya maombi kitu ambacho kinaongeza uwezekano wa rushwa na ubadhirifu. Tanzanianjema
«
Previous Thread
|
Next Thread
»
Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako! All times are GMT +3. The time now is 02:06 AM.
Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||