Attention Bodi Ya Mikopo Ya Elimu Ya Juu Kwa Wanafuzi(heslb) - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Education, Science & Technology Forums > Jukwaa la Elimu (Education Forum)


Jukwaa la Elimu (Education Forum) Educational discussions in here... If you have some College/School materials and you wanna give them to your fellows pls do that favour to them. Let them get educated here! Become a Member to enjoy more stuffs


Reply
 
LinkBack Thread Tools Display Modes
Old 23rd April 2007, 01:14 PM   #1
Elimu ya juu haki lazima ishinde!
HKiboka HKiboka is offline 23rd April 2007, 01:14 PM

Watanzania masikini wasiwe na wasiwasi kwani sisi watoto wao kamwe hatutakubali kunyanyaswa kwa sababu ya umasikini wetu, tumeanza na tutaendelea hadi dakika ya mwisho pale haki itakaposhinda dhulma.
Tunabaguliwa na wanasiasa kwa kuwatumia wasomi vibaraka na wanaotaka kujipendekeza ili wapewe madaraka.
Mkopo ni haki yetu ya kisheria kwani tuna vigezo kwa mujibu wa sheria na sisi kutodai ni sawa na kukubali dhulma itawale! tutadai mpaka kieleweke kamwe hatuwezi kupumbazika na ahadi za kisiasa zisizo na muda maalum wa utekelezaji. Kama tukishindwa kujitetea hata sisi wenyewe ni dhahiri kuwa hatutaweza kuitetea jamii yetu fukara pindi tutakapopata kazi. Kitu cha msingi ni wazazi kutuunga mkono si kutuona wahunu na wakorofi kama watuitavyo wanasiasa na wasomi vibaraka. Wazazi wanalipa kodi ili sote tupate huduma na si kugharamia safari na posho za viongozi ndumilakuwili waliowadanganya watanzania kuwa wataleta maisha bora kwa kila mmoja wao kitu kilchogeuka ndoto.
TUNAPASWA KUJIFUNZA KWA HILO!

HKiboka
Member
Points: 164,086, Level: 100 Points: 164,086, Level: 100 Points: 164,086, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Tue Feb 2007
Posts: 21
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Views: 16418
Reply With Quote
  #2  
Old 26th May 2007, 03:11 PM
Mtoto wa Mkulima Mtoto wa Mkulima is offline
Mtoto wa Mkulima has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 366,246, Level: 100 Points: 366,246, Level: 100 Points: 366,246, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Apr 2007
Posts: 960
Thanks: 0
Thanked 7 Times in 3 Posts
Rep Power: 24
Mtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enough
Default Bodi ya Mikopo na vigezo vipya

Quote:
Bodi ya mikopo elimu ya juu yaja na vigezo vipya

2007-05-26 10:27:41
Na Mwandishi Wetu


Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HELSB), imetangaza vigezo vipya vitakavyotumika kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ambavyo vitazingatia uwezo wa kiuchumi wa waombaji.

Kwa mujibu wa tangazo la HELSB lililotolewa kwenye vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, utaratibu huo mpya wa mikopo, utaanza kutumika mwaka wa masomo wa 2007/08.

Chini ya utaratibu huo, waombaji wamegawanywa katika makundi matano yaani A, B, C, D, E na F.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa, wanafunzi katika A watapata asilimia 100 ya mkopo, B asilimia 80 na waombaji wa kundi C, watapewa asilimia 60.

Iliongeza kuwa, waombaji katika kundi D, watalipiwa kwa asilimia 40, E watapewa asilimia 20 na kundi F ambao hawatakopeshwa hata senti.

Wanafunzi watakaokubaliwa mikopo hiyo watalipiwa gharama kadhaa ikiwemo mafunzo, posho ya chakula, malazi, tahadhari, tiba, vitabu na mafunzo ya vitendo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kupewa mkopo kutategemea uchambuzi na mchujo utakaofanywa ili kuona hali ya kiuchumi ya mwombaji, wazazi ama walezi wake na hivyo mikopo itatofautiana kutoka mwanafunzi mmoja hadi mwingine.

Utaoaji wa mikopo utafanywa kwa kuchunguza waombaji kwa utaratibu utakaotolewa na HELSB ambao hata hivyo haukufafanuliwa.

Aidha, Bodi imewaonya waombaji watakaobainika kutoa taarifa za uongo ama kwa maandishi au mazungumzo ambayo yataathiri taratibu za maombi ya mkopo, kuwa watapewa adhabu ya kifungo cha miezi sita au kulipa faini ya Sh. milioni 1.5.

Kadhalika, ilisema iwapo mwombaji atakuwa amepewa mkopo kutokana na udanganyifu, Bodi itauzuia na kuufuta mara moja na mhusika kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo, taarifa hiyo imesisitiza kuwa, utaratibu wa wanafunzi wa Kidato cha Sita waliofaulu Daraja la Kwanza kwa wanaume na Daraja la Kwanza na la Pili kwa wanawake, utaendelea kutumika katika utoaji wa mikopo hiyo.

Ilifafanua kuwa, kipaumbele kitatolewa kwa wanafunzi wanaosomea kozi za Tiba, Sayansi, Kilimo, Ualimu, Uhandisi na Teknolojia.

SOURCE: Nipashe
Wadau hii mnaiona je? linatekelezeka? je mambo kama haya kuwepo na vitambulisho vya uraia vyenye details za watu si ingerahisisha? Hofu yangu itakuwa ngumu kwa walengwa kupata mikopo kama ilivyokusudiwa.
__________________
ONE OF THE STRONGEST WEAPONS IS DIALOGUE
Reply With Quote
  #3  
Old 26th May 2007, 03:53 PM
Saidi Yakubu Saidi Yakubu is offline
Saidi Yakubu has no status.
Senior Member
Points: 217,238, Level: 100 Points: 217,238, Level: 100 Points: 217,238, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Mar 2006
Location: colchester,united Kingdom
Posts: 109
Thanks: 0
Thanked 6 Times in 1 Post
Rep Power: 25
Saidi Yakubu will become famous soon enoughSaidi Yakubu will become famous soon enoughSaidi Yakubu will become famous soon enoughSaidi Yakubu will become famous soon enoughSaidi Yakubu will become famous soon enoughSaidi Yakubu will become famous soon enoughSaidi Yakubu will become famous soon enoughSaidi Yakubu will become famous soon enough
Send a message via MSN to Saidi Yakubu Send a message via Yahoo to Saidi Yakubu
Default bodi inalenga nje ya goli

Bodi ya mikopo hata ije na vigezo vya aina gani itakuwa ni vigumu kubadilika kama mambo ya msingi hayaguswi:

1. Wale waliosoma kwa mikopo kuna haja ya kuwekewa utaratibu warudishe. Ni rahisi bila hata hivyo vitambulisho vya taifa inawezekana. Kwa mfano ikiwekwa sheria/kanuni kwamba kila mwajiri wa Tanzania anaeajiri 'graduate' wa vyuo vikuu lazima afanye makato maalum kwa mfanyakazi huyo yatakayopelekwa TRA/MAMLAKA MPYA YA KUKUSANYA FEDHA HIZI ZA MALIPO YA MKOPO na mlipaji awe ametia saini kabisa kukubali kisheria kwamba analipa mkopo wake. Kiwe ni kiwango kidogo kinachoendana na mshahara wa mhusika.

2. Ikifanyika hivyo manake ni kuwa kutakuwa na hela toka kwa wananchi wenyewe waliowahi kuchukua mkopo, ambao watakuwa wanafadhili wanafunzi wengine. Kutakuwa na mzunguko maalum wa fedha zinazolipwa na kukopesha wanafunzi wengine. Hii ndio ilivyo kwa STUDENT LOANS COMPANY hapa Uingereza.

3. Nijuavyo ni kuwa tuna wanafunzi kidogo sana [tunahitaji vyuo vingi] ambao honestly ukiangalia kwa makini wangeweza kabisa kulipwa wote kwa asilimia mia moja bila kuathiri sekta nyingine. Kama tungekuwa tunazingatia kuwa hizi fedha ni mikopo sio misaada, niliwahi kuandika huko nyuma kuwa ukiangalia ni kama msaada kwa vile hamna utaratibu wa kurudisha. Kama wanafunzi japo elfu kumi waliowahi kupata mkopo wangekuwa wanarudisha kiasi cha shilingi elfu kumi tu kwa mwezi kila mmoja hii ingekuwa ni sawa na milioni mia moja kwa mwezi, bilioni moja nukta mbili kwa mwaka! Sasa hiki ni kiwango cha chini sana kuweka lakini tukiweka takwimu halisia ni kuwa tuna wanafunzi waliowahi kuchukua mkopo zaidi ya elfu kumi na wanaweza kulipa zaidi ya elfu kumi...

4. Kama shirika la mikopo ya wanafunzi lingefanya kazi kama mashirika ya NSSF,PSPF nk ingekuwa ni fursa nzuri kwao, wapewe mtaji kwa njia moja iweze kuwekeza na kuwakopesha wanafunzi kutoka matunda ya uwekezaji huo huku wakiendelea kukusanya malipo kwa upande mwingine.

5. Tukubali kwamba mambo ya mikopo yalipoanza hakukuwa na utaratibu mzuri wa kuchanganua nani alipwe nani asilipwe, nilipokuwa Dar miaka miwili iliyopita baadhi ya jamaa niliosoma nao Tambaza wakiwa wanafanya shahada ya pili walipewa mikopo! Kuna walakini katika mfumo huu.

6. Bado inawezekana kujipanga upya wakaweza kuanza vizuri in time for September. Vinginevyo tunaweza kuwa na vigezo vingiii lakini visisaidie...
Reply With Quote
  #4  
Old 26th May 2007, 04:19 PM
Samvulachole Samvulachole is offline
Samvulachole has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 985,986, Level: 100 Points: 985,986, Level: 100 Points: 985,986, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Sun Oct 2006
Posts: 741
Thanks: 0
Thanked 2 Times in 1 Post
Rep Power: 25
Samvulachole will become famous soon enoughSamvulachole will become famous soon enoughSamvulachole will become famous soon enoughSamvulachole will become famous soon enoughSamvulachole will become famous soon enoughSamvulachole will become famous soon enoughSamvulachole will become famous soon enoughSamvulachole will become famous soon enough
Default

idea nzuri lakini kuna maswal mengi yakuuuliza
Reply With Quote
  #5  
Old 26th May 2007, 06:16 PM
Mtoto wa Mkulima Mtoto wa Mkulima is offline
Mtoto wa Mkulima has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 366,246, Level: 100 Points: 366,246, Level: 100 Points: 366,246, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Apr 2007
Posts: 960
Thanks: 0
Thanked 7 Times in 3 Posts
Rep Power: 24
Mtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enough
Default

Saidi uliyosema ni kweli acha hata UK bali Kenya wenyewe bodi ya mikopo ya vyuo vikuu inafanya kazi vizuri sana. Hapa waliparamia hii program bila ya maandalizi ya misingi both istitutional and legal aspects ili kuwaridhisha warold bank na IMF kwenye sera zao za cost sharing. Wanatakiwa wakae chini wapange zaidi, huu mfuko unaweza ukafanya kazi vizuri tuu kama mifuko mingine kama watarekebisha kasoro ambazo nadhani bado ni nyingi sana.
__________________
ONE OF THE STRONGEST WEAPONS IS DIALOGUE
Reply With Quote
  #6  
Old 26th May 2007, 06:21 PM
Mtoto wa Mkulima Mtoto wa Mkulima is offline
Mtoto wa Mkulima has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 366,246, Level: 100 Points: 366,246, Level: 100 Points: 366,246, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Apr 2007
Posts: 960
Thanks: 0
Thanked 7 Times in 3 Posts
Rep Power: 24
Mtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enoughMtoto wa Mkulima will become famous soon enough
Default

mkuu Samvulachole hebu anika hayo maswali hapa nadhani hawa jamaa wa loan bord wakipita humu yanaweza kuwasaidia mkuu.
__________________
ONE OF THE STRONGEST WEAPONS IS DIALOGUE
Reply With Quote
  #7  
Old 26th May 2007, 06:44 PM
KadaMpinzani's Avatar
KadaMpinzani KadaMpinzani is offline
KadaMpinzani has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 773,793, Level: 100 Points: 773,793, Level: 100 Points: 773,793, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Wed Jan 2007
Location: Chadema Restaurant
Posts: 5,013
Thanks: 2
Thanked 12 Times in 9 Posts
Rep Power: 33
KadaMpinzani will become famous soon enoughKadaMpinzani will become famous soon enoughKadaMpinzani will become famous soon enoughKadaMpinzani will become famous soon enoughKadaMpinzani will become famous soon enoughKadaMpinzani will become famous soon enoughKadaMpinzani will become famous soon enoughKadaMpinzani will become famous soon enough
Default

kila siku mtasikia vigezo vya mikopo, hivi na hivi na vile. lakini mshawahi kusikia mtu yeyote mmoja tu unayemjua amepata huo mkopo ? mimi sijawahi
Reply With Quote
  #8  
Old 26th May 2007, 07:22 PM
omarilyas omarilyas is offline
omarilyas has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 253,938, Level: 100 Points: 253,938, Level: 100 Points: 253,938, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Jan 2007
Location: Morogoro
Posts: 1,611
Thanks: 31
Thanked 109 Times in 57 Posts
Rep Power: 27
omarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enough
Send a message via MSN to omarilyas
Default

Hawa jamaa wanarudia makosa yaleyale. Unapotoa mashartia hayo leo karibia na mwezi wa June, uteuzi wa watakaopata mkopo utafanyika kwa muda gani na ni vipi wataweza kupitia na kuhakiki fomu zaidi ya elfu thelathini kama sio zaidi kwa muda huo.

Ushauri wangu masharti waliyoyatangaza sasa yatumike kwa watakaojiunga na vyuo 2008/2009 ambao watakiwe kuanza kufanya maombi ya awali mkopo tangia wakiwa kidato cha sita na baadae kuthibitisha maombi yao mara tu majibu ya kidato cha sita yatakapotoka. Hii itaipa bodi muda wa kutosha kufanya uchanganuzi wao kwa uhakika zaidi na utatoa nafasi kwa wanafunzi na wazazi kujipanga vizuri na majukumu yao.


Tanzanianjema
__________________
NYENYERE ANAPO "MDHIBITI" SISIMIZI MBELE YA MSAFARA WA TEMBO
Reply With Quote
  #9  
Old 26th May 2007, 07:35 PM
omarilyas omarilyas is offline
omarilyas has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 253,938, Level: 100 Points: 253,938, Level: 100 Points: 253,938, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Jan 2007
Location: Morogoro
Posts: 1,611
Thanks: 31
Thanked 109 Times in 57 Posts
Rep Power: 27
omarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enough
Send a message via MSN to omarilyas
Default

Quote:
View Post
1. Wale waliosoma kwa mikopo kuna haja ya kuwekewa utaratibu warudishe. Ni rahisi bila hata hivyo vitambulisho vya taifa inawezekana. Kwa mfano ikiwekwa sheria/kanuni kwamba kila mwajiri wa Tanzania anaeajiri 'graduate' wa vyuo vikuu lazima afanye makato maalum kwa mfanyakazi huyo yatakayopelekwa TRA/MAMLAKA MPYA YA KUKUSANYA FEDHA HIZI ZA MALIPO YA MKOPO na mlipaji awe ametia saini kabisa kukubali kisheria kwamba analipa mkopo wake. Kiwe ni kiwango kidogo kinachoendana na mshahara wa mhusika.

2. Ikifanyika hivyo manake ni kuwa kutakuwa na hela toka kwa wananchi wenyewe waliowahi kuchukua mkopo, ambao watakuwa wanafadhili wanafunzi wengine. Kutakuwa na mzunguko maalum wa fedha zinazolipwa na kukopesha wanafunzi wengine. Hii ndio ilivyo kwa STUDENT LOANS COMPANY hapa Uingereza.

Kaka Said mbona haya yote yapo katika sheria ya kuanzisha bodi ya mikopo 2004 na kutiwa sahihi na rais mwaka 2005. Ipitie katika website ya serikali ama ile ya bunge. Hata ufuatiliaji wa hilo tayari umeshika kasi.

Tatizo ni kuwa wengi wa hao wanaotakiwa kulipa walilazimishwa kujiunga na mpango huo wa mikopo katika hali fulani ya vitisho. Wengi walilazimishwa kujaza fomu hizo kama sharti la wao kurudi chuoni mara baada ya chuo haswa UDSM kufungwa kutokana na migomo mbalimbali inayohusiana na suala hilohilo la mikopo. Kitu ambacho kinabatilisha uwezo wa kisheria wa mikatba ya mikopo hiyo.

Fomu zilizotumika zina makosa mengi kisheria na hata hiyo sheria inakiuka vifungu muhimu vya katiba. Yaani mikataba hiyo kwa kweli ni dhaifu sana kisheria na wala haihitaji mtikila kuipiga chini kabisa kisheria.


Ni wazi tuna safari ndefu hapa......

Tanzanianjema
__________________
NYENYERE ANAPO "MDHIBITI" SISIMIZI MBELE YA MSAFARA WA TEMBO
Reply With Quote
  #10  
Old 26th May 2007, 07:46 PM
omarilyas omarilyas is offline
omarilyas has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 253,938, Level: 100 Points: 253,938, Level: 100 Points: 253,938, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Wed Jan 2007
Location: Morogoro
Posts: 1,611
Thanks: 31
Thanked 109 Times in 57 Posts
Rep Power: 27
omarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enoughomarilyas will become famous soon enough
Send a message via MSN to omarilyas
Default

Bodi ya mikopo yenyewe ina mapungufu mengi mno.

Moja ni ukosefu wa watendanji waaminifu. Wengi wa watendaji wakuu ambao wamekuwa katika kazi hiyo kwa miaka mingi wanahusika na ulaji mkubwa wa mikopo na scholarship hewa kwa miaka mingi.

Wale walioajiriwa karibuni wengi ni wajanjawajanja wa mjini na wengine wameingia humo kwa upendeleo kama kawaida yetu. Tunajuana maana tunatambiana sana mitaani. Sidhani kama wana uwezo wa kutenda majukumu yao kwa nidhamu inayohitajika ili kufanikisha zoezi hilo la uchambuzi wa waombaji wa mikopo hiyo.

Vilevile bila ya watu binafsi kujitokeza na kusaidiwa na serikali kuanzisha mifuko binafsi ya kutoa mikopo kwa wanafunzi ni wazi Bodi ya Mikopo itakuwa inakinzwa na presha kubwa ya maombi kitu ambacho kinaongeza uwezekano wa rushwa na ubadhirifu.

Tanzanianjema
__________________
NYENYERE ANAPO "MDHIBITI" SISIMIZI MBELE YA MSAFARA WA TEMBO
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
attention, bodi, elimu, juu, mikopo, wanafuziheslb


Currently Active Users Viewing This Thread: 2 (0 members and 2 guests)
 
Thread Tools
Display Modes

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Majambazi Arusha: Mabomu, Bunduki, Risasi, Bastola - Hii ni Kashfa JWTZ Hasara Jukwaa la Siasa 225 11th December 2009 03:53 PM
Ni wakati wa kuacha woga! Invisible Habari na Hoja mchanganyiko 6 4th June 2009 10:01 PM
[Economist]: President Kikwete's hard road ahead Alpha Jukwaa la Siasa 19 2nd September 2007 02:37 PM
Majibu ya Mwanakijiji kwa Bodi ya Mikopo Halisi Jukwaa la Elimu (Education Forum) 36 22nd July 2007 08:24 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 02:06 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com