Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

    Report Post
    Results 1 to 8 of 8
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,181
      Rep Power : 19209
      Likes Received
      8137
      Likes Given
      26606

      Default Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      BI.ROSEMARY OTHUMANI [54] mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, amejikuta akipata aibu ya mwaka kwa watoto na majirani zake baada ya vijana wawili kupigana na kutoana ngeu kwa madai ya kila mmoja akidai ni mpenzi wa mama huyo
      Tukio hilo la kusisimua na kwa upande mwingine la kusikitisha lilitokea jana majIra ya saa 1 jioni nyumbani kwa mwanamke huyo

      Mtandao huu ulishuhudia nusu mpambano huo na watu wengi wakiwa wamepatwa na bumbuwazi kutokana na tukio hilo

      Mmoja wa shuhuda ambaye aliwahi kuona picha kamili aliyejitambulisha kwa jina la Saada [27] ambaye jirani na mama huyo alidai kuwa mama huyo aligonganisha magari na ndio chanzo cha kutokea kwa ugomvi huo

      Ameda kuwa, mama huyo mjane miaka mitano iliyopita baada ya kupoteza mume wake kwa maradhi ya kansa amekuwa na tabia ya kujihusisha na mapenzi na vijana wadogo ambao ni saizi ya watoto wake tabia ambayo alishazoeleka nayo mtaani hapo

      Amedai, tabia hiyo ambayo watoto wake wa kike walishaipigia makelele bila ya mafanikio na mama yao huyo kudai mapenzi hutua sehemu yoyote na mwishowe watoto walinawa mikono kuhusiana na suala hilo la kumuonya mama yao

      Amedai, mama huyo alikuwa akijihusisha kimapenzi na kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Beka [30] na watu wengi walifahamu mahusiano yao na baadae baada ya kuzidiwa alimtaka kijana huyo ahamie nyumbani kwake na kudaiwa alihamia

      Mpashaji habari hii bi. Saada aliendelea kupasha habari kwenye mtandao huu kuwa, Beka baada ya miezi kadhaa alidaiwa alifunguliwa biashara na mama huyo ambapo ilimladhimu asafiri mara kwa mara kusimamia biashara hizo

      Imedaiwa kuwa, wakati mwingine husafiri na huchukua hata mwezi mmoja au mawiki kadhaa katika biashara hizo

      Imedaiwa, mama huyo alitumia mwanye wa kusafiri kwa Beka kwa kujihusisha kimapenzi na kijana mwingine kwa kudhani amepata bahati ya mtende kwa kutumia mali za mama huyo bila kujua kama ana mume mwenza

      Imedaiwa kuna baadhi ya watu waliokuwa wakimuona na mama huyo walijaribu kumuibia siri lakini kijana huyo alidhani huenda ni kumchukia kulingana na anavyojihusisha kimapenzi na mwanamke aliyemzidi umri

      Imeendelea kupashwa kuwa kijana huyo alikuwa akifika nyumbani kwa mama huyo mara chache

      Siku ya tukio, ambapo waswahili walisema lisemwalo lipo ama halipo basi liko njiani, Beka alirudi jijini Dar es salaam akitokea mkoani Mwanza kwa ndege ya Precision Air na alitinga jijini humu majira ya saa 10 jioni bila ya kumpa taarifa mama huyo kama anarudi

      Ndipo majira ya saa 12 Beka aliwasili nyumbani kwa mama huyo bila ya taarifa kwa kujiamini, huku akimpa mshituko mwenyeji wake kwa kutokutoa taarifa

      Mbaya zaidi mama huyo alimpa mwaliko Yule kijana mwingine aje nyumbani kwake kwa siku hiyo ndipo hapo magari yalipogongana na kuleta mshike mshike nguo kuchanika mtaani hapo huku kila mmoja akitunisha misuli yake na kila mmoja akidai kummiki huyo mama

      Vijana hao walikutana huku kila mmoja akiwa anamshangaa mwenzake na mama huyo alimtumia ujumbe mfupi wa maneno Yule kijana mwingine kwa kumwambia aondoke kwa muda huo kwani alifikwa na mgeni ujumbe ambao Beka aliushitukia na kudaka simu ya mkononi ya kijana huyo na kugundua kinachoendelea na kuanza kumkunja na hatma yake ugomvi kukua

      Hali ilikuwa mbaya kwa mama huyo na kupelekea kuomba msaada kwa walinzi na majirani waje kugombelezea ugomvi huo na hatma yake watoto waliokuwa wakiishi karibu nae walipigiwa simu na majirani na kufika hapo na matokeo askari waliingilia ugomvi huo

      Mama huyo alichukuliwa ili kwenda kutoa maelezo kituo cha polisi na kuwaacha watoto na wajukuuu wakiwa na aibu tele mtaani hapo

      Imedaiwa mama huyo ni mfanyabiashara ambapo biashara hiyo haijawekwa wazi, na marehemu mume wake aliweza kumuachia mali zikiwemo nyumba mbili na magari mawili ya kutembelelea gari moja ilidaiwa alichukua binti yake mkubwa aliyedaiwa kuwa na umri wa miaka 32

      Mama huyo alijaaliwa kuwa na watoto watatu ambapo wawili wa kike na mmoja ni wa kiume mdogo aliyedaiwa kuwa mwaka wa nne UDOM

      Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Dar
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. Miaka 50

    3. #2
      Kibwebwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2012
      Posts : 279
      Rep Power : 403
      Likes Received
      30
      Likes Given
      11

      Default Re: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      Makubwa haya

    4. #3
      amiride's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th August 2011
      Posts : 187
      Rep Power : 428
      Likes Received
      31
      Likes Given
      4

      Default Re: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      surua mwenzie mtoto

    5. #4
      Man KKK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Location : Ndani ya Laptop
      Posts : 788
      Rep Power : 517
      Likes Received
      94
      Likes Given
      45

      Default Re: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      mbona ndo life style ya masharobalo wengi tu daslam hii

    6. #5
      Luluka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2011
      Posts : 576
      Rep Power : 565
      Likes Received
      117
      Likes Given
      74

      Default Re: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      Dah!aibu ya mwaka hiyo!

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Kilahunja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th December 2011
      Posts : 935
      Rep Power : 562
      Likes Received
      161
      Likes Given
      3

      Default Re: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      Kila cku nyiny tu ndo m2chue kikongwe miaka 64 na bint wa 20, na sisi zam ye2 jaman, hak sawa mnachoshangaa nini?

    9. #7
      kimeloki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th July 2012
      Posts : 554
      Rep Power : 456
      Likes Received
      56
      Likes Given
      6

      Default Re: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      dunia kwa sasa ipo upside down.

    10. #8
      Kunta Kinte's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Posts : 2,570
      Rep Power : 2536
      Likes Received
      604
      Likes Given
      762

      Default Re: Masharobaro wagombania penzi la bi mkubwa - Da

      Huyu bado hajaingia menopause tu anangoja nini?
      Have patience with all things, but chiefly have patience with yourself.- Saint Francis de Sales

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...