Nakumbuka siku moja nikiwa o-level form 1 kibaha sec,si unajua ule utaratibu wa misosi,watu kadhaa mnaunda kikosi,maybe watu 13 mnakuwa na dishi lenu moja la ugali/wali na moja la mboga.
Ugumu ulikuwa unatokea ikifika zamu yako, unafuata msosi jikoni,unagawa kwa wenzio na kuosha madishi na kuyarudisha jikoni.siku moja jamaa alipojua ni zamu yake akaamua kutokuja kabisa.
Tulikuwa form one 5,form two 4 na form four 2.Form four mmoja akashauri form one(nyoya,salamanda,nyoka) mmoja ajitolee lakini tuligoma wote. Wale form iv walijitolea ku-save msosi,ila walichofanya sitasahau.
Waligawana msosi wao wawili wakatosheka, baada ya hapo walimwaga wali wote uliobaki chini na mchuzi wakaugeuza maji ya kunawa,kiufupi tulipigwa dash.
Dah!vp wewe ulipokuwa form one,tupe kisanga kilichokukuta!
Nakumbuka enzi za afande miraji makongo basi kulikuwa na mti wa maembe karibu na canteen ya shule ile kuona maembe yameiva akajua kuna madenti waroho wa maembe basi akaandika kibao 'ANGUA EMBE' akakitundika juu yake. Looh hakuna hata dent aliyedhubutu kusogea karibu. Kulikua na matoz wa pre form 5 walikuja kurudia masomo kuona kile kibao wakajua ruksa wakapanda kuangua embe afande miraj akawakamata kwenda kuwapa adhabu wakajua ni kwenda kupewa msitu kufyeka cha kushangaza kawapeleka kwenye ofis yake ilikuwa banda la mabati mbele yake kulikuwa na kisima cha taka basi kawaambia nisubirin hapa aingia ndan karudi na redio kaweka Taarab(mipasho) akawaambia haya vidole juu na muanze kuimba atakae onyesha mautundu atasamehewa.ilkuwa very funy
nakumbuka shule moja ya gals,form5 kpnd hicho, maji yalikuwa ya shida kinoma! Kisimani ilikuwa ni kugombana daily! Na kuibiana maji ilikua kawaida! Sasa ili kukomoana mtu asikuibie maji ikawa watu wanaloweka chupi zao chafu ndani ya ndoo ya maji ili yasiibiwe! Cha kushangaza asbh mtu akiamka anakuta chupi imetolewa,imewekwa kando,na maji yameogewa kama kawaida!
Last edited by Nyangiez; 20th April 2011 at 09:06.
Kwa wale PUGU BOYZ wanakumbuka sana kwenda pondi na foleni za mihogo kwa mama pendo(RIP),bila kusahau watu tulivyokuwa tunakata weeks bila kuoga coz shule haina maji...mvua ikinyesha ndo kila mtu anavua nguo akaoge kwenye mvua.
kwa wale pugu boyz wanakumbuka sana kwenda pondi na foleni za mihogo kwa mama pendo(rip),bila kusahau watu tulivyokuwa tunakata weeks bila kuoga coz shule haina maji...mvua ikinyesha ndo kila mtu anavua nguo akaoge kwenye mvua.
daaah umenikumbusha mbali wewe, rough paper zilikuwa muhimu sana pugu
Mi nilikuwa nashangaa sana,Tanga tech siku ya vyoo vya shimo kuzibuliwa,yanatolewa mawe,magunzi,sahani,vijiko,vik ombe n.k,sasa sijui watu wanakula msosi na kunywa chai chooni au hivi ndo vifaa alternative vya kutawadhia,na cha ajabu zaidi ukutani kuna maandishi,herufi zimeundwa vizuri sana kwa kinyesi!
Mkuu umegusa penyewe, namkumbuka "Braza" Mpande na mambo yake ya kuja kuamsha watu kwenda mchaka mchaka. Kuna siku alikuja na kali ya mwaka: Eti akiwaona watu mjini alikuwa anawakariri uso, sasa watu wamegundua wakimwona tu wanageuka upesi na anashindwa kuwakariri uso, basi akasema atakuwa anakariri visogo. Baada ya majuma kadhaa akasema wanafunzi wakimwona basi wanageuka na kuvua mashati wanayafunga kichwani ili kuficha visogo, sasa akasema basi nitakuwa nakariri (ashakum siyo matusi) ******, nikiliona linaenda hivi au hivi basi nitajua ni la fulani,,, alikuja kutuacha hoi siku alipo-prove jinsi mbinu yake inavyofanya kazi kwa kumtolea mfano jamaa mmoja aliyemwona town Moshi,,
Yule Mwalimu sintokaa nimsahau aisee..
ha ha ha ha ha ha I won't forget Mr. Mpande either. anavyoongea " ebana, nasema hivi, kesho asubuhi, wote mchaka mchaka" wa Moshi Tech watajua nachomaanisha.
"God is Good......All the time, and All the time.....God is Good"
kazi ilikuwako iyunga wazee!WAULIZENI JAMAA (KINA HEMSO KABOGI,NIGA NA WENGINEO) WALE WALIOTOKA TAMBAZA BAADA YA KUFANYA FUJO MIAKA YA 94/5 NA KUHAMISHIWA IYUNGA!!WALIBEBESHWA MIZINGA yao toka stendi ya tazara mpaka shuleni iyunga Tech (aka Kambi ya Jeshi) kipindi hicho chini ya Headmaster Mwaipopo!!
Mkwawa Complex and Casino, I just love it...Nilikwenda kufanya 'hijja' pale but was sad coz sasa imekuwa university. The government needs to preserve some sites for historic interests.
Kweli mkuu hasa yale maeneo ya bomba tatu na kibanda simama....
Mkuu umegusa penyewe, namkumbuka "Braza" Mpande na mambo yake ya kuja kuamsha watu kwenda mchaka mchaka. Kuna siku alikuja na kali ya mwaka: Eti akiwaona watu mjini alikuwa anawakariri uso, sasa watu wamegundua wakimwona tu wanageuka upesi na anashindwa kuwakariri uso, basi akasema atakuwa anakariri visogo. Baada ya majuma kadhaa akasema wanafunzi wakimwona basi wanageuka na kuvua mashati wanayafunga kichwani ili kuficha visogo, sasa akasema basi nitakuwa nakariri (ashakum siyo matusi) ******, nikiliona linaenda hivi au hivi basi nitajua ni la fulani,,, alikuja kutuacha hoi siku alipo-prove jinsi mbinu yake inavyofanya kazi kwa kumtolea mfano jamaa mmoja aliyemwona town Moshi,,
Yule Mwalimu sintokaa nimsahau aisee..
Mkuu umenikumbusha sana Moshi Tech...
Kuna siku mpande alikuja dom letu no. 39 Karume kule na kutudaka kisa eti mshkaji mmoja alizima taa wakati tu kaingia bwenini. Sasa akatupeleka pale TYL ofisini na kuanza mikwara na vibao kibao kwa yule mshkaji ili amtaje aliezima taa. Jamaa kuona vibao akamtaja mshkaji wangu basi alikula vibaooo na wakati akiendelea kula vibao akamwambia Mpande... "..Basi ticha umeshinda..." Dah!! Utafikiri ndo alichochea mafuta kwenye moto, alikula makofi, vichwa, nakoz za kufa mtu mpaka tukataka kumzuia ticha ila mshkaji mwingine akadai tuache tu. Iliniuma sana hata kesho yake siku tuliyokuwa tunamaliza shule mshkaji aliepigwa akataka tukamuage ila nikamchomolea as hasira zilikuwa bado zipo..
Kwa waliosoma ile shule hawatomsahau Mpande aisee...
nikiwa Makuyuni sec(jkt) arusha 1997 kama njuka jamaa wa bweni la serengeti walijaza -----(miiba midogo dogo) kitandani kwangu
natoka prepo najilaza wee nliwashwa usiku mzima nlitamani kurudi home.Jion yake nli miss ngama(ugali) na asubuhi tulikuwa tunapiga uji nao nika miss sasa kuna mke wa mwl anauza maandazi ikabidi nikanunue 10 nipige,wakajua nna poket ya kutosha usiku wakajafungua mzinga
wangu(tranker) wakapiga sachi kumbe nlikuwa nimeweka kwa ticha basi waka komba blu band na sukari wakafunga vizuri(walikuwa wanatumia funguo malaya kufungua mizinga ya watu na hicho kitendo walikuwa wanaita kut..mbesha na kulikuwa na watu maalumu wanaenda taun kutafuta key kwa kufuli ngumu dduuu tulikuwa tunalimishwa hatua 4 kwa 70 urefu du kupalilia robo heka baada yakutoka class mchana ilikuwa kawaida tu,ukifanya kosa unapewa 1/2heka nawamiss sana wamasai akina loning'o, melemi,menga'ang'ie wanga komesha,mzee ole medutiek ................
KAMA UNA HELA NYINGI NIGAWIE, NAMI NIMILIKI NYUMBA NA KA USAFIRI
KAMA WEWE!
Enzi hizo Mkwawa Complex, ni marufuku kupeleka chakula bwenini ila watu wanapeleka ki mtindo. Za mwizi arobaini kaka mmoja (sb Majura) akakamatwa asubuhi na kikombe cha uji anaingia nacho dom, akapewa adhabu ya kufyeka maeneo ya dining hole na kusafisha mtaro wa maji machafu. Wakati anafanya zoezi hilo akang'atwa na manyigu akavimba uso kinoma. Ikawa balaa 1kwa1, majura likawa sio jina tena bali tendo. ukileta za kuleta utaambiwa "usituletee ujura wako hapa", lione jura hilo. Yaani raha na karaha mumo.
nakumbuka mwaka 1998 nikiwa form 3 pale vunjo sekondari tulimvamia mpishi tukamwambia kuwa tunauza sweta ya pull neck kwa bai ya mia tano.jamaa akaingia kingi si akajaribi na ilikuwa mida ya saa 6 na nusu huku tukiwa tunasubiri msosi jamaa alipojaribu sweter si akabana kwenye shingo isiweze kutoka ndo washkaji tukala mawali ya walimu kibao na ndo ikawa mwisho wa wanafunzi kwenda jikoni
Dah i can't 4ge da girls. Nilipokua adv Bwiru boyz,waschana wa bwiru gals walikua wanakuja mara kwa mara kucheza mpira wa miguu kwenye uwanja wa boyz wakiwa na waalim wao 2kawa 2nawashangilia bana,sasa cku moja walikua na mechi na watoto wa seminary watoto wa Loreto. Waliingia na gari yao. Wakati huo hawa bwiru galz wao wanakanyaga guu 2. Kuwaona Loreto wanashuka garin 2 wa2 walishangilia balaa,wakaanza kuwazomea girlz,girls nao waka2zomea,aise zilichumwa fimbo. Walitembezewa fimbo,men it was so funny. Wakarudi kwao wanakimbizwa na fimbo huku wakiambiwa
"Tokeni hapa mnatuchafulia hewa 2 hapa,mnataka kuchafua watoto wanaogea dasani..." na kula fimbo zaidi,na mahusiano ya 'bugi' sis na wao likafa kwanzia hapo,dah men it was the funniest thing i've ever seen.
Mkuu umenikumbusha sana Moshi Tech...
Kuna siku mpande alikuja dom letu no. 39 Karume kule na kutudaka kisa eti mshkaji mmoja alizima taa wakati tu kaingia bwenini. Sasa akatupeleka pale TYL ofisini na kuanza mikwara na vibao kibao kwa yule mshkaji ili amtaje aliezima taa. Jamaa kuona vibao akamtaja mshkaji wangu basi alikula vibaooo na wakati akiendelea kula vibao akamwambia Mpande... "..Basi ticha umeshinda..." Dah!! Utafikiri ndo alichochea mafuta kwenye moto, alikula makofi, vichwa, nakoz za kufa mtu mpaka tukataka kumzuia ticha ila mshkaji mwingine akadai tuache tu. Iliniuma sana hata kesho yake siku tuliyokuwa tunamaliza shule mshkaji aliepigwa akataka tukamuage ila nikamchomolea as hasira zilikuwa bado zipo..
Kwa waliosoma ile shule hawatomsahau Mpande aisee...
Watu waliosoma tanga tech hawatamsahau mr.mdoe.Nakumbuka ile mida ya saa 12 jioni tulikuwa na utaratibu wa roll call.Basi inapowadia saa 12,wanaume tulikuwa na tabia ya kujongea taratibu eneo la parade,basi akiwaona kitaa tu,utamwona anavyotoka nduki kuwa overtake ili akahesabishe roll call kabla hamjafika,halafu alikuwa na'ikibinda nkoi'fulani kama demu,yaani alikuwa na visa!
Mkwawa high school kwa sisi tuliosoma o level seminari tulipata shida sana nyakati za mwanzo kusoma na mabinti hasa nyakati za prepo. Kombolela hasa siku za jumatatu katika mabweni ya wavulana...
Enzi hizo headmaster nani, mr mbao? Nakumbuka ili kutatua tatizo la purukushani za chakula mesini makanyagio ilikua kimbilio langu la kudumu asubuhi, mchana na usiku.
Mi nakumbuka mwaka 1994 tukiwa sengerema secondary a.k.a Singapore, ile tunaingia form 5 kuna mwalimu mmoja tulimkuta anaitwa mwalimu BUGA.kumbe bwana lilikuwa jina la utani...siku moja akanikamata sijaenda parade, basi akawa ananiuliza namjua yeye ni nani? me kwa kujiamini nikamwambia wewe si mwalimu BUGA.. aiseeeeeee nilichezea kichapo cha hatari..kumbe bwana BUGA lilikuwa jina la utani,,kwa vile alikuwa anavaa suruali zile BUGA..yaani ile juu imebana afu chini umemwagika..ahahaha sitasahau kabisa..
Huruma si angeenda tu kumwambia mwl mkuu mkasa wote kuliko kuingia toilet
By safety last
nakumbukuka niko sec siha ,siku moja jioni kuna jamaa kutoka kigoma alienda kujisadia ,na alikuwa na ada kwenye walet ghafla ikadondoka chooni,alikuwa form 6,akaanza kutindua choo kwa pembeni, akaingia na kuitoa ada ,bahati nzuri kulikuwa na vyoo vya kulenga set mbili.alinyoa nywele zote mpaka kwenye kope,he had a strange personality.
I submit to you that if a man hasn't discovered something that he will die for he isn't fit to live.
Follow Us Here