Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Magonjwa ya Zinaa

    Report Post
    Results 1 to 17 of 17
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,869
      Rep Power : 19446
      Likes Received
      8653
      Likes Given
      28271

      Default Magonjwa ya Zinaa

      Aina za magonjwa ya zinaa, ishara na dalili zake

      STDs ni magonjwa ya zinaa, pia hujulikana kama maambukizo ya zinaa (STIs). Kwa maneno mengine ni maaambukizo yanayopitishwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kupitia ngono. STIs husababishwa na bakteria na virusi.

      STIs za kawaida ambazo husababishwa na bakteria zinajumuisha; Kaswende, Kisonono na Klamidia. Magonjwa ya zinaa yanayosababishwa na virusi yanajumuisha; Ukimwi na Genital Herpes. Genital Herpes ni ugonjwa wa malengelenge ya neva ngozini unaoathiri viungo vya uzazi.

      Unaweza kuathirika na magonjwa ya zinaa zaidi ya moja kwa wakati mmoja na mara kwa mara ikiwa umepatikana kuwa na ambukizo moja, unahitajika kupimwa ikiwa una magonjwa mengine ya zinaa ukijumuisha HIV.

      Ni muhimu kufahamu ya kwamba mtu aliye na magonjwa ya zinaa yuko katika hatari kubwa ya kuambukizwa na HIV, kwa sababu STI hufungulia virusi njia ya kuingia mwilini. Ikiwa umepatikana na STI, unafaa kupimwa ikiwa una HIV. Wale ambao wameathirika na STI na HIV pia husambaza HIV kwa haraka kwa watu wengine. Kwa hivyo ni muhimu watibiwe haraka iwezekanavyo.
      RedDevil likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]


    2. #2
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,869
      Rep Power : 19446
      Likes Received
      8653
      Likes Given
      28271

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Kaswende

      Mtu anapoambukizwa ugonjwa wa kaswende, mwanzoni huwa haonyeshi dalili zozote. Baada ya wiki mbili atapata kidonda ambacho hakina uchungu katika sehemu nyeti. Kwa sababu kidonda huwa hakina uchungu, watu wengi hawatakibaini kwa urahisi na kitapotea baada ya majuma 4-6.

      Mara nyingine baada ya kidonda, kaswende huingia kwenye msururu wa damu na huleta homa, kuumwa na mwili na vidonda kwenye mdomo na sehemu nyeti. Wakati huu, mtu huwa na bakteria nyingi kwenye damu na anaweza kumuambukiza mtu mwingine kwa urahisi ikiwa watashiriki ngono. Ikiwa watu hawa hawatatibiwa, kaswende itabakia mwilini na inaweza kuleta matatizo kwenye ubongo ama kwenye moyo baada ya miaka kadhaa.

      Kaswende inaweza kutibiwa kwa kutumia kiua vijasumu au Antibiotics kwa Kiingereza. Matibabu haya huua bakteria zinazosababisha kaswende. Ni muhimu kumaliza kiwango chako chote cha dawa ili kuhakikisha ya kwamba umepona vizuri. Ikiwa mama mja mzito ameambukizwa kisonono, mtoto ambaye hajazaliwa anaweza pia kuambukizwa. Wanawake wote waja wazito hupimwa ikiwa wana kisonono katika kliniki ili watibiwe mapema na kumlinda mtoto dhidi ya kuambukizwa.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    3. #3
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,869
      Rep Power : 19446
      Likes Received
      8653
      Likes Given
      28271

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Kisonono

      Huu ni ugonjwa wa zinaa ambao ni wa kawaida na huathiri wanawake na wanaume kwa njia tofauti. Katika wanaume, dalili hutokea baada ya siku 2-5 baada ya kufanya mapenzi. Dalili dhahiri ni utetelezi ama usa mzito wa manjano kutoka kwenye uume. Hili husababisha hali ya kuchomeka na uchungu wakati unapokojoa. Uume unaweza kuwa mwekundu, kuvimba na huhisi uchungu unapoguzwa.Wanaume wachache huwa hawaonyeshi dalili zozote. Ikiwa hautatibiwa, unaweza kuharibu uume na kuzuia kupita kwa mkojo na manii.

      Katika wanawake, dalili huwa sio dhahiri. Nusu ya wanawake ambao wameathiriwa na kisonono huwa hawaonyeshi dalili zozote na kwa hivyo huwa hawatibiwi. Wao huzidi kuambukiza watu wengine na mara kwa mara huathirika na matatizo ya vifuko vilivyo jifunga, ugumba na uchungu unaojirudia rudia katika sehemu ya chini ya tumbo (chronic pelvic pain). Wale ambao wana dalili hizi hupata homa, huhisi uchungu wanapokojoa na hutoa usaha kutoka kwenye uke baada ya siku 2-5.

      Kisonono hutibiwa kwa urahisi haswa ikiwa matibabu yataanza mapema. Mtu huhitaji tu kutumia kiua vijasumu (antibiotics) kwa siku 7-10 ili apone. Mtoto anayezaliwa na mama ambaye hajatibiwa kisonono anaweza kupata ambukizo hatari la macho wakati wa kuzaliwa. Hili litahitaji matibabu na matone ya macho ya kiua vijasumu (antibiotics).
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    4. #4
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,869
      Rep Power : 19446
      Likes Received
      8653
      Likes Given
      28271

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Klamidia

      Huu unaweza kuwa ugonjwa wa zinaa ulio wa kawaida kuliko ugonjwa mwingine wowote wa zinaa unaoathiri wanaume na wanawake. Ugonjwa huu una dalili ambazo zinafanana na zile za kisonono lakini katika wanawake na wanaume, mara nyingi huwa hakuna dalili zozote.

      Klamidia ni ambukizo ambalo huja na maambukizo mengine kama kaswende,kisonono na HIV. Ukiwa hautatibiwa, vifuko vya wanawake na wanaume vinaweza kijifunga na hivyo kusababisha ugumba (hali ya kutoweza kupata watoto). Ugonjwa huu hutibiwa kwa urahisi kwa kutumia kiua vijasumu.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    5. #5
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,869
      Rep Power : 19446
      Likes Received
      8653
      Likes Given
      28271

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      UKIMWI

      Huu ni ugonjwa wa zinaa ulio hatari zaidi kwa binadamu. Unasababishwa na kirusi kinacho sambazwa kwa urahisi wakati unapofanya mapenzi. Pia huambukiza watoto ambao hawajazaliwa wakati wa kuzaliwa na wanaponyonyeshwa. Hakuna tiba ya HIV na hivi sasa zaidi ya watu milioni 30 wameambukizwa kote ulimwenguni. Wengi wa watu walioambukizwa huishi katika nchi za Afrika zilizoko chini ya jangwa la Sahara na Wakenya 700 hufariki kila siku kutokana na Ukimwi.

      Virusi huingia mwilini na kuharibu seli za ulinzi katika mwilini (kinga ya mwili). Pindi tu kinga ya mwili imedhoofika, mwili huathirika na maambukizo mengine mengi ambayo husababisha kuharisha, kutapika, kuumwa na kichwa, homa ya uti wa mgongo (menengitis), maambukizo ya ngozi na nimonia na hatimaye mtu hufariki kutokana na moja ya maambukizi hayo.

      Kuna madawa yanayopatikana katika hospitali za wilaya ambazo hupunguza kiwango cha ukuaji wa virusi katika mwili. Madawa haya kwa hivyo yataendeleza afya ya mtu na kurefusha maisha yake. Hata hivyo hii sio tiba na virusi vitabakia mwilini. Mtu aliyeathirika anaweza kumuambukiza mtu mwengine na mbaya zaidi anaweza kujiambukiza tena mara tena. Na kwa kila ambukizo, kinga ya mwili hudhoofika na afya ya mtu hudhoofika.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]


    6. #6
      Bahama's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th December 2010
      Posts : 19
      Rep Power : 434
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Hv wewe n doctor au? Mbona yaonekana wayajua sana magonjwa haya.
      MziziMkavu likes this.

    7. #7
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,722
      Rep Power : 68646
      Likes Received
      7102
      Likes Given
      5609

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Mkuu MziziMkavu huwa kweli unatoa shule asante sana
      MziziMkavu likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    8. #8
      ummu kulthum's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2012
      Location : singida
      Posts : 2,596
      Rep Power : 7005
      Likes Received
      1189
      Likes Given
      587

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      wa ukweli umeshashusha mistari, si ugombee ubunge mwakani tukupe uwaziri wa afya mkuu
      MziziMkavu likes this.
      ASIYEUMBA HAUMBUI

    9. #9
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,869
      Rep Power : 19446
      Likes Received
      8653
      Likes Given
      28271

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Quote By ummu kulthum View Post
      wa ukweli umeshashusha mistari, si ugombee ubunge mwakani tukupe uwaziri wa afya mkuu
      Nitakuja kugombea Ubunge kukiwa na Serikali nyingine sio hii Serikali ya Mafisadi. Vyama au chama kingine kikiongoza Serikali ninaweza kuja kuomba Ubunge sio serikali iliyoko madarakani ummu kulthum
      ummu kulthum likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    10. #10
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,869
      Rep Power : 19446
      Likes Received
      8653
      Likes Given
      28271

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Quote By Mr Rocky View Post
      Mkuu MziziMkavu huwa kweli unatoa shule asante sana
      yes of course Shule lazima kuna Watu Wengi hawajuwi Maradhi wanayoumwa nayo lazima tuwatahadharishe na maradhi ili wawe waangalifu kuhusu Maradhi Mr Rocky
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    11. #11
      RedDevil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2009
      Location : Hapa Hapa
      Posts : 1,457
      Rep Power : 807
      Likes Received
      271
      Likes Given
      516

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Mkuu mie nakukubali kwa data!! natamani siku moja niwe kama wewe!!
      MziziMkavu likes this.
      "Never argue with stupid people, they will drag you down to their level and then beat you with experience" Mark Twain

    12. #12
      Tuesmda's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 7th July 2012
      Posts : 6
      Rep Power : 351
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Vipele vidogo vidogo vimetokea na kukizunguka kichwa cha uume.HUU NI UGONJWA GANI NA DAWA NINI?
      MziziMkavu likes this.

    13. #13
      Katavi's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 31st August 2009
      Location : Lyamba Lya Mfipa
      Posts : 19,931
      Rep Power : 16839
      Likes Received
      2650
      Likes Given
      2034

      Default

      Quote By Tuesmda View Post
      Vipele vidogo vidogo vimetokea na kukizunguka kichwa cha uume.HUU NI UGONJWA GANI NA DAWA NINI?
      Utakuwa ugonjwa wa zinaa nenda hospitali haraka.
      MziziMkavu likes this.

    14. #14
      Hute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 1,424
      Rep Power : 718
      Likes Received
      358
      Likes Given
      23

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      k ya hawara yangu inakuwa inanuka afu inatoa ute mzito asubuhi, yaani ute ule wingi wake ni kama shahawa za mabao mawili...hata siku zile ambazo nilipumzika sikumduuu manake kama sivyo ningesema shahawa zangu ndo zinatoka...huo ni ugonjwa gani? na hapohapo anaumwa figo na zinakuwa kama zinamsumbua.
      MziziMkavu likes this.
      Tanzania ni tajiri,tena tajiri sanaaaa, lakini dah we acha tu! sijui kwanini watu wake masikini?

    15. #15
      Nzenzu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2011
      Posts : 827
      Rep Power : 563
      Likes Received
      155
      Likes Given
      38

      Default

      Quote By Hute View Post
      k ya hawara yangu inakuwa inanuka afu inatoa ute mzito asubuhi, yaani ute ule wingi wake ni kama shahawa za mabao mawili...hata siku zile ambazo nilipumzika sikumduuu manake kama sivyo ningesema shahawa zangu ndo zinatoka...huo ni ugonjwa gani? na hapohapo anaumwa figo na zinakuwa kama zinamsumbua.
      Mshauri aende hospital
      MziziMkavu likes this.

    16. #16
      Paloma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd January 2008
      Posts : 3,560
      Rep Power : 26474
      Likes Received
      3138
      Likes Given
      2994

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      asant kwa elimu Mzizi Mkavu
      MziziMkavu likes this.
      ""Nothing you wear is more important than your smile""

    17. #17
      KABOBA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th January 2013
      Posts : 108
      Rep Power : 345
      Likes Received
      24
      Likes Given
      17

      Default Re: Magonjwa ya Zinaa

      Wakenya 700 hufariki kila siku kutokana na Ukimwi.
      mkuu hizi takwimu mbona zinatia shaka?
      MziziMkavu likes this.

    Similar Topics

    1. Replies: 0
      Last Post: 31st August 2011, 11:38
    2. Replies: 37
      Last Post: 25th August 2011, 18:11
    3. Replies: 4
      Last Post: 20th July 2011, 14:10
    4. Yote Kuhusu Magonjwa Ya Zinaa
      By MziziMkavu in forum JF Doctor
      Replies: 0
      Last Post: 14th August 2010, 04:19
    5. Magonjwa haya ya zinaa
      By Babu Swahili in forum JF Doctor
      Replies: 8
      Last Post: 18th March 2009, 09:52

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...