Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kuumwa tumbo wakati wa hedhi - Part 1

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,161
      Rep Power : 19205
      Likes Received
      8115
      Likes Given
      26566

      Default Kuumwa tumbo wakati wa hedhi - Part 1


      Tumbo la hedhi au maumivu wakati wa hedhi (period pains) au kitaalamu dismenorrhea, ni maumivu yanayojitokeza sehemu ya chini ya tumbo au kiunoni wakati mwanamke anapoanza kupata siku zake au kabla ya hapo. Maumivu hayo huweza kuwa madogo au ya wastani huku baadhi ya wanawake wakipata maumivu makali sana. Maumivu ya tumbo wakati wa hedhi huanza pale mayai yanapotoka katika mirija (fallopian tubes) na kuteremka chini ya mirija hiyo wakati wa Ovulation.

      Maumivu ya tumbo la hedhi yapo ya aina mbili. Aina ya kwanza au (Primary Dysmenorrhea) ni maumivu yasiyokuwa na sababu zozote za kimsingi za kitiba. Katika aina hii maumivu ni ya kawaida na huhisiwa sehemu ya chini ya tumbo na kiunoni. Maumivu hayo huanza siku moja au mbili kabla ya hedhi na humalizika baada ya siku mbili au nne.

      Aina ya pili au (Secondary Dysmenorrhea) ni yale maumivu yanayojumuisha maumivu yanayosababishwa na sababu nyinginezo za kitiba kama vile matatizo katika kizazi, ugonjwa wa nyonga (PID) na matatizo katika mirija ya mayai.

      Karibu nusu ya wasichana na wanawake hupata maumivu wakati wa hedhi na karibu asilimia 15 wanasema kuwa hupata maumivu makali. Uchunguzi unaonyesha kuwa kuna sababu mbalimbali zinazoweza kuongeza uwezekano wa kuumwa tumbo wakati wa hedhi.

      • Kuwa na umri wa chini ya miaka 20.
      • Kuvunja ungo wakati wa miaka 11 au chini ya miaka hiyo.
      • Kutoka na damu nyingi wakati wa hedhi. (suala hilo linaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali ya kitiba).
      • Wanawake ambao hawajawahi kuzaa.

      Maumivu ya Tumbo la Hedhi... Sehemu ya Pili




      kukasababisha mtu kupatwa na maumivu ya tumbo la hedhi. Miongoni mwa magonjwa hayo ni:
      • Endometriosis. Hii ni hali ambayo seli za ndani ya mfuko wa uzazi huanza kuoka nje ya fuko hilo, au hta sehemu nyinginezo.
      • Adenomyosis: Huu ni ugonjwa wa wanawake ambapo tezi au uvimbe (tumors) zinaoota katika mfuko wa uzazi.
      • PID au Ugonjwa wa uvimbe katika nyonga.
      • Magonjwa ya zinaa yanayotokana na bakteria au magonjwa ya kuambukiza ya zinaa.
      • Mlango wa uzazi unapokuwa mdogo kiasi kwamba unazuia damu ya hedhi isitoke kwa urahisi.

      Baada ya kujua baadhi ya matatizo ya wanawake yanayoweza kusabibisha hedhi inayoambatana na maumivu ya tumbo, hebu sasa na tuzijue tumbo la mwezi linaumaje?

      1. Maumivu mara nyingi si makali.
      2. Muumivu huja na kuondoka, na kwa kiwango tofauti (spasmodic).
      3. Maumivu zaidi huhisiwa sehemu ya chini ya tumbo.
      4. Huchanganyika na maumivu ya sehemu ya chini ya mgongoni ambayo husambaa mpaka mapajani.
      5. Kujihisi kutapika, kichefuchefu na wakati mwingine hata kutokwa jasho.
      6. Kupata choo kilaini au hata kuharisha.
      7. Kufunga choo.
      8. Tumbo kuwa kubwa au kuwa gumu.
      9. Kuhisi maumivu ya kichwa.
      10. Kutojihisi vizuri au kujisikia kuchoka.

      Inapasa kujua kuwa, kiwango cha maumivu ya tumbo la hedhi na mchanganyiko wa dalili inategemea mtu na mtu, mtu mwingine anaweza akawa anapata karibu dalili zote nilizozitaja hapo juu na mwingine ni baadhi tu au hata dalili moja. Wanawake wengi hutambua wanapopata tumbo la hedhi bila hata msaada wa daktari. Wanawake wanashauri iwapo watapata maumivu makali sana ni bora

      wakamuone daktari ili wafanye vipimo kama vile Ultrasound, CT na CT-Scan, MRI na vinginevyo ili kufahamu iwapo **** matatizo mengine ya kitiba yanayosababisha maumivu hayo kuwa makali.
      Matibabu ya maumivu ya tumbo la hedhi kwa kawaida huweza kutibika kwa urahisi kwa kutumia vidonge vya kupunguza maumivu, kama

      vile Ibuprofen, naproxen au aina nyinginezo za vidonge visivyokuwa na steroids (NSAIDS). Pia kuna wakati madaktari wanaweza kumshauri mgonjwa kutumia vidonge vya kuzuia mimba, Vidonge hivyo huzuia mzunguko wa yai au Ovulation na kupunguza ukali wa maumivu ya tumbo la hedhi.

      Kuna baadhi ya tiba za mitishamba pia ambazo husadia kupunguza muamivu ya tumbo la hedhi. Hapa namaanisha herbal, wenzetu Wachina ni watalamu wazuri katika ujuzi huo. Vilevile wanawake washauriwa kufanya baadhi ya vitendo ambavyo hupunguza maumivu

      hayo, baadhi ya hivyo vimetaja kama kuoga maji moto, kutumia hot bottle na hata kuweka kitambaa chenye joto katika sehemu ya chini ya tumbo. Kuna baadhi husaidia kwa kufanya mazoezi kama yoga, meditation, kusuliwa, tiba ya sindano (Acupunture), TENS au kushituliwa

      mishipa ya fahamu ( Transcitaneous Electric Nerve Stimulation na hata wengine husaidiwa kwa tendo la kujamiiana. Vilevile kutumia vidonge vya vitamin E, Thiamine na Omega 3 kumetajwa kuwa husaidia katika suala hilo. Wanawake wanaopatwa na matatizo kama hayo ni bora wapumzike vyema na kupata usingizi wa kutosha.

      Tunaelezwa kuwa tunaweza kujiepusha na kupatwa na maumivu ya tumbo la mwezi kwa kufanya yafuatayo:
       Kujitahidi kula matunda, mbogamboga na kupunguza kula vyakula vyenye mafuta mengi, pombe, cofeini, Sodium na sukari.
       Kufanya mazoezi.
       Kujiepusha na wasiwasi na mawazo.
       Kuepuka kufuta sigara.
      … Haya kina mama na kina dada, Mkumbuke kuwa afya ni zenu na inabidi Muzitunze!
      http://mashosti.blogspot.com/2009/11...sehemu-ya.html

      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      itnojec's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2011
      Location : the under world
      Posts : 1,721
      Rep Power : 760
      Likes Received
      250
      Likes Given
      64

      Default Re: Kuumwa tumbo wakati wa hedhi - Part 1

      naamini wengi wao wameelewa. asante kwa taarifa muhimu
      MziziMkavu likes this.

    4. #3
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,680
      Rep Power : 27091
      Likes Received
      10054
      Likes Given
      13953

      Default Re: Kuumwa tumbo wakati wa hedhi - Part 1

      kushukuru sana kwa huu uzi manake menigusa kunako. sasa tuanze hivi jamani haya dysmenrrhoea jamani iko na utata sana. mfano halisi mimi huwa ninaumwa sana nimeshafanya hadi ulta sound na MRI lakin huwez kuamni hakuna tatizo ambalo ni la kitabibu. nakumbuka ilifika wakati dr kamugisha akasema ishu ipo kwenye mirija kwamba imebana hivyo huwa haitanuki irahisi kuachia damu kutoka ila bado sikupata furaha na jiabu hili manake nimezaa 3 times na zote ni kawaida na katika zote sijawah kupata tearing sasa iweje kwenye hedhi iwe midogo na kuniletea maumivu?

      istoshe niliamini kwamba kama tatizo ni kwenye kutanuka basi nikisha zaa tatizo litaisha nikajikuta wapi, regardless ya kuzaa kwenye umri ambao unaruhusiwa kiafya. hadi leo hii nina maumivu ambayo hayasikii dawa yeyete ya maumivu na huwa najichukia kwakweli to me ni heri niwe mjamzito kuliko niwe kawaida. haya mra kuna wengine wakanipa darasa la kitaa kwamba nikibadili jinsia nitapona lakin nimejiuliza pana mahusiano gani hapa sipati jibu. istoshe nikisema niendelee kuzaa ili nipate kadada mbona nitajaza nyumba mikia pasi kumpata huyo dada?

      uamzi niliofikia nakwenda kufunga uzazi kwa kukata mirija ya kizazi ili nisitumike tena na nisiumwe what do you suggest?
      MziziMkavu likes this.
      "thought takes man out of servitude into freedom"
      'daima tudumu katika upendo'

    5. Miaka 50

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...