Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 81
    1. #1
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Dr. T. R. Msigwa, baada ya miaka 12 ya utafiti amehitimisha hatua yake ya mwanzo ya utafiti na amevumbuwa dawa mbadala ya UKIMWI kutokana na miti shamba na samaki.

      Kwa mujibu wa Dr. Msigwa, dawa hiyo kwa jina la 4A9 Medicine, anasema imepata baraka zote za Mkemia Mkuu na TFDA.

      Msikilize mwenyewe anasemaje: Dr. Msigwa, Radio Imaan - YouTube
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Sizinga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th October 2007
      Location : Mars
      Posts : 3,939
      Rep Power : 1432
      Likes Received
      1510
      Likes Given
      1619

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Habari njema if it real works....nimesikia mataifa makubwa(scientists) huko New York yanahaha na bajeti ingawa wamejipambanua kwamba wamefikia mahala pazuri kufight against virus..

      So let this be good news globally.
      GESI KWANZA KOROSHO BAADAE!!

    4. #3
      MadameX's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th December 2009
      Location : Timbaktu
      Posts : 6,106
      Rep Power : 6545
      Likes Received
      2662
      Likes Given
      1302

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      another scammer
      MziziMkavu likes this.
      Blessed are hearts that bend but shall never broken

    5. #4
      stephot's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st March 2012
      Location : DSM
      Posts : 776
      Rep Power : 585
      Likes Received
      212
      Likes Given
      587

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Huyo aangaliwe vizuri asituletee mambo ya kubahatisha kama yale ya Babu wa Loliondo.

    6. #5
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By MadameX
      another scammer
      Huyu dawa yake sio ya miujiza kama ya babu wa samunge. Hii anadai kwenye kitabi chake (ambacho nakisoma sasa hivi) kuwa imefanyiwa utafiri kwa miaka 12 na humu kwenye kitabu ana data za utafiti.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    7. Miaka 50

    8. #6
      paty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : never never land
      Posts : 1,024
      Rep Power : 974
      Likes Received
      270
      Likes Given
      62

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By MadameX
      another scammer
      ha ha ha ha bibi wa tabora, kijana wa mbeya na babu wa Lo....****o , simaliziii wananchi wasije wakanipiga mawe
      CHADEMA mwendo mdundo - T 2015 CDM

    9. #7
      Ozzie's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 9th October 2007
      Location : Jo'burg
      Posts : 1,008
      Rep Power : 795
      Likes Received
      271
      Likes Given
      74

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By zomba
      dawa hiyo kwa jina la 4A9 Medicine
      Japo tunahitaji sana dawa ya VVU, lakini hawa watu wa mitishamba wanatudanganya sana. Hawajui hata pathophysiology ya HIV na wanaleta uongo wa kuvumbua dawa. Ulaghai tupu. Hata jina la dawa yake linaonesha ushamba wa kung'ang'aniza kuingiza neno la kiingereza. Ni kama vile mvumbuzi wa Quinine, angeiita Quinine, Quinine Medicine. Hakuna kitu hapo.
      "It's not the votes that count. It's who counts the votes" - Josef Stalin

    10. #8
      MadameX's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th December 2009
      Location : Timbaktu
      Posts : 6,106
      Rep Power : 6545
      Likes Received
      2662
      Likes Given
      1302

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By zomba
      Huyu dawa yake sio ya miujiza kama ya babu wa samunge. Hii anadai kwenye kitabi chake (ambacho nakisoma sasa hivi) kuwa imefanyiwa utafiri kwa miaka 12 na humu kwenye kitabu ana data za utafiti.
      Kitabu kitabu....hata mimi naweza kuandika kitabu and convince you. Kwanini utafiti huo pia usifanywe na expert wengine ikithibitika na afanye patent ya dawa yake akaokoa mamilioni ya watu duniani.
      MziziMkavu likes this.
      Blessed are hearts that bend but shall never broken

    11. #9
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By MadameX
      Kitabu kitabu....hata mimi naweza kuandika kitabu and convince you. Kwanini utafiti huo pia usifanywe na expert wengine ikithibitika na afanye patent ya dawa yake akaokoa mamilioni ya watu duniani.
      Amefanya na watafiti wengine wengi tu, sasa kwaa upande wake amemaliza awamu ya kwanza ya utafiti wake na daawa imepimwa na kuonekana mjarab, kwa sasa ni mtu mwenye matatizo anapima, anapewa dawa anaeleza matokeo within the first two weeks (kwa mujibu wa hizo kanda zake kama umezisikiliza).

      Kwanini hauzisikikilizi halafu kama una maswali kaweka namba yake hapo hapo kwenye youtube.

      Excerpts za kwenye kitabu:

      Jaribio la kutibu wagonjwa wenye VVU kwa kutumia dawa hii (4A9 Medicine) lilifanyika kwenye mikoa mbalimbali Tanzania ikiwemo; Kigoma, Dar Es Salaam, Tanga, Iringa, Mtwara, Zanzibar, Morogoro, Shinyanga, Arusha, Mwanza.

      Msikilize: http://www.youtube.com/watch?v=EzLnnwr6EJk&feature=plcp

      Last edited by zomba; 30th July 2012 at 20:07.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    12. #10
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By Ozzie
      Japo tunahitaji sana dawa ya VVU, lakini hawa watu wa mitishamba wanatudanganya sana. Hawajui hata pathophysiology ya HIV na wanaleta uongo wa kuvumbua dawa. Ulaghai tupu. Hata jina la dawa yake linaonesha ushamba wa kung'ang'aniza kuingiza neno la kiingereza. Ni kama vile mvumbuzi wa Quinine, angeiita Quinine, Quinine Medicine. Hakuna kitu hapo.
      Ulitaka lazima awe sawa na aliyevumbuwa Quinine? Tatizo hauna ubunifu, mwenzenu ndio hiyo dawa anayo, kama una matatizo muone tu. Sisi ujumbe tumefikisha, usije kusema hujaambiwa!
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    13. #11
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,182
      Rep Power : 19209
      Likes Received
      8137
      Likes Given
      26611

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Dk. Msigwa hajapata Baraka ya kutibu Ukimwi – Bodi ya Madawa


      Na Fatma Kassim, MaelezoBODI ya Chakula Dawa na Vipodozi imesema kuwa haijampa Baraka Dk. Msigwa ya kuwa dawa yake inatibu Virusi vya Ukimwi au kupunguza virusi hivyo.Mrajis wa Bodi hiyo Dk Burhan Othman Simai alisema dawa ya daktari huyo imefanyiwa

      uchunguzi na maabara yake na kugundua kuwa haina sumu, na sio kutibu ukimwi.
      Alisema kitengo cha kuitangaza dawa yake hiyo inajulikana 499 medicine kuwa inatibu ukimwi si jambo zuri na linapotesha umma na kuonekana ni mtibabu wa maradhi hayo na wakati

      dawa yake hiyo imeandikwa kuwa inatibu Kisukari, kuondoa uchovu na sumu mwilini.
      Amewataka wananchi kuwa makini na matumizi ya dawa hizo ambazo nyengine hazina viwango na kudai kuwa zinatubu ukimwi jambo ambalo si sahihi kutokana na kuwa dawa ya kutibu VVU

      haijapatikana mpaka sasa.
      Kwa upande wake Mrajis wa Tiba asili na tiba Mbala Mohammed Omar Mohammed alisema kuwa kutokana na Dk Msigwa kudai kuwa dawa yake inatibu Ukimwi baraza hilo limemtaka awapeleke wagonjwa aliwaowapatia matibabu jambo ambalo

      ameshindwa.
      Alifahamisha kuwa baraza lake limemtaka afuate taratibu na asitangaze dawa zake kuwa zinatibu Ukimwi pamoja na kufanya usajili upya na kutibu kwa tiba asili.Aidha baraza hilo la tiba asili limetaka Dk Msigwa kuwa lugha anayotumia katika kipindi chake cha Radio

      Adhana JITAMBUE airekebishe na asiiseme kuwa “dawa yake inatibu Virusi Vya Ukimwi na badala yake aseme kuwa inayopunguza maradhi nyemelezi yanayoambatana na Virusi Vya Ukimwi au dawa inayoongeza kinga ya mwili , CD4”.
      Aidha alifahamisha kuwa hatakiwi

      kuwaachisha wagonjwa walioanza dawa za ARV kwa kutumia dawa yake hiyo ambapo anaweza kuwasababishia madhara makubwa.
      Dk. Msigwa hajapata Baraka ya kutibu Ukimwi – Bodi ya Madawa | Ministry of Health Zanzibar
      PainKiller, kvelia, mama D and 1 others like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    14. #12
      zaleo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 791
      Rep Power : 535
      Likes Received
      234
      Likes Given
      528

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By zomba
      Huyu dawa yake sio ya miujiza kama ya babu wa samunge. Hii anadai kwenye kitabi chake (ambacho nakisoma sasa hivi) kuwa imefanyiwa utafiri kwa miaka 12 na humu kwenye kitabu ana data za utafiti.
      Mara ngapi unamsikia mtu akijenga hoja asikilizwe husema "Katika utafiti wangu nimegundua kwamba...."? Wanajisemea tu mara nyingi, utafiti una nidhamu yake, yeye aandike na jopo la wanasayansi liyapitie na kupitisha maandiko yake tujue utafiti wake ni utafiti kweli. Sio porojo. Hizo tumezisikia nyingi na mbado.
      MziziMkavu likes this.
      “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” by Hon Lema, MP - Arusha

    15. #13
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By zaleo
      Mara ngapi unamsikia mtu akijenga hoja asikilizwe husema "Katika utafiti wangu nimegundua kwamba...."? Wanajisemea tu mara nyingi, utafiti una nidhamu yake, yeye aandike na jopo la wanasayansi liyapitie na kupitisha maandiko yake tujue utafiti wake ni utafiti kweli. Sio porojo. Hizo tumezisikia nyingi na mbado.
      Hao ma scientist wanangoja nini? si ndio kina mkemia mkuu waliyoipima hiyo dawa na kusema ni salama? si ndio kina tfda hao? sasa na wewe kwanini usihahakikishe ?
      Last edited by zomba; 31st July 2012 at 12:31.
      zaleo likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    16. #14
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By MziziMkavu
      Adhana JITAMBUE airekebishe na asiiseme kuwa “dawa yake inatibu Virusi Vya Ukimwi na badala yake aseme kuwa inayopunguza maradhi nyemelezi yanayoambatana na Virusi Vya Ukimwi au dawa inayoongeza kinga ya mwili , CD4”.Aidha alifahamisha kuwa hatakiwi
      Hii ina maana wanaitambuwa rasmi kuwa dawa hii ina manufaa na inaonaongeza CD4. Hata mimi nimesiikiliza mikanda ya huyu Msigwa na nimeona anasema kuwa dawa yake inaongeza CD4 kwa wingi na kwa muda mfupi kuliko dawa nyingine yoyote iliyoko madukani kwa sasa, iwe ya hospital au ya mitishamba.

      MziziMkavu, mbona hiyo taarifa ulyoleta inajichanganya? hivi kuna dawa gani inayotibu VVU? mimi sijawahi kusikia, nnachojuwa anaetibiwa ni mgonjwa wa VVU kwa kumuongezea kinga mwilini CD4 na kupunguza VVU mwilini (viral load). Sasa uanze kutibu VVU ili vishambulie zaidi?
      Last edited by zomba; 31st July 2012 at 16:10.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    17. #15
      zaleo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 791
      Rep Power : 535
      Likes Received
      234
      Likes Given
      528

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By zomba
      Hao ma scientist wanangoja nini? si ndio kina mkemia mkuu waliyoipima hiyo dawa na kusema ni salama? si ndio kina tfda hao? sasa na wewe kwanini usihahakikishe ?
      Zomba, unaweza usinielewe nasema nini leo hii, lakini kuna siku hapo baadaye utanielewa nasema nini. Hata yule bwana wa Formula one kule ubungo alisema kama alivyosema huyo bwana, lakini haikuchukuwa muda kukawa na ugomvi mkubwa sana na wanasayansi. Unajua, mara nyingi hao mabwana hutumia majinamakubwa sana ili bidhaa zao zipate kuaminika. Sasa kwa kuwa watanzania ninavyowafahamu kutopenda kutafuta majibu sahihi na kwa subira kwa maswali magumu, wanapokea maneno hayo na kuanza kuyafanyia kazi kwa kmtafuta na kujikuta baadaye wamepotea, halafu ndipo wanaanza kulaumu serikali ilikuwa wapi wakati tunasikia kwenye vyombo, rais kwa nini amechagua wasaidizi wabovu, nk. Kumbe ni ujinga wetu unaotumaliza sisi wenyewe, bahati mbaya marehemu harudi tena kuja kutusimulia ilivyotokea akafa kijinga (kama ni kijinga kweli).

      Kuna taratibu na mlolongo mrefu sana juu ya tiba kama hiyo hata ikubalike. TFDA hawana sauti ya mwisho katika hilo. Kwa kweli hata wizara haina sauti ya mwisho, lazima WHO wakubaliane kwanza kufanyia majaribio kwa mwili wa binadamu baada ya kutafiti nje ya mwili na kisha kwa wanyama wanaofanana fanana na mtu, ndipo ipitishwe kwa kujihakikishia kwamba inayo nguvu asilimia ngapi kupambana na ugonjwa na kwa namna gani, athari yake nini kwa matumizi na namna ya kudhibiti athari hizo, na mambo kadha wa kadha. Sasa huyo bwana ametafiti miaka 10 ndio leo tunamsikia yeye, umewasikia TFDA wakitangaza au yeye ndio anakuambia. Unayaamini maneno yake asilimia ngapi? Wangetangaza hao anaowasema kidogo ningekua na chembe ya imani naye. Lakini huenda kweli inatibu, dawa nyingi mbadala zinatibu magonjwa mengi, lakini tunashindwa kufika mwisho sababu ya kukurupuka kwenda sokoni hata kabla ya matokeo ya mwisho. Hata Alovera na Mlonge vinaweza kuongeza kinga mwilini na kwa kufanya hivyo kudhibiti virusi vya ukimwi, hata hivyo mtu akitoka mkuku kututangazia dawa hiyo inatibu sikubaliani mpaka nipate majibu. Tena unaniambia nitafiti mimi, haisaidii, nami nikitangaza sitakuwa tofauti na mganga wa jadi huyo.

      Pale Muhimbili kuna kitengo cha madawa asili, ingawa nao ni wachakachuaji sana na pametokea malalamiko mengi kwa waganga wa jadi wanaopeleka dawa zao pale wanakatishwa tamaa na kuibiwa siri ya dawa hizo kwa sababu ya kutokuwa waaminifu tu. Lakini ndo chombo pekee rasmi inabidi ugangamale, wizi upo kila kona.
      MziziMkavu likes this.
      “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” by Hon Lema, MP - Arusha

    18. #16
      chomboko's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 18th July 2012
      Posts : 2
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      1

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      teh! teh!
      sound tu hizo! tumesikia wengi... wakaja wakapita... kisha wakapotea!!!

      chomboko

    19. #17
      Mangaline's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th May 2012
      Posts : 1,001
      Rep Power : 614
      Likes Received
      205
      Likes Given
      54

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Dawa akivumbua Mzungu ni Dawa, akivumbua Mwafrika ni Uchawi.

    20. #18
      kirumonjeta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2008
      Location : Mogadishu
      Posts : 425
      Rep Power : 661
      Likes Received
      76
      Likes Given
      118

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Mvumbuzi lazima awe mzungu au,hebu tumpe moyo mwenzetu huyu kuliko kumkandia
      NI TAMAA YA UFISADI TU INAYOKUSABABISHA UENDELEE KUBAKIA CCM

    21. #19
      Opaque's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th October 2008
      Posts : 953
      Rep Power : 729
      Likes Received
      227
      Likes Given
      84

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Quote By zomba
      ....Sasa uanze kutibu VVU ili vishambulie zaidi?
      Hii kali!



    22. #20
      SASATELE's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th September 2011
      Posts : 149
      Rep Power : 418
      Likes Received
      81
      Likes Given
      22

      Default Re: Msigwa Avumbuwa Dawa Mbadala ya UKIMWI

      Wewe zomba mbona unatetea sana. Nahisi wewe ndio Dr Msigwa mwenyewe. Haiwezekani ujibu almost kila hoja inayochallenge kama huna maslahi na hii issue!! sema tu kaka!!

    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...