Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: UHANITHI baada ya kitovu cha mtoto kukatika na kudondokea sehemu zake za siri

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 56
    1. #1
      Kipanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Posts : 687
      Rep Power : 707
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default UHANITHI baada ya kitovu cha mtoto kukatika na kudondokea sehemu zake za siri

      Wandugu,

      Napenda kufahamu kitaalamu juu ya imani au uvumi kuwa mtoto mchanga anapozaliwa lazima mzazi na hasa mama ahakikishe kuwa kitovu cha mtoto huyo kitakapokauka na kudondoka basi kisiguse sehemu nyeti za huyo mtoto. Inasemekana kuwa ikitokea kuwa kitovu hicho kimedondoka na kugusa sehemu hizo nyeti basi mtoto huyo kama ni wa kiume atakuwa bwabwa na kama ni wa kike nae atakuwa msagaji? (hatakuwa na feeling za kuhitaji mwanaume)..

      Nahitaji maelezo ya kitaalamu na hasa kwenu nyie wataalamu wa tiba kuhusu hili kwani yanazungumzwa lakini hakuna justification ya kitaalamu inayotolewa zaidi ya kuonekana ni mapokeo ya imani tu.
      Quote By Mr Kiroboto
      Kitaalamu hilo suala la kitovu kinapoangua na kugusa sehemu nyeti za mtoto na kumfanya awe hanidhi si ukweli. Mie nahisi ni mila za baadhi ya makabila.

      Kitaalam mtoto kila anapokuwa katika kipindi fulani basi kuna mambo lazima atapitia,sasa mzazi ambaye atamkataza huyu mtoto kufanya haya mambo yanaweza kumuhathiri kisaikologia.

      Mfano watoto wengi katika umri fulani huwa wanacheza kama vile wazazi katika familia,mtoto wa kiume baba na mtoto wa kike ni mama,so hawatakiwi kukatazwa,kwani ni mambo ya kupitia na baadae wataacha.

      Pia kuna umri fulani watoto huwa wanajisaidia haja kubwa au ndogo pasipo kujielewa,mzazi hautakiwi kumpiga na kumtisha mtoto, kwasababu hiyo ni hali kutokana na kutokomaa kwa mfumo wake wa fahamu,pindi mzazi utapokuwa unampiga na kumtishia ili aache hiyo tabia ni kweli ataacha ila yaweza kuwa ikamuathiri ukubwani.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      mgirima's Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th May 2008
      Posts : 83
      Rep Power : 577
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Nini uhusiano wa kitovu na uhanithi???

      Inadaiwa kuwa kitovu cha mtoto aliyezaliwa huwa kinaandamana na mikosi na mabalaa mengi kutoka kwa mama. na ndio maana hutakiwa kuzikwa ardhini (kwa kiasili) na sio kutupa sehemu yoyote. Maelezo haya hayana utaalamu wo wote ila ni mambo ya kimila tu. ajabu ni kuwa makabila mengi hapa nchini yanaamini hivyo!

    4. #3
      Mr Kiroboto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2008
      Posts : 270
      Rep Power : 618
      Likes Received
      5
      Likes Given
      9

      Default Re: Nini uhusiano wa kitovu na uhanithi???

      Kitaalamu hilo suala la kitovu kinapoangua na kugusa sehemu nyeti za mtoto na kumfanya awe hanidhi si ukweli. Mie nahisi ni mila za baadhi ya makabila.

      Kitaalam mtoto kila anapokuwa katika kipindi fulani basi kuna mambo lazima atapitia,sasa mzazi ambaye atamkataza huyu mtoto kufanya haya mambo yanaweza kumuhathiri kisaikologia.

      Mfano watoto wengi katika umri fulani huwa wanacheza kama vile wazazi katika familia,mtoto wa kiume baba na mtoto wa kike ni mama,so hawatakiwi kukatazwa,kwani ni mambo ya kupitia na baadae wataacha.

      Pia kuna umri fulani watoto huwa wanajisaidia haja kubwa au ndogo pasipo kujielewa,mzazi hautakiwi kumpiga na kumtisha mtoto, kwasababu hiyo ni hali kutokana na kutokomaa kwa mfumo wake wa fahamu,pindi mzazi utapokuwa unampiga na kumtishia ili aache hiyo tabia ni kweli ataacha ila yaweza kuwa ikamuathiri ukubwani.

    5. #4
      Haika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 1,688
      Rep Power : 914
      Likes Received
      239
      Likes Given
      358

      Default Re: Nini uhusiano wa kitovu na uhanithi???

      zamani wazazi waliambiwa kuwa kitovu kikidondokea kwenye sehemu za uzazi itasababisha uhanithi kuwatisha kinamama ili wawe waangalifu na kidonda cha mtoto mchanga kitovuni, wasisahau kukiangalia na maendeleo yake kuepusha vifo vya infection, lakini hakuna uhusiano
      kvelia, MIGNON, Maty and 1 others like this.

    6. #5
      Che Kalizozele's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th July 2008
      Location : Area C
      Posts : 782
      Rep Power : 709
      Likes Received
      23
      Likes Given
      11

      Default Mtoto akiangukiwa na kitovu

      Hii nilipata kuisikia siku nyingi kidogo ya kwamba kama mtoto mdogo ataangukiwa na kitovu(Kile kijipande cha nyama kinachodondoka baada ya kitovu kukauka na kupona siku kadhaa baada ya mtoto kuzaliwa),sasa hicho kijipande kikimuangukia sehemu zake za siri,basi kama mtoto huyo ni wa kiume hatoweza kuattain erection maisha yake yote.

      Huyu aliyeniambia akazidi kusema,ndo mana wakina mama uwa makini sana vitovu hivi,vinadondokea wapi?Mnaoshinda mawodini na mahospitalini tuambieni,jee hii ni kweli na kama ni kweli what is the mechanism behind.
      SIWEZI KUMRIDHISHA RUHANI WAKATI KITI ANAUMIA.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Kipanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Posts : 687
      Rep Power : 707
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Mtoto akiangukiwa na kitovu

      Quote By Baba watatu
      Hii nilipata kuisikia siku nyingi kidogo ya kwamba kama mtoto mdogo ataangukiwa na kitovu(Kile kijipande cha nyama kinachodondoka baada ya kitovu kukauka na kupona siku kadhaa baada ya mtoto kuzaliwa),sasa hicho kijipande kikimuangukia sehemu zake za siri,basi kama mtoto huyo ni wa kiume hatoweza kuattain erection maisha yake yote.

      Huyu aliyeniambia akazidi kusema,ndo mana wakina mama uwa makini sana vitovu hivi,vinadondokea wapi?Mnaoshinda mawodini na mahospitalini tuambieni,jee hii ni kweli na kama ni kweli what is the mechanism behind.
      ...Bora Baba watatu umeweka hii thread hapa tunaweza kupata ufumbuzi wa kitaalam kuhusu hiyo mi naiita imani au mtazamo wa mashaka. Niliwahi kuichomeka thread inayohusiana na hili jambo lakini kwa mshangao ikayeyuka.....Haya matabibu mtujuze kuna connection gani kati ya kuangukia kitovu sehemu ya siri ya mtoto na uhanithi.

      Baba watatu, wengine hudai hata kwa mtoto wa kike pia ikimtokea anapokuja kupevuka hatakuwa na msisimko wa mapenzi??????????????
      "All things are created twice. There is a Mental or first creation ,and a physical or second creation to all things"

    9. #7
      Mwanafunzi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th December 2007
      Posts : 31
      Rep Power : 592
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Mtoto akiangukiwa na kitovu

      Jambo la kujiuliza Baba watatu na Kipanga ni Je kuna mtu mzima aliyekuwa na matatizo ( kutopata erection au kutokuwa na msisimko) ambaye alisema nilipokuwa mtoto kitovu kiliangukia sehemu za siri?

      Kwa jamii yetu ninavyoielewa, mtu hawezi kusema matatizo yake au kwenda kuuliza mama kuwa nilipokuwa mdogo kitovu kiliangukia wapi. Pia jinsi akina mama kwa imani wanavyo protect hicho kitovu kisiangukie pabaya, ni ajabu kuwa watu wengi wana hayo matatizo.

      Je, wote hao vitovu viliangukia pale??

    10. #8
      Kipanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Posts : 687
      Rep Power : 707
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Mtoto akiangukiwa na kitovu

      Quote By MWANAFUNZI
      Jambo la kujiuliza Baba watatu na Kipanga ni Je kuna mtu mzima aliyekuwa na matatizo ( kutopata erection au kutokuwa na msisimko) ambaye alisema nilipokuwa mtoto kitovu kiliangukia sehemu za siri?

      Kwa jamii yetu ninavyoielewa, mtu hawezi kusema matatizo yake au kwenda kuuliza mama kuwa nilipokuwa mdogo kitovu kiliangukia wapi. Pia jinsi akina mama kwa imani wanavyo protect hicho kitovu kisiangukie pabaya, ni ajabu kuwa watu wengi wana hayo matatizo.

      Je, wote hao vitovu viliangukia pale??
      ...Ndio maana tulitaka wataalamu wa tiba watujuze kwani imeshakuwa mazoea kuwa mtu akishindwa ku-erect inaaminika aliangukiwa na kitovu sasa mimi binafsi nashindwa kuelewa kitovu kina nini mpaka kiathiri erection ya mtu ingawa kiukweli erection inaendana sana na jinsi brain inavyosense kile kitendo kinachotegemewa kufanyika (mapenzi/sex)

      Unajua hata wakati mtoto wangu wa pili anazaliwa bibi yake mzaa mimi alimfatilia sana huyo mtoto hadi alipohakikisha kitovu kimekauka na kimedondokea maeneo aliyoita mwenyewe salama....Mi nilikuwa mtazamaji tu kwani si mama wala bibi wa mtoto aliyekuwa tayari kunielezea nini kinachoendelea.....WANA JF hebu tutoeni tongo tongo basi....
      "All things are created twice. There is a Mental or first creation ,and a physical or second creation to all things"

    11. #9
      Malila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2007
      Posts : 2,605
      Rep Power : 10971
      Likes Received
      828
      Likes Given
      447

      Angry Kudondokewa na kitovu

      Nimepata kusikia huko uswahilini kuwa, eti mtoto wa kiume akidondokewa na kitovu chake ndo basi tena. Yaani jogoo halitapanda mlima. Mimi sioni uhusiano wa kisayansi hapo. Je kuna ye yote ajuaye anisaidie/atusaidie kupata ukweli wa jambo hili?

    12. #10
      macinkus's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th September 2007
      Posts : 265
      Rep Power : 650
      Likes Received
      10
      Likes Given
      5

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      kitovu kudondoka ndio kufanya nini wandugu

      macinkus

    13. #11
      Malila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2007
      Posts : 2,605
      Rep Power : 10971
      Likes Received
      828
      Likes Given
      447

      Thumbs up Re: kudondokewa na kitovu

      Hata mimi niliposikia nikakosa jibu,lakini ni jambo la kawaida mitaani kusikika hasa huku Pwani.

    14. #12
      HM Hafif's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th August 2009
      Posts : 1,372
      Rep Power : 771
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      kituvo kikidondokea uume kwa mtoto mchanga, basi jogoo hilo litakuwa haliwiki na kama litawika basi litakuwa na walakini. Hizo ni imani za kale

    15. #13
      Babuyao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th June 2009
      Posts : 1,719
      Rep Power : 850
      Likes Received
      177
      Likes Given
      148

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      Quote By Malila
      Hata mimi niliposikia nikakosa jibu,lakini ni jambo la kawaida mitaani kusikika hasa huku Pwani.
      Sehemu nyingi tu wanaamini hivyo. Ni kweli kabisa. Kitovu kikiangukia uume wa mtoto mchanga wakati kinapokatika mara baada ya mtoto kuzaliwa mtoto hukua bila nguvu za kiume. Ndo maana wamama huwa wako makini sana na watoto wao. Yaani ndo basi tena, jogoo hatapanda mtungi. Sababu zenyewe ni za kisaikolojia zaidi. Mtoto anakuwa affected kitovu kikigonga uume kinapokatika.
      God writes straight with crooked lines.

    16. #14
      Askofu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th February 2009
      Location : Synagogue
      Posts : 1,672
      Rep Power : 857
      Likes Received
      77
      Likes Given
      64

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      Hii hadithi imakuwa ikisimuliwa for ages, especially kwa wanawake. Na hata pale unapotoka kujifungua nurses wanakwambia namna ya kuangalia kitovu cha mtoto, kusafisha mpaka kikauke, na hapo ndipo wanakwambia kwamba uwe makini kitovu kisidondoke kwenye uume wa mtoto. Sasa hili ni la ki-medical au ki-imani?
      Politicians and Diapers needs to be changed for the same reason...

    17. #15
      agika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2009
      Posts : 385
      Rep Power : 584
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      mhhhh mwenzangu hata mimi nilipojifungua mwanangu niliambiwa hivyohivyo, ila bwana i culdnt dare kubisha, nikasema hata kama siamini sitaki mwanangu awe ndo test na ukizingatia psychology ya mama anapotoka tu kujifungua akili yote inakuwa kwa mtoto na hutaki baya lolote litokee juu yake,basi nilikuwa nawatch kile kitovu kama nini sijui, kilikatika siku ya saba ndio nikaanza hata kulala usingizi, nadhani ni imani tu ila mama akiambiwa hivyo huwa anaamini kwa wakati ule, nani anyetaka mtoto wake asiwe rijali? akamletea mkwe na vijukulu jamani?
      ---------------------
      " To the Degree that you believe you will achieve"

    18. #16
      Oxlade-Chamberlain's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2009
      Location : dodoma
      Posts : 7,616
      Rep Power : 4422
      Likes Received
      789
      Likes Given
      750

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      mimi nilisikia kitovu kikimdondokea mtoto wakike kwenye sehemu zake za siri atakuwa anajikojolea mpaka ukubwani sasa sijui kweli.
      "Nobody has enough talent to live on talent alone. Even when you have talent, a life without work goes nowhere". A. Wenger

    19. #17
      Mshiiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th June 2008
      Location : Sillicon Valley - USA
      Posts : 1,351
      Rep Power : 1233
      Likes Received
      58
      Likes Given
      17

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      Anecdote!
      “You will not be punished for your anger; you will be punished by your anger.”

    20. #18
      Ng'azagala's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 7th June 2008
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 988
      Rep Power : 756
      Likes Received
      79
      Likes Given
      296

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      Quote By agika
      mhhhh mwenzangu hata mimi nilipojifungua mwanangu niliambiwa hivyohivyo, ila bwana i culdnt dare kubisha, nikasema hata kama siamini sitaki mwanangu awe ndo test na ukizingatia psychology ya mama anapotoka tu kujifungua akili yote inakuwa kwa mtoto na hutaki baya lolote litokee juu yake,basi nilikuwa nawatch kile kitovu kama nini sijui, kilikatika siku ya saba ndio nikaanza hata kulala usingizi, nadhani ni imani tu ila mama akiambiwa hivyo huwa anaamini kwa wakati ule, nani anyetaka mtoto wake asiwe rijali? akamletea mkwe na vijukulu jamani?
      ni kweli ni vigumu kudharau suala hili, hata my wife wangu alipata shida sana kwani alielekezwa hivyo pale Mhimbili, na hatukudhubutu kufikiria kudharau kwani suala lenyewe linagusa mahali pabaya sana (kama Rais Mstaafu Mzee Mwinyi alivyokuwa akisema).

    21. #19
      X-PASTER's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Firdaws (Paradise)
      Posts : 11,859
      Rep Power : 7687
      Likes Received
      1467
      Likes Given
      0

      Default Re: kudondokewa na kitovu

      Quote By Malila
      Nimepata kusikia huko uswahilini kuwa, eti mtoto wa kiume akidondokewa na kitovu chake ndo basi tena. Yaani jogoo halitapanda mlima. Mimi sioni uhusiano wa kisayansi hapo. Je kuna ye yote ajuaye anisaidie/atusaidie kupata ukweli wa jambo hili?
      Hii ni mila ya siku nyingi sana, na imerithishwa kizazi hadi kizazi.

      Madhumuni haswa ya kina mama kuambiwa hivyo, ni kuwataka wawe makini sana na kidonda kilichopo hapo (Kitovuni), kwani wakifanya mchezo na kidonda kikipata athali yoyote (Bacteria na Vijidudu vya Pepo punda), Mama anaweza kumkosa mtoto wake.

      Ili wazazi (wakina mama) wawe makini na kumuangalia mtoto, ndio ikaja dhana hiyo ya Kitovu cha mtoto kiangaliwe sana ili kisije kumuangukia mtoto na kuwa na matatizo hayo yaliyo tajwa, na hii ni kuwa tunazingatia sana urijali na kuendeleza familia zetu.
      “I am the punishment of God... If you had not committed great sins, God would not have sent a punishment like me upon you.”

      'O Allah! Keep me alive as long as life is better for me, and let me die if death is better for me.

      (¯`·._.•X-Paster™•._.·´¯)


    22. #20
      Malila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2007
      Posts : 2,605
      Rep Power : 10971
      Likes Received
      828
      Likes Given
      447

      Thumbs up Re: kudondokewa na kitovu

      Quote By X-PASTER
      Hii ni mila ya siku nyingi sana, na imerithishwa kizazi hadi kizazi.

      Madhumuni haswa ya kina mama kuambiwa hivyo, ni kuwataka wawe makini sana na kidonda kilichopo hapo (Kitovuni), kwani wakifanya mchezo na kidonda kikipata athali yoyote (Bacteria na Vijidudu vya Pepo punda), Mama anaweza kumkosa mtoto wake.

      Ili wazazi (wakina mama) wawe makini na kumuangalia mtoto, ndio ikaja dhana hiyo ya Kitovu cha mtoto kiangaliwe sana ili kisije kumuangukia mtoto na kuwa na matatizo hayo yaliyo tajwa, na hii ni kuwa tunazingatia sana urijali na kuendeleza familia zetu.
      Naweza kukubaliana na wewe,yaani wana-draw attention ya wazazi juu ya kidonda. Kitovu kinapodondoka hakina tena communication na sehemu nyingine ya mwili,kwanza huwa kimekufa,sasa taarifa toka kwenye kitovu mfu kwenda kwenye mwili hai ni ngumu kidogo. Kateni nondo tuendelee kufaidi.

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...