Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nifanyeje kuacha kabisa kunywa pombe?

    Report Post
    Page 2 of 16 FirstFirst 123412 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 319
    1. #1
      Makanyagio's Avatar
      Member Array
      Join Date : 25th June 2009
      Location : Nyakato Mwanza
      Posts : 82
      Rep Power : 520
      Likes Received
      8
      Likes Given
      2

      Default Msaada dawa ya kuacha pombe

      Wana JF,
      Kwa yeyote anejua dawa au mbinu ya kumfanya mlevi kuacha pombe. Nina ndugu yangu yeye bila kilevi cha pombe siku haiendi kabisaa na hii imekuwa inarudisha maendekleo yake nyuma.
      Wanaoijua tiba mnijuze niokoe maisha yake na familia yake.
      snochet likes this.
      'There is no fair in this world'

    2. FemaTV & Radio

    3. #21
      Ladslaus Modest's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th June 2008
      Location : Nachunga Kondoo
      Posts : 638
      Rep Power : 683
      Likes Received
      3
      Likes Given
      1

      Default Re: Msaada dawa ya kuacha pombe

      Quote By Makanyagio
      Wana JF,
      Kwa yeyote anejua dawa au mbinu ya kumfanya mlevi kuacha pombe. Nina ndugu yangu yeye bila kilevi cha pombe siku haiendi kabisaa na hii imekuwa inarudisha maendekleo yake nyuma.
      Wanaoijua tiba mnijuze niokoe maisha yake na familia yake.
      Ndugu yangu, Dawa ni moja tu nayo ni YESU

      Aokoke kwa kumchagua Yesu kuwa Mungu na Bwana na Mwokozi wa Maisha yake.

      Yesu ameponya walevi wengi.

      Kwa Yesu yote yanawezekana.
      KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI; KIDUMU CHAMA TAWALA; CCM NI NAMBARI WANI. CCM HOYEEEEEEE!
      "Mungu katika Jina la Yesu akusamehe Maovu yako yote, na Kukuponya Magonjwa yako yote
      (Zaburi 103:3)"

    4. #22
      Anyisile Obheli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th December 2009
      Location : Rohoni
      Posts : 3,261
      Rep Power : 1125
      Likes Received
      68
      Likes Given
      82

      Default Re: Msaada dawa ya kuacha pombe

      kwani alinzaje? na ataacha kama alivyoanza
      ........................HAKUNA TIBA YA KIFO............
      HESHIMU WATU NA PIA JIHESHIMU, KISHA, MPENDE MUNGU

    5. #23
      Sipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th July 2008
      Location : SIPAJUI
      Posts : 2,167
      Rep Power : 985
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default Re: Msaada dawa ya kuacha pombe

      Quote By anyisile obheli
      kwani alinzaje? na ataacha kama alivyoanza
      i recomend this piece of advice to everyone of us
      "Ficha Upumbavu wako, husifiche hekima yako'' Invisible

    6. #24
      kakuruvi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2009
      Posts : 609
      Rep Power : 620
      Likes Received
      108
      Likes Given
      59

      Default Uliacha vipi pombe?

      Pombe ni kitu ambacho hakikubaliki kabisa kwa baadhi ya madhehebu ya dini, na wanaotumia huwa wanajifichaficha, pombe ni bidhaa ambayo ikikukolea kuacha ni tabu kweli kweli.
      Sikiliza hii. Bibie mmoja alikuwa akikasirishwa na tabia ya mumewe kulewa tena kila siku, kila anapomsihi aache pombe ilikuwa ni ugomvi mkubwa, siku moja alimuomba atakaporudi arudi na kitoweo cha nyama kwani tangu Christmas ya mwaka uliopita hawajawahi kula nyama tena hapo nyumbani, jamaa aliafiki kwani yeye huwa akila akiwa baa.
      Kabla ya kurudi jamaa alipitia butcher na kununua nyama lakini alionelea apitie baa japo apate moja mbili. Waliendelea kunywa na rafiki zake huku akimuomba mchoma mishikaki akate japo kidogo ile nyama ya kupeleka nyumbani, waliendelea kidogo kidogo mpaka yote ikaisha.
      Saa za kurudi jamaa alirudi akiwa chakali, na mkewe alimfungulia na kwa bahati mbaya jamaa alitapika sebuleni, na vipande vya nyama vilionekana dhahiri. Mkewe hakutaka shari akamkokota mpaka chumbani akamlaza vizuri na kumfunika. Jamaa akachapa usingizi. Mkewe akarudi kupiga deki matapishi na kuokota vipande vyote vya nyama na kuvihifadhi kwenye bakuli.
      Asubuhi mkewe aliamka mapema na kusonga ugali nakuandaa meza likiwemo bakuli la nyama aliyoitapika jamaa usiku akafunika vizuri kwa KAWA. Jamaa alipoamka na kuoga alikaribishwa mezani, hamadi! alipofunua bakuli alikumbana na nyama yenye harufu ya matapishi ya kilevi akapandisha hasira na kufoka '' umepata wapi nyama hii?'' Mkewe kwa kujiamini na sauti ya upendo akajibu ''Ulituletea jana mume wangu, mimi na watoto tulishakula ya kwetu usiku''
      Jamaa alifedheheka sana, na akaamua toka siku hiyo pombe basi na kila akipata pesa mboga nzuri ikiwemo nyama ililiwa nyumbani kwake sio mpaka siku ya Christmas. Wana JF leteni mikasa iliyosababisha watu fulani kuacha kabisa pombe. Ijumaa njema na wikiendi njema.

    7. #25
      Kimbweka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th July 2009
      Posts : 7,878
      Rep Power : 7239
      Likes Received
      1281
      Likes Given
      105

      Default Re: uliacha vipi pombe?

      Jamaa mmoja alikuwa ni mshindaa baa mpaka asubuhi ! Sasa ikatokea kaenda kwa wakwe kijijini siyo mbali sana na mjini anapoishi! Basi baada ya kuwajulia hali na vijizawadi vya hapa na pale akaaga kurudi mjini kwa mkewe na watoto! Wakwe kwa ukarimu wakampatia jogoo ili watoto wakinjoi minofu yake! Kwakuwa ilikuwa ni wikiendi, jamaa alipofika mjini kama kawa wakawasiliana na washikaji zake na kupanga pa kukutana ili kutuanga masanga kisawasawa! Basi wakakutana kwenye baa waliyoizoea wakaanza kutwanga pombe na yule jogoo wakamuweka chini ya meza! Mjamaa ikapiga pombe na kusahau kama kuna jogoo anatakiwa kufikishwa nyumbani ... saa 2 usiku 3,4,5...8,9...10 alfajiri.....mara jogoo likawika chini ya meza kokolikooooooooooooo....! Jamaa walizinduka na kutimuka mbio wakizani ni wanga wameingia! Kufika home huku akihema kagonga hodi kwa nguvu na kufunguliwa ...mkewe kwa upole kamuuliza vp mbona umechelewa sana na yule jogoo wazazi waliyekupa umlete yuko wapi... Jamaa ndiyo akili ikamrudi kuwa aliyewika ni wake na si Mwanga ....ila sijui kama aliacha pombe
      "Life comes once only: No retake/replay/rewind/once-more. One should enjoy it, be happy & keep happy others too."

    8. Miaka 50

    9. #26
      Ngalikihinja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2009
      Posts : 4,466
      Rep Power : 1456
      Likes Received
      1018
      Likes Given
      97

      Default Re: uliacha vipi pombe?

      Pombe huwa inaachwa kwa sababuza kiafya (mpaka daktari aseme) au uchafu utakaokutana nao kwenye pombe.............

      kuna jamaa alikuwa anagombana na mkewe kila kukicha kwa sababu y apombe za kienyezi maarufu kama mataputapu. Bi mkubwa alichofanya ni kuongea na mama muuza amletee pombe nyumbani. Bi mkubwa kaitunza ile pombe mpaka siku ya pili jamaa alikuwa nyumbani akapewa ile pombe. Jamaa akawa anakunywa tar-tiiiibu. Ile kufika mwisho si akakutana na vitoto vitogo viwili vya panya........ Jamaa kwa kichefuchefu alichokuwa nacho alitapika sana na mwisho akaamua kuacha pombe maana kila akisogeza pombe mdomoni, ile picha ya vitoto vya panya visivyo na manyoya inamjia na hapo hapo anaanza kutapi.

    10. #27
      Masaki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 3,042
      Rep Power : 1285
      Likes Received
      333
      Likes Given
      770

      Default Re: uliacha vipi pombe?

      Quote By Ngalikihinja
      Pombe huwa inaachwa kwa sababuza kiafya (mpaka daktari aseme) au uchafu utakaokutana nao kwenye pombe.............

      kuna jamaa alikuwa anagombana na mkewe kila kukicha kwa sababu y apombe za kienyezi maarufu kama mataputapu. Bi mkubwa alichofanya ni kuongea na mama muuza amletee pombe nyumbani. Bi mkubwa kaitunza ile pombe mpaka siku ya pili jamaa alikuwa nyumbani akapewa ile pombe. Jamaa akawa anakunywa tar-tiiiibu. Ile kufika mwisho si akakutana na vitoto vitogo viwili vya panya........ Jamaa kwa kichefuchefu alichokuwa nacho alitapika sana na mwisho akaamua kuacha pombe maana kila akisogeza pombe mdomoni, ile picha ya vitoto vya panya visivyo na manyoya inamjia na hapo hapo anaanza kutapi.
      Mmmmmh! Hii hata mimi ningeacha pombe!
      Ability may get you to the top, but it takes character to keep you there.

    11. #28
      kakuruvi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2009
      Posts : 609
      Rep Power : 620
      Likes Received
      108
      Likes Given
      59

      Default Re: uliacha vipi pombe?

      Hata kama ni wewe ile kufikiri tu unakula vipanya ukisogelea tu kichefuchefu, lazima uache...

    12. #29
      kakuruvi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2009
      Posts : 609
      Rep Power : 620
      Likes Received
      108
      Likes Given
      59

      Default Re: uliacha vipi pombe?

      Quote By Kimbweka
      Basi wakakutana kwenye baa waliyoizoea wakaanza kutwanga pombe na yule jogoo wakamuweka chini ya meza! Mjamaa ikapiga pombe na kusahau kama kuna jogoo anatakiwa kufikishwa nyumbani ... saa 2 usiku 3,4,5...8,9...10 alfajiri.....mara jogoo likawika chini ya meza kokolikooooooooooooo....! sijui kama aliacha pombe?
      Aliacha huyo.

    13. #30
      kakuruvi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2009
      Posts : 609
      Rep Power : 620
      Likes Received
      108
      Likes Given
      59

      Default Re: uliacha vipi pombe?

      Kwa kawaida simba hali binadamu mpaka aonje japo mara moja hapo ataendelea, Jamaa mmoja alipokuwa anarudi kilabuni akakutana na mnyama huku akifikiri ni mbwa, kwa sauti ya kilevi akamfokea ''we, kijimbwa koko nta-ntafuta ni-niniii saa izi'' kumbe alikuwa simba, aligundua kesho yake asubuhi alipokuta dume lake kubwa la ngombe halipo zizini na michirizi ya damu kuelekea porini na baada ya msako walimkurupusha simba akila ng'ombe wake si mbali sana na nyumbani, akawaungurumia wakakimbia naye akapotelea porini, kwa kunusurika huko jamaa hajanywa pombe tena mpaka leo.

    14. #31
      Baba_Enock's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Bunju "B"
      Posts : 5,818
      Rep Power : 1899
      Likes Received
      1161
      Likes Given
      977

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Siwezi kuacha Pombe!
      Ad Majorem Dei Gloriam - "For the greater glory of God"

    15. #32
      Utamaduni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Home
      Posts : 744
      Rep Power : 744
      Likes Received
      82
      Likes Given
      53

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Bibi yangu mzaa mama alikuwa mlevi sana wa pombe, yaani ni lazima anywe kila siku tena zile pombe za watu wa songea plus ulanzi.

      Watoto wake walikaa na kupanga jinsi ya kumfanya mama yao aache pombe, kwani kila siku anapokunywa anatukana hovyo na kuleta tabia mbaya mbaya mbele ya wajukuu na wao pia. wakamvisia siku moja akiwa amelewa sanaaaa, (kijijini) wakachukua kinye** cha mtoto mdogo na kumuwekea kwenye nguo zake ili aonekane yeye ndio amejiny*a kisha wakambeba na kumlaza nje.

      Asubuhi alipoamka aliona aibu sana kwamba analewa hadi anajisaidia na kulala nje. Toka siku hiyo akaacha pombe yeye mwenyewe bila kuambiwa, na sasa hivi pamoja na ukongwe wake alionao walau ana afya kuliko angeendelea kunywa sijui kama mimi ningelimuona hadi leo.
      JK Ni Rais wa watu mil.5 kwenye nchi ya watu mil.50 (By vote)

    16. #33
      Malila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2007
      Posts : 2,605
      Rep Power : 10971
      Likes Received
      828
      Likes Given
      447

      Talking Re: Uliacha vipi pombe?

      Sasa hicho kitendo mbele za Mungu si dhambi kubwa,yaani kumfanya bibi yenu adhani amejinyea kumbe sio,hata hivyo ilikuwa dawa poa sana.
      Mtu mwema huacha urithi kwa wana wa wanawe.

    17. bht
      #34
      bht's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2009
      Posts : 9,949
      Rep Power : 2499
      Likes Received
      1434
      Likes Given
      909

      Default Re: uliacha vipi pombe?

      Quote By Masaki
      Mmmmmh! Hii hata mimi ningeacha pombe!
      ntajitolea kukuwekea Masaki............
      You dont have to win every Argument, Agree to Disagree

    18. #35
      kakuruvi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2009
      Posts : 609
      Rep Power : 620
      Likes Received
      108
      Likes Given
      59

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Quote By Baba_Enock
      Siwezi kuacha Pombe!
      Wakati Marijani Rajabu anaimba wimbo wa Masudi kuna beti inasema ''mkaidi hafaidi mpaka yamkute''
      MziziMkavu likes this.

    19. #36
      kakuruvi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2009
      Posts : 609
      Rep Power : 620
      Likes Received
      108
      Likes Given
      59

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Quote By Malila
      Sasa hicho kitendo mbele za Mungu si dhambi kubwa,yaani kumfanya bibi yenu adhani amejinyea kumbe sio,hata hivyo ilikuwa dawa poa sana.
      Heri lawama kuliko fedheha.

    20. #37
      Ngalikihinja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2009
      Posts : 4,466
      Rep Power : 1456
      Likes Received
      1018
      Likes Given
      97

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Quote By Baba_Enock
      Siwezi kuacha Pombe!
      Tutakutafuta ukiwa umelewa chakali halafu tunakuwekea ute wa yai "HUKO MCHAMBAWIMA" kesho yake ukikagua ukakuta utelezi.......... LAZIMA UTAACHA............

    21. #38
      Kichwa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 15th March 2007
      Posts : 120
      Rep Power : 647
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Mimi niliacha pombe baada ya kusahau nyumbani nakupitiliza mochwari na mlinzi alivyo mhuni akanilaza kwenye jokofu kwa dakika 3 mpaka leo nimeokoka.
      MziziMkavu likes this.
      The brave man is not he who does not feel afraid, but he who conquer that fear . Neslon Mandela

    22. #39
      Mahai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th January 2010
      Posts : 351
      Rep Power : 545
      Likes Received
      26
      Likes Given
      29

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Hii yangu ni ya kweli kabisa.

      Kaka mmoja alikuwa mlevi kupindukia. Alibahatika kuchumbia mwanamke ambaye wanatoka kijiji kimoja huko moshi marangu ila yeye anakaa mjini. Mwezi mmoja kabla ya harusi yake akiwa huko marangu kama kawaida yake akatoka kwenda kunywa. Akalewa sana na bahati mbaya mvua kubwa ikaanza kunyesha so ikabidi ajikongoje kwenda nyumbani. Hakufika mbali akaanguka kwenye matope chini ya mgomba akawa anajikongoja kuamka ila anashidwa maana amelewa sana. Bahati mbaya wakwe zake watarajiwa wakapita wakamuona wakamuokota na kumkokota mpaka nyumbani kwao (kwa wakwe), kesho yake asubuhi anaamka nyumba tofauti amechafuka matope wakwe wanamtolea macho... Je hivi ndivyo utaenda kututesea mtoto wetu?

    23. #40
      Ngalikihinja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2009
      Posts : 4,466
      Rep Power : 1456
      Likes Received
      1018
      Likes Given
      97

      Default Re: Uliacha vipi pombe?

      Quote By Kichwa
      Mimi niliacha pombe baada ya kusahau nyumbani nakupitiliza mochwari na mlinzi alivyo mhuni akanilaza kwenye jokofu kwa dakika 3 mpaka leo nimeokoka.
      Hii ndo shida ya kunywa karibu na mochwari............
      MziziMkavu likes this.

    Page 2 of 16 FirstFirst 123412 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...