Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Madhara ya Bangi

    Report Post
    Results 1 to 16 of 16
    1. #1
      Maasai_'s Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th June 2012
      Posts : 17
      Rep Power : 351
      Likes Received
      2
      Likes Given
      6

      Default Madhara ya Bangi

      Naomba kufahamu madhara ya Bangi kwani wengine wanasema ni dawa na mi natumia
      Last edited by Maasai_; 5th July 2012 at 17:12.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Adrian Stepp's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2011
      Posts : 1,573
      Rep Power : 714
      Likes Received
      438
      Likes Given
      2560

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Quote By Maasai_
      Nipe madhara ya Bangi kwani wengine wanasema ni dawa
      Tukupe? we nani mbaka upewe?? sema naomba kufahamu..nyama we
      Watu wakimya wamejaliwa busara, ufahamu na midomo inayonuka!

    4. #3
      paty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : never never land
      Posts : 1,025
      Rep Power : 975
      Likes Received
      270
      Likes Given
      62

      Default Re: Madhara ya Bangi

      haina madhara .
      CHADEMA mwendo mdundo - T 2015 CDM

    5. #4
      Mbimbinho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st August 2009
      Posts : 1,834
      Rep Power : 866
      Likes Received
      470
      Likes Given
      210

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Bangi can cure cancer I heard.
      Mbwa ukimjua jina wala hakupi shida....

    6. #5
      Maasai_'s Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th June 2012
      Posts : 17
      Rep Power : 351
      Likes Received
      2
      Likes Given
      6

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Kiswahili kigumu mkuu huoni we mwenyewe badala ya kutype mpaka umetype mbaka
      Quote By anders batta
      Tukupe? we nani mbaka upewe?? sema naomba kufahamu..nyama we


    7. C6
      #6
      C6's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2011
      Location : Mtaa Wa Saba
      Posts : 3,084
      Rep Power : 19361
      Likes Received
      1775
      Likes Given
      1513

      Default

      Quote By Maasai_
      Naomba kufahamu madhara ya Bangi kwani wengine wanasema ni dawa na mi natumia
      bangi ni majani yaliyokaushwa ya mmea ujulikanao kitaalamu kama canabis sativa na mwingine ujulikanao kama canabis indica. bangi ina majina meeeengi kutokana na maeneo inakotumika, marijuana, hashish, na mengineyo

      kemikali iliyo ndani ya bangi hujulikana kama delta-9-tetrahydrocannabinol kwa kifupi (Δ9-THC). kiasi kidogo kabisa kinachoweza kusababisha effect mwilini mwako ni kuanzia microgram 10 kwa kila kilo ya uzito wako...


      baadhi ya matumizi ya bangi kiafya ni pamoja na;

      hutumika kwenye dawa za kutuliza kikohozi na kichefuchefu,

      pia inatumika kwenye dawa za glaucoma (presha kwenye macho)

      Marihuana pia hutumika kupunguza maumivu kwa wagonjwa wa kansa na ukimwi walio kwenye hatua ya mwisho


      madhara ya bangi ni: euforia(kujisikia haireee), midomo kukauka, heat sensation, mapigo ya moyo kuongezeka........ etc



      ngoja nikomeee hapo kwa sasa
      MziziMkavu and Maasai_ like this.

    8. #7
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,243
      Rep Power : 19221
      Likes Received
      8175
      Likes Given
      26702

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Hasara ya Kuvuta Sigara kubwa ''Bangi''

      BAADA ya kuwepo kwa baadhi ya tafiti zilizokuwa zikiruhusu uvutaji wa bangi kwa madai kwamba ilisaidia wagonjwa waliosumbuliwa na msongo wa mawazo, hali hiyo imesababisha baadhi ya nchi kuruhusu matumizi yake.

      Pamoja na mawazo ya wengi kufikiria kuwa kutokana na nchi ya Jamaica ndiyo ilikuwa mstari wa mbele kwa watumiaji wengi ingekuwa ya kwanza kuruhusu bangi, lakini ukweli ni kwamba nchi ya Canada

      ndiyo ilikuwa ya kwanza kukubali bangi kutumiwa kama dawa ya maradhi.
      Baada ya utafiti huo wa awali hivi karibuni watafiti wengine wamegundua kuwa matumizi ya bangi kwa muda mrefu yanasababisha kujiongezea madhara badala ya kutibu kama ilivyokuwa ikisemekana hapo awali.

      Watafiti hao wamekwenda kinyume na wale wa kwanza kwa kusema kuwa matumizi yake yana uwezekano mkubwa wa kumletea mtumiaji magonjwa ya kupungua uzito mara kwa mara, magonjwa ya figo, ini na ugonjwa wa akili.

      Watafiti waliogundua athari hizo ni wale wanaotokea nchini Australia ambao katika utafiti wao wamegundua kuwa zaidi ya vijana 3,100 walio katika umri wa miaka 20 ndio wamekuwa watumiaji wakubwa wa bangi.

      Utafiti wao umekwenda mbali na kubaini kwamba asilimia 18 ya vijana hao ni wale waliojiingiza katika matumizi ya dawa hizo za kulevya kwa muda wa miaka miwili au mitatu.
      Asilimia nyingine 16 ya vijana wa umri huo wamebainika kutumia kwa muda wa kati ya miaka minne hadi mitano.

      65 kati ya watumiaji wamegundulika wameshaathirika na maradhi ya ugonjwa wa akili.
      Wakati hao wakisumbuliwa na tatizo hilo wengine 233 wamebainika kuathirika kwa figo na ini.

      Watafiti wamebaini vijana wengine kati yao wanasumbuliwa na tatizo la kupata uchizi (wehu).
      Baada ya kubaini hayo watafiti wametoa ushauri kwa vijana kutotumia dawa hizo za kulevya kwa vijana kwa zaidi ya miaka sita au zaidi tangu pale siku ya kwanza alipoanza kutumia.

      Wanasema kuwa kwa wale ambao sasa wamevuta kwa muda mrefu kati ya miaka 15 na zaidi wengi wao wamekumbwa na tatizo la kiakili.

      Kwa mujibu wa Dk. John McGrath, wa kituo cha uchunguzi wa afya ya wagonjwa wenye mtindio wa ubongo cha Queensland, nchini Marekani, anasema: “Wengi wa wagonjwa ambao wamekumbwa na matatizo hayo tumegundua ni wale waliowahi kutumia bangi kwa muda mrefu na hatimaye kujikuta wakipata tatizo la akili.”

      Daktari huyo anasema kuwa ni nadra sana kukutana na wagonjwa wa akili vijana halafu wakawa hawajawahi kutumia bangi, iwe mwaka mmoja au zaidi.
      Anasema kuwa iwapo matumizi ya bangi yatakomeshwa tatizo la vijana kupata matatizo ya utaahira yatapungua kwa kiasi kikubwa duniani.

      Bangi ni nini, inatumiwaje?

      Kwa hapa nchini na baadhi ya nchi, bangi imetambulika kama dawa ya kulevya ambayo imekuwa na majina mengi kutokana na kutumiwa na kundi la vijana zaidi kuliko watu wazima.
      Bangi imekuwa ikijulikana kwa majina mengi ikiwamo, dawa, ganja, hashish, kijiti, marijuana, kaya blunt na mengineyo, ilimradi kutegemeana na sehemu inapotoka.

      Watumiaji wengi wamekuwa wakiitumia kwa kuvuta kama sigara au wengine hutumia kwenye kiko kwa kuvuta.

      Bangi ni bidhaa iliyochanganyika na kemikali hatari ambazo ni sumu na huathiri afya.
      Wapo baadhi ya watumiaji wa bangi ambao wamekuwa wakiitumia kwa kuiweka katika maji wakiifanya kama majani ya chai na wengine huchanganya kwenye chakula.
      Bangi inaathiri vipi ubongo?

      Wanasayansi wamebaini kuwa matatizo makubwa yanaanza kupatikana kutokana na bangi kuingia kwenye ubongo wa mtumiaji na huathiri mfumo mzima wa akili.

      Tatizo kubwa linalomkumba mvuta bangi ni kunyemelewa na magonjwa ya ugonjwa wa shinikizo la damu (BP), kupoteza kumbukumbu, mawazo, anaridhika hata kama ana matatizo.

      Pia mtumiaji wa kila siku anakuwa akikumbwa na mabadiliko ya mara kwa mara katika ubongo wake.
      Imebainika kuwa bangi inachangia kuongeza mapigo ya moyo kutoka asilimia 20 hadi 100, muda mfupi tu wa saa tatu baada ya kuvuta.
      Bangi huaribu mapafu, kwani ina zaidi ya asilimia 50–70 ya kemikali aina ya carcinogenic hydrocarbons kuliko mvutaji wa tumbaku.

      Mtumiaji wa bangi hupumua kwa tabu sana kuliko yule anayevuta tumbaku ingawa wote wanaharibu mapafu, pamoja na kuwa na uwezekano mkubwa wa kukaribisha ugonjwa wa kansa.

      Imebainika kuwa watu wanaovuta bangi wamekuwa wakisumbuliwa zaidi na matatizo mengi ya kiafya.
      Watafiti wamegundua kuwa wavutaji wengi wa bangi wamekuwa hawana mahusiano mema na watu walionao karibu kwani wamekuwa chanzo cha matatizo kutokana na wao kuona kila wanachofanya ndiyo sahihi na cha wenzao si sahihi.@
      Maasai_
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    9. #8
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,243
      Rep Power : 19221
      Likes Received
      8175
      Likes Given
      26702

      Default Re: Madhara ya Bangi

      ATHARI ZA BANGI


      BANGI


      Bangi ni mmea wenye rangi ya kijani,ambao hutoa majani na maua ambayo hutumika kama kilevi.Bangi hustawi karibu maeneo yote hapa nchini na hutumika zaidi kuliko dawa zingine za kulevya.


      Bangi hupatikana kwa wingi katika mikoa ya Mara,Iringa,Arusha,Kilimanjaro ,Shinyanga,Tabora,Tanga,Kagera ,Mbeya.Morogoro.n.k


      Madhara ya Bangi


      Matumizi ya bangi husababisha madhara mbali mbali ikiwa ni pamoja na:


      · Kuchanganyikiwa,ukatili,ukorof i,uhalifu,n.k.


      · Kuona,kusikia na kuhisi vitu visivyokuwepo.


      · Kupoteza kumbukumbu


      · Utegemezi na usugu


      · Moshi wa bangi unapoingia kwenye mapafu hutengeneza kitu kama lami ambayo huganda na kuathiri utendaji kazi wa mapafu.


      · Bangi ni kemikali (sumu) inayosababisha (saratani) zaidi ya tumbaku (sigara).


      · Kupunguza kinga ya mwili


      · Mtumiaji kuridhika na hali duni aliyonayo hivyo kukosa mwamko wa maendeleo huku akijihisi ni mwenye mafanikio makubwa.


      · Kuumwa koo,kupata kikohozi na saratani ya mapafu.


      · Kuathirika kwa mfumo wa uzazi ikiwa ni pamoja na kuzaa watoto wenye mtindio wa ubongo na mabadiliko ya hedhi kwa wanawake.


      · Kuharibika mimba


      · Kuzaa mtoto njiti


      Imani na hisia potofu kuhusu uvutaji wa bangi


      Je ni kweli bangi huongeza uwezo wa kusoma na kuelewa zaidi?Hapan.Bangi hufanya mishipa ya damu na ubongo kusinyaa,kunakosababisha kupungua kwa uwezo wa kufikiri na kukumbuka.Utafiti umebainisha kuwa wanafunzi waliovuta bangi kwa matarajio hayo wameshindwa kufaulu.


      Utajiepushaje na utumiaji wa bangi?


      · Jiepushe na makundi ya watumia bangi


      · Shiriki kwenye michezo


      · Jifunze na kuzingatia stadi za maisha


      Sheria inasemaje kuhusu bangi?


      Kutumia,kuhamasisha matumizi,kuuza,kusafirisha,kuh ifadhi au kujihusisha kwa namna yoyote ile na bangi ni kosa la jinai.Adhabu kwa makosa haya hufikia hadi kifungo cha maisha
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    10. #9
      Baba V's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Location : Buguruni Mnyamani
      Posts : 10,962
      Rep Power : 30234
      Likes Received
      4726
      Likes Given
      3477

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Canabis,jani, ndumu,kijiti,cha arusha,herb,hemp....

    11. #10
      BAGAH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2012
      Posts : 4,364
      Rep Power : 8786
      Likes Received
      954
      Likes Given
      1418

      Default Re: Madhara ya Bangi

      tangu nimeanza kutumia sijapata MADHARA.!
      Amsterdam likes this.

    12. #11
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,243
      Rep Power : 19221
      Likes Received
      8175
      Likes Given
      26702

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Quote By BAGAH
      tangu nimeanza kutumia sijapata MADHARA.!
      Subiri mkuu Madhara yake utayaona baadae sio sasa wakati utakapoumwa au kushauriwa na Daktari uache ndio hapo Madhara yatakuwa yameshakuingia BAGAH
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    13. #12
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,706
      Rep Power : 16252
      Likes Received
      3155
      Likes Given
      4076

      Default Re: Madhara ya Bangi

      hebu cheki hizi faida alafu unasema bangi inaasara wacha habari yako
      http://www.jamiiforums.com/jamii-int...onspiracy.html

    14. #13
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,706
      Rep Power : 16252
      Likes Received
      3155
      Likes Given
      4076

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Quote By BAGAH
      tangu nimeanza kutumia sijapata MADHARA.!
      http://www.jamiiforums.com/jamii-int...onspiracy.html

    15. #14
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,706
      Rep Power : 16252
      Likes Received
      3155
      Likes Given
      4076

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Quote By MziziMkavu
      Subiri mkuu Madhara yake utayaona baadae sio sasa wakati utakapoumwa au kushauriwa na Daktari uache ndio hapo Madhara yatakuwa yameshakuingia BAGAH
      mzizi mkavu ulikutana na hii
      http://www.jamiiforums.com/jamii-int...onspiracy.html

    16. #15
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,706
      Rep Power : 16252
      Likes Received
      3155
      Likes Given
      4076

      Default Re: Madhara ya Bangi

      Quote By MtotoSix
      bangi ni majani yaliyokaushwa ya mmea ujulikanao kitaalamu kama canabis sativa na mwingine ujulikanao kama canabis indica. bangi ina majina meeeengi kutokana na maeneo inakotumika, marijuana, hashish, na mengineyo

      kemikali iliyo ndani ya bangi hujulikana kama delta-9-tetrahydrocannabinol kwa kifupi (Δ9-THC). kiasi kidogo kabisa kinachoweza kusababisha effect mwilini mwako ni kuanzia microgram 10 kwa kila kilo ya uzito wako...


      baadhi ya matumizi ya bangi kiafya ni pamoja na;

      hutumika kwenye dawa za kutuliza kikohozi na kichefuchefu,

      pia inatumika kwenye dawa za glaucoma (presha kwenye macho)

      Marihuana pia hutumika kupunguza maumivu kwa wagonjwa wa kansa na ukimwi walio kwenye hatua ya mwisho


      madhara ya bangi ni: euforia(kujisikia haireee), midomo kukauka, heat sensation, mapigo ya moyo kuongezeka........ etc



      ngoja nikomeee hapo kwa sasa
      kwa maana hiyo basi wengi wetu tumeshakula sana bangi kwakutokujua eeeeeeeeeee

    17. #16
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,706
      Rep Power : 16252
      Likes Received
      3155
      Likes Given
      4076

      Default Re: Madhara ya Bangi


    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...