Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: new HIV

    Report Post
    Results 1 to 16 of 16
    1. #1
      njoro's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st December 2010
      Posts : 178
      Rep Power : 462
      Likes Received
      5
      Likes Given
      5

      Default new HIV

      Mara baada ya kuambukizwa HIV, dalili za mwanzo ni zipi? na inachukua muda gani hizo dalili kuanza kujitokeza? Naombeni kujuzwa jamani

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Mchaka Mchaka's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 20th July 2010
      Location : Ashmore and Cartier Islands
      Posts : 3,660
      Rep Power : 1206
      Likes Received
      915
      Likes Given
      457

      Default Re: new HIV

      Ndio shida ya kupiga kavu,,,,unakuwa na wasiwasi kibao!
      Miili ya waliokufa katika ajali ya Meli ya Spice Islander ipimwe DNA ili kutambua Ndugu zao - Dk. Jakaya .M. Kikwete,, September 2011.

    4. #3
      alex50's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th January 2008
      Posts : 86
      Rep Power : 595
      Likes Received
      10
      Likes Given
      341

      Default Re: new HIV

      Nenda Angaza

    5. #4
      GABLLE's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th January 2011
      Posts : 60
      Rep Power : 433
      Likes Received
      6
      Likes Given
      1

      Default Re: new HIV

      Ukienda kupima na kukuta umeathirika watakupa ushauri wa nini cha kufanya. Kama umepima mwenyewe na hivi test tube wanazouza mitaani nenda kajisalimishe kwa wataalamu watakupa ushauri nasaha!!
      Delegate likes this.

    6. #5
      nkyalomkonza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2012
      Posts : 668
      Rep Power : 581
      Likes Received
      242
      Likes Given
      75

      Default Re: new HIV

      ole kaka yaelekea ulipiga kavu kavu.

    7. Miaka 50

    8. #6
      njoro's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st December 2010
      Posts : 178
      Rep Power : 462
      Likes Received
      5
      Likes Given
      5

      Default Re: new HIV

      nasubiri miezi 3 ipite ndio nikapime

    9. #7
      njoro's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st December 2010
      Posts : 178
      Rep Power : 462
      Likes Received
      5
      Likes Given
      5

      Default Re: new HIV

      bado nasubiri jibu

    10. #8
      njiwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2009
      Location : ax^2+bx+c=0
      Posts : 4,955
      Rep Power : 2368
      Likes Received
      958
      Likes Given
      172

      Default Re: new HIV

      nenda zahati iliyokaribu watakufahamisha vizuri na kukutoa wasiwasi
      Pure Matrimony >> Purity starts here (Quran 24:26)
      My loyalty is to reason,and as a reasonable person I reserve the right to change my mind when presented with new information that alters my perspective" Njiwa"ᵀᴴᴱ'ᴼᴿᴵᴳᴵᴻᴬᴸ✯


    11. #9
      stroke's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th February 2012
      Posts : 1,427
      Rep Power : 0
      Likes Received
      153
      Likes Given
      4

      Default Re: new HIV

      pombe mbaya mkuu..inatokea ila ukipima kama hauna usirudie tena..jifunze kujizuia mkuu inasaidia..majuto ni mjukuu...halafu ngoma si kama malaria...ngoma hauponi mkuu ndo ntolee so kua makini next time

    12. #10
      Muarubaini's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 223
      Rep Power : 403
      Likes Received
      47
      Likes Given
      0

      Default Re: new HIV

      Umenikumbusha wasiwasi niliokuwa nao kipindi fulani. Ila baada ya kupima kama mara tu hiv na kukuta niko fiti, sa hiv mna mchumba wangu mmoja na nategemea kumuweka ndani soon. Vicheche mwiko kwani hamna faida zaida ya kukuharibia ndoto zako tu.
      stephot likes this.

    13. #11
      Muarubaini's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 223
      Rep Power : 403
      Likes Received
      47
      Likes Given
      0

      Default Re: new HIV

      Umenikumbusha wasiwasi niliokuwa nao kipindi fulani. Ila baada ya kupima kama mara tatu hiv na kukuta niko fiti, sa hiv mna mchumba wangu mmoja na nategemea kumuweka ndani soon. Vicheche mwiko kwani hamna faida zaida ya kukuharibia ndoto zako tu.

    14. #12
      bidada's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th January 2012
      Location : Mpunguti
      Posts : 105
      Rep Power : 392
      Likes Received
      28
      Likes Given
      32

      Default Re: new HIV

      Ni ngumu sana ndugu yangu kujua kama umeambukizwa ukimwi bila ya kupima kwa siku za mwanzo. Maana kuna wengine huwa hawaonyeshi dalili zozote zile hata kwa miaka kumi.Kwa mujibu wa uanishaji uliofanywa na wataalamu wa shirika la Afya Duniani yaani WHO, kuna hatua (stages) kuu nne za ugonjwa wa VVU/UKIMWI ambazo ni:

      1. Hatua ya kwanza [Primary HIV Infection]
      Hatua hii huwa kwa muda wa wiki nne. Ni asilimia 20 tu ya watu wenye maambukizi ya VVU walio kwenye hatua hii ambao hupata dalili na viashiria vikali vya ugonjwa huu lakini mara nyingi madaktari hushindwa kutambua kama mgonjwa amepata maambukizi ya VVU kutokana na dalili na viashiria vyake hapa kufanana sana na dalili za magonjwa mengine. Mgonjwa aliye katika hatua hii ya kwanza ya maambukizi ya VVU huweza kuonesha dalili na viashiria kama vile kuvimba tezi (swollen lymph glands), kupatwa na homa kali, kuumwa koo (sore throat), kujihisi mchovu, kujihisi maumivu sehemu mbalimbali mwilini (body aches), kutokwa na vipele mwilini (skin rash), na pia kutapika, kuharisha au kuumwa tumbo

      Mgonjwa anayepata dalili na viashiria hivi tunasema kwamba amepata “Acute HIV infection/Acute HIV retroviral infection au seroconversion illness.” Dalili hizi hutokana na mwili wa mtu mwenye maambukizi ya VVU kuanza kutengeneza kinga dhidhi ya VVU.
      Hatua ya Pili (Clinically Asymptomatic Stage)

      Katika hatua hii ambayo inaweza kudumu kwa muda wa miaka kumi, mgonjwa anakuwa haonyeshi dalili/viashiria vyovyote vile isipokuwa anaweza kuwa na tezi zilizovimba [swollen lymph nodes]. Kiwango cha VVU kwenye damu hupungua sana lakini mgonjwa anaweza kuambukiza mtu mwingine yoyote na vipimo vya VVU vina uwezo wa kutambua uwepo wa maambukizi y VVU katika damu.

      Tafiti mablimbali zimeonesha kwamba VVU katika mwili huwa bado zinazaliana [active] na hukimbilia/hujificha kwenye tezi [lymph nodes]. Kutokana na kujificha kwake katika hatua hii, kipimo cha kupima wingi wa virusi vya ukimwi (Viral load test) katika mwili hutumiwa sana ili kuweza kutambua uwepo wa VVU. Kipimo hiki pia husaidia katika kumpangia mgonjwa tiba yake.

      Hatua ya Tatu [Symptomatic HIV infection]
      Kutokana na kuongezeka kwa wingi wa VVU katika mwili, kinga ya mwili huzidi kudhoofika na hii husababishwa na;
      • Tezi na tishu zilizoathiriwa na VVU huharibika kutokana na maambukizi ya muda mrefu
      • VVU hubadilika badilika na kuwa na uwezo zaidi wa kuathiri tishu na sehemu mbalimbali za mwili na hata kuziua/kuziharibu seli zinazokinga mwili kutokana na maambukizi zinazojulikana kama T helper cell
      • Mwili hushindwa kumudu uharibifu wa T helper cell na kushindwa kuzalisha seli nyingine mpya.


      Kama mgonjwa wa VVU hatumii dawa za kuvubaisha VVU au anatumia ARV's ambazo hazimsaidii au hazifanyi kazi vizuri mwilini mwake, basi mgonjwa ataendelea kuingia kwenye hatua ya nne ya Ukosefu wa Kinga Mwilini (Ukimwi) au AIDS.


      Hatua ya Nne [UKIMWI]
      Hatua hii hujulikana kama Ukosefu wa Kinga Mwilini [UKIMWI] au AIDS, ambapo mgonjwa hupata maambukizi ya magonjwa nyemelezi pamoja na saratani za aina mbalimbali kutokana na kupungua kwa kinga mwilini.

      Hivyo ni vyema ukapime tu ndugu yangu ili uondokane na hofu.. ukishapima utajiona kama umetua mzigo.

    15. #13
      bidada's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th January 2012
      Location : Mpunguti
      Posts : 105
      Rep Power : 392
      Likes Received
      28
      Likes Given
      32

      Default Re: new HIV

      Muarubaini nami iliwahi kunitokea kama wewe, yani ilichukua kama mwaka mzima kujishahuri kwenda kupima. Nakumbuka Bf wangu aliniambia tukapime nilimzungusha sana, mwisho nikafunga safari peke yangu kwenda kupima...nilipopata majibu siku hiyo hiyo nikampigia simu tukapime, nilipomu hadithia alicheka sana. Toka hapo nimetulia kwa mpenzi wangu na nimejijengea tabia ya kupima mara kwa mara.

    16. #14
      Las Mas Bobos's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th June 2012
      Posts : 924
      Rep Power : 533
      Likes Received
      300
      Likes Given
      84

      Default Re: new HIV

      Quote By Muarubaini
      Umenikumbusha wasiwasi niliokuwa nao kipindi fulani. Ila baada ya kupima kama mara tu hiv na kukuta niko fiti, sa hiv mna mchumba wangu mmoja na nategemea kumuweka ndani soon. Vicheche mwiko kwani hamna faida zaida ya kukuharibia ndoto zako tu.
      Kipi hapo kinagarantii huyo mchumba wako kutokwenda kuutafuta unakopatikana na kukuambukiza?

      Mpk hapa hamna aliyejibu swali lililoulizwa
      By the time a man comes to realize that his father was right, he usually has a son who think he is wrong.

    17. #15
      njoro's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st December 2010
      Posts : 178
      Rep Power : 462
      Likes Received
      5
      Likes Given
      5

      Default Re: new HIV

      asante mkuu

    18. #16
      kipkarich's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 5th July 2012
      Posts : 1
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: new HIV

      huu niushauri mzuri sana wa kuelimisha. hongera

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...