Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

    Report Post
    Results 1 to 16 of 16
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,833
      Rep Power : 19439
      Likes Received
      8627
      Likes Given
      28184

      Default Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani



      Aina mpya ya vimelea vya ugonjwa wa kisonono au "gono" ambavyo vinahimili dawa(resistant to drugs) zinazotumika kutibu ugojwa huu imegundulika duniani. Taarifa iliyotolewa na shirika la afya duniani (WHO) hivi karibuni imesema, ugonjwa wa kisonono unaoathiri mamilioni ya

      watu ulimwenguni umeanza kuwa sugu dhidhi ya dawa zinazotumiwa kuutibu na hivyo kuna hatari ya kutoweza kutibika kabisa.


      Shirika la afya duniani limetoa wito kwa serikali na madaktari kuongeza ufuatlijiaji wa aina hii ya kisonono kutokana na ugonjwa wa kisonono kuwa

      na athari nyingi kama mcharuko (inflammation), ugumba, matatizo wakati wa ujauzito na hata vifo vya kina mama wajawazito.


      “Aina hii mpya ya vimelea vya kisonono vinaonyesha usugu dhidhi ya dawa zote za antibiotiki tunazotumia dhidhi yake ikiwemo dawa za jamii ya

      cephalosporins ambazo ni dawa za mwisho katika kutibu ugonjwa wa kisonono, “ alisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan, mmoja wa wanasayansi wa shirika la afya duniani katika kitengo cha magonjwa ya zinaa.


      Miaka michache ijayo, aina hii mpya ya kisonono itakuwa sugu dhidhi ya dawa zote ambazo tunazo saizi “aliendelea kusema Dk. Manjula Lusti-

      Narasimhan wakati wa mahojiano na shirika la habari la The Associated Press kabla WHO haijatangaza rasmi hatua na mwongozo mpya wa kukabiliana na tishio la aina hii mpya ya kisonono.


      Inakisiwa watu milioni 106 ulimwenguni kote huathiriwa na ugonjwa wa kisonono kila mwaka.Ugonjwa wa kisonono pia huongeza hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa Virusi vya Ukimwi (VVU).


      “Ugonjwa sugu wa kisonono sio tatizo la bara la Ulaya au Afrika pekee bali ni tatizo la dunia nzima kwa sasa,’” alinukuliwa akisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan.


      Kwa mara ya kwanza, vimelea sugu vya ugonjwa wa kisonono dhidhi ya dawa aina ya cephalosporins viliripotiwa katika nchi ya Japan, ikifuatiwa na Uingereza, Hongkong na Norway.


      Wanasayansi wanaamini matumizi mabaya ya dawa aina ya antibiotiki pamoja na uwezo wa vimelea vya ugonjwa wa kisonono kubadilika na kuzoea

      mazingira mapya ndio chanzo kikuu cha kutokea kwa ugonjwa sugu wa kisonono na hivyo muda si mrefu ugonjwa huu utakuwa janga kubwa dunia

      nzima kama hatua za haraka hazitachukuliwa. Kuna uwezekano wa vimelea hivi sugu vya kisonono vinasambaa kwa sasa duniani bila kuweza

      kugundulika kutokana na nchi nyingi kutokuwa na ufuatiliaji na utunzaji kumbukumbu mzuri wa wagonjwa wake.


      Shirika la afya duniani limesema nchi zinatakiwa kuongeza ufuatiliaji wa wagonjwa wake pamoja na kudhibiti matumizi holela ya dawa za antibiotiki mpaka pale taarifa kamili za ugonjwa huu zitakapojulikana.


      “Elimu ya masuala ya kujamiana pamoja na matumizi sahihi ya mipira ya kondomu inahitajika ili kutokomeza kabisa ugonjwa huu sugu wa kisonono.

      Hatuwezi kuutokomeza kabisa ugonjwa huu bali tunaweza kuzuia usambaaji wake,”alisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan.

      Kwa taarifa zaidi za ugonjwa huu
      Mr Rocky and manushiboy like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]


    2. #2
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,833
      Rep Power : 19439
      Likes Received
      8627
      Likes Given
      28184

      Default Re: Onyo wanawake msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      MAGONJWA YA ZINAA - 1: (SEXUAL TRANSMITTED DISEASES)

      Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga

      denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe

      kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators).

      Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

      Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni;

      • Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
      • Chlamydia
      • Kaswende (Syphillis)
      • Human papilloma virus (HPV)
      • HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
      • Hepatitis B, C, A
      • Herpes virus
      • Trichomoniasis
      • Bacteria Vaginosis
      • Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
      • Chancroid

      Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.


      Visababishi vya magonjwa ya zinaa


      • Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
      • Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
      • Kuwa na wapenzi wengi
      • Kufanya mapenzi ambao sio salama
      • Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.

      Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

      Nitaanza kuzungumzia ugonjwa wa gono (gonorrhea) kwa leo na makala zitakazofuata nitakuwa nazungumzia ugonjwa mmoja baada ya mwengine


      Kisonono (gonorrhea) ni nini?


      Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa

      wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.

      Ugonjwa huu huambukizwa vipi?

      Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex).

      Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). Ugonjwa wa gono

      huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya
      kulevya.

      Dalili za ugonjwa wa kisonono


      Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo;

      Kwa wanaume:


      • Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
      • Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
      • Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
      • Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.

      Kwa wanawake:


      • Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
      • Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
      • Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
      • Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
      • Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
      • Kichefuchefu
      • Homa (fever)
      • Kutapika

      Vipimo vya ugonjwa wa kisonono


      • Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
      • Polymerase Chain Reaction (PCR) – Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.


      Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?


      Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi

      (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide

      antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa

      wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano. Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia
      dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.

      Madhara ya ugonjwa wa kisonono



      • Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
      • Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
      • Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
      • Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
      • Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
      • Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).


      Kinga ya kisonono



      • Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
      • Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
      • Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
      • Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
      • Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
      • Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.


      “Kumbuka ya kwamba hakuna kitu kama ngono salama kwani huwezi kujua kama wewe au mwenzako wakati wa kujamiana ameathirika au la, au una michibuko au umekatika kwenye ngozi au la kwani michibuko mengine inaweza isionekane au

      kugundulika kwa urahisi. Njia pekee na nzuri ni kuacha au kujikinga na vitendo vya ngono”. Mtu aliyepata gono awali anaweza kupata tena.
      Magonjwa ya Zinaa - 1: (Sexual Transmitted Diseases)
      Mr Rocky likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    3. #3
      kisukari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th July 2010
      Posts : 2,629
      Rep Power : 3888
      Likes Received
      1415
      Likes Given
      661

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      mmh,yanatisha.thanks mzizi mkavu
      MziziMkavu likes this.

    4. #4
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,836
      Rep Power : 5674
      Likes Received
      6319
      Likes Given
      2418

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      tobaaaaaaaaa
      MziziMkavu likes this.

    5. #5
      Sibhonike's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Posts : 91
      Rep Power : 433
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Somo zuri.
      Asante Mzizi.
      MziziMkavu likes this.


    6. #6
      sister's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd November 2011
      Location : MBEZI YA KIMARA, DSM
      Posts : 1,457
      Rep Power : 965
      Likes Received
      462
      Likes Given
      475

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      kazi ipo.
      MziziMkavu likes this.

    7. #7
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,706
      Rep Power : 68642
      Likes Received
      7079
      Likes Given
      5587

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      MziziMkavu asante sana kwa somo hili na tahadhari pia
      halafu mbona hukunijibu mkuu
      MziziMkavu likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    8. #8
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,833
      Rep Power : 19439
      Likes Received
      8627
      Likes Given
      28184

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Quote By Mr Rocky View Post
      MziziMkavu asante sana kwa somo hili na tahadhari pia
      halafu mbona hukunijibu mkuu
      Sikukujibu kitu gani?kwani umenitumia PM.?mkuu Mr Rocky nitumie tena basi hiyo PM.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    9. #9
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,706
      Rep Power : 68642
      Likes Received
      7079
      Likes Given
      5587

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Quote By MziziMkavu View Post
      Sikukujibu kitu gani?kwani umenitumia PM.?mkuu Mr Rocky nitumie tena basi hiyo PM.

      @
      MziziMkavu nilituma pm aise
      Ngoja niitume tena mkuu
      MziziMkavu likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    10. #10
      MWAKIKALI's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th June 2012
      Posts : 13
      Rep Power : 356
      Likes Received
      4
      Likes Given
      4

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      shukrani Rocky kwa taarifa, UGONJWA HUO UMEENEA SANA MAENEO YA MKOA WA KAGERA HASAHASA KARAGWE, RAFIKI ZANGU WENGI SANA WAMEUGUA NA UPONAJI WAKE SI WA UHAKIKA MAANA WANASEMA WAKITIBU NA KUPONA HUWA UNAJIRUDIA BAADA YA SIKU TATU HADI NNE MARA BAADA YA KUMALIZA DAWA.
      MMOJA ALIPEWA DAWA ZA AINA TATU KWA WAKATI NA SINDANO NDO KIDOGO YEYE HAUJARUDI.
      Mr Rocky and MziziMkavu like this.

    11. #11
      mayenga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th September 2009
      Posts : 1,595
      Rep Power : 817
      Likes Received
      320
      Likes Given
      446

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Ahsante Mzizimkavu!
      MziziMkavu likes this.

    12. #12
      ERIC JOSEPH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2011
      Location : MBEYA TANZANIA
      Posts : 340
      Rep Power : 465
      Likes Received
      34
      Likes Given
      2

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      thanks xo much 4education
      MziziMkavu likes this.

    13. #13
      cement's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2012
      Location : Tanganyika-Dar es salaam
      Posts : 438
      Rep Power : 446
      Likes Received
      152
      Likes Given
      173

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Nakukubali kaka katika hili!
      MziziMkavu likes this.

    14. #14
      Emma.'s Avatar
      Banned Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 910
      Rep Power : 0
      Likes Received
      119
      Likes Given
      0

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Madaa nzuri pongezi sana ubarikiwa
      MziziMkavu likes this.

    15. #15
      siralola's Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th April 2012
      Posts : 40
      Rep Power : 369
      Likes Received
      5
      Likes Given
      16

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Somo zuri sana doctor asante kwa kutujuza.
      MziziMkavu likes this.

    16. #16
      manushiboy's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd August 2011
      Posts : 32
      Rep Power : 404
      Likes Received
      9
      Likes Given
      2

      Default Re: Onyo wanawake hapa msiingie hapa hatari:aina mpya ya kisonono yasambaa duniani

      Mungu akupe nguvu uendelee kuelimisha watu wake asante sana mkuu
      MziziMkavu likes this.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...