Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania

    Report Post
    Results 1 to 7 of 7
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,216
      Rep Power : 19216
      Likes Received
      8171
      Likes Given
      26685

      Default Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania



      Florence Majani
      UTAFTI mpya umebaini kuwa nusu ya wanaume nchini ni wagumba ukipingana madai ya wengi kuwa tatizo hilo linawaathiri zaidi wanawake.Kwa mujibu wa utafiti huo, uliofanywa na Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili kati ya mwaka 2009 na Septemba 2010 unaonyesha, asilimia 47.05 ya wanaume wanaokwenda kupima afya zao za uzazi, hawana uwezo wa kutungisha mimba.Malengo ya utafiti huo uliosimamiwa na Dk Henry Mwakyoma, yalikuwa ni kubaini ni kwa kiasi gani wanaume huweza kuathiriwa katika via vyao vya uzazi na hatimaye kushindwa kutungisha mimba.
      Utafiti huo ulionyesha kati ya wanaume 221 waliopimwa, asilimia 30.03 walikuwa na mbegu dhaifu na asilimia 17.02 walikuwa hawana kabisa mbegu zenye uwezo wa kutungisha mimba, zaidi ya maji tu.
      Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi, Dk Mwakyoma alisema, ugumba kwa wanaume limekuwa tatizo sugu katika miaka ya hivi karibuni.
      “Nasisitiza kuwa, pengine mwanaume aliwahi kupata watoto hapo awali, lakini sasa hivi hapati, bado atakuwa mgumba,” alisema Dk Mwakyoma.Alisema hapo awali ilikuwa vigumu kupata idadi kamili ya wanaume wenye ugumba kwa sababu walikuwa hawajitokezi kupima.“Angalau sasa hivi wanakuja na tunawapima, ingawa ni kazi ngumu kuwapa majibu yao,” alisema Mwakyoma.
      Sababu za ugumba

      Mwakyoma alitaja sababu za ugumba kwa wanaume kuwa ni uambukizo katika tezi inayozalisha manii.
      Alitaja sababu nyingine kuwa ni kemikali zinazoingia katika miili yetu, mionzi na wakati mwingine ajali inapoathiri tezi hiyo.
      Dk Mwakyoma aliongeza kuwa, wanaoathirika zaidi ni wanaofanya kazi migodini, jeshini au wanaozungukwa na kemikali kwa muda mrefu.“Sababu nyingine ni joto kuzidi katika sehemu za siri za mwanaume, kubeba laptop, unene kupita kiasi na mazingira,” alisema.


      Dk Mwakyoma akifafanua jinsi kitengo chake kinavyopima manii ili kujua kama zina matatizo au zipo salama, alisema, " rangi ya mbegu pamoja na umbile huangaliwa ili kutambua ubora wake. Hata kwa kuziangalia tu, mbegu zenye rangi aidha kijivu au nyeupe si salama.”

      Kwa upande wake, Dk Innocent Mosha, ambaye ni daktari wa uchunguzi wa magonjwa katika Hospitali ya Muhimbili alisema, wamefanikiwa kupata takwimu hizo kutokana na wanandoa wengi kufika hospitalini hapo kwa ajili ya kujua

      sababu ya kutokuwa na watoto katika ndoa yao."Mara nyingi matokeo huonyesha tatizo liko kwa mwanaume. Lakini kuna tabu ya kuwaeleza ukweli, wengi hawataki kukubali," alisema Dk Mosha.

      Aliongeza, “Kesi kama hizo huleta migogoro ya kifamilia, kwani huenda mwanamke huyo amekwishamzalia mumewe watoto ambao kimantiki si wa kwake,” alisema Dk Mosha.

      Dk Mosha alisema, kuna ugumba wa aina mbili; wa kuzawa nao na ugumba unaopatikana ukubwani.
      “Wapo wanaozaliwa na ugumba, yaani mbegu zao aidha ni dhaifu au hawana kabisa mbegu tangu kuzaliwa kwao,” alisema Dk Mosha.

      Shirika la Afya duniani (WHO) linathibitisha kuwa, ujazo wa manii anaopaswa kuwa nao mwanaume ili aweze kutungisha mimba ni milligram moja na nusu hadi nne na nusu na kuongeza, “Ujazo wa manii ukipungua au ukizidi basi mbegu hizo zina matatizo” alisema Dk Mwakyoma.

      Naye Dk Joshua Noreh wa kituo cha upandikizaji cha jijini Nairobi (IVF centre) alisema, tatizo la ugumba alianza kuliona tangu mwaka 2006 baada ya kupokea wanandoa wengi kutoka Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania waliofika kutafuta

      huduma ya upandikizaji wa mbegu ili kupata watoto.
      Utafiti uliofanywa na WHO mwaka 2009 duniani, ulibainisha kuwa, mwanaume mmoja kati ya saba wanaofika kupima afya ya uzazi hugundulika na matatizo ya ugumba.
      Chanzo:Mwananchi
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      mashambani kwao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th December 2011
      Posts : 369
      Rep Power : 450
      Likes Received
      52
      Likes Given
      0

      Default Re: Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania

      tunashukuru kwa ujumbe.
      MziziMkavu likes this.

    4. #3
      Nakapanya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd May 2012
      Location : DOWNTOWN
      Posts : 471
      Rep Power : 4174
      Likes Received
      102
      Likes Given
      147

      Default Re: Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania

      Naona mpango umeanza kutimia,kila leo chanjo,mara vitamini A cjui vitami Z,itafikia wakati wote tutakuwa wagumba,wadhungu wajanja sanaaa.
      MziziMkavu likes this.

    5. #4
      Magu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Posts : 131
      Rep Power : 428
      Likes Received
      42
      Likes Given
      8

      Default Re: Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania

      Tatizo la tafti zetu hazitoi solution kitu kinachofanya zisiwe na maana kwa wasomaji na wadau kwa ujumla.

      Unapotoa matokeo ya utafiti unapaswa kuja na suggested sulution.

      Watafiti wenu na matokeo yake ni questionable
      MziziMkavu and Bejajunior like this.

    6. #5
      androidi's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 27th June 2012
      Posts : 2
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania

      kumbe ata kubeba laptop ni noma,sasa ndugu zangu wanachuo ambao utumia vifaa hivi mara kwa mara kwa ajili ya masomo yao sindio wako atarini zaidi
      MziziMkavu likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      stephot's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st March 2012
      Location : DSM
      Posts : 777
      Rep Power : 586
      Likes Received
      214
      Likes Given
      589

      Default Re: Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania

      Quote By androidi
      kumbe ata kubeba laptop ni noma,sasa ndugu zangu wanachuo ambao utumia vifaa hivi mara kwa mara kwa ajili ya masomo yao sindio wako atarini zaidi
      http://androidi mie matumizi ya Laptop nilisha yashtukia siku nyingi sana,na hata ninapofanya kazi kwa kutumia desktop monitor yangu naiweka kama mita 2 kutokea nilipo,unajua ilikuwaje kuna kipindi nilianza kuhisi ukakamavu nyumbani unakuwa mdogo kuna mtu akanishtua nilipojaribu hiyo idea nikaona imenirudishia hesima back kwa mamaa.
      MziziMkavu likes this.

    9. #7
      iishmmael's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd April 2012
      Posts : 205
      Rep Power : 398
      Likes Received
      31
      Likes Given
      19

      Default Re: Nusu ya Wanaume Wagumba Nchini Tanzania

      watu wakapime wajue... so ndo maana siku hizi unakuta mtu ana vitoto vitatu havifanani hata na wazazi wao!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! !!!!!
      MziziMkavu likes this.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...