Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Maradhi ya Wasiwasi

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 21
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,106
      Rep Power : 19193
      Likes Received
      8049
      Likes Given
      26489

      Default Maradhi ya Wasiwasi

      Wasiwasi (Anxiety) ni jina linalotumika kufafanua vile mtu anavyohisi wakati wa hatari maumivu au matatizo. Watu wakiwa kwa hali hii na wasiwasi huwa wanjihisi kukasirika na kufadhaika.

      Hali ya wasiwasi inaweza kutokana na hali ya maisha, kufutwa kazi, uhusiano kuvunjika, ugonjwa, ajali kubwa au kifo cha mpendwa. Kuwa na wasiwasi ni jambo la kawaida katika nyakati hizi kwa muda tu.

      Kwa sababu wasiwasi ni jambo la kawaida, ni muhimu kutofautisha baina ya kuwa na wasiwasi unaoletwa na matokeo ya kawaida ya maisha na dalili za ugonjwa wa wasiwasi (anxiety disorder).

      Magonjwa ya wasiwasi ni kundi la magonjwa yaliyo na dalili za kuwa na wasiwasi mwingi mno usio wa kawaida kwa muda mrefu.

      Watu huathiriwa na anxiety disorder wakati kipimo cha wasiwasi kimezidi sana mpaka kinatatiza maisha yao ya kawaida.

      Magonjwa ya wasiwasi ni magonjwa ya ubongo yanayoathiri watu wengi zaidi. Mmoja kati ya watu ishirini huathirika. Magonjwa haya huanza mapema mtu anapokomaa lakini pia yanaweza kuanzia utotoni ama baadaye maishani. Wanawake huathiriwa zaidi kuliko wanaume.

      Magonjwa ya wasiwasi hutokea kighafla tu mara nyingi bila sababu.
      Aliyeathiriwa huwa na shida ya kupumua na mpapatiko wa moyo. Dalili zingine ni kutokwa na jasho, kutetemeka, kuhisi

      kukabwa chevuchevu, maumivu ya tumbo, kuzirai, kuhisi ni kama mtu anadungwadungwa na sindano,
      kushindwa kujimudu na/ama kupoteza tumaini.

      Magonjwa ya wasiwasi huathiri mtu anavyofikiri , anavyohisi na pia tabia zake .Asipotibiwa mapema ,maisha yake hutatizika mno. Hata hivyo, matibabu ya wasiwasi humtibu mtu kikamilifu.
      Ni zipi aina kuu za ugonjwa wa wasiwasi?
      Kuna aina tofauti za ugonjwa wa wasiwasi (anxiety disorder).
      Wasiwasi kijumla

      (Generalised anxiety disorder)

      Ugonjwa huu huwa na dalili za kubabaika sana kwa jambo lolote maishani kama afya, jamii, marafiki, hela ama kazi.
      Watu walioathiriwa hujibabaisha kuhusu hatari inayoweza wajia au wapendwa wao na kubabaika huja na huzuni na pia hali ya kushtuka.

      Walioathiriwa na hofu ya ghafla wanaweza kuwa, au wasiwe, na woga wa mahali (Panic disorder with and without agoraphobia)

      Walioathiriwa na ugonjwa huu hushutuka sana kwa mambo ambayo wengine huona ni kawaida tu. Wao huhisi ni kama mioyo yao inasimama. Huwa wanaogopa kutiwa kichaa, kuwa mwishowe watakufa, ama kupoteza kujimudu.

      Woga huu huwa ni chanzo cha woga wa mahali panapoweza kutatiza maisha yao mno. Woga wa mahali ni aina ya woga wa kuwa katika mahali au hali ambazo ni vigumu kuzihepa mahali pia ni woga wa kutopata usaidizi wakati mtu anapouhitaji.

      Watu walio na woga wa mahali (Agoraphobia) huwa na woga wakiwa katika maduka makubwa au sokoni, kunapo umati wa watu, sehemu wanapoweza kuzuiliwa kama kichumba, magari ya umma, lifti ama mabarabara makuu.

      Watu walio na woga wa mahali hutulia wakiwa na mtu wanayemuamini au pia chombo. Mtu huyu aweza kuwa ni mumewe au bibiye, rafiki, mnyama au dawa .
      Woga maalumu (Specific phobia)

      Kila mtu huwa na woga usio na sababu lakini woga maalmu ni woga uliozidi wa kitu fulani au tukio fulani unaoweza kutatiza maisha ya mtu.

      maji, mbwa, sehemu pasipo wazi, nyoka au buibui.
      Mtu aliye na woga maalumu hutulia wakati kitu aogopacho hakipo. Hata hivyo, akitazama hicho kitu hushtuka na kushikwa na wasiwasi.
      Watu walio na woga maalumu hufanya chochote kiwezekanavyo kuepukana na hicho kitu waogopacho.
      Woga wa wa watu

      (Social phobia)

      Woga wa watu ni woga uliozidi wa watu au hali ya kijamii. Aliyeathiriwa hudhani atatuhumiwa na kupelelezwa na wengine. Watu walio na woga wa watu hutatizika na hufanya iwezekanavyo kuepukana na watu au kuwavumilia.
      Wao huwa hawafanyi mambo ambayo wangefanya kwa kawaida kwa sababu wamo mbele ya watu .Watajaribu kujizuia kula, kuongea, kuandika au kunywa kwa njia ya kawaida ama kujitenga kutoka watu.
      Ugonjwa wa kujilazimisha

      (Obsessive-compulsive disorder)


      Hali hii humfanya aliyeathiriwa kuwa na mawazo yasiyofaa. Yeye hutenda matendo fulani ili ajaribu kuondoa hayo mawazo.
      Matendo hayo hupoteza muda na hutatiza maisha ya kila siku. Kwa mfano, watu hujilazimu kunawa mikono, kutazama kama mlango

      umefungwa au jiko limezimwa na hufuata amri au masharti.
      Watu walio na ugonjwa wa kujilazimisha husikia aibu sana na huficha matendo yao hata kutoka jamii zao.
      Wasiwasi wa baadaye

      (Post traumatic stress disorder PTSD)

      Watu waliopata masaibu makubwa kama vita, dhuluma , ajali, moto au hatari ya kibinafsi huendelea kuwa na woga kwa muda mrefu baadaye . Sio watu wote ambao hupitia haya masaibu hupata wasiwasi wa baadaye.

      Watu walio na (PTSD) huyapitia masaibu hayo mara kwa mara kila wanapokumbuka hayo matokeo ama wapatapo jinamizi. Mara nyingi ni jambo fulani ndilo huwasababishia makumbusho ya hayo masaibu na hujaribu kuepuka hili jambo. Kupoteza hisia ni dalili ya (PTSD) pia.
      Shida za afya ya ubongo

      Watu walio na ugonjwa wa wasiwasi wa aina fulani wana nafasi ya kushikwa na huzuni pia. Kwa habari zaidi za huzuni , soma kijarida “Ni nini hali ya huzuni?”
      Utumizi wa pombe na madawa ya kulevya huonekana na wale walio na wasiwasi. Hii hufanya kutibiwa kwao inakuwa vigumu. Ni muhimu kupunguza unywaji wa pombe na Madawa.


      Ugonjwa wa wasiwasi unasabibishwa na nini?

      Kuna sababu nyingi zinazosababisha ugonjwa wa wasiwasi na zinahusiana. Sababu za aina ya magonjwa fulani ni tofauti na sio rahisi kutambulika.
      Sababu za kigenitiki (kurithiana)

      Inafahamika kuwa magonjwa ya wasiwasi hupatikana katika jamii fulani.
      Hali hii ni kama ile ipatikanayo katika jamii za watu walio na ugonjwa wa kisukari ama ugonjwa wa moyo. Watu waweza pia kushika hii tabia ya wasiwasi kutoka wazazi au watu wengine wa jamii.
      Sababu za kemikali

      Aina ya magonjwa ya wasiwasi mengine husababishwa, kidogo tu, na kukosekana na uzanifu wa kemikali zilizo kwenye ubongo Chembe akili (fahamu) ya bongo inayochunga hisia na tabia ya mtu linaweza kuhusika.
      Tabia

      Watu walio na tabia fulani hushikwa na magonjwa ya wasiwasi kwa njia rahisi kuliko wengine. Watu wanaoghafilika au kukasirika kwa haraka hushikwa na ugonjwa wa wasiwasi kwa urahisi.
      BAK, jmushi1, Mokoyo and 5 others like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,106
      Rep Power : 19193
      Likes Received
      8049
      Likes Given
      26489

      Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

      Watu ambao walikuwa wanaona aibu wakiwa watoto hushikwa na ugonjwa wa wasiwasi, kwa mfano woga wa watu.
      Tabia za kuigwa

      Watu wengine huiga tabia fulani wanapopatana na matukio fulani, watu au vitu vinavyowaudhi au vinavyosababisha ugonjwa wa wasiwasi. Tabia hii hutendeka mtu anapopitia hili tukio au anapolifikiri au anapokutana na mtu au kitu kinachosababisha wasiwasi.

      Matatizo
      Matatizo ya maisha husababisha ugonjwa wa wasiwasi, haswa wasiwasi wa baadaye.
      Je, kuna matibabu?

      Magonjwa ya wasiwasi yanatibika kikamilifu ingawaje kila ugonjwa au aina ya Ugonjwa wa wasiwasi una dalili zake.

      Magonjwa mengi hutibika kupitia matibabu ya kisaikolojia ama madawa.
      Matibabu yanayotumia mbinu za kisaikolojia pamoja na madawa huwa na matokeo bora yanayodumu.
      Matibabu kamili ya anxiety disorder ni kama.

      • Mbinu za kisaikolojia kama urekebishajiwa tabia (Cognitive Behavioural Therapy CBT) zinazolenga kubadilisha mawazo, tabia na imani zinazoleta wasiwas. Mbinu hizi zaweza pia kumfanya

      aliyeathiriwa kupitia yale mambo yanayosababisha wasiwasi (yaani desensitization).
      • Mbinu za kupunguza wasiwasi na kutulia.
      • Dawa zinazopunguza huzuni ni muhimu katika kutibu wasiwasi fulani na pia kutibu huzuni.
      • Madawa ya wasiwasi yanayolenga akili pia ni muhimu
      • Madawa hayatatibu wasiwasi disorders lakini hupunguza dalili za ugonjwa huu mtu apatapo matibabu ya kisaikolojia.
      Jamii na marafiki wa watu walio na wasiwasi mara nyingi hutatizika. Usaidizi na elimu ni muhimu kwa kutibu ugonjwa huu.

      Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa Wasiwasi Kwa Tiba Mbadala za Kienyeji yaani Mitishamba Mgonjwa anashauriwa kula kwa wingi Lozi kwa lugha ya kiingereza (Almond) itamsaidia sana kuondosha huo Ugonjwa wa Wasiwasi.


      Lozi (Almond)

      Source. http://www.jamiiforums.com/jf-doctor...zi-almond.html
      BAK, mshihiri and stephot like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    4. BAK
      #3
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,544
      Rep Power : 44953
      Likes Received
      8282
      Likes Given
      8280

      Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

      Hakuna tena hapa jamvini kama MziziMkavu katika jitihada za kutuelimisha katika mambo mbali mbali kuhusu vyakula, magonjwa na mambo mengine mbali mbali. Ubarikiwe sana Mkuu.
      MziziMkavu and Rutashubanyuma like this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    5. #4
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

      Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa Wasiwasi Kwa Tiba Mbadala za Kienyeji yaani Mitishamba Mgonjwa anashauriwa kula kwa wingi Lozi kwa lugha ya kiingereza (Almond) itamsaidia sana kuondosha huo Ugonjwa wa Wasiwasi.


      Lozi (Almond)

      Source. FAIDA YA LOZI Almond
      Mie wasiwasi ukipisha hodi hujikumbusha mstari huu wa nENO LA MWENYEZI MUNGU......................"Who by worrying will ad a one cubit size to his stature? SO I say to you Do not worry about what you will eat, drink, or put on your bodies.......for your heavenly Father knows you need them......"..Mathew 6:21-34
      MziziMkavu, Mziba, Mokoyo and 1 others like this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    6. #5
      Mziba's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th February 2010
      Posts : 228
      Rep Power : 517
      Likes Received
      34
      Likes Given
      73

      Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

      Asanteni Wakuu, haya maradhi hamna mwenye garantii kua hayata mtambalia. Baadhi yetu tumetwaa tabia zakusimamia majum mengi na kukimbizana na wakati, nadhani zinachangia. Hizi karanga Almond zitasaidia Professionals wengi na jamii kiujumla. MziziMkavu asante
      MziziMkavu likes this.

    Rubi is offline

    #6
    Rubi's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 5th October 2009
    style="display:none;visibility:hidden;" data-cfsrc="images/icons/icon1.png" alt="Default" /> Re: Maradhi ya Wasiwasi
    Quote By Mziba
    Asanteni Wakuu, haya maradhi hamna mwenye garantii kua hayata mtambalia. Baadhi yetu tumetwaa tabia zakusimamia majum mengi na kukimbizana na wakati, nadhani zinachangia. Hizi karanga Almond zitasaidia Professionals wengi na jamii kiujumla. MziziMkavu asante
    lakini pia matumizi ya kitunguu swaumu husaidia kuondoa wasiwasi na kuleta kujiamini na kumbukumbu pia.
    MziziMkavu likes this.
    Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.

  • #7
    jmushi1's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 2nd November 2007
    Posts : 14,376
    Rep Power : 16492
    Likes Received
    4299
    Likes Given
    5491

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Mtu akiwa na "obssesive compulsive disorder" bongo watamwita mchawi.lol!Kiukweli,hakuna mtu ambaye ni 100% normal.Its just a matter of deggree.
    MziziMkavu and Roulette like this.
    "One of the penalties for refusing to participate in politics is that you end up being governed by your inferiors"-Plato

  • #8
    lutamyo's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 13th April 2011
    Posts : 347
    Rep Power : 539
    Likes Received
    66
    Likes Given
    202

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By MziziMkavu

    Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa Wasiwasi Kwa Tiba Mbadala za Kienyeji yaani Mitishamba Mgonjwa anashauriwa kula kwa wingi Lozi kwa lugha ya kiingereza (Almond) itamsaidia sana kuondosha huo Ugonjwa wa Wasiwasi.


    Lozi (Almond)

    Source. http://www.jamiiforums.com/jf-doctor...zi-almond.html
    Mkuu hizi Lozi zinapatikanaje pia zinaliwa namna gani kamanda maana mtu kama mie sijawahi zioona kabisa.
    MziziMkavu likes this.

  • #9
    MziziMkavu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 3rd February 2009
    Location : European Union
    Posts : 22,106
    Rep Power : 19193
    Likes Received
    8049
    Likes Given
    26489

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By Mziba
    Asanteni Wakuu, haya maradhi hamna mwenye garantii kua hayata mtambalia. Baadhi yetu tumetwaa tabia zakusimamia majum mengi na kukimbizana na wakati, nadhani zinachangia. Hizi karanga Almond zitasaidia Professionals wengi na jamii kiujumla. MziziMkavu asante
    Mkuu hayo maradhi ya Wasiwasi yanatokana na shetani mbaya Pepo wachafu pia mimi ninaweza kuyatibu na mtu mwenye huo ugonjwa ukamuondokea mara moja licha ya hiyo dawa ya lozi kuitowa mimi mwenyewe kunako miaka ya 1990 nilikuwa nayo nikatumia dawa hiyo ya Lozi Almond Maradhi yakaniondoka. Mkuu hakuna maradhi yasiyokuwa na Dawa ila kifo tu ndio hakina Dawa mkuu................. Mziba
    Mziba likes this.
    Only Do What Your Heart Tells You




    Allah
    Has Not Revealed A Disease without Treatment....
    (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

  • #10
    MziziMkavu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 3rd February 2009
    Location : European Union
    Posts : 22,106
    Rep Power : 19193
    Likes Received
    8049
    Likes Given
    26489

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By lutamyo
    Mkuu hizi Lozi zinapatikanaje pia zinaliwa namna gani kamanda maana mtu kama mie sijawahi zioona kabisa.
    Mkuu Hizo Lozi zinapatika Sehemu nyingi hapo kwetu Tanzania nenda kwenye Ma SuperMarket Makubwa utapata hiyo Lozi au kama upo Dar nenda sokoni Kariakoo utapata . Na Hizo Lozi zinaliwa kama zilivyo pamoja

    na maganda yake au waweza kumenya ila itakuwa ni vizuri kula na maganda yake unapata Vitamin yake kamili, pia hiyo Lozi inasaidia ugonjwa wa kumbukumbu ugonjwa wa kusahau Amnesia (lose memory) nguvu za kiume ukitumia muda

    mrefu sana. Lozi kwa lugha ya kiingereza inaitwa (Almond) Na Kama unataka Dawa za Nguvu ya kiume bonyeza hapa http://www.jamiiforums.com/jf-doctor/........................... lutamyo
    Only Do What Your Heart Tells You




    Allah
    Has Not Revealed A Disease without Treatment....
    (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

  • #11
    lutamyo's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 13th April 2011
    Posts : 347
    Rep Power : 539
    Likes Received
    66
    Likes Given
    202

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By MziziMkavu
    Mkuu Hizo Lozi zinapatika Sehemu nyingi hapo kwetu Tanzania nenda kwenye Ma SuperMarket Makubwa utapata hiyo Lozi au kama upo Dar nenda sokoni Kariakoo utapata . Na Hizo Lozi zinaliwa kama zilivyo pamoja

    na maganda yake au waweza kumenya ila itakuwa ni vizuri kula na maganda yake unapata Vitamin yake kamili, pia hiyo Lozi inasaidia ugonjwa wa kumbukumbu ugonjwa wa kusahau Amnesia (lose memory) nguvu za kiume ukitumia muda

    mrefu sana. Lozi kwa lugha ya kiingereza inaitwa (Almond) Na Kama unataka Dawa za Nguvu ya kiume bonyeza hapa http://www.jamiiforums.com/jf-doctor/........................... lutamyo
    Mungu akubariki ndugu yangu, kuhusu nguvu za kiume kwa sasa sijaoa hivyo naamini ni mzima ila tu nilikuwa nataka kujua ili kubust suala la kumbukumbu. Aidha vitu kama hivi ni muhimu sana ukizingatia tunatumia sana vyakula vyenye kemikali
    MziziMkavu likes this.

  • #12
    Kongosho's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 21st March 2011
    Location : Location loading...
    Posts : 25,104
    Rep Power : 13052
    Likes Received
    14067
    Likes Given
    14838

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    duh, nitatulia niisome hii mada lol
    MziziMkavu likes this.

  • #13
    korino's Avatar
    Senior Member Array
    Join Date : 6th December 2011
    Posts : 132
    Rep Power : 402
    Likes Received
    13
    Likes Given
    49

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By MziziMkavu
    Mkuu hayo maradhi ya Wasiwasi yanatokana na shetani mbaya Pepo wachafu pia mimi ninaweza kuyatibu na mtu mwenye huo ugonjwa ukamuondokea mara moja licha ya hiyo dawa ya lozi kuitowa mimi mwenyewe kunako miaka ya 1990 nilikuwa nayo nikatumia dawa hiyo ya Lozi Almond Maradhi yakaniondoka. Mkuu hakuna maradhi yasiyokuwa na Dawa ila kifo tu ndio hakina Dawa mkuu................. Mziba
    ahsante sana kaka kwa darsa zuri! sasa hizo loz zinaliwa ngapi kwa cku?shukran
    MziziMkavu likes this.

  • #14
    MziziMkavu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 3rd February 2009
    Location : European Union
    Posts : 22,106
    Rep Power : 19193
    Likes Received
    8049
    Likes Given
    26489

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By korino
    ahsante sana kaka kwa darsa zuri! sasa hizo loz zinaliwa ngapi kwa cku?shukran
    Utakazo hata ukichukuwa kwenye gao la mkono wako inatosha kula kama unavyokula njugu au karanga Mkuu......... korino
    Only Do What Your Heart Tells You




    Allah
    Has Not Revealed A Disease without Treatment....
    (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

  • #15
    Mwanaweja's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 8th February 2011
    Posts : 3,450
    Rep Power : 1109
    Likes Received
    457
    Likes Given
    925

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    haya mzizimkavu nimekusoma ntunashukru kwa maelezo yako
    MziziMkavu likes this.

  • #16
    korino's Avatar
    Senior Member Array
    Join Date : 6th December 2011
    Posts : 132
    Rep Power : 402
    Likes Received
    13
    Likes Given
    49

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By MziziMkavu
    Watu ambao walikuwa wanaona aibu wakiwa watoto hushikwa na ugonjwa wa wasiwasi, kwa mfano woga wa watu.
    Tabia za kuigwa

    Watu wengine huiga tabia fulani wanapopatana na matukio fulani, watu au vitu vinavyowaudhi au vinavyosababisha ugonjwa wa wasiwasi. Tabia hii hutendeka mtu anapopitia hili tukio au anapolifikiri au anapokutana na mtu au kitu kinachosababisha wasiwasi.

    Matatizo
    Matatizo ya maisha husababisha ugonjwa wa wasiwasi, haswa wasiwasi wa baadaye.
    Je, kuna matibabu?

    Magonjwa ya wasiwasi yanatibika kikamilifu ingawaje kila ugonjwa au aina ya Ugonjwa wa wasiwasi una dalili zake.

    Magonjwa mengi hutibika kupitia matibabu ya kisaikolojia ama madawa.
    Matibabu yanayotumia mbinu za kisaikolojia pamoja na madawa huwa na matokeo bora yanayodumu.
    Matibabu kamili ya anxiety disorder ni kama.

    • Mbinu za kisaikolojia kama urekebishajiwa tabia (Cognitive Behavioural Therapy CBT) zinazolenga kubadilisha mawazo, tabia na imani zinazoleta wasiwas. Mbinu hizi zaweza pia kumfanya

    aliyeathiriwa kupitia yale mambo yanayosababisha wasiwasi (yaani desensitization).
    • Mbinu za kupunguza wasiwasi na kutulia.
    • Dawa zinazopunguza huzuni ni muhimu katika kutibu wasiwasi fulani na pia kutibu huzuni.
    • Madawa ya wasiwasi yanayolenga akili pia ni muhimu
    • Madawa hayatatibu wasiwasi disorders lakini hupunguza dalili za ugonjwa huu mtu apatapo matibabu ya kisaikolojia.
    Jamii na marafiki wa watu walio na wasiwasi mara nyingi hutatizika. Usaidizi na elimu ni muhimu kwa kutibu ugonjwa huu.

    Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa Wasiwasi Kwa Tiba Mbadala za Kienyeji yaani Mitishamba Mgonjwa anashauriwa kula kwa wingi Lozi kwa lugha ya kiingereza (Almond) itamsaidia sana kuondosha huo Ugonjwa wa Wasiwasi.


    Lozi (Almond)

    Source. http://www.jamiiforums.com/jf-doctor...zi-almond.html
    samahani kaka! je hizi mbegu hazina madhara kwa wajawazito?
    MziziMkavu likes this.

  • #17
    Red Giant's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 9th March 2012
    Posts : 730
    Rep Power : 3610
    Likes Received
    233
    Likes Given
    282

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    ili mtu athibitishwe ni mgonjwa wa akili(matatizo ya kisaikolojia)
    1. shughuli zake za kila siku za maisha ziwe zimeathiriwa
    2. ugonjwa uweke maisha yake at risk
    3.nimesahau!
    asante mzizi kwa uzi mzuri
    MziziMkavu likes this.
    COAL UNDER PRESSURE BECOMES DIAMOND

  • #18
    Tusker Bariiiidi's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 3rd July 2007
    Location : Sinza Dar es Salaam.
    Posts : 3,230
    Rep Power : 1253
    Likes Received
    375
    Likes Given
    51

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Asante sana Mzizi Mkavu.
    MziziMkavu likes this.

  • #19
    MziziMkavu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 3rd February 2009
    Location : European Union
    Posts : 22,106
    Rep Power : 19193
    Likes Received
    8049
    Likes Given
    26489

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Quote By korino
    samahani kaka! je hizi mbegu hazina madhara kwa wajawazito?
    Mkuu korino hazina madhara hizo Lozi kwa mwanamke mjamzito anaweza kula tu ni kama njugu tu hizo Lozi.
    korino likes this.
    Only Do What Your Heart Tells You




    Allah
    Has Not Revealed A Disease without Treatment....
    (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

  • #20
    MziziMkavu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 3rd February 2009
    Location : European Union
    Posts : 22,106
    Rep Power : 19193
    Likes Received
    8049
    Likes Given
    26489

    Default Re: Maradhi ya Wasiwasi

    Dawa Zingine za Tiba Mbadala Zinazotibu Ugonjwa wa Wasiwasi :


    Natural anxiety remedies that really make a difference

    When people think about anxiety meds, the first option in their mind is pharmaceuticals. And that is actually a shame, since anxiety meds are known to have many unpleasant side effects. They should be used only on extreme scenarios where no other anxiety treatment option seems to work.

    Conversely, there are various herbal remedies available, which more and more people are turning to these days, for good reason too. Besides being healthier than pharmaceuticals, these remedies have little side effects. And if you think that herbal remedies are limited to relaxation inducing herbs such as chamomile and kava, think again.


    This article will provide you with a comprehensive selection of herbs that can be used to treat specific manifestations of anxiety. From heart palpitations to irritable bowel syndrome, there are many symptoms that can be appeased with the right herbal medicine. You should try these herbs as a complement to your treatment. You will be pleasantly surprised with the results!


    Natural herbal remedies that reduce anxiety symptoms


    Catnip soothes your mind and helps you relax.

    This herb is part of the mint family, and it can be used to alleviate stomach cramps, spasms and irritations. It’s also helpful to reduce pain from localized inflammations (such as rheumatism) and even help overcome discomforts caused by conditions such as smallpox and scarlet fever. Most commonly, catnip tea is used as a natural medicine for headaches caused by insomnia, to stimulate appetite and even to normalize menstruation periods in women. This herb can be used by anyone, even children.


    Chamomile
    is an amazing natural sedative.


    Many people suffering from anxiety use this common herb to reduce nervousness, headaches and even hysteria. It’s also effective in reducing digestive discomforts and lack of appetite. Chamomile can be used by anyone (even babies) and it’s good for the liver and lungs. This herb has countless benefits, but it should not be used for extended periods of time.


    Fennel
    helps relieve gastrointestinal disturbances.


    The seeds of this herb are widely used for culinary purposes, but they’re also a great natural medicine if you need something with analgesic, diuretic or antispasmodic properties. They can be used to facilitate digestion, reduce coughing, manage asthma and bronchitis, minimize intestinal spasms, and even treat urinary infections. It also helps relieve fluid retention and aid elimination of toxins; as such, fennel seeds can also be used to treat food poisoning. This herb can be used by anyone, although pregnant women should avoid over-using it.


    Kava Kava
    directly confronts and reduces anxiety.


    This is a popular natural sedative, which is popular with people with stress, insomnia and anxiety problems. It’s known to relax muscles and has anti-convulsant properties. It’s actually fairly potent, and should not be used for extended periods of time without medical guidance. Intoxication with Kava can cause adverse reactions such as headache, dizziness and allergic reactions. People with liver problems should avoid using this herb.


    Hops
    will help calm down your nervous system.


    A climbing plant with a long history of medicinal applications, Hops can be used to treat insomnia, stress, headaches, indigestion and nervousness in general. It helps reduce fever, skin ulcerations and it can be used to treat infections and certain skin problems. Moreover, it’s also known to provide relief from rheumatism and lower uric acid levels. Hops can be used safely by anyone, unless ingested in high dosages or through extended periods of time.


    Motherwort
    is known to help stabilize emotions.


    This plant is a popular choice for treating menstrual discomforts. It’s also favored by pregnant women looking for a natural way to manage stress and pregnancy related tensions, although it should not be taken in the first two trimesters. Motherwort is known to stimulate circulation without increasing pulse rate, so it can be used to treat lower blood pressure and treat certain heart disorders such as arrhythmias and palpitations. Motherwort will help induce calmness without making you feel drowsy, and it’s also a mild anti-depressant.


    Passionflower
    will induce peace of mind and relaxation.


    A wonderful relaxer, passionflower tea is great for reducing muscle tension and spasms caused by anxiety, as well as helping with insomnia. It works great for calming your nerves and it will effectively help you overcome states of agitation, mood swings, headaches and even common anxiety symptoms such as hot flashes. Word of caution: this herb must not be used by patients being treated with medicines of the MAO inhibitor class.


    Skullcap
    stabilizes mood and promotes drowsiness.


    With its sedative, tonic, and anti-inflammatory properties, the skullcap herb can be used to soothe twitching muscles, overcome seizures, trembling and even to manage epilepsy. It will also help minimize heart palpitations, depressions, insomnia and restlessness. It should not be used by pregnant women, and everyone else should use it in moderate quantities.


    St. John’s Wort
    works wonders to reduce depression.


    This herb is known to prevent viral infections in the chest, lungs and genitalia, as well as soothe muscles pains, but it’s arguably more popular as a mood lifter. As such, it’s a favored choice by people suffering from anxiety and depression. Anyone can use this herb safely, and its potential benefits go as far as helping overcome diarrhea and gastroenteritis.


    Valerian
    is another potent natural sedative.


    The reason why this herbal medicine is so popular to treat insomnia is because it promotes drowsiness without affecting the stages of sleep (a common side effect of sedatives). It may help relieve stomach and uterine cramps, bronchial spasms and persistent coughs. Moreoever, it’s a wonderful muscle relaxant and a great tranquilizer. It should not be used by children under 12 years of age, pregnant women and patients taking antidepressants or anti-anxiety drugs.


    General guidelines when using natural herbal remedies to treat anxiety:


    • Avoid mixing natural herbs with pharmaceuticals without consulting your doctor
    • Do not abuse these herbal remedies, or use them for extended periods
    • Make sure you don’t have allergies to specific herbs, before you use them
    • Herbal remedies produce best results when combined with a healthy lifestyle


    Natural anxiety remedies beyond herbal solutions

    If you’re looking for natural anxiety remedies, there are many options you should also explore in addition to herbal medicine. Many anxiety sufferers find relief once they learn breathing exercises and practice them consistently. Others find the most improvement after they become adepts of regular physical exercise. For some people, avoiding stimulants has proven most effective to help reduce their anxiety levels.


    And if you’re too lazy to change your life around drastically right away, not all hope is lost. There are natural anxiety remedies that don’t even require much activity or effort! For example, you may want to learn about desensitization and improving your internal dialogue.

    There’s also a visualization technique that can actually be both fun and relaxing and deliver certain other benefits asides from reducing your anxiety.
    Only Do What Your Heart Tells You




    Allah
    Has Not Revealed A Disease without Treatment....
    (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

  • Miaka 50
    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...