Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Lets talk about HAJA KUBWA...

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 53
    1. #1
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,315
      Rep Power : 18677
      Likes Received
      1097
      Likes Given
      1049

      Default Lets talk about HAJA KUBWA...

      Wakuu poleni na majukumu ya ujenzi wa taifa hili, linalofaidiwa na wachache waliopewa jina la ‘wajanja’.
      Poleni sana…
      Leo nataka tusemezane kitu cha tofauti kabisa, sio kigeni kwa yeyote ila masuala yake huwa hayasemwi mara kwa mara.
      Leo nataka tuzungumzie KINYESI, unashangaa nini? Namaanisha nisemalo, leo nataka tufunguke kuhusu uchafu ambao ni matokeo ya mfumo wa umen’genyaji chakula a.k.a ‘kimba’ a.k.a mavi ukipenda haja kubwa, lakini kwa Kiswahili sanifu ni kinyesi.
      Mada yangu kuhusu haja kubwa itazingatia zaidi uhusiano kati yacho na maisha yetu ya kila siku katika muktadha halisi. Sawasawa?
      UTANGULIZI

      Kama tunavyojua (ukibisha una yako), kwenda haja kubwa ni suala la muhimu na la lazima kwa binadamu yeyote, kama tu ilivyo kula na ndio maana ili nyumba ikamilike ni shurti iwe na jiko na choo. Hivyo tu ndio vinaipa legacy nyumba ya kuishi, sio bafu wala chumba cha kulala. Kutokana na unyeti wa suala husika, sina budi kuweka wazi mtazamo wangu juu ya masuala kadhaa kuhusu haja kubwa, ambayo pengine (weka msisitizo hapa) yanaweza kuboresha mazingira ya huduma hii muhimu kwetu baada ya chakula.
      CHOO

      Kama ilivyodhihiri hapo juu (hutaki unaacha), choo ni kati ya sehemu muhimu zaidi katika nyumba. Ili kuwe na unyaji wa starehe na uliotukuka ni lazima choo kiwe safi na chenye mazingira rafiki kwa mtumiaji wacho. Kuna vyoo vya aina nyingi, hata ule unyaji wa kuchimba kishimo na kufukia unaweza kutafsiriwa kama choo endapo utakuwa ni wa kudumu. Kuna hivi ‘Western Type’ (vya kukaa) ambavyo wanaita vyoo vya kizungu, na kuna vyoo vya Kiafrika almaarufu kama squart toilets, au ‘drop in’, yaani vya shimo among many other types. Binafsi ni mshabiki wa vyoo vya shimo (siku hizi kina option ya kuweka shank kikafanana na cha kizungu) kwa kuwa kinaleta hali fulani ya comfortability wakati wa kukata gogo. Vyoo vya kukaa huwa vinaleta hali ya kuhisi kama unajinyea kwa vile unajisaidia huku mapaja yakiwa yamebanana, tofauti na kanuni za unyaji ambapo kunya huku umechuchumaa is much better, kiafya na kiakili. Sifa nyingine ya choo ninachokipenda (though it may sound ridiculous), ni hali ya choo kutokuwa na paa, yaani kiwe hakijaezekwa. Hii itapelekea choo (hasa kinapokuwa cha shimo) kuwa kikavu muda mwingi na hivyo kupunguza hali ya kinyaa inayopatikana chooni. Vilevile, kunakupa view nzuri ya anga wakati unakata gogo, hivyo kuchochea fikra za mnyaji. Ni mara nyingi watu wamekuwa wakisema kuwa wakati wa haja kubwa ni wakati mzuri wa kutafakari na kupanga mikakati ya kimaisha, if that is true, a blue sky is even much better. Ubaya wa feature hii ya choo ni kuwa si nzuri sana wakati wa mvua au jua linapokuwa kali sana kwani huondoa ladha ya gogo. KUNYA STAREHE BWANA!
      Mwisho, choo kiwacho chochote, lazima kiwe katika hali ya usafi muda wote, ulazima huu unatokana na ukweli kwamba kama choo sio safi, kinaweza kusababisha magonjwa kadha wa kadha ya kuambukiza.
      MIUNDOMBINU
      Asikudanganye mtu, muundombinu mkubwa wa choo ni maji, haijalishi ni cha aina gani, ingawa uhitaji wa maji kwa wale wanaotumia vyoo vya kizungu vya kuflash ni mkubwa ukilinganisha na sie wa vyoo vya kulenga. Kwa watumiaji wa ‘Western type’, kuwa na mfumo kamili wa maji katika vyoo vyao haikwepeki, kwa wanaotumia vya shimo si lazima sana kuwa na mfumo kamili wa maji, unaweza kuweka ndoo ya maji ambayo italazimu kuwa na maji muda wote, au kama umenganishwa na mfumo wa maji wa manispaa uliyomo unaweza kuweka bomba la maji chooni, au just nje ya choo. Maji haya yatakuwa kwa ajili ya kusafisha ‘privates’ baada ya kukata gogo (endapo unatumia maji), yatatumika kunawa mikono baada ya shughuli kwisha na pia yatatumika kusafidha choo (tundu, sakafu na kuta). Miundombinu mingine ni pamoja na taa na misumari ya kutundikia nguo wakati unafanya mambo yako.
      UNYAJI

      Hi indio shuguli yenyewe sasa baada ya shuguli zote za awali za maandalizi kuwa ziko sawa na hapa ndipo kuna matatizo mengi ya kujitakia ambayo watu hawataki kuyasema. Matatizo yanaweza kuwa yamesababishwa na aina ya choo unachotumia au kutokaa sawa kwa miundombinu ya choo unachotumia, mfano, baadhi ya watu (mimi kwa mfano) huwa hawako comfortable na vyoo vya kukaa aina ya Western, kwani kujisaidia ukiwa umechuchumaa ni vizuri kwa kuwa mapaja yanakuwa yameachana vya kutosha hivyo kinyesi hutoka kwa urahisi na bila bugudha yoyote. Unyaji katika mazigira ya vyoo vya kukaa hufanya mapaja kubanana, hivyo kupelekea hatari ya maambukizi katika mapaja na kuongeza hatari ya maambukizi katika njia ya mkojo (UTI) hasa kwa wanawake.
      Katika kipengele hiki ningependa pia niseme kuhusu aina za haja kubwa na changamoto zake kwa wanyaji. Kimsingi, **** mbari kuu tatu za haja, ngumu, laini na majimaji au uharo. Aina mbili za mwanzo zinatokana na tabia za ulaji na hii ya mwisho inasababishwa na magonjwa, hasa yanayohusu tumbo. Walio wengi wanapendelea kupata choo laini, na wachache hupenda choo ngumu, pasi na shaka yoyote hakuna anayependa kuharisha kwa vile kunaambatana na kugonjeka. Choo kigumu sana kinaweza kusababisha mipasuko kwenye njia ya haja.
      Tumesema kuwa aina za haja hutokana na vyakula tulavyo, haja ngumu inatokana na kupendelea vyakula vikavu na vigumu, pia kutokunywa maji ya kutosha wakati ili upate choo laini inakulazimu kunywa maji ya kutosha (3-5 litres kwa siku), kutumia mboga na matunda jamii ya nyuzinyuzi pamoja na aina fulani ya matunda kama vile papai na parachichi. Kwa wanaopata choo majimaji au uharo, tiba ya haraka ni supu ya ngano, lakini pia wanatakiwa kunywa kiasi kikubwa cha maji ili kufidia maji yanayopotea mwilini kwa njia ya kuharisha, lakini pia ni muhimu na lazima kutibu ugonjwa wa msingi ambao umepelekea kupata choo majimaji.
      Changamoto nyingine ni ulaji wa pilipili kupita kiasi ambao husababisha muwasho katika njia ya haja kubwa wakati wa unyaji na wakati mwingine vidonda kwenye puru (sehemu ya ndani ya njia ya haja kubwa).
      USAFI

      Kuna namna nyingi za kusafisha njia ya haja kubwa baada ya kujisaidia. Kujiswafi huku wengine huita kuchamba au kutawaza, lakini kwa ujumla ni kusafisha tundu la haja kubwa na maeneo yanayolizunguka ili kuondoa mabaki ya kinyesi.
      Namna kuu na iliyozoeleka kwenye mazingira yetu ni maji, nimesema kuwa hii ni namna kuu kwa vile hata baadhi ya vitabu vya dini vimetaja waziwazi kama namna pekee ya kujiswafi. Baadhi ya watu hutumia karatasi laini maarufu kama toilet papers na wengine hutumia vyote yaani toilet paper na maji kwa kuanza kupunguza uchafu kwa karatasi hizo na kasha baadae kumalizia na maji. Kimsingi kila njia ina faida na hasara zake, mfano, utumiaji wa karatasi huwafaa zaidi wale wasio na vinyweleo vingi katika tundu la haja kubwa na maji ni mazuri zaidi kwa wale waliojaliwa haya makatamavi. Utumiaji wa vyote viwili ni mahususi kwa wale wanaopata choo laini (sio majimaji) kwa kuwa aina hii ya kinyesi huacha mabaki mengi.
      Faida za kutumia karatasi laini ni pamoja na kuepuka kinyaa cha kushika kinyesi kwa mkono ingawa wanaopinga matumizi ya tishu wanaona kama ni sawa na kujisiliba uchafu badala ya kujisafisha. Maji ndio njia inayopendekezwa na wengi katika mtazamo wa Kiafrika, ingawa nayo huleta hali flani ya kutojisikia vizuri kwa vile unalazimika kuvaa nguo huku makalio yakiwa yamelowa maji.
      Aina nyingine za uchambaji ni pamoja na matumizi ya majani, mawe au kujisugua ukutani au kwenye shina la mti, ingawa njia hizi zinatafsiriwa na wengi kama zisizokuwa za kistaarabu.
      Cha mwisho na cha muhimu baada ya kujiswafi ni kunawa mikono kwa maji sabuni ili kuondoa uwezekano wa kuondoka na vimelea wa ugonjwa katika mikono.
      HITIMISHO

      Kwa muda huu ni hayo tu niliyokuandalia kuhusu KINYESI, unaweza kutumia wasaa wako kutoa maoni, ushauri au maswali yako kuhusu makala hii.

      Enjoy your shit,
      Mphamvu.
      "...kukaa kimya ni jibu la mjinga!"
      -Leila Rashid (Jahazi Modern Taarab)

    2. Miaka 50

    3. #2
      King'asti's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th November 2009
      Location : The Jungle
      Posts : 17,115
      Rep Power : 28888
      Likes Received
      11618
      Likes Given
      4783

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Yaani nimesoma mwanzo hadi namaliza mwishoni, nimekumbuka kila aina ya choo ambacho nimewahi kutumia maishani mwangu. Nimeanzia kutengwa na mama, poti, na kuendelea!

      Umesahau kusema kama mandhari ya choo inaruhusu sio mbaya kuwepo majarida ya kusoma wakati unaendeleza starehe hii muhimu.

      Pia kuna issue ya ku-train your bowel movement. Ukifundisha mwili wako discipline unaweza kujikuta unakuwa na ratiba nzuri sana ambayo ni convenient.
      TIMING likes this.

    4. #3
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,553
      Rep Power : 5612
      Likes Received
      6210
      Likes Given
      2281

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      raha ya kunya uwe na kijarida, au unaingia jf, huku unachangia mada, huku unashusha vitu......

      King'asti, kalale mama, mie naenda kulala, jf mpaka saa tisa kumi usiku itatuua...
      MziziMkavu likes this.

    5. #4
      Tripo9's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2009
      Posts : 1,616
      Rep Power : 816
      Likes Received
      254
      Likes Given
      458

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Puuuuu.... Hii thread inanukaaaaaaaaaaaa! khaaaa.........
      "Smile though your heart is aching"...Me says

    6. #5
      BAGAH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2012
      Posts : 4,363
      Rep Power : 8785
      Likes Received
      954
      Likes Given
      1418

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Mphamvu usiku wa saa nane ukawazaje hii mambo jameni...kweli hii ndo Jf!
      MziziMkavu likes this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Kapalampya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th December 2010
      Location : COUNTER
      Posts : 1,530
      Rep Power : 806
      Likes Received
      210
      Likes Given
      326

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      hivi kibongo bongo ipo kwenda kunya na kijarida mi nkajua tunaenda na sport tu kweli kua uyaone..

    9. #7
      Smile's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th July 2011
      Location : paradise
      Posts : 11,129
      Rep Power : 23366
      Likes Received
      8110
      Likes Given
      5852

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      khaa jf kuna mambo loh....
      Batta Hb Boy likes this.
      It’s good to test a guy first before you believe him. But don’t let him wait that long

    10. #8
      Judgement's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th November 2011
      Location : Town
      Posts : 7,009
      Rep Power : 7209
      Likes Received
      2768
      Likes Given
      12

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Niliwahi kwenda mkoa flani Magharibi mwa Tz nikawa na mizunguko ya kibiashara ktk baadhi ya vijiji, kuna siku nikalala kwa Mzee mmoja hapo kijijini , akiwa ndiye mwenyeji wangu.
      Mzee yule alikua anamiliki wake 6 , kilichoniachia historia ni pale mgeni mie nilipoomba kwenda msalani, nikapewa jembe tena bila hata kopo la maji then nikaonyeshwa chaka , hapo nikaambiwa hua wanajisaidiaga mchana, na ikiwa usiku hua wanashuka ziwani. Kwani nyumba haikua mbali na Ziwa.
      HAINA UBISHI NYUMBA CHOO.

    11. #9
      TANMO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Tanzagiza
      Posts : 5,045
      Rep Power : 7769
      Likes Received
      1806
      Likes Given
      3439

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Duh..!
      Do Something......

    12. #10
      Globu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2011
      Location : Giningi
      Posts : 4,842
      Rep Power : 3302
      Likes Received
      535
      Likes Given
      30

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Dah!!! Hii thread safi sana.

    13. #11
      Ambitious's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th December 2011
      Posts : 1,802
      Rep Power : 733
      Likes Received
      559
      Likes Given
      243

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      RIP my breakfast.
      sijui nini likes this.

    14. #12
      Adrian Stepp's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2011
      Posts : 1,573
      Rep Power : 713
      Likes Received
      438
      Likes Given
      2560

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Hii thread wala sijaisoma nimescroll down na kuanzakucheka..hata sijui Mphamvu uliwaza nini..nimecheka sana!
      Watu wakimya wamejaliwa busara, ufahamu na midomo inayonuka!

    15. #13
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,553
      Rep Power : 5612
      Likes Received
      6210
      Likes Given
      2281

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      hakuna kitu kinaniboa kama nikisafiri, kukata gogo kwenye vyoo vya hoteli.......
      LE GAGNANT and Sashel like this.

    16. #14
      Cantalisia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2011
      Location : Dar es salaam
      Posts : 4,953
      Rep Power : 3053
      Likes Received
      2630
      Likes Given
      2829

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Mweeeeeeeeeee!
      "Be good to the people on your way up,coz you might meet them on your way down"

    17. #15
      mtu chake's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2010
      Location : Kivu
      Posts : 2,159
      Rep Power : 1761
      Likes Received
      1010
      Likes Given
      1327

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      ....uwiiiii.....
      @@

    18. #16
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,315
      Rep Power : 18677
      Likes Received
      1097
      Likes Given
      1049

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Quote By King'asti
      Yaani nimesoma mwanzo hadi namaliza mwishoni, nimekumbuka kila aina ya choo ambacho nimewahi kutumia maishani mwangu. Nimeanzia kutengwa na mama, poti, na kuendelea!

      Umesahau kusema kama mandhari ya choo inaruhusu sio mbaya kuwepo majarida ya kusoma wakati unaendeleza starehe hii muhimu.

      Pia kuna issue ya ku-train your bowel movement. Ukifundisha mwili wako discipline unaweza kujikuta unakuwa na ratiba nzuri sana ambayo ni convenient.
      Una miaka mingapi King'asti, maana kama umekelia poti kwa mazingira ya kibongo utakuwa mtoto sana.
      Ishu ya majarida inawezekana katika vyoo vya kukaa, ambako ni rahisi kuwa na balance ya kushikia hilo gazeti. Bowel movement, ni rahisi sana, you just eat with dicipline, kuwa na ratiba maalum ya kula, muda na kiasi cha chakula ambacho hakibadiliki badiliki kunafanya uwe na muda mahususi wa kukata gogo. And thats pretty cool!
      "...kukaa kimya ni jibu la mjinga!"
      -Leila Rashid (Jahazi Modern Taarab)

    19. #17
      sijui nini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2010
      Location : home
      Posts : 1,743
      Rep Power : 7635
      Likes Received
      497
      Likes Given
      445

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      zis is JF....
      The signature you are looking at now does not exist.....

    20. #18
      vicent tibaijuka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2012
      Location : Iceland
      Posts : 263
      Rep Power : 413
      Likes Received
      30
      Likes Given
      38

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      nilifikiri hapa tunaongelea magonjwa kumbe......................... .........!!!!!!!!!!!!!!!

    21. #19
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,315
      Rep Power : 18677
      Likes Received
      1097
      Likes Given
      1049

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Rudisheni topic yangu mulikoitoa, mimi sio taahira mpaka nikaiweka pale.
      Nina uzoefu wa miezi 12+ humu JF, zaidi ya post 3500 bila kusahau ban 5 katika maisha yangu ya JF.
      Twafadhall?
      MziziMkavu and Consigliere like this.
      "...kukaa kimya ni jibu la mjinga!"
      -Leila Rashid (Jahazi Modern Taarab)

    22. #20
      Rubi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2009
      Posts : 1,237
      Rep Power : 736
      Likes Received
      154
      Likes Given
      132

      Default re: Lets talk about HAJA KUBWA...

      Thanx ni nzuri ina mafundisho.
      Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.

    23. Study Abroad
    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...