Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 39 of 39
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,189
      Rep Power : 19210
      Likes Received
      8154
      Likes Given
      26620

      Thumbs up Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)




      FAIDA YA TUNDA LA PARACHICHI - PEA (AVOCADO)
      Ndani ya tunda hili kuna maji kiasi kidogo sana ukilinganisha na matunda mengine lakini kuna mafuta mengi na unaweza kuchanganya kula na tunda lingine kama vile apple, ndizi, chungwa au hata maziwa kwa kutengeneza juisi.

      TINDIKALI
      Licha ya kuwa na mafuta parachichi lina tindikali (acid) mbalimbali ikiwemo inayojulikana kama amino ambayo husaidia sana kukinga na kutibu maradhi katika mwili wa binadamu. Tunda hili pia lina protini ya kiwango cha juu.
      Pia kuna tindikali inayoitwa oleic acid kwenye parachichi ambayo husaidia kukinga magonjwa ya moyo, kiharusi na kansa.

      VITAMINI “E” NA B6
      Imeelezwa na wataalamu kuwa tunda hili lina kiwango kikubwa cha vitamini E kuliko ile inayopatikana kutoka kwenye mazao ya wanyama.Parachichi lina vitamini hiyo nyingi kuliko inayopatikana katika mayai ambayo yanasifika kwa kuwa na vitamini e, hivyo hii inathibitisha kuwa lina faida kubwa mwilini.

      Licha ya vitamini E pia ndani ya parachichi kuna vitamini B6 na kuna madini ya chuma (Iron) kwa wingi na madini ya potassium, pamoja na vitamin B6 na E mlaji anaweza kuletawa nafuu sana kama alikuwa na matatizo ya stress, matatizo ya uzazi kama ugumba na jogoo kutopanda mtungi Nguvu za kiume pia tunda hili linasaidia (impotence) .

      FAIDA ZA PARACHICHI
      Licha ya binadamu kufaidika na virutubisho vya tunda hili kuna faida nyingi za parachichi kama vile majani ya mti wake pamoja na magamba, baadhi ya watu hutumia kutibu maradhi ya kuharisha.

      Majani na magamba hayo hutibu pia tatizo la gesi tumboni, kutuliza kikohozi pamoja na matatizo ya ini na kusafisha njia ya mkojo.

      Hata hivyo, kwa mujibu wa wataalamu wa dawa za mitishamba, dawa hii haifai kutumiwa na wanawake ambao wana mimba kwani wakitumia inaweza kusababisha kuharibika kwa ujauzito.


      HEDHI
      Hata hivyo, wataalamu wa tiba mbadala wanasema dawa hiyo inaweza kuwasaidia sana wanawake ambao wameshindwa kuona siku zao kwa wakati, na wakitumia vyema wanaweza kuanza kuona siku zao.

      Aidha, tunda
      hili linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, kwani parachichi lina nyuzinyuzi “fiber” ambayo ni muhimu kukinga kuta za utumbo. Watu wenye maradhi ya anaemia, diabetes, matatizo ya mfumo wa neva, matatizo ya mishipa ya moyo hasa wa artery wanashauriwa kula tunda hili mara nyingi.

      Lakini pia tunda hili limethibitishwa na wataalamu kuwa linapunguza kwa kiwango kikubwa cholesterol kutoka kwenye damu hasa kwa watu wanene.

      Tunda hili husaidia kulainisha ngozi na kuondoa mikunjo, hung`arisha na kulainisha nywele na kuzisaidia kukua pia kuziimarisha na kuzuia kukatikakatika.

      Parachichi unaweza kulila kwa kulimenya au kwa kulisaga na kutengeneza juisi na kama nilivyoeleza hapo juu unaweza kuchanganya na matunda mengine kama tulivyoyataja na hutaharibu virutubisho vilivyomo badala yake utaongeza ubora wa juisi yako.

      Watoto wadogo pia unaweza kuwapa tunda hili na wakafaidika na haya tuliyoyaandika.
      Parachichi pia huweza kutumika kama siagi kwa kupaka kwenye mkate au kuchanganya na wali.

      Haya wale wanaopenda ngozi zao za mwilini zisijikunje hata wakiwa watu wazima wadumu kula tunda hili kila siku katika maisha yao basi ngozi za mwili wao hazitajikunja hata usoni watakuwa kila siku vijana hata wakiwa wazee.
      Kibunango, BAK, Mahmood and 23 others like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. Miaka 50

    3. #21
      Tumaah's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 29th May 2012
      Posts : 8
      Rep Power : 353
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Mziz mkavu,thanks....
      nina tatizo la vidonda vya tumbo natumain tunda hili litanisaidia...
      MziziMkavu likes this.

    4. #22
      Mafuluto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2009
      Posts : 797
      Rep Power : 2973
      Likes Received
      165
      Likes Given
      306

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Ndiyo fiber hiyo, ambayo inapatikana na wingi ktk tunda hili !!
      Quote By BADILI TABIA
      mzizi mkavu nisaidie, nikila avocado nashiba siku nzima, yaani haijalishi nimekula kiasi gani...... Inatokana na nini?
      MziziMkavu likes this.

    5. #23
      Kifulufumbii's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 29th May 2012
      Posts : 1
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Hiyo imetulia Mzizimkavu
      MziziMkavu likes this.

    6. #24
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,189
      Rep Power : 19210
      Likes Received
      8154
      Likes Given
      26620

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Quote By BADILI TABIA
      mzizi mkavu nisaidie, nikila avocado nashiba siku nzima, yaani haijalishi nimekula kiasi gani...... Inatokana na nini?
      @BADILI TABIA mkuu kama alivyokujibu mkuu@Mafuluto kuwa ndani ya tunda la avucado kuna fiber nyingi ndio inayokufanya unakuwa husikii njaa ukilila hilo tunda la avucado hakuna madhara yoyote endelea kulila hilo tunda

      Quote By Mafuluto
      Ndiyo fiber hiyo, ambayo inapatikana na wingi ktk tunda hili !!
      mkuu@Mafuluto asante kwa msaada wako wa kuelimisha watu ubarikiwe
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    7. #25
      Kaparatus's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th October 2011
      Posts : 29
      Rep Power : 389
      Likes Received
      4
      Likes Given
      6

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      MziziMkavu nikitia sukari au asali katika juice ya parachichi kuna madhara yoyote?
      MziziMkavu likes this.

    8. RukaaJuu Final

    9. #26
      King Kong III's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Enaboishu-Umenyeni
      Posts : 11,920
      Rep Power : 5062
      Likes Received
      3199
      Likes Given
      2653

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      ujumbe mzuri.
      MziziMkavu likes this.

    10. #27
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 14,973
      Rep Power : 3703
      Likes Received
      3579
      Likes Given
      5769

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      MziziMkavu
      naomba kuuliza niliambiwa ukila sana avocado linaongeza uzito kwa haraka ni kweli?
      MziziMkavu likes this.
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..

    11. #28
      Kaunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Wild wild west
      Posts : 8,438
      Rep Power : 13324
      Likes Received
      7667
      Likes Given
      6911

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Thanks MziziMkavu
      weekend hii nimetengeneza juice ambayo ilikuwa na vitu vifuatavyo:-
      2 Nanasi
      2 Avocado
      2 Bananas
      2 Cucumber
      2 Carrots
      Fungu la tembere na
      20 passion fruits.

      Nimepata si tu 5ltrs of juice, bali chakula. Nikinywa glass moja, inanitosha kabisa kulalia. Ofisini ndicho nitachoshindia today. Nina uhakika ninapta manutrients ya kutosha tu na weight naiangalia pia.

      Thanks kwa tips nzuri za afya!
      ..........When you run out of rope; grab onto faith.......... T.B Joshua

    12. #29
      Manumbu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2009
      Location : Close to U
      Posts : 1,127
      Rep Power : 724
      Likes Received
      259
      Likes Given
      760

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Asante kwa elimu nzuri.
      MziziMkavu likes this.
      "Falling Down does not mean being Buried" - Manumbu on 1st June 2011

    13. #30
      Mamndenyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 12,121
      Rep Power : 31822
      Likes Received
      6000
      Likes Given
      19570

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Asante sana mwalimu.
      MziziMkavu likes this.
      SIYO WOTE WANAOTANGATANGA WAMEPOTEA

    14. #31
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,873
      Rep Power : 1977
      Likes Received
      2352
      Likes Given
      3037

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Kaunga,

      Unakaa mitaa ipi umenitamanisha sanaa.


      Quote By Kaunga
      Thanks MziziMkavu
      weekend hii nimetengeneza juice ambayo ilikuwa na vitu vifuatavyo:-
      2 Nanasi
      2 Avocado
      2 Bananas
      2 Cucumber
      2 Carrots
      Fungu la tembere na
      20 passion fruits.

      Nimepata si tu 5ltrs of juice, bali chakula. Nikinywa glass moja, inanitosha kabisa kulalia. Ofisini ndicho nitachoshindia today. Nina uhakika ninapta manutrients ya kutosha tu na weight naiangalia pia.

      Thanks kwa tips nzuri za afya!
      MziziMkavu likes this.

    15. #32
      Kaunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Wild wild west
      Posts : 8,438
      Rep Power : 13324
      Likes Received
      7667
      Likes Given
      6911

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Quote By Ngongo
      Kaunga,

      Unakaa mitaa ipi umenitamanisha sanaa.
      Karibu Ngaramtoni karibu na kwa Ray! LOL
      MziziMkavu likes this.
      ..........When you run out of rope; grab onto faith.......... T.B Joshua

    16. #33
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 14,973
      Rep Power : 3703
      Likes Received
      3579
      Likes Given
      5769

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Quote By Kaunga
      Thanks MziziMkavu
      weekend hii nimetengeneza juice ambayo ilikuwa na vitu vifuatavyo:-
      2 Nanasi
      2 Avocado
      2 Bananas
      2 Cucumber
      2 Carrots
      Fungu la tembere na
      20 passion fruits.

      Nimepata si tu 5ltrs of juice, bali chakula. Nikinywa glass moja, inanitosha kabisa kulalia. Ofisini ndicho nitachoshindia today. Nina uhakika ninapta manutrients ya kutosha tu na weight naiangalia pia.

      Thanks kwa tips nzuri za afya!
      ooh mama Kaunga fungu la tembele tena oops will try this over the weekend ..
      Niambie test madame kabla sijaharibu siku yangu
      MziziMkavu likes this.
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..

    17. #34
      Baba_Enock's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Bunju "B"
      Posts : 5,818
      Rep Power : 1900
      Likes Received
      1161
      Likes Given
      977

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Aminia Dokta... Thanks
      MziziMkavu likes this.
      Ad Majorem Dei Gloriam - "For the greater glory of God"

    18. #35
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,189
      Rep Power : 19210
      Likes Received
      8154
      Likes Given
      26620

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Quote By Tumaah
      Mziz mkavu,thanks....
      nina tatizo la vidonda vya tumbo natumain tunda hili litanisaidia...
      @Tumaah Aidha, tunda hili linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, kwani parachichi lina nyuzinyuzi “fiber” ambayo ni muhimu kukinga kuta za utumbo. Watu wenye maradhi ya anaemia, diabetes, matatizo ya mfumo wa neva, matatizo ya mishipa ya moyo hasa wa artery wanashauriwa kula tunda hili mara nyingi.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    19. #36
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,189
      Rep Power : 19210
      Likes Received
      8154
      Likes Given
      26620

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Quote By Kaparatus
      MziziMkavu nikitia sukari au asali katika juice ya parachichi kuna madhara yoyote?
      @Kaparatus hakuna madhara yoyote yale ila haipendezi tu kuchanganya Asalina hilo tunda la Parachichi kunywa asali kisha kula hilo tunda kila kitu na faida zake.

      Quote By manasa
      Faida zake zimenifurahisha nitazidi kulitumia
      Swali- mafuta yake je hatanenepeshi?
      @manasa mafuta yake hayanenepeshi wala hayana madhara hebu soma hapa VIRUTUBISHO VYA PARACHICHI

      Kwa ujumla, parachichi ni chanzo kizuri cha Vitamini K, Vitamini B6 na Vitamini C.
      Aidha, tunda hili lina kiwango kizuri cha virutubisho aina ya Folate, kopa na ufumwele (Fiber). Fiber ni muhimu katika kuwezesha mtu kupata choo


      laini na bila matatizo. Bila kusahau kwamba tunda hili ni chanzo kizuri pia cha madini ya Potasiamu: ina kiwango kikubwa kuliko hata ndizi.
      Ingawa parachichi ni tunda, lakini lina kiwango kikubwa cha mafuta (fats) ambayo yanakadiriwa kuwa kati ya asilimia 71 – 88, kiwango ambacho ni cha juu kwa asilimia 20 ukilinganisha na matunda mengine. Kwa wastani, parachichi moja lina gramu 30 za mafuta, lakini kati ya hizo, gramu 20 ni za


      mafuta mazuri kiafya (Monounsaturated fats na Aloic Acid) ambayo husaidia kujenga afya bora mwilini.
      Utafiti zaidi kuhusu tunda hili unamalizia kwa kusema kwamba parachichi lina takribani aina 20 za Vitamin, madini na virutubisho muhimu


      (Phytonutriens) ambavyo hutuo kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mengi hatari. Baadhi ya Vitamini zilizomo na asilimia zake kwenye mabano ni pamoja na Vitamin E (4%), Vitamin C (4%), Folate (6%), Fiber (4%), Iron (2%) na Potasium (4%).


      Kwa ujumla tunda la Parachichi lina faida nyingi kiafya na tunatakiwa tuyale kwa wingi, hasa ukizingatia huu ndiyo msimu wake. ni jambo la kushangaza sana kuona kwamba watu wengine msimu wa maparachichi unaingia hadi unakwisha, mtu hajala hata moja.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    20. #37
      Mgalatia's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 28th November 2007
      Posts : 137
      Rep Power : 614
      Likes Received
      12
      Likes Given
      31

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Quote By MziziMkavu



      FAIDA YA TUNDA LA PARACHICHI - PEA (AVOCADO)
      Ndani ya tunda hili kuna maji kiasi kidogo sana ukilinganisha na matunda mengine lakini kuna mafuta mengi na unaweza kuchanganya kula na tunda lingine kama vile apple, ndizi, chungwa au hata maziwa kwa kutengeneza juisi.

      TINDIKALI
      Licha ya kuwa na mafuta parachichi lina tindikali (acid) mbalimbali ikiwemo inayojulikana kama amino ambayo husaidia sana kukinga na kutibu maradhi katika mwili wa binadamu. Tunda hili pia lina protini ya kiwango cha juu.
      Pia kuna tindikali inayoitwa oleic acid kwenye parachichi ambayo husaidia kukinga magonjwa ya moyo, kiharusi na kansa.

      VITAMINI “E” NA B6
      Imeelezwa na wataalamu kuwa tunda hili lina kiwango kikubwa cha vitamini E kuliko ile inayopatikana kutoka kwenye mazao ya wanyama.Parachichi lina vitamini hiyo nyingi kuliko inayopatikana katika mayai ambayo yanasifika kwa kuwa na vitamini e, hivyo hii inathibitisha kuwa lina faida kubwa mwilini.

      Licha ya vitamini E pia ndani ya parachichi kuna vitamini B6 na kuna madini ya chuma (Iron) kwa wingi na madini ya potassium, pamoja na vitamin B6 na E mlaji anaweza kuletawa nafuu sana kama alikuwa na matatizo ya stress, matatizo ya uzazi kama ugumba na jogoo kutopanda mtungi Nguvu za kiume pia tunda hili linasaidia (impotence) .

      FAIDA ZA PARACHICHI
      Licha ya binadamu kufaidika na virutubisho vya tunda hili kuna faida nyingi za parachichi kama vile majani ya mti wake pamoja na magamba, baadhi ya watu hutumia kutibu maradhi ya kuharisha.

      Majani na magamba hayo hutibu pia tatizo la gesi tumboni, kutuliza kikohozi pamoja na matatizo ya ini na kusafisha njia ya mkojo.
      Hata hivyo, kwa mujibu wa wataalamu wa dawa za mitishamba, dawa hii haifai kutumiwa na wanawake ambao wana mimba kwani wakitumia inaweza kusababisha kuharibika kwa ujauzito.


      HEDHI
      Hata hivyo, wataalamu wa tiba mbadala wanasema dawa hiyo inaweza kuwasaidia sana wanawake ambao wameshindwa kuona siku zao kwa wakati, na wakitumia vyema wanaweza kuanza kuona siku zao.

      Aidha, tunda
      hili linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, kwani parachichi lina nyuzinyuzi “fiber” ambayo ni muhimu kukinga kuta za utumbo. Watu wenye maradhi ya anaemia, diabetes, matatizo ya mfumo wa neva, matatizo ya mishipa ya moyo hasa wa artery wanashauriwa kula tunda hili mara nyingi.

      Lakini pia tunda hili limethibitishwa na wataalamu kuwa linapunguza kwa kiwango kikubwa cholesterol kutoka kwenye damu hasa kwa watu wanene.

      Tunda hili husaidia kulainisha ngozi na kuondoa mikunjo, hung`arisha na kulainisha nywele na kuzisaidia kukua pia kuziimarisha na kuzuia kukatikakatika.

      Parachichi unaweza kulila kwa kulimenya au kwa kulisaga na kutengeneza juisi na kama nilivyoeleza hapo juu unaweza kuchanganya na matunda mengine kama tulivyoyataja na hutaharibu virutubisho vilivyomo badala yake utaongeza ubora wa juisi yako.

      Watoto wadogo pia unaweza kuwapa tunda hili na wakafaidika na haya tuliyoyaandika.
      Parachichi pia huweza kutumika kama siagi kwa kupaka kwenye mkate au kuchanganya na wali.

      Haya wale wanaopenda ngozi zao za mwilini zisijikunje hata wakiwa watu wazima wadumu kula tunda hili kila siku katika maisha yao basi ngozi za mwili wao hazitajikunja hata usoni watakuwa kila siku vijana hata wakiwa wazee.
      Naomba ufafanuzi zaidi hapo kwenye Red.
      MziziMkavu likes this.

    21. #38
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,189
      Rep Power : 19210
      Likes Received
      8154
      Likes Given
      26620

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Quote By Mgalatia
      Naomba ufafanuzi zaidi hapo kwenye Red.
      @Mgalatia (Majani na magamba hayo hutibu pia tatizo la gesi tumboni, kutuliza kikohozi pamoja na matatizo ya ini na kusafisha njia ya mkojo) Ukichemsha hayo magamba na majani yake husaidia kuondowa Gesi iliyo tumboni kwako, na pia husaidia kuondosha hayo matatizo ya ini na kusafisha njia ya mkojo chemcha pamoja unywe.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    22. #39
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 573
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default Re: Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)

      Aksanteeee

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...