Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 33
    1. #1
      Simba Mkali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2012
      Posts : 375
      Rep Power : 443
      Likes Received
      79
      Likes Given
      118

      Post Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Nimesikia mengi kuhusiana na mti wa Mlonge lakini hii ni kali zaidi
      CAPE TOWN, (IPS). Wakati tatizo linalipolikabili Bara la Afrika, watu wanaangalia uwezekano wa kupata misaada kutoka kwenye mashirika ya kimataifa kutoka nje ya bara hilo.

      Lakini hali ya ukame inayoongezeka kwa kasi, miti yenye kuhimili ukame huku ikiwa na majani yenye viini lishe vingi inaweza kuwasaidia watu maskini, pia maeneo ya usalama wa chakula na utapiamlo, wao wenyewe.

      Shamba lenye hekta 15 lilipandwa miti ya Mlonge au wengine huuita mti wa miujiza ambao kwa Kiingereza unaitwa Moringa Oleifera, tayari umeshaanza kuleta mabadiliko katika jimbo moja maskini zaidi la Afrika Kusini la Limpopo.

      Majani ya Mlonge yamepachikwa jina la chakula chenye viwango kwasababu wanasayansi waligundua yana kiasi cha madini ya Kalisium yanayoweza kupatiakana katika glasi nne za maziwa, kiasi cha vitamini c inayopatikana kwenye machungwa saba, Potasium ya kwenye ndizi mbivu tatu. Pia unapata kiasi cha madini ya chuma mara nne zaidi ya kiasi kile kinachopatikana kwenye spinachi. kiasi cha vitamani A mara nne zaidi ya kile kinachopatikana kwenye karoti na kiasi cha protini mara mbili zaidi ya kile kinachopatikana kwenye maziwa. Ukiwa na mti wa Mlonge ni sawa na kuwa na Supermarket kwenye mti.
      Mavis Mathabatha aliyewahi kuwa mwalimu kutoka Tooseng, amekuwa akifanya bidii ya kufungua mashamba ya Mlonge kwa kipindi cha miaka mitatu sasa ambalo litamuwezesha kuzalisha majani ya kutosha ya Mlonge ili kusaidia kuleta mabadiliko katika jamii yake.
      "Nataka kuleta mabadiliko katika jimbo langu na nchi nzima kupitia mradi huu," alisema.
      Mwaka 2009, alianza kuvuna na kuyakausha na kisha kuyasaga majini ya Mlonge kutoka kwenye miti michache aliyokuwa ameipabnda.
      Unga huo wa Mlonge alikuwa ukiwachanganyia watoto 400 kutoka katika familia masikini waliokuwa wakipata chakula kutoka kwenye kituo maalum.
      Kituo hicho kinalisha watoto wanaotoka katika familia zenye kipato kidogo ambacho kiko chini ya dola 250 kwa mwezi.
      Hii inahusuisha watoto wote wa kike na kiume kutoka kwenye jamii hiyo ambayo ina tatizo la ukosefu wa ajira, umasikini na utapiamlo, wengine wana maambukizi ya UKIMWI.

      "Matokeo yake yalikuwa dhahiri kwa muda mfupi sana, Afya za watoto ziliboreka kwa muda mfupi.
      Anasema Elizabeth Serogole, meneja wa kituo hicho cha kulisha watoto ambaye anafanya kazi kwa kushirikiana na Mathabatha.
      Anasema watoto wengi waliokuwa wakionesha kuwa na utapiamlo, kama vile vidonda kwenye ngozi walianza kupona mara baada ya kula mlo huo uliochanganywa na unga wa Mlonge.

      Nyongeza hiyo ya Mlonge kwenye chakula chao iliwasaidia kupambana na magonjwa mengine yaliyojitokeza, pia iliwasaidia kuboresha uwezo wao wa kiakili," anasema Seregole.

      "Wengi sasa wanaweza kusoma vizuri shuleni," anasema. Walichokuwa wanahitaji ni kjiko kimoja cha unga wa molonge katika chakula chao kwa siku. Dk.Samson Tesfay anayseoma Afrika Kusini kwenye chuo kikuu cha Zulu Natal idara inayohusika na masuala ya mbogamboga na matunda,alisema Mlonge ni mmea wenye kutenda maajabu kwenye lishe.

      "Mlonge ni mmea wa kipekeeunaoweza kuutumia kwa faida nyingi, kama vile dawa, chakula, kuponyesha viungo mwilini na kusaidia kupambana na utapiamlo," anasema.

      Source-Gazeti la Nipashe Ijumaa Februari 24, 2012

      Binafsi nimeshasikia kuwa Mlonge unatibu magonjwa 300, bila ya kusahau kansa,maralia,vidonda vya tumbo,kuondoa sumu mwilini na hata kuongeza nguvu za kiume. Maderava wengi wa safari ndefu hutumia Mlonge kuondoa uchovu. Mlonge watu wa kule Tanga wanatumia kama mti wa kujengea fensi, Uzaramoni umepandwa karibu kabisa na vyoo vyao, Dodoma na Morogoro umejaaa tele. Dar mbegu zake zinauzwa kwa Shilingi 1000 kwa pakti.

      Mbegu hizo zina dozi ya 3x3x3 na ukizila kwa wingi huweza kukufanya kuhalisha na kutoa uchafu mwilini. Tafakari ndugu yangu dawa tunazo tunatimia madawa yenye sumu yaliyotayalishwa na wazungu.... Tafakari.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Tikerra's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2008
      Location : Morogoro
      Posts : 1,588
      Rep Power : 863
      Likes Received
      100
      Likes Given
      3

      Default

      Hii ni thread educative, hongera sana.These are the kind of threads one would like to read,sio thread za kijinga jinga tu.Okay,ninayo Milongelonge shambani kwangu.

      Lakini taste ya mbegu zake au unga wake mm, inahitaji moyo.Sijawahi kula majani yake kama mboga,lakini nasikia nayo ni extremely nutritious.Kwa wale wanaoweza kula unga wake while mixed with warm water,nasikia ni dawa nzuri ya kisukari pia.
      Mamndenyi likes this.

    4. #3
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,591
      Rep Power : 22053
      Likes Received
      992
      Likes Given
      769

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Visenti likes this.
      WB Tanzania lead economist Jacques Morisset said the GDP doubled in 10 years, but it has failed to produce any significant decline in poverty levels.

    5. #4
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,308
      Rep Power : 36527
      Likes Received
      7468
      Likes Given
      4604

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Huwa natumia moringa powder kwa kutibu malaria, inakinga malaria pia kama ukijizoesha kunywa kama chai, jaribu na hakika malaria utaisikia redioni..,.

      Inatibu na sukari, iwe ya kupanda au kushuka..

      pia ikichanganywa na asali ya nyuki wadogo ni dawa nzuri sana kwa kifua/kikohozi na mafua!
      LiverpoolFC likes this.

    6. #5
      Babuu blessed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2010
      Location : machame
      Posts : 1,129
      Rep Power : 739
      Likes Received
      265
      Likes Given
      54

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      du mi upo hapa home majirani wanakuja chuma samtimes mbwa wanakula majani yake ,kuku .kumbe dili ngoja niupalilie
      Mamndenyi likes this.

    7. Study Abroad

    8. #6
      sweke 34's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2012
      Posts : 694
      Rep Power : 507
      Likes Received
      216
      Likes Given
      257

      Default

      Mkuu , mlonge nimeupanda hapa home yaani ndani ya miezi nane limekuwa ni bonge la mti inabidi kukata matawi. Yaani kila kitu kuanzia majani, maua, mbegu n.k kina virubisho vingi. Mimi huwa nayatafuna majani kama mbuzi. Bado najiuliza kwanini huu mmea hautangazwi sana hapa tanzania.
      Mamndenyi likes this.

    9. #7
      flora msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : under a coconut tree
      Posts : 4,120
      Rep Power : 1258
      Likes Received
      499
      Likes Given
      371

      Default

      Quote By sweetlady
      huwa natumia moringa powder kwa kutibu malaria, inakinga malaria pia kama ukijizoesha kunywa kama chai, jaribu na hakika malaria utaisikia redioni..,.

      Inatibu na sukari, iwe ya kupanda au kushuka..

      Pia ikichanganywa na asali ya nyuki wadogo ni dawa nzuri sana kwa kifua/kikohozi na mafua!
      ila asali za town hapo mmm unawza kukupa molasense!

    10. #8
      LiverpoolFC's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2011
      Posts : 6,645
      Rep Power : 11271
      Likes Received
      1465
      Likes Given
      570

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Hii itapatikanaje ktk mikoa tulizopo?

    11. #9
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,308
      Rep Power : 36527
      Likes Received
      7468
      Likes Given
      4604

      Default

      Quote By flora msoffe
      ila asali za town hapo mmm unawza kukupa molasense!
      Yes flora, ukiingia kichwa kichwa lazima uuziwe molasesi, ila kuna watu mie nawajua wanauza original kabisa...

    12. #10
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,308
      Rep Power : 36527
      Likes Received
      7468
      Likes Given
      4604

      Default

      Quote By LiverpoolFC
      Hii itapatikanaje ktk mikoa tulizopo?
      Kama upo arusha nenda pale makumbusho kuna watu wana banda lao wanauza, kama sikosei sh 5000/= kwa pakiti sikumbuki ni gm ngapi!
      LiverpoolFC likes this.

    13. #11
      NasDaz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2009
      Location : Ushenzini
      Posts : 3,034
      Rep Power : 5339
      Likes Received
      1403
      Likes Given
      1625

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Duh! Yaani pamoja na sifa zote hizo lakini bado wala sifahamu huo mti unafananaje!! Kwa wakazi wa dar, je kuna mtu anaweza kunijuza unapatikana sehemu zipi ili angalau nikauone ulivyo?!
      I am a free thinker! It's only my free thinking that leads me, to what am commenting. Thus, I've no doubt that today I can be your fellow but tomorrow your enemy, and the agent between us being my comments!! So, If today we agree with cheers, tomorrow we'd not disagree with jeers!


    14. #12
      Nguto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 598
      Rep Power : 529
      Likes Received
      80
      Likes Given
      3

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Si lazima utafune yale majani. Chuma yatupie kwenye mboga inapoungwa taste haibadiliki. Ila isichemke sana.
      Quote By Tikerra
      Hii ni thread educative, hongera sana.These are the kind of threads one would like to read,sio thread za kijinga jinga tu.Okay,ninayo Milongelonge shambani kwangu.Lakini taste ya mbegu zake au unga wake mm,inahitaji moyo.Sijawahi kula majani yake kama mboga,lakini nasikia nayo ni extremely nutritious.Kwa wale wanaoweza kula unga wake while mixed with warm water,nasikia ni dawa nzuri ya kisukari pia.

    15. ram
      #13
      ram's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Posts : 1,862
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      670
      Likes Given
      347

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Jamani mimi hata sijui huu mti unafananaje, naweza kuuita ni mti wa maajabu
      ''1 Samweli 7:12 - Eben-ezeri - Hata sasa BWANA ametusaidia''

    16. ram
      #14
      ram's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Posts : 1,862
      Rep Power : 1098
      Likes Received
      670
      Likes Given
      347

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Naweza kupata huo mti kwa hawa wauza miti na maua? Naomba picha ya huo mti plz ili na mimi nikapande kwa nyumba yangu

      Quote By Tikerra
      Hii ni thread educative, hongera sana.These are the kind of threads one would like to read,sio thread za kijinga jinga tu.Okay,ninayo Milongelonge shambani kwangu.

      Lakini taste ya mbegu zake au unga wake mm, inahitaji moyo.Sijawahi kula majani yake kama mboga,lakini nasikia nayo ni extremely nutritious.Kwa wale wanaoweza kula unga wake while mixed with warm water,nasikia ni dawa nzuri ya kisukari pia.
      ''1 Samweli 7:12 - Eben-ezeri - Hata sasa BWANA ametusaidia''

    17. #15
      Bulesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2008
      Posts : 3,327
      Rep Power : 1236
      Likes Received
      339
      Likes Given
      72

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Quote By NasDaz
      Duh! Yaani pamoja na sifa zote hizo lakini bado wala sifahamu huo mti unafananaje!! Kwa wakazi wa dar, je kuna mtu anaweza kunijuza unapatikana sehemu zipi ili angalau nikauone ulivyo?!
      Nenda pale makumbusho ndani ya zile nyumba za makabila ya Tanzania kuna watu watakuonesha Mlonge ulivyo!!

    18. #16
      Anita Baby's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2011
      Posts : 436
      Rep Power : 1348
      Likes Received
      70
      Likes Given
      1

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Niwekeeni picha yk niujue nataka ku2mia mlonge

    19. #17
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,553
      Rep Power : 5612
      Likes Received
      6210
      Likes Given
      2281

      Default

      Quote By Nguto
      Si lazima utafune yale majani. Chuma yatupie kwenye mboga inapoungwa taste haibadiliki. Ila isichemke sana.
      sikuwaza kufanya hvyi. Nitaanza sasa.

    20. #18
      Mamndenyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 11,900
      Rep Power : 31777
      Likes Received
      5876
      Likes Given
      19165

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      MLONGE
      Unga wa majani ya Mlonge ambao ni lishe, tiba na kinga hutibu magonjwa kama shinikizo la damu, kupooza viungo au kufa ganzi, homa ya matumbo(typhoid), kuwashwa mwili,vidonda vya tumbo, malaria sugu, enia, upele n.k.
      Mbegu za Mlonge hutibu Malaria, Saratani ya tumbo, hupungusa sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji,huongeza kinga ya mwili CD4s. (Tumia mbegu 3x3 muhimu kila ukitafuna mbegu tatu kumbuka kutumia maji glass 3 au zaidi).
      Maganda(magome) ya Mlonge husaidia kusafisha maji(water treatment).

      Mizizi hutumika kutibu watu walio na malaria sugu au watu wanaopata homa ya usiku au wanaotiririka sana jasho wakati wa homa. Mizizi hutumika kwa kusaga unga wake na kutumia kijiko cha chai mara tatu kwa siku.

      Dozi ya Ukimwi. Dozi ya ukimwi ni kutumia unga wa majani kijiko cha chai mara tatu kutwa kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita. Pia mgonjwa anatakiwa kutafuna mbegu tatu mara tatu kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita.

      Unahamasishwa na kushauriwa angalao nyumbani kwako uwe na mashina kadhaa ya mmea huu kwa matumizi yako.
      SIYO WOTE WANAOTANGATANGA WAMEPOTEA

    21. #19
      Nyati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2009
      Posts : 633
      Rep Power : 646
      Likes Received
      141
      Likes Given
      48

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Quote By NasDaz
      Duh! Yaani pamoja na sifa zote hizo lakini bado wala sifahamu huo mti unafananaje!! Kwa wakazi wa dar, je kuna mtu anaweza kunijuza unapatikana sehemu zipi ili angalau nikauone ulivyo?!
      Kama unakaa Dar Es Salaam, pale Ocean Road karibu na ofisi za MKURABITA upo mti wake ni mkubwa tu, pitia siku moja utauona. Ukikata tawi na kupanda hasa wakati huu wa mvua hapa Dar Es Salaam utaota tu

      Nyati
      tocolyitics and bungeni like this.
      I am not the same person today as I was 10, 20, or 30 years ago, for I have welcomed life's changes on my heart, face, and mind.

    22. #20
      Nyati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2009
      Posts : 633
      Rep Power : 646
      Likes Received
      141
      Likes Given
      48

      Default Re: Jamani Mlonge ni dawa na tiba kubwa sana

      Quote By Mamndenyi
      MLONGE
      Unga wa majani ya Mlonge ambao ni lishe, tiba na kinga hutibu magonjwa kama shinikizo la damu, kupooza viungo au kufa ganzi, homa ya matumbo(typhoid), kuwashwa mwili,vidonda vya tumbo, malaria sugu, enia, upele n.k.
      Mbegu za Mlonge hutibu Malaria, Saratani ya tumbo, hupungusa sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji,huongeza kinga ya mwili CD4s. (Tumia mbegu 3x3 muhimu kila ukitafuna mbegu tatu kumbuka kutumia maji glass 3 au zaidi).

      Maganda(magome) ya Mlonge husaidia kusafisha maji(water treatment).

      Mizizi hutumika kutibu watu walio na malaria sugu au watu wanaopata homa ya usiku au wanaotiririka sana jasho wakati wa homa. Mizizi hutumika kwa kusaga unga wake na kutumia kijiko cha chai mara tatu kwa siku.

      Dozi ya Ukimwi. Dozi ya ukimwi ni kutumia unga wa majani kijiko cha chai mara tatu kutwa kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita. Pia mgonjwa anatakiwa kutafuna mbegu tatu mara tatu kwa muda wa siku arobaini na tano sawa na wiki sita.

      Unahamasishwa na kushauriwa angalao nyumbani kwako uwe na mashina kadhaa ya mmea huu kwa matumizi yako.

      Tuwe makini na hapo kwenye RED. Kwani siamini, na ingekuwa vizuri tusiwadanganye wenzetu
      Mamndenyi and bungeni like this.
      I am not the same person today as I was 10, 20, or 30 years ago, for I have welcomed life's changes on my heart, face, and mind.

    23. Miaka 50
    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...