Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 45
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,115
      Rep Power : 19195
      Likes Received
      8061
      Likes Given
      26515

      Thumbs up Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured


      Kitunguu swaumu ni jamii ya vitunguu ambayo kwa kitaalamu huitwa Allium sativum. Jamii hii ilianza kutumika katika mabara mbalimbali duniani hususani Asia, Afrika na Ulaya takribani miaka 6000 iliyopita. Matumizi makuu nyakati hizo yakiwa viungo katika mboga na tiba.


      Kitunguu swaumu kimetajwa kwenye vitabu mbalimbali vya dini vikielezea faida zake katika kutibu maradhi mbalimbali yasababishwayo na bakteria, matatizo katika mapafu, matatizo katika mfumo wa umen'genyaji chakula, na matatizo ya kuishiwa nguvu.


      Historia inaonesha kuwa, vitunguu swaumu vilianza kutumika China mwaka 510 K.K na pia vilitumiwa na wanajeshi wa Ugiriki na Roma. Aidha wasafiri wa vyombo vya baharini na vijijini pamoja na wakulima barani Afrika walivitumia sana.


      Mwaka 1858, mtafiti na mwanasayansi wa nyakati hizo, Louis Pasteur aligundua uwezo wa kitunguu swaumu katika kuua vimelea mbalimbali vinavyosababisha magonjwa, na hivyo vikaanza kutumika kama dawa ya kusafishia vidonda na kuzuia kidonda ndugu hasa zama za vita ya kwanza na pili ya dunia. Isitoshe, mpaka sasa zipo dawa kadhaa zilizotengenewa kwa kutumia jamii hii ya vitunguu swaumu ikiwemo dawa ya kusafisha mdomo (mouth wash) ingawa watumaiji wake wengi huilalamikia dawa hiyo kwa sababu ya harufu mbaya ya dawa hiyo inayowasababishia kunuka kwa mdomo.


      Faida za vitunguu swaumu


      Katika tafiti mbalimbali vitunguu swaumu vimeonekana kuwa na uwezo wa kutibu maambukizi ya bakteria, fangasi na virusi vya aina mbalimbali. Aidha husaidia kuzuia magonjwa ya moyo ikiwemo kuondoa lijamu katika mishipa ya damu na hivyo kusaidia katika kurekebisha shinikizo la damu. Faida nyingine za vitunguu swaumu ni pamoja na

      • Kutibu saratani ikiwemo saratani ya tumbo na utumbo mkubwa. Tafiti zinaonesha idadi ndogo ya wagonjwa wa saratani katika nchi ambazo wakazi wake wana utamaduni wa kutumia vitunguu swaumu kwa wingi.
      • Vitunguu swaumu husaidia kudhibiti kiwango cha sukari katika damu. Hata hivyo inashauriwa kwamba wagonjwa wa kisukari wanaotumia sindano za insulin wasitumie kitunguu swaumu kwa wingi mpaka watakaposhauriwa na daktari.
      • Huzuia kusanyiko la chembe sahani zinazosaidia kuganda kwa damu (platelet aggregation)
      • Husaidia ufyozwaji wa thiamin, hivyo kusaidia kuepusha mwili na ugonjwa wa beriberi
      • Ina kiasi kikubwa cha vitamini C ambayo husaidia kuzuia ugonjwa wa kiseyeye
      • Hutumika kutibu magonjwa nyemelezi kama toxoplasmosis, hasa kwa watu wenye upungufu wa kinga mwilini.

      Ushahidi wa Kitafiti

      Katika utafiti uliofanyika nchini Czech ilionekana kuwa matumizi ya vitunguu swaumu yalisaidia sana katika kupunguza kusanyiko la lijamu (cholesterol) pamoja na mafuta yasiyofaa mwilini (low density lipoproteins) katika mishipa ya damu. Aidha, mwaka 2007 BBC iliripoti matumizi ya vitunguu swaumu katika kusaidia kumkinga mtumiaji dhidi ya aina fulani ya mafua iliyosababishwa na virusi. Mwaka 2010, ulifanyika utafiti mwingine ambao ulijumuisha wagonjwa 50 wenye shinikizo la damu sugu ambalo lilikuwa ni vigumu kudhibitiwa hata kwa matibabu yaliyozoeleka ya dawa na njia nyingine. Kama njia ya kuchunguza ufanisi wa vitunguu swaumu katika kutibu shinikizo la damu, baadhi ya wagonjwa hao walipewa vitunguu swaumu wakati wengine walipewa dawa isiyohusika na matibabu ya shinikizo la damu (au placebo). Ilionekana kuwa wale waliopewa vitunguu swaumu kama dawa ya shinikizo la damu walionesha maendeleo mazuri kwa vitunguu swaumu kuweza kushusha vizuri kiwango cha shinikizo la damu, hususani systolic pressure, tofauti na wale waliopewa placebo.


      Nini siri ya kitunguu swaumu?


      Sifa kuu zinazokifanya kitunguu swaumu kuwa na uwezo na faida zilizoainishwa hapo juu ni kule kuwa kwake na viasili kadhaa (ingredients) ambavyo vinafanya kazi tofauti tofauti. Uwezo wake wa kiutendaji unatokana na mambo yafuatayo;

      • Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu (vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu.
      • Husaidia uthibiti wa kiwango cha sukari mwilini kwa kushusha kiwango cha kemikali ya homocystine na kupunguza madhara ya kisukari.
      • Iwapo vitapondwa pondwa vizuri, vitunguu swaumu hutoa kemikali iitwayo Allicin ambayo ni dawa dhidi ya bateria, na phytoncide ambayo huua fangasi wa aina mbalimbali.
      • Harufu mbaya ya kitunguuu swaumu hutokana na gesi aina ya hydrogen sulfide ambayo inayotolewa baada ya kuvila.

      Nini Madhara ya vitunguu swaumu?


      Ukiacha faida zake, vitunguu swaumu pia vina hasara na madhara mbalimbali kwa mtumiaji. Madhara hayo ni pamoja na;

      • Harufu mbaya mdomoni ambayo hutokana na kemikali ya AMS (allyl methyl sulfide). Harufu mbaya hii, hata hivyo, yaweza kupunguzwa kwa kunywa maziwa au kunywa maji mengi.
      • Kwa baadhi ya watumiaji, vinaweza kuwaletea mzio au mcharuko mwili (allergies au inflammatory reactions)
      • Kichefuchefu, Kutapika na kuharisha.
      • Huweza kusababisha hatari ya kuvuja damu, kwa sababu huzuia kazi ya seli sahani (platelets) zenye kusaidia kuganda kwa damu kushindwa kufanya kazi yake vizuri, na hususani kwa mama wajawazito, baada ya upasuaji au mara baada ya kujifungua.
      • Huingiliana katika utendaji kazi wake na dawa kadhaa kama vile warfarin, antiplatelets, saquinavir, dawa za shinikizo la damu kwa ujumla hasa calcium channel blockers, na antibiotiki za jamii ya quinolone kama vile ciproflaxacillin.
      • Aidha, vinaelezwa pia kuwa na madhara kwa wanyama jamii ya paka na mbwa.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. Miaka 50

    3. #2
      afrodenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Location : sweet home
      Posts : 15,615
      Rep Power : 26573
      Likes Received
      5845
      Likes Given
      5721

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Santee..
      Ingawa nimesoma faida tu...
      MziziMkavu likes this.

    4. #3
      Daffi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2011
      Location : Arachuga
      Posts : 2,934
      Rep Power : 986
      Likes Received
      516
      Likes Given
      239

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      NIMEIPOKEA,thanks
      MziziMkavu likes this.
      Walk your talk

    5. #4
      ndetichia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Location : Mwime - Buswangili
      Posts : 18,191
      Rep Power : 5099
      Likes Received
      2772
      Likes Given
      231

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      nipoa mkuu je inakuwaje ukiweka kama kwenye upele ili uive ina maaana hakuna madhara mengine baada ya uvimbe kuwa umeisha pasuliwa..
      MziziMkavu likes this.

    6. #5
      zaratustra's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 632
      Rep Power : 629
      Likes Received
      85
      Likes Given
      116

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Nashukuru kwa habari hii ya vitungu swaumu. Mimi ni mmoja wa watumiaji wazuri wa "dawa" hii tangu muda mrefu baada ya kuambiwa na rafiki yangu mmoja mzungu kuwa inasaidia sana kutibu mafua (niko allergic na moshi (hasa wa sigara), vumbi, perfume zenye harufu kali, hata maji ya baridi ya kuoga). Sijui kwa maelezo ya mleta thread, inatumiwaje kama tiba? Mimi nilishauriwa kuwa nameza nzima nzima kisehemu kimoja cha kile kitunguu, at least kila asubuhi kabla ya kutia chochote tumboni! Je kuna namna nyingine, eg. kutafuna, kumung'unya, n.k.?
      MziziMkavu likes this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Jeji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2011
      Location : hapa hapa
      Posts : 1,479
      Rep Power : 694
      Likes Received
      217
      Likes Given
      288

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Asante kwa kutuelimisha, nilikuwa sijui.
      MziziMkavu likes this.
      Yeremia 33:3

    9. #7
      TANMO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Tanzagiza
      Posts : 5,045
      Rep Power : 7769
      Likes Received
      1806
      Likes Given
      3439

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Quote By zaratustra
      Nashukuru kwa habari hii ya vitungu swaumu. Mimi ni mmoja wa watumiaji wazuri wa "dawa" hii tangu muda mrefu baada ya kuambiwa na rafiki yangu mmoja mzungu kuwa inasaidia sana kutibu mafua (niko allergic na moshi (hasa wa sigara), vumbi, perfume zenye harufu kali, hata maji ya baridi ya kuoga). Sijui kwa maelezo ya mleta thread, inatumiwaje kama tiba? Mimi nilishauriwa kuwa nameza nzima nzima kisehemu kimoja cha kile kitunguu, at least kila asubuhi kabla ya kutia chochote tumboni! Je kuna namna nyingine, eg. kutafuna, kumung'unya, n.k.?
      Mkuu hii ya kumeza chembe nzima bila kuitafuna matokeo yake huwa ni kutoka kikiwa kizima vile vile kwa kupitia njia ya haja kubwa. Ninakushauri ujaribu kukitafuna kabla hujakimeza, hii itasaidia kurahisisha mmeng'enyo wake tumboni.
      MziziMkavu likes this.
      Do Something......

    10. #8
      Mamndenyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 11,944
      Rep Power : 31786
      Likes Received
      5899
      Likes Given
      19252

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Asante sana.
      MziziMkavu likes this.

    11. #9
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,404
      Rep Power : 1031
      Likes Received
      1166
      Likes Given
      598

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Thank you for the useful information!
      MziziMkavu likes this.

    12. #10
      Kivumah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2008
      Posts : 2,035
      Rep Power : 5284
      Likes Received
      659
      Likes Given
      677

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Asante Mzizi
      MziziMkavu likes this.

    13. #11
      drphone's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2009
      Posts : 3,514
      Rep Power : 1192
      Likes Received
      99
      Likes Given
      10

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      nanikinga kubwa ya kipindupindu niliwamsikia dr ndodi
      MziziMkavu likes this.
      THE BEST IS YET TO COME.

      THE GREATEST EXPERIENCE IS TO MEET YOURSELF AND FALL IN LOVE WITH YOURSELF.

    14. #12
      Mgariga's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st April 2011
      Posts : 136
      Rep Power : 439
      Likes Received
      14
      Likes Given
      41

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      very useful information, great indeed.
      MziziMkavu likes this.

    15. #13
      upele's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2010
      Posts : 364
      Rep Power : 532
      Likes Received
      30
      Likes Given
      1

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      be blessed mwana yeeah yap i like jf
      MziziMkavu likes this.

    16. #14
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,115
      Rep Power : 19195
      Likes Received
      8061
      Likes Given
      26515

      Thumbs up Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      KITUNGUU saumu kimekuwa kikitumika kutibu na kuboresha afya ya mwili na hivyo kumfanya mtumiaji awe mrembo na mwenye afya bora.
      Matumizi ya kitunguu saumu kibichi yamekuwa yakisaidia vitu vingi sana mwilini.

      Baadhi ya hayo ni pamoja na kupambana na virusi, bakteria, fangasi na pia sumu mbalimbali hasa zile zinazosababishwa na baadhi ya vyakula mwilini.

      Kutokana na hilo, matumizi ya kitunguu saumu kama tiba na kipodozi, ni jambo linalopendekezwa na wataalamu wa urembo wa asili.
      Katika matumizi yake kitunguu saumu hutumika kwa kula na wakati mwingine kupaka, ambapo hili hutegemea zaidi na mahitaji au matatizo ya mtumiaji husika.

      Pamoja na njia hizo nilizotaja hapo juu, lakini wataalamu wanashauri ulaji wa kitunguu saumu kibichi kila siku, kwani husaidia kuboresha afya ya muhusika.

      Ikiwa utashindwa kukitafuna chenyewe, unaweza kuchanganya kwenye chakula kingine ambacho unatumia alimradi tu ukipate kikiwa halisi.
      Kwenye urembo, kitunguu saumu husaidia kuondoa matatizo yafuatayo;
      Chunusi

      Changanya kitunguu saumu kilichosagwa kijiko kimoja na kijiko kimoja cha juisi ya ndimu. Chukua pamba na paka sehemu zote zilizoathirika. Kaa na mchangyiko huo kwa muda wa dakika 15 hadi nusu saa.Ikiwa utaendelea kwa muda wa wiki moja. Tatizo la chunusi litakuwa limeondoka kabisa.

      Kunyonyoka kwa nywele

      Ni kwa muda mrefu sasa kitunguu saumu kimekuwa kikitumika kama tiba ya kunyonyoka kwa nywele. Unachotakiwa kufanya ni kutumia mafuta yake kwa kupakaa kwenye ngozi ya kichwa kila siku kabla ya kulala.
      Fanya hivyo mara kwa mara kwa muda usiopungua miezi mitatu na utaona matokeo yake. Ikiwa utakosa mafuta yake, si vibaya ikiwa utatumia kitunguu chenyewe kilichosagwa kwa kupaka kwenye ngozi ya kichwa kila siku usiku na kuosha asubuhi yake.

      Fangasi vidoleni

      Kupambana na fangasi kwenye vidole vya miguu na mikono, unashauriwa kutumia kitunguu saumu kilichosagwa kwa kupaka eneo lililoathirika. Hakikisha unakaa nacho usiku kucha ukiwa umevaa soksi ama glavu. Fanya hivyo kila siku hadi utakapoona muwasho na maumivu yameisha.

      Mba

      Paka kitunguu saumu kilichosagwa katika ngozi ya kichwa ama sehemu yeyote iliyoathirika. Hakikisha unatumia hadi pale ugonjwa utakapokuwa umetoweka kabisa.
      Kimox Kimokole and Poriposha like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    17. #15
      majogajo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th October 2011
      Posts : 321
      Rep Power : 449
      Likes Received
      30
      Likes Given
      0

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      kwa nguvu za kiume je?
      MziziMkavu likes this.

    18. #16
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,115
      Rep Power : 19195
      Likes Received
      8061
      Likes Given
      26515

      Thumbs up Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Quote By majogajo
      kwa nguvu za kiume je?
      Mbona nimeandika Dawa nyingi tu za nguvu ya Kiume? Unataka Dawa ya nguvu ya Kiume wewe? haya chukuwa hii hapa Chukua Mdalasini pamoja na asali uchanganye kwa pamoja atie na maji ya Uvuguvugu , halafu kila chakula chako kisikose kipande cha tango..

      Sababu 9 muhimu zinazo sababisha upungufu wa nguvu za kiume
      Zipo sababu nyingi zinazosababisha wanaume kupungua nguvu za kiume katika hizo ni hizi zifuatazo:
      1.ubugiaji wa tumbaku .
      2.uvutaji wa sigara.
      3.utafunaji wa mirungi.
      4.unywaji wa pombe.
      5.kupooza kwa mwili kunakosababishwa na maradhi.
      6.ugonjwa wa kisukari.
      7.kujisaidia kwa njia ya mkono. (Punyeto)
      8.kuwa na mawazo kupita kiasi.
      9.kufanya kazi ngumu.

      TIBA YAKE:
      chukua mbegu za tikiti maji zikaange halafu zitwange ili zitoe unga, chukua juici ya kitunguu thaumu lita moja na asali lita moja changanya pamoja juisi ya kitunguu thaumu na asali weka na vijiko kumi vikubwa vya unga wa tikiti maji koroga vizuri na uwe unakunya dawa hii kikombe kimoja cha kahawa mara tatu kila siku kwa muda wa wiki moja.

      Chanzo: Mzizimkavu




      Namna kujitibu maradhi ya kuwahi kushusha manii haraka wakati la tendo la ndoa na bila kujitibu wanaathirika wote khususan mwanamke.
      Madawa yake ni:

      1.Tangawizi.
      2.Uwatu.
      3.Asali.
      4.Mdalasini.

      Chukua unga wa tangawizi kiasi cha vijiko vitatu vya chakula kisha changanya na dawa iitwayo uwatu unga wake kiasi cha vijiko vitatu vya chakula, na hakikisha madawa haya ni ya unga yaani yatwange hadi yawe unga kisha chemsha kwa maji glasi tatu baada ya kuchemsha hakikisha

      glasi moja inapotea kwa kuchemsha, halafu mgonjwa wa tatizo hilo atakuwa akijipaka kwenye dhakari yake na kwenye korodani kila siku mara moja na wakati anatumia dawa hiyo itamlazimika atumie asali kijiko kimoja c
      Poriposha likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    19. #17
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,115
      Rep Power : 19195
      Likes Received
      8061
      Likes Given
      26515

      Thumbs up Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Garlic: Bad for Your Breath, Good for Your Brain






      Garlic is known to be a breath destroyer, but is it possible that what’s known as the stinking rose could help stave off dementia? In the quest to find a potential cure and treatment for Alzheimer’s disease, a by-product of garlic called aged garlic extract was recently studied on mice and it showed some serious promise. Alzheimer’s disease, the most common form of dementia and now the 7th leading cause of death in the United States, results from the deposit of proteins called amyloid-beta protein peptides that can cause inflammation and form plaque in the brain.


      The available drugs today only treat the symptoms, so serious efforts are underway to search for a cure, or at least to stop the disease progression. Currently, treatment costs associated with Alzheimer’s disease are climbing and therefore, cheaper, natural food substancesfor treatment drugs are being investigated worldwide. One of such substances being tested is garlic. When reviewing preliminary results of various animal and laboratory studies

      involving aged garlic extract and one of its key compounds, S-allyl-L-cysteine, garlic extract treatment showed protective effects against inflammatory process and chemical changes in the brain that occur in Alzheimer’s disease patients. In the study on mice, the four-month-long treatment with aged garlic extract decreased the number of plaques in their brains.


      Where does this extract come from? Garlic has sulfur-containing compounds that can be unfavorable and undesirable. When garlic is soaked in ethanol-water mixture for 20 months, unfavorable compounds are destroyed and useful ones become soluble resulting in aged garlic extract, which it contains S-allyl-L-cysteine or SAC.


      Thus far, studies conducted in the area of Alzheimer’s disease and potential benefits of treatments with natural food substances are still conflicting. While more research is in dire need, researchers are hopeful that remedies including garlic and curcumin (turmeric) are potentially beneficial in the treatment of

      Alzheimer’s disease. Like garlic, curcumin also has shown to help alleviate all types of inflammation, helping to fight various intestinal diseases or even slow down cancer growth.

      So while further human studies need to be done to verify and expand on these results, it wouldn’t hurt you to add some fresh garlic to your spaghetti tonight or pop an aged garlic extract supplement pill. Just remember to buy some breath mints, too.


      Active Ingredient in Aged Garlic Extract Studied on Mice for Effect on Alzheimer’s Disease


      Summary
      Alzheimer’s disease is the most common form of dementia in older people and the 7th leading cause of death in the United States. Years before symptoms of Alzheimer’s disease appear, peptides called amyloid-beta start depositing in the brain. This results in destabilization of microtubules that are responsible for transportation of cellular material, as well as swelling in the brain. The swelling causes damage to neurons and neuronal networks, resulting in dementia in older people. The available treatments do not completely cure Alzheimer’s disease, and new drug targets are being investigated. Garlic extract and S-allyl-L-cysteine (SAC), a component present in the extract, were tested for their effect on neuronal degeneration related to Alzheimer’s disease on mice.


      Introduction
      The proportion of elderly population with Alzheimer’s disease is increasing worldwide. Three main features of this disease are: deposition of amyloid-beta peptides causing brain inflammation that damages neurons; chemical changes in tau protein affecting cellular transport via microtubules; and loss of neurons releasing acetylcholine that controls the functions of heart and muscles. The available drugs that target single steps in the progression of the

      disease can provide some symptomatic relief, but these drugs cannot control or cure the disease. “We hypothesize that an agent effective in modulating multiple pathological pathways could be an appropriate therapeutic agent in preventing and restricting Alzheimer’s disease progression.” Natural substances such as garlic and turmeric are tested because of their low costs, easy availability and fewer possible side effects. Garlic affects different aspects of the progression of the disease, showing the potential to be a possible cure for Alzheimer’s disease.


      Methods

      * Garlic has sulfur-containing compounds that can be unfavorable. When garlic is soaked in ethanol-water mixture for 20 months, unfavorable compounds are destroyed and useful ones become solubilized. The result is aged garlic extract (AGE) and it contains S-allyl-L-cysteine or SAC.
      * In vitro and in vivo studies were performed on mouse and rat models of Alzheimer’s disease using these extracts.
      * The changed chemical status (phosphorylation) of tau protein was tested in mice with Alzheimer’s disease treated with or without AGE and SAC.
      * The chemicals that increase upon inflammation were recorded.


      Results

      * In vitro studies with SAC showed that it can dissolve amyloid-beta plaques. In vivo, four-month-long treatment with AGE and SAC decreased the number of plaques in the brains of mice.
      * Mice with Alzheimer’s disease showed tangled neuronal microtubules due to chemical changes in tau protein. The treatment with AGE and SAC showed decreased levels of the changed tau protein.
      * Garlic extract treatment showed increase in the levels of glutathione, an enzyme that protects neurons from inflammatory agents.
      * The changes in various other factors seen in the disease improved with AGE or SAC treatment.


      Shortcomings/Next steps

      Authors recommend more research and have confirmed that the “current FDA-approved drugs for the treatment of Alzheimer’s disease fail to completely cure the disease.” Most of the new drugs that have been tried in clinical trials have failed to demonstrate definite curative effects in these trials. The authors also propose a combined formulation of curcumin with AGE or SAC, which can produce synergistic properties to alleviate the pathology of Alzheimer’s disease, and its associated symptoms, and these types of combinations would also require further research in preclinical and clinical settings.


      Conclusions

      The numbers and cost of treatment of patients with Alzheimer’s disease is increasing, emphasizing the need for a cheaper and more successful new treatment. The authors suggest that the failure to find a cure is because of the multi-faceted nature of this disease. A drug will have to address all these

      aspects of the pathology to prove to be successful as a treatment for Alzheimer’s disease. The ingredients present in AGE seem to reduce the chemical changes in proteins affecting transport in brain cells, and also affect many aspects of interconnected chemical pathways to reduce swelling in the brain. While more research is needed, remedies such as garlic and curcumin (turmeric) are potentially beneficial in restricting the symptoms of Alzheimer’s disease.
      Poriposha likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    20. #18
      kashengo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2011
      Location : ROCK CITY
      Posts : 1,123
      Rep Power : 637
      Likes Received
      296
      Likes Given
      110

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Thank yuo MZIZI MKAVU
      MziziMkavu likes this.

    21. #19
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,115
      Rep Power : 19195
      Likes Received
      8061
      Likes Given
      26515

      Thumbs up Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      kasopa likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    22. #20
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,115
      Rep Power : 19195
      Likes Received
      8061
      Likes Given
      26515

      Default Re: Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic) Featured

      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    Page 1 of 3 123 LastLast

    Similar Topics

    1. Zijue faida za TENDE kiafya
      By Bajabiri in forum JF Doctor
      Replies: 20
      Last Post: 29th August 2011, 07:46
    2. Zijue faida za papai kiafya
      By MziziMkavu in forum JF Doctor
      Replies: 4
      Last Post: 8th July 2011, 08:10
    3. Kitunguu Swaumu!
      By Masanilo in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 54
      Last Post: 8th February 2011, 13:45
    4. Kitunguu swaumu kinazuia influenza!
      By MziziMkavu in forum JF Doctor
      Replies: 4
      Last Post: 31st January 2010, 22:33
    5. Kitunguu swaumu kinaongeza kuvu za kiume?
      By Serendipity in forum JF Doctor
      Replies: 25
      Last Post: 11th December 2009, 11:02

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...