Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mtoto kukojoa kitandani

    Report Post
    Page 10 of 11 FirstFirst ... 891011 LastLast
    Results 181 to 200 of 201
    1. #1
      FRANKMIBONO's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 1st March 2011
      Posts : 6
      Rep Power : 418
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Mtoto kukojoa kitandani

      Wadau naomba ushauri na tiba kama ipo kwa binti yangu mwenye umri wa miaka 10 sasa.

      Amekuwa akisumbuliwa na tatizo la kukojoa kitandni tangu alipokuwa mdogo, mbaya zaidi ni kwamba sasa hivi tumempeleka Boarding school-shule ya msingi.

      Tatizo hili linaonekana kumuathiri kiakili na nina waswasi na maendeleo yake kwa sababu nilipomtembelea kwa mara ya mwisho anaona aibu kutoa godoro kulianika.

      Nimeongea na Matron wake anasema hilo tatizo wanalo wengi ila yeye 'frequence' yake ni kubwa kulinganisha na wengine.

      Je, tatizo hililinatibika wadau?

    2. Miaka 50

    3. #181
      NZURI PESA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th March 2011
      Posts : 604
      Rep Power : 533
      Likes Received
      50
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By MziziMkavu
      Whilst bedwetting is a very common problem, people are reluctant to discuss what is perceived to be an embarrassing subject.

      A number of children will outgrow bedwetting but for others this condition might persist into adulthood. Unfortunately this condition may interfere with social activities, relationships and performance at school. In addition their self-esteem may also suffer. Bedwetting may be caused by several factors and it is encouraging to know that this condition can be managed in several ways. Don’t give up and don’t delay – take the bedwetting challenge today to enable you to start a conversation with your doctor.

      Request your free DVD“Understanding Bedwetting” and listen to other people share their experiences on bedwetting.









      Mtoto mzuri wa kizungu ana miaka 19 anakojowa kitandani pole sana .
      Bed Wetting, bedwetting
      Dawa ya kukojoa kitandani ni KWATO YA NG'OMBE
      IKOSHE VIZURI KISHA ICHEMSHE,KISHA UMPE SUPU YAKE MHUSIKA MILS 100 MARA 3 KUTWA BAADA YA SIKU 2-3 ATAKUWA KAPONA. NINA USHAHIDI NILIELEKEZWA NA NIKAMPATIA BINTI YANGU WA KAZI MIAKA 5 ILIYOPITA HADI SASA NI MZIMA
      MziziMkavu likes this.

    4. #182
      J mubago's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 25th May 2012
      Location : tanga tz
      Posts : 1
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Post kukojoa kitandani

      nisaidieni dawa ya kukojoa kwani mwanangu wa miaka 13 bado anakojoa hadi leo ameshindwa kwenda boading school

    5. #183
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,178
      Rep Power : 19208
      Likes Received
      8121
      Likes Given
      26593

      Default Re: kukojoa kitandani

      Dawa ya Mtoto kukojowa Kitandani Fanya hivi [email]Mkuu@J mubago

      Pata Kwato la N'gombe tiya ndani yake kaa la Moto kisha huyo Mtoto wako alinuse hilo kwato lililo na Moto kisha Avue nguo awe uchi apande juu ya Mti kisha huko juu ya Mti akojee Mkojo na akisha maliza kukojowa ashuke avae nguo zake Afanye hiyo Dawa kwa muda wa siku 7 atapona inshallah kwa uwezo wake Mwenyeezi Mungu . Fanya hivyo Mkuu J mubagokisha utanijibu baada ya Siku 7 Hakuna Dawa ya Kutibu mtoto anaye kojowa Kitandani Mahospitalini. Usikose kunipa FeedBack.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    6. #184
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,178
      Rep Power : 19208
      Likes Received
      8121
      Likes Given
      26593

      Default UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Nini maana ya Enuresisi?


      Enuresisi ni neno la kitaalamu linalomaanisha hali ya kutoa mkojo bila ridhaa ya muhusika(involuntary),aina mojawapo tuliyoizoea ni ukojozi kitandani wakati mtu akiwa amelala hasa wakati wa usiku.


      Ukojozi kitandani huwapata zaidi watoto na mara nyingi ni hali ya kawaida tu katika ukuaji wao. Ukojozi kitandani hutokea zaidi kwa watoto wa kiume kuliko wa kike.


      Vitu gani husababisha ukojozi kitandani?


      Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha ukojozi kitandani. Baadhi ya njia hizo ni hizi zifuatazo:


      Kurithi (Katika familia)
      Kushindwa kuamka kutoka usingizini
      Msongo wa mawazo
      Ukuaji wa taratibu wa mishipa za fahamu kutofanya kazi inavyotakiwa ( hali ambayo humpunguzia mtoto uwezo wa kuzuia kibofu kutoa mkojo)
      Matatizo ya homoni (kuzalishwa katika kiwango kidogo kwa homoni zinazopunguza kuzalishwa kwa mkojo wakati wa usiku)
      Maambukizi katika njia ya mkojo
      Matatizo katika mrija wa mkojo kwa wavulana au kwenye njia ya mkojo kwa wavulana na wasichana.
      Matatizo kwenye uti wa mgongo
      Kibofu cha mkojo kuwa kidogo
      Ukojozi kitandani sio tatizo la akili au tabia. Tatizo hili halitokei eti kwa sababu mtoto ni mvivu kiasi kwamba hawezi kuamka kitandani na kwenda msalani.




      Je ni kipindi gani watoto wengi huweza kudhibiti hali ya mahitaji ya kukojoa?





      Watoto huweza kudhibiti kibofu cha mkojo katika umri tofauti. Wakifikia umri wa miaka 6, watoto wengi huacha kukojoa kitandani. Ukojozi wa kitandani hadi katika umri wa miaka 6 siyo kitendo cha ajabu, ingawa inaweza kuwanyima amani wazazi na walezi wengi.Kama mtoto yuko chini ya umri wa miaka 6, tiba kwa tatizo la ukojozi kitandani kwa kawaida siyo mara nyingi watoto wengi huacha kukojoa bila aina yoyote ya matibabu.


      Daktari anaweza kusaidia lolote?




      Ingawa watoto wengi wanaokojoa kitandani hawana tatizo lolote la kiafya, daktari anaweza kusaidia kugundua kama tatizo la mtoto wako kukojoa kitandani linasababishwa na matatizo mbalimbali ya kiafya. Kwanza daktari atakuuliza iwapo mwanao hukojoa mchana na usiku. Halafu daktari atampima na anaweza kuchukua vipimo vya mkojo kuangalia kama kuna maambukizi au kisukari au matatizo mengine.


      Daktari anaweza kutaka kujua mwenendo wa kimaisha wa mwanao anapokuwa nyumbani na hata shuleni.Ingawa unaweza kuogopa mtoto wako anapokojoa kitandani, tafiti zimeonyesha kuwa sio rahisi kwa watoto wanaokojoa kitandani kuwa na matatizo ya hisia tofauti na watoto wengine wasio kojoa kitandani.Daktari pia atakuuliza jinsi mnavyoishi katika familia kwa sababu m matibabu yanaweza kuhusisha mabadiliko kadhaa ya kimaisha hapo nyumbani.





      Je kuna matibabu yoyote kwa tatizo la ukojozi kitandani?


      Watoto wengi huacha kukojoa kitandani bila kupata matibabu yoyote.Ingawa wakati mwingine wewe na daktari wako anayemuona mtoto wako mnaweza kuamua kwamba mtoto anahitaji tiba fulani.Kuna aina 2 za tiba: kumbadili mtoto kitabia, na kumpatia dawa. Kumbadili mwanao kitabia husaidia kumfanya mwanao aache tabia ya kukojoa kitandani.Baadhi ya njia za kumbadili mwanao kitabia ni hizi zifuatazo:


      Mzuie mwanao asinywe vinywaji/maji kwa wingi kabla ya kulala
      Hakikisha mwanao anenda msalani kila mara kabla ya muda wa kulala na pia mara tu anapo anza kusinzia.
      Tumia kengele itakayolia pindi kitanda kinapolowa ,hii humfundisha mtoto kufahamu pindi kibofu kinapojaa wakati wa usiku
      Mpe zawadi mtoto anapoamka bila kukojoa kitandani
      Mwambie mtoto wako kubadili matandiko mwenyewe kila anapokojoa kitandani
      Mpe mwanao mazoezi ya kibofu: muelekeze mwanao akae muda mrefu bila kukojoa kipidi cha mchana, ili kibofu kiwe na uwezo wa kutunza mkojo mwingi zaidi


      Ni dawa gani zinazotumika kutibu ukojozi kitandani?


      Daktari wako anaweza kumpa mwanao dawa kama ana umri wa miaka zaidi ya saba(7) iwapo njia za kumbadilisha kitabia zilizotajwa hapo hazijasaidia. Hata hivyo dawa hazitibu ukojozi kitandani, Aina mojawapo ya dawa husaidia kibofu kutunza mkojo zaidi, na dawa nyingine husaidia figo kutengeneza kiwango kidogo cha mkojo. Dawa hizi zinaweza kuwa na madhara kiafya kwa mfano, mdomo kukauka na mashavu kuwa na rangi nyekundu.







      UJUMBE WA KUPELEKA NYUMBANI:


      Ukojozi kitandani unaweza kusababisha matatizo ya kitabia kwa sababu mtoto anaweza kuhisi ana makosa na kujisikia aibu. Ni kweli kwamba mwanao anatakiwa kuwajibika kwa kitendo hicho cha kukojoa kitandani (hii ina maana mwanao anatakiwa kufanya usafi). Lakini usimfanye mwanao ahisi kwamba yeye ndio mwenye makosa.Ni muhimu kwa mwanao kujua kwamba ukojozi kitandani siyo kosa lake. Kitendo cha kumuadhibu mwanao kwa kosa la kukojoa kitandani haitasaidia kutatua tatizo.


      Itamsaidia mwanao kujua kwamba hakuna anayejua sababu kubwa inayopelekea ukojozi kitandani.Muelimishe kwamba mambo hayo hutokea katika familia (Kwa mfano, kama mwanao akikojoa kitandani, unatakiwa kujadiliana naye na kumhaidi kumsaidia kupambana na hali hiyo).


      Msisitizie mwanao kwamba anatakiwa aende msalani wakati wa usiku. Muwekee taa kuelekea msalani ili imuwie rahisi kuona njia ya kuelekea msalani. Unaweza pia kumfunika na blanketi pamoja na tandiko lingine la plastiki ili iwe rahisi zaidi wakati wa kufanya usafi.Endapo mwanao atajaribu kukusaidia, msifie kwa kujaribu na kwa kusaidia kufanya usafi.


      Imeandaliwa na Dkt. RAYMOND BANDIO (MD)
      UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis
      FP likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    7. #185
      Nivea's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,680
      Rep Power : 0
      Likes Received
      3141
      Likes Given
      4053

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Asante na mungu akubariki maana hiyo imekuwa issu kubwa kwenye familia yangu
      MziziMkavu likes this.

    8. FemaTV & Radio

    9. #186
      Remmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2009
      Location : home
      Posts : 4,342
      Rep Power : 7768
      Likes Received
      1545
      Likes Given
      1793

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Asante kwa tiba hii. tutajitahidi kwa watoto zetu.
      MziziMkavu likes this.

    10. #187
      Mzawa Halisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2009
      Posts : 470
      Rep Power : 615
      Likes Received
      139
      Likes Given
      333

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Mkuu asante sana. Imebidi nimuamshe mwenzangu tusome wote post yako. Asante tena.
      Chuma Chakavu likes this.

    11. FP
      #188
      FP's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 30th September 2009
      Posts : 7,240
      Rep Power : 46347
      Likes Received
      6944
      Likes Given
      6847

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      ubarikiwe sana mkuu, zoezi litaanza mara moja
      MziziMkavu likes this.
      Don't wait for the Perfect Moment,
      Take the Moment and make it Perfect


    12. #189
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,178
      Rep Power : 19208
      Likes Received
      8121
      Likes Given
      26593

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Quote By Fixed Point
      ubarikiwe sana mkuu, zoezi litaanza mara moja
      @Fixed Point na wewe pia Bibie mpendwa hujambo lakini?
      FP likes this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    13. #190
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,682
      Rep Power : 27091
      Likes Received
      10056
      Likes Given
      13955

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Lakini kuna swala la kuweza kurekebisha hali kwa kuongezea tu.

      kwa watoto wenye miaka 6> basi waeuke kula vitu aina ya vimiminika baada ya saa kumi na mbili jion. hali hii itamfanya mtoto awe ameshakojoa japo mara 3 kabla ya muda wake wa kulala saa mbili usiku. hii inapunguza kiwango cha mkojo utakao tengenezwa usiku na pia kama mzazi akifanikiwa kumwamsha saa 7 usiku ili akoje basi over time tabia hii itastop.
      MziziMkavu likes this.

    14. FP
      #191
      FP's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 30th September 2009
      Posts : 7,240
      Rep Power : 46347
      Likes Received
      6944
      Likes Given
      6847

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Quote By MziziMkavu
      @Fixed Point na wewe pia Bibie mpendwa hujambo lakini?
      Hofu kwako MziziMkavu
      MziziMkavu likes this.
      Don't wait for the Perfect Moment,
      Take the Moment and make it Perfect


    15. #192
      Doreen22's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd June 2012
      Posts : 478
      Rep Power : 604
      Likes Received
      69
      Likes Given
      7

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Ahsante sana Doctor kwa kutuelewesha vitu kama hivi, ujue kumlaumulaumu sana mtoto na kumsemasema in a negative way kila mara kunampunguzia confidence, anakuwa hajiamini vya kutosha mbele za watu, moto afundishwe na aelimishwe, apewe maneno positive na kuwa uencouraged katika kufanya mambo mazuri katika maisha yake ili ajiamini, sio kumuita mpumbavu, mshenzi, toka utotoni mpaka kuwa mtu mzima, lazima akose confidence na wengine wanakuwa watukutu
      MziziMkavu likes this.

    16. #193
      Doreen22's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd June 2012
      Posts : 478
      Rep Power : 604
      Likes Received
      69
      Likes Given
      7

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Tuondoe nidamu ya uoga kwa watoto wetu, tuwafanye wawe na nidhamu ya kweli na wawe karibu na sisi, tuwe na urafiki nao wa karibu ili waweze kutueleza matatizo yao, wajiamini, wasimhofie mtu, wakitueleza matatizo yao na mambo yanayowatatiza tuwasaidie kwa ukaribu mkubwa, tusiwapuuze, ili matatizo yanayowakabili yasiwaharibie maisha yao, yaweza kuwa uonevu shuleni, yaweza kuwa kudhalilishwa kijinsia na Mwalimu wake au mlinzi wa hapo nyumbani.

      Wazazi wote wawe karibu na watoto, hata kama Baba anamnyemelea mwanae wa kike, amwambia Mama yake, na Mama asipuuze na kuona ni uongo, alifuatilie na amsaidie mwanae ili asimfanye ajione ambaye hana mtetezi mwingine apart ya Mungu, wakati yeye pia au polisi wapo kwa ajili yake pia

    17. #194
      Bichau's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th April 2012
      Posts : 63
      Rep Power : 371
      Likes Received
      21
      Likes Given
      57

      Default Re: UKOJOZI KITANDANI KWA WATOTO (Bed-Wetting) -Enuresis

      Quote By gfsonwin
      Lakini kuna swala la kuweza kurekebisha hali kwa kuongezea tu.

      kwa watoto wenye miaka 6> basi waeuke kula vitu aina ya vimiminika baada ya saa kumi na mbili jion. hali hii itamfanya mtoto awe ameshakojoa japo mara 3 kabla ya muda wake wa kulala saa mbili usiku. hii inapunguza kiwango cha mkojo utakao tengenezwa usiku na pia kama mzazi akifanikiwa kumwamsha saa 7 usiku ili akoje basi over time tabia hii itastop.
      Ni kweli ulichoelezea kuhusu kuamsha watoto usiku inasaidia sana, binafsi huwa namfanyia hivyo mwanangu wa miaka 3, muda wowote nikishtuka usiku namtoa au ile alfajiri kwa kuwa naamka saa kumi na nusu huwa namtoa maana mara nyingine kumekucha lakini kwa kuwa yu usingizini basi hukojoa nisipomuwahi.
      gfsonwin likes this.

    18. #195
      Kifimbo Cheza's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th November 2011
      Location : jupiter's north pole
      Posts : 94
      Rep Power : 398
      Likes Received
      10
      Likes Given
      25

      Default Tiba ya kukojoa kitandani.

      Nina binti yangu kwa sasa ana umri wa miaka 14 na anatatizo la kukojoa kitandani wakati akiwa amelala.

      Tafadhali ninaomba mnisaidie dawa ya kuzuia tatizo hilo jamani.

    19. REX
      #196
      REX's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th March 2012
      Location : KCMC-MOSHI
      Posts : 182
      Rep Power : 397
      Likes Received
      24
      Likes Given
      2

      Default Re: Tiba ya kukojoa kitandani.

      Ok! Call 0715720276.

    20. #197
      Invisible's Avatar
      Robot Array
      Join Date : 11th February 2006
      Location : Here...!
      Posts : 9,326
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      4884
      Likes Given
      5670

      Default Re: Mtoto kukojoa kitandani

      Quote By MziziMkavu
      Dawa ya Kumtibu Mtoto kukojowa Kitandani Vifaa vyake upate hivi:

      Upate Kwato La N'gombe tiya ndani yake Kaa La Moto kisha yule mgonjwa wa kukojowa Kitandani alinuse lile kwato la N'gombe lilio na Kaa la Moto ndani yake, kisha Avue nguo zake awe uchi Apande juu ya mti kisha juu ya huo mti akojoe mkojo ushuke chini afanye hiyo Dawa kwa Muda wa siku 7 atapona kabisa.

      Hakuna dawa Mahospitalini kutibu mtoto kukojowa kitandani
      Hahaha,

      Dah!
      MziziMkavu likes this.
      Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako!
      24/7 Email SUPPORT: [email protected]


    21. #198
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,626
      Rep Power : 1447
      Likes Received
      844
      Likes Given
      347

      Default Re: Mtoto kukojoa kitandani

      Quote By Invisible
      Hahaha,

      Dah!
      Invisible nakusubiri leo na kwato lako la ng'ombe......hahahahhahahahahh hhhhhh huyo ndio mzizimkavu aka babu wa loliondo...hahahhahahahahaaaaa aaaaaaaaaaaaaa mama mbavu zangu zinachomoka....
      MziziMkavu likes this.

    22. #199
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,178
      Rep Power : 19208
      Likes Received
      8121
      Likes Given
      26593

      Default Re: Mtoto kukojoa kitandani

      Quote By Invisible
      Hahaha,

      Dah!
      Mkuu kama una mtoto wako au mtoto wa jamaa yako anakojoa kitandani jaribu dawa yangu itamsaidia inshallah.@Invisible

      Quote By Jestina
      Invisible nakusubiri leo na kwato lako la ng'ombe......hahahahhahahahahh hhhhhh huyo ndio mzizimkavu aka babu wa loliondo...hahahhahahahahaaaaa aaaaaaaaaaaaaa mama mbavu zangu zinachomoka....
      MziziMkavu Ph.D. Babu wa Jamii Forums hahahahahahah karibuni sana Kwato la Ng'ombe linatibu maradhi mengi tu sio Maradhi ya kikojozi. Kwato la Ng'ombe nikianza kusema faida yake ninafikiri naweza kujaza hii Server ya Jamii forums Jestina
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    23. #200
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,178
      Rep Power : 19208
      Likes Received
      8121
      Likes Given
      26593

      Default Re: Dawa ya kuacha kukojoa kitandani

      Quote By Jomse
      mbona dawa ngumu na ina masharti ivyo.
      Ndio maana ikaitwa Dawa kuna Dawa Rahisi Dawa lazima şwe ngumu ndipo itakapofanya kazi mkuu Jomse
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    Page 10 of 11 FirstFirst ... 891011 LastLast

    Similar Topics

    1. Faini ya Tsh 10,000 kwa kukojoa...
      By Kibunango in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 28th July 2008, 12:12

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...