Wadau naomba ushauri na tiba kama ipo kwa binti yangu mwenye umri wa miaka 10 sasa.
Amekuwa akisumbuliwa na tatizo la kukojoa kitandni tangu alipokuwa mdogo, mbaya zaidi ni kwamba sasa hivi tumempeleka Boarding school-shule ya msingi.
Tatizo hili linaonekana kumuathiri kiakili na nina waswasi na maendeleo yake kwa sababu nilipomtembelea kwa mara ya mwisho anaona aibu kutoa godoro kulianika.
Nimeongea na Matron wake anasema hilo tatizo wanalo wengi ila yeye 'frequence' yake ni kubwa kulinganisha na wengine.
Je, tatizo hililinatibika wadau?

Reply With Quote









Follow Us Here