Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

    Report Post
    Page 1 of 6 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 101
    1. #1
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2095
      Likes Given
      1495

      Thumbs up 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Mchezo wa kanga moja maarufu kama kanga moko, umewatisha wabunge. Hali hiyo ilitokea bungeni jana wakati wabunge hao walipokuwa wakichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka wa fedha 2012/2013.

      Akichangia ktk mjadala huo, Mbunge wa Viti Maalum, Dk. Getrude Lwakatare (CCM), alisema kuna haja Serikali kuangalia mwenendo wa muziki huo, kwa kuwa unakiuka maadili ya Kibongo.

      “Hebu ngoja nizungumzie huu muziki wa kanga moja, huu ni mchezo mbaya sana, tena kanga inalowanishwa na maji halafu binti anaivaa.

      “Baada ya kuivaa anaanza kufanya manenguo, hivi itakuwaje kama mwenye umbo nene akiivaa na kunengua, ni aibu tupu hapa.

      “Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie namna ya kudhibiti hii kanga moja kwa sababu inachezwa kinyume cha maadili,” alisema Dk. Lwakatare.

      Kwa upande wa Mbunge wa Viti Maalum, Mwanamrisho Taratibu Abama (CHADEMA)...alisema muziki huo unafaa kupigwa marufuku kwa kuwa unawadhalilishwa wachezaji.

      “Huu muziki wa kanga moja haufai, nasikia mara nyingine wanauita kanga moko, huu ni udhalilishaji lazima upigwe marufuku.

      “Pamoja na kwamba unakiuka maadili ya Kitanzania, wanaume wanaupenda sana kwa sababu kila unapochezwa wanajaa ukumbini, Serikali iupige marufuku huu,” alisema Abama.





      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    2. Miaka 50

    3. #2
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,212
      Rep Power : 19215
      Likes Received
      8168
      Likes Given
      26659

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Kwahiyo wanaipaka hiyo Kanga maji kisha ndio wakakata hicho kiuno? bora waivue hiyo kanga wacheze uchi kuliko kutia maji hiyo kanga Young_Master
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    4. #3
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      76

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      ​hebu niweke video yake

    5. #4
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2095
      Likes Given
      1495

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Quote By MziziMkavu
      Kwahiyo wanaipaka hiyo Kanga maji kisha ndio wakakata hicho kiuno? bora waivue hiyo kanga wacheze uchi kuliko kutia maji hiyo kanga Young_Master
      Ha ha haaaa!!! Sasa wakikaa uchi si itakuwa kama danguro?
      MziziMkavu likes this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    6. #5
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2095
      Likes Given
      1495

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Quote By kapasi
      ​hebu niweke video yake
      haya hiyo hapo video. hayo ndio mambo ya kanga moko ambay serikali inataka kuyapiga marufuku

      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Nyani Ngabu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 15th May 2006
      Location : Ikungulyabashashi
      Posts : 39,263
      Rep Power : 36770
      Likes Received
      9630
      Likes Given
      686

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Quote By Young_Master
      Akichangia ktk mjadala huo, Mbunge wa Viti Maalum, Dk. Getrude Lwakatare (CCM), alisema kuna haja Serikali kuangalia mwenendo wa muziki huo, kwa kuwa unakiuka maadili ya Kibongo.

      “Hebu ngoja nizungumzie huu muziki wa kanga moja, huu ni mchezo mbaya sana, tena kanga inalowanishwa na maji halafu binti anaivaa.

      “Baada ya kuivaa anaanza kufanya manenguo, hivi itakuwaje kama mwenye umbo nene akiivaa na kunengua, ni aibu tupu hapa.

      “Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie namna ya kudhibiti hii kanga moja kwa sababu inachezwa kinyume cha maadili,” alisema Dk. Lwakatare.

      Kwa upande wa Mbunge wa Viti Maalum, Mwanamrisho Taratibu Abama (CHADEMA)...alisema muziki huo unafaa kupigwa marufuku kwa kuwa unawadhalilishwa wachezaji.

      “Huu muziki wa kanga moja haufai, nasikia mara nyingine wanauita kanga moko, huu ni udhalilishaji lazima upigwe marufuku.

      “Pamoja na kwamba unakiuka maadili ya Kitanzania, wanaume wanaupenda sana kwa sababu kila unapochezwa wanajaa ukumbini, Serikali iupige marufuku huu,” alisema Abama.
      Kwanza maadili ya Kitanzania ndiyo yapi hayo?

      Mbona hayo madanguro bubu aka ma 'guest houses' hawayashikii bango wakati ukweli wa mambo kwa asilimia kubwa sana yanatumika kama sehemu za watu kwenda kufanya ngono? Tena yamejaa kwenye sehemu za makazi ya watu....

      Hayo ma gesti hayakiuki maadili ya Kitanzania? Hivi nyie wabunge mliteuliwa kwenda huko bungeni kuongea pumba?

      Mnapokea mishahara ya bure kabisa. Hamstahili kulipwa hata shilingi moja. Na ingekuwa ni juu yangu mimi ningefutilia mbali huo ubunge wa aina yenu.

      Yaani mnasimama bungeni mnajadili khanga moko ndembendembe laki si pesa milioni chenji? Halafu mnadiriki kusema khanga moko zipigwe marufuku?

      Msitake kutuharibia watu starehe zetu bana, ebo!!!
      Miafrika Ndivyo Tulivyo.

    9. #7
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,530
      Rep Power : 1799
      Likes Received
      656
      Likes Given
      0

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Kuna mambo mengi sana ambayo yatakiwa kufutwa zaidi ya hiyo kanga moko,wamesahau night club zoote wadada wanavaa nusu uchi hapo je?madanguro je,?wacheza show wa bendi zetu je?hakuna cha kinyume na utamadiuni,waje na sera mbadala kupambana na utandawazi wa dunia kijiji ,kuanzia mashindano urembo hadi vipindi vya TV....majumba kulala wageni na uthibiti wake,Bar na Grosary zilizojaa kila mtaa na muda wa kuuuza na kunywa pombe....yako mengi sana!!waje na hoja mbadala wa mfumo mzima
      Young Master likes this.

    10. #8
      mymy's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd December 2011
      Posts : 119
      Rep Power : 398
      Likes Received
      33
      Likes Given
      27

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      ....wanaacha kujadili mambo ya maana wanajadili kanga moko. wawaache kwani ndo mtaji wao wenyewe....

    11. #9
      nachid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th April 2011
      Location : IRINGA
      Posts : 545
      Rep Power : 520
      Likes Received
      75
      Likes Given
      9

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      inaonekana waheshimiwa nao memba wa kuangalia kanga moko ndembendembe laki si pesa million..... huh huh huh huh

    12. #10
      King'asti's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th November 2009
      Location : The Jungle
      Posts : 17,236
      Rep Power : 28913
      Likes Received
      11716
      Likes Given
      4819

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Akili ya huyo mama inatikiswa na vitu vidogo tu maskini. Haoni issues za maana?
      Viariability ndo infanya maisha kuweka interesting.
      Kongosho and gfsonwin like this.
      I can be changed by what happens to me. But I refuse to be reduced by it-Maya Angelou


    13. #11
      adakiss23's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2011
      Posts : 1,248
      Rep Power : 671
      Likes Received
      281
      Likes Given
      32

      Default

      Kila mtu na starehe zake.. Watuachie starehe zetu!

      Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

    14. #12
      Mkereketwa_Huyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2011
      Location : London | Dar Es Salaam
      Posts : 1,820
      Rep Power : 4589
      Likes Received
      579
      Likes Given
      420

      Default

      Kanga moko na bongo fleva zote zipigwe marufuku Tanzania, ila kuhusu maadili ya Tanzania hilo sijuwi. lnachekesha kuona ni wabunge wanawake tu wanaopiga kelele kina baba kimyaaaa wanawaza watapata wapi starehe kama hii. Wabunge wetu hawa, basi tu!

    15. #13
      flora msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : under a coconut tree
      Posts : 4,144
      Rep Power : 1263
      Likes Received
      509
      Likes Given
      373

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      khaaaaaaaa kumbe na ww ni muumin wa dini hii?

      Quote By Nyani Ngabu
      Kwanza maadili ya Kitanzania ndiyo yapi hayo?

      Mbona hayo madanguro bubu aka ma 'guest houses' hawayashikii bango wakati ukweli wa mambo kwa asilimia kubwa sana yanatumika kama sehemu za watu kwenda kufanya ngono? Tena yamejaa kwenye sehemu za makazi ya watu....

      Hayo ma gesti hayakiuki maadili ya Kitanzania? Hivi nyie wabunge mliteuliwa kwenda huko bungeni kuongea pumba?

      Mnapokea mishahara ya bure kabisa. Hamstahili kulipwa hata shilingi moja. Na ingekuwa ni juu yangu mimi ningefutilia mbali huo ubunge wa aina yenu.

      Yaani mnasimama bungeni mnajadili khanga moko ndembendembe laki si pesa milioni chenji? Halafu mnadiriki kusema khanga moko zipigwe marufuku?

      Msitake kutuharibia watu starehe zetu bana, ebo!!!

      Never hate people who are jealous of you,
      Instead love them because they're the ones,
      who think you are better than them…

    16. #14
      Mkereketwa_Huyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2011
      Location : London | Dar Es Salaam
      Posts : 1,820
      Rep Power : 4589
      Likes Received
      579
      Likes Given
      420

      Default

      Quote By Skills4Ever
      Kuna mambo mengi sana ambayo yatakiwa kufutwa zaidi ya hiyo kanga moko,wamesahau night club zoote wadada wanavaa nusu uchi hapo je?madanguro je,?wacheza show wa bendi zetu je?hakuna cha kinyume na utamadiuni,waje na sera mbadala kupambana na utandawazi wa dunia kijiji ,kuanzia mashindano urembo hadi vipindi vya TV....majumba kulala wageni na uthibiti wake,Bar na Grosary zilizojaa kila mtaa na muda wa kuuuza na kunywa pombe....yako mengi sana!!waje na hoja mbadala wa mfumo mzima
      Nakubaliana nawe asilimia moja (100%).
      NG'ONGOVE likes this.

    17. #15
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,953
      Rep Power : 754
      Likes Received
      281
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Mkereketwa_Huyu
      Kanga moko na bongo
      fleva zote zipigwe marufuku Tanzania, ila kuhusu maadili ya Tanzania
      hilo sijuwi. lnachekesha kuona ni wabunge wanawake tu wanaopiga kelele
      kina baba kimyaaaa wanawaza watapata wapi starehe kama hii. Wabunge wetu
      hawa, basi tu!
      kuna mbunge mwanamke aliwahi kuonyesha hofu ya wao 'kukosa soko' kama wanaume wataruhusiwa kuoana!

    18. #16
      Mkereketwa_Huyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2011
      Location : London | Dar Es Salaam
      Posts : 1,820
      Rep Power : 4589
      Likes Received
      579
      Likes Given
      420

      Default

      Quote By adakiss23
      Kila mtu na starehe zake.. Watuachie starehe zetu!
      Ni kweli...na starehe za wabunge wetu ni hizi (kanga moko, ufuska, ulevi, kujirusha, utoro bungeni) na kutochangia mada muhimu kwenye vikao vya bunge. Sitashangaa akija mbunge na hoja ya kutaka kanga moko iwe vazi la taifa kwa kina mama. Ah Tanzania, nakusikitikia mama yangu!

    19. #17
      Baba V's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Location : Buguruni Mnyamani
      Posts : 10,962
      Rep Power : 30234
      Likes Received
      4722
      Likes Given
      3477

      Default

      Wavivu wa kufikiri,akili zao znaweza ku deal na vitu kama hivyo na wala sio mambo ya msingi. Simpleton represantatives!

    20. #18
      Msalagambwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th July 2012
      Posts : 538
      Rep Power : 453
      Likes Received
      178
      Likes Given
      532

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Safi sana na imetulia.

      Kelele za mpita njia,
      Hazimtoi pangoni mwenyewe,
      Wapi kanga moko huchezwa?
      kama zi kwenye majumba ya starehe!

      Huchezwa hadharani?
      Au mbele ya watoto mashuleni,
      Huchezwa stendi ya basi Ubungo?
      Palipo wote na watoto pia?

      Huko Kilabuni wacha ichezwe,
      Acheni wanengue mpaka wakatike,
      mikono mfukoni iwekwe,
      mijengo isimame imara,
      atazamaye kaipenda mwenyewe,
      Kiingilio si bure ni ngawira,
      Kanga moko wenyewe twaipenda,
      Kama huipendi waifwatiani?

      Mbunge alalama sauti juu apaza,
      eti ipigwe mafuruku nchini kote,
      mbona ujinga na ununda bungeni,
      mwashindwa piga marufuku???
      Matusi ruksa bungeni,
      Mwatukana mpendwavyo,
      Mangapi ya kuudhi bungeni twayasikia,
      Lakini pingu mwaitia Kanga Moko?

      Mwaendeleza ujinga wenu bungeni,
      michango mwashindwa toa kwa kiswahili,
      Ujumbe haufiki mpaka neno libane matusi,
      mmekomaa mashavu ndimi za chuma,
      Midomo yenu yanena ukengeufu,
      Vichwa vyenu vimejaa mvi
      Vichwani akili fupi kaa za makinda,
      Bunge gani la misonyo na utusitusi JUU.

      Msiiguse wala msiiseme vibaya kanga moko,
      kanga moko siye yatuburudisha,
      jadilini hoja maridhawa bungeni,
      kanga moko ni upepo wapita,
      Msiitaje kanga moko Bungeni,
      Suala la Kanga Moko liko Mahakamani.


      Msikomae na ulimbukeni komaeni na;
      Uhaba wa maji safi,
      Uovyo wa maji taka,
      Wizi na ubadhirifu serikalini,
      Ufisadi rushwa na ufuska,
      foleni za magari ubungo,
      Ndege mbovu TBS nyanya,
      Mauti Kuzama kwa meli,
      Mabilioni Iba ficha Uswiss,
      CCM sheria chini wao JUU,
      Watiwa mfukuko na mabilionea,
      Rais kiguu na njia,
      Muhimbili ife sie na APOLO,
      Ritz! Milionea,
      Kapata wapi kinda yule pochi????
      Haya basi mgawie kidogo Willie!!!
      Last edited by Msalagambwe; 26th July 2012 at 10:25.
      Kaizer, Edson and NG'ONGOVE like this.

    21. #19
      Mkereketwa_Huyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2011
      Location : London | Dar Es Salaam
      Posts : 1,820
      Rep Power : 4589
      Likes Received
      579
      Likes Given
      420

      Default

      Msalagambwe utarogwa. Wewe hujuwi wasifu wa wabunge wa Tanzania kuwa ni kuroga ili uogopwe? Haya yote uliyoyazungumza ni ya kweli na bahati mbaya watanzania hatupendi kuambiwa ukweli kwani ukiwa mkweli unaonekana adui. Mi nakuombea tu hawa wabunge wasije kuku Ulimboka (umafia aliowafanyiwa Dr. Ulimboka).
      Young Master and Msalagambwe like this.

    22. #20
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,777
      Rep Power : 27111
      Likes Received
      10114
      Likes Given
      14052

      Default Re: 'KANGA MOKO' yatikisa BUNGENI!

      Lakini jamani hivi hii kanga moko moko mambo ndembe ndembe laki si pesa million chenji unawakosesha wabunge amani???? kwanini wasikoseshwe amani ya hela ya NSSF wanayoikopa kwetu kiulazima? kwanini wasikoseshwe amani na mazingira mabaya watu tunayofanyia kazi?

      hivi hii wizara ina mambo mangapi ya kudiscuss? hebu angalia mavipindi yaliyopo kwenye tv na redio yanayopata coverage kubwa may be tz yote yanaachwa tena yasiyokuwa na maadili istoshe gesti za uchochoroni ndo usiseme huku uswazi halafu wanaongelea haya yanayoonekana hapa dar tu tena kwa watu wachache sana ambao hawazidi hata 100 kwa mara moja?
      "thought takes man out of servitude into freedom"
      'daima tudumu katika upendo'

    Page 1 of 6 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...