Huu ni mkasa wa kweli umemtokea ndugu yangu
Nilikutana na binti mmoja ambaye alikuwa akiishi kwa shemeji yake (mume wa dada yake) ambaye alikuwa rafiki yangu wa karibu sana. Nikampenda sana binti huyu na tukawa na uhusiano wa karibu kwa muda mrefu. Baada ya kuona tabia njema ya binti huyu niliamua kuweka kitu ndani (kumuoa) na nikalipa mahari nyumbani kwao na tukaanza maisha. Baada ya mwaka mmoja mke wangu akajifungua salama mtoto wa kiume. Kuzaliwa mtoto huyu ilikuwa mwanzo wa machungu ya maisha kwangu kwani mtoto alikuwa mweupee wakati mimi na mke wangu ni weusi kama mpoki. Sikuwa na wasiwasi sana kwani nimesoma biology kidogo, nikajua ni rangi ya bibi mzaa babu hiyo. Kadiri mtoto alivyozidi kukua alianza kufanana kwa kila kitu na yule rafiki yangu ambaye ni shemeji ya mke wangu. Mke wangu alikuwa akinifariji kwa kauli za kizamani eti mtoto wetu anafanana na mtoto wa shemeji yake kwasababu wakati mjamzito alikuwa anapenda kukaa naye. Mwenzenu sina raha kabisa kwa sababu mtoto ameota meno na mwanya unaoshabihiana na wa huyu rafiki yangu na kwetu hatuna mwenye mwanya wala ndugu za mke wangu hakuna kitu mwanya. Naombeni ushauri nimechanganyikiwa!

Reply With Quote





Follow Us Here