Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 28
    1. #1
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Well, hello guys!
      It is Mei Mosi again, zamani zetu Rais wa Jamhuri ilikuwa ni lazima atoe hotuba kwa wafanyikazi, na matarajio yetu mara nyingi ilikuwa ni kupanda kwa viwango vya mishahara. Ikifika siku ya leo, mfanyakazi lazima uhakikishe redio yako ina betri za kutosha, na ume-tune Radio Tanzania Dar es salaam (kwani kulikuwa na stesheni nyingine?), au kama uko Dar es salaam ujue Karimjee panakuhusu. Sijui kipindi hiki hali ikoje, I mean uhusiano kati ya serikali na wafanyikazi katika siku yao hii, I don’t bother anyways!

      Yangu mie leo sio hayo, ya kuwarudisha enzi za mwalimu, wala!

      Leo nataka nitoe pongezi zangu kwa makundi ya wafanyikazi wa sekta zisizo rasmi, tena ambao ni kama wanasahaulika kila yanapotajwa makundi ya wafanyikazi wengine.

      Wa kwanza ni mama lishe, au mama ntilie, kama hujanielewa, hawa ni watu wanaotoa huduma za chakula kwa bei nafuu katika vibanda vyao wenyewe, kama maisha yako ni safi au hauishi maeneo ya mjini, au kama umeoa huwezi kujua nazungumzia nini. Ndiyo, ili uwe mteja wa hawa kina mama kuna masharti kadhaa, kipato chako kiwe kidogo, uwe hujaoa na uwe mkazi wa mijini. Hawa ndio wanalisha kundi kubwa la wafanyakazi wa kiwango cha chini ambao ndio wengi na vijana. Kundi hili linalolishwa nao ndio nguvukazi ya taifa haswa, sipati picha bila huduma ya kinamama hawa maisha yetu yangekuwaje? Kazi yao ina changamoto nyingi, kushughulika na moto muda mwingi si mchezo, lakini bado hakujawa na tija sana katika biashara zao. Kutokana na kasumba, kinamama hawa hawakopesheki na mabenki, na ikitokea ni haya mashirika ya kina Iddi Simba, tena kwa riba ya asilimia 50. Biashara yao ni challenge tosha, achilia mbali matusi wanayovurumishiwa na wateja wao. Its realy painfull. My shout outs to you kinamama!

      Kundi la pili ni vibarua wa ujenzi maarufu kama wabeba zege. Hivi umeshawahi kujitwisha mfuko wa saruji wa kg. 50? Ni mzito asikwambie mtu, sasa maisha ya vijana hawa ni zaidi ya kubeba huo mfuko, ni kazi ngumu na nzito kuwahi kutokea chini ya jua. Pamoja na dharau wanayoipata kutokana na kazi yao, achilia mbali malipo duni wanayopata (Sh.T 4000/= kwa siku), ukweli ni kwamba hili ndilo kundi muhimu kabisa katika sekta ya ujenzi, hasa miradi mikubwa. Pata picha ile mijengo yote kule Posta na kwingineko, mabarabara yote nchi nzima, uwanja mkuu wa Taifa, ni kazi ya mikono yao. But when it comes to credits, everyone turns to so called ‘wakandarasi’, ambao ndio kupitia kwao majengo yanaanguka, barabara zinaumuka na uwanja hauna viwango. Nitumie kalamu hii kuwatia moyo vibarua wote wa ujenzi, natambua mchango wenu kwa taifa hili.

      Kundi la tatu ni wafanyabiashara wadogo wadogo wa vyakula na mbogamboga. Kwa sisi wakazi wa mjini tusiofuga wala kulima walau tuta moja la matembele, hawa ndio wakombozi wetu. Unajua mtu unaweza kuchukulia poa kwa vile ukihitaji nyama unaifuata tu buchani, hujui kuwa mwenzako ameamka saa tisa ya usiku kuwahi Vingunguti, na vibaka wote njiani, bado mvua haijanyesha hapo. Wauza genge vilevile huwalazimu kuamka saa 10 alfajiri ili kuwahi Kariakoo na Buguruni ili kuwaletea ninyi makulaji yenu ya kila siku, sijawasahau pia wafanyabiashara wa samaki ambao nusu ya maisha yao ni kukabiliana na lile shombo lenye harufu mbaya. Hawa niliowataja hapo juu wana maana kwenye maisha yangu ya kila siku kuliko Afisa Kilimo aliyehitimu SUA ambaye sioni delivery yake kwangu (samahani kama nimekukwaza).

      Kundi linguine katika kumbo hii ni wafanyakazi wote wa mifumo ya takataka. Yaani kuanzia wasafisha mitaro, wazoa takataka mpaka wazibua vyoo. Hizi ni kazi za kinyaa kuwahi kutokea kwenye uso wa nchi, really shit job, lakini wameifanya kwa moyo na kwa bidii siku zote za uhai wao. Hawa wana hatari kubwa ya kupata magonjwa ya kuambukiza but no one cares, hata vijisemina vya safety and precaution jamani? Wanakaa kujilaza kwenye mahoteli makubwa mpaka wanaibiwa huko, wala hawaangalii maslahi ya hawa watu. Ushawahi kufanya kazi mahali ambapo chemba ya uchafu imezibuka, hakyanani hapakaliki mahala hapo, na kama una roho nyepesi utashinda njaa siku nzima, utakulaje chakula mbele ya kinyesi? Kuhusu wazoa taka wala sina haja ya kuwaelezea sana, nadhani wote mmeshawahi kukatiza karibu na gari la taka, and you know the msala here, zimeshawahi kupita siku kadhaa bila gari ya taka kupita mtaani kwenu? How was it look like, uhm? Naomba nitambue uwepo wenu na umuhimu wenu katika kuweka mazingira tulivu kwa ajili ya kazi, masomo, na shughuli zingine.

      Wengine ni madereva, mtaani kwetu unawaita sukas. Hapa simaanishi kila mwenye leseni.\, nope! Namaanisha watu ambao udereva ndio kula yao, kuanzia madereva taksi, madereva wa daladala, wanaosafirisha abiria mikoani na wanaosafirisha mizigo ndani na nje ya nchi. Hii ni kazi ambayo hakuna uvivu, lazima unapokuwa nyuma ya usukani uwe macho muda wote na uweke akili yako barabarani, bado kuna changamoto za vyombo kupata hitlafu barabarani bila kusahau ajali, hakuna dereva anayependa ajali wakuu, hasa kwa vile na maisha yake nayo yanahusika. Na bado kikinuka, cha kwanza ni polisi kumtia pingu dereva, bila kujua kuwa si kila ajali inasababishwa na uzembe, ndo maana wengi wanakimbiaga. Bado kitengo cha usalama barabarani hakijishughulishi na kutoa elimu kwa madereva, wao ni kuandika notifikesheni tu na kupokea rushwa. Mwishoni mwa mwaka jana kama sikosei, ndio Said Salim Bakhressa aliandaa semina kwa ajili ya madereva wa mizigo wa kampuni lake na akakaribisha madereva wengine kujifunza bure, lakini waliopewa dhamana hiyo, wala hawana habari. Changamoto zingine kwa madereva ni pamoja na kuvamiwa na majambazi kwa wanaosafiri mbali na taxi drivers. Kingine ni ugonjwa wa UKIMWI hasa kwa madereva wa mizigo masafa marefu, wakati umefika kwa mashirika ya kupambana na UKIMWI yaandae semina zaidi kwa hawa madereva, wako katika hatari kwa kweli. Mbali na yote, natambua mchango wao katika kuendeleza taifa hili, wote mmeshuhudia adha ya mgomo wa madereva na mnajua madhara ya sekta ya usafirishaji kwa uchumi wa nchi.

      Kundi la mwisho katika andiko langu hili, naomba niguse wafagizi wa barabara. Kwanza hawa mara nyingi ni kinamama wazee, sijui kwanini imekuwa hivyo? Miili yao imechoka na uwezo wa kuona umepungua kwa kiasi fulani, yet wanafanya kazi katika mazingira ya kupishana na magari, aloo? Yupo mmoja ambaye ni jirani yangu, kila baada ya siku kadhaa lazima anijie na stori ya koswakoswa za magari, what a risk? Thanks god madereva wanajitahidi wawezavyo kuwajali, na matukio ya hawa kugongwa si mengi sana. Pamoja na hatari hizo, bado maslahi ya kazi yao ni kiduchu, hardly wanalipwa Tsh. 40000/= kwa mwezi, hakuna tips, per diem wala sijui nini nini allowances, lakina maisha yanasonga. Natambua mchango wao katika kuweka mazingira ya miji yetu safi, hasa kutokana na sisi kutokuwa na ustaarabu wa utupaji taka njiani. My appreciatin to you!

      Hao ndio nilioona ni vema niwaangazie katika andiko langu kwa leo, maana sidhani hata kama wanajua kuwa leo ni sikukuu yao. Hardly they work, hardly they earn!

      Mei Mosi njema!
      Mphamvu.
      "...kukaa kimya ni jibu la mjinga!"
      -Leila Rashid (Jahazi Modern Taarab)


    2. #2
      gambachovu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2011
      Posts : 1,865
      Rep Power : 2196
      Likes Received
      256
      Likes Given
      379

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      May Day juu! Juu! Juu zaidi!

      Makuli mbona sijawaona kwenye uzi wako mkuu Mphamvu

    3. #3
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Quote By gambachovu View Post
      May Day juu! Juu! Juu zaidi!

      Makuli mbona sijawaona kwenye uzi wako mkuu Mphamvu
      Dah, kweli nimewasahau, unajua inategemea na jinsi unavokuwa na exposure, mimi sijawahi kuingia bandarini na masokoni sio mtenbeleaji sana kwa hiyi wakanitoka kidogo.
      Samahani kwa hilo mkuu gambachovu...
      Invisible likes this.
      "...kukaa kimya ni jibu la mjinga!"
      -Leila Rashid (Jahazi Modern Taarab)

    4. #4
      Mtazamaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th February 2008
      Location : global village
      Posts : 5,979
      Rep Power : 1779
      Likes Received
      1326
      Likes Given
      2661

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Quote By Mphamvu View Post
      Dah, kweli nimewasahau, unajua inategemea na jinsi unavokuwa na exposure, mimi sijawahi kuingia bandarini na masokoni sio mtenbeleaji sana kwa hiyi wakanitoka kidogo.
      Samahani kwa hilo mkuu gambachovu...
      Sisi huku kanda ya ziwa tunao pia wavuvi. wale wanao tumia kokoro(Nyavu zinazotumika kutega samaki) na mtumbwi(tena mitumbiw sio ya engineya kasia) .Aisee kazi yao ni ngumu sana. Japo tunafurahia utamuwa samhawa jamaahuwa sometime hawalali usikuhata wiki nzima .USiku kwao ni mchana namchana ni usiku

      kuna kundi lingine tata na linazua mjadala na gumzo japo siliungimkono kutokana ugumu wa kazi zao na "demokrasia ya kizungu "inabidi tukubali kweli wamejitoa.Ni madadapoa na makaka poa. Kuna mmoja nasikia aliuwawa kwarisasi na mteja wake pale makaburini kinondoni

      Kuna mmoja nasikia aliuwawa kwarisasi na mteja wake pale makaburini kinondoni
      Tazama michezo live katika gym nayotumia kukuzia misuli ya IT- http://teknohama.x10.mx/live-sports/


    5. #5
      dazipozi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2011
      Location : Dar.Tanzania
      Posts : 1,143
      Rep Power : 709
      Likes Received
      101
      Likes Given
      59

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Sure maneno mazima
      Call me Mr. President or call me Mr. Ever Care or Mr. Everywhere or Mr. Never Care


    6. #6
      Yegomasika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2009
      Location : Mwanza
      Posts : 1,916
      Rep Power : 905
      Likes Received
      447
      Likes Given
      308

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Asante kwa kutukumbuka sisi wavuvi, kwani shughuli yetu kwa kweli si ndogo. Kupiga kasia wakati mwingine ukishindana na upepo ni shughuli pevu...wavuvi oyee!@ Mtazamaji.
      Mtazamaji likes this.
      Happiness Begins With Facing Life With A Smile And A Wink.

    7. #7
      Mtazamaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th February 2008
      Location : global village
      Posts : 5,979
      Rep Power : 1779
      Likes Received
      1326
      Likes Given
      2661

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Quote By Yegomasika View Post
      Asante kwa kutukumbuka sisi wavuvi, kwani shughuli yetu kwa kweli si ndogo. Kupiga kasia wakati mwingine ukishindana na upepo ni shughuli pevu...wavuvi oyee!@ Mtazamaji.
      Yegokutigigo. Waongera
      yego mwamba na yegomasika. Hahahahahaha


      Ile shughuli si ndogo sijui kulekwenu bado watu wanatumiana mamba
      Tazama michezo live katika gym nayotumia kukuzia misuli ya IT- http://teknohama.x10.mx/live-sports/


    8. #8
      Mamndenyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 13,546
      Rep Power : 35838
      Likes Received
      6922
      Likes Given
      21198

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Mmmh kubwa mno jamani.

    9. #9
      Yegomasika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2009
      Location : Mwanza
      Posts : 1,916
      Rep Power : 905
      Likes Received
      447
      Likes Given
      308

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Quote By Mtazamaji View Post
      Yegokutigigo. Waongera
      yego mwamba na yegomasika. Hahahahahaha


      Ile shughuli si ndogo sijui kulekwenu bado watu wanatumiana mamba
      Taratibu bana, watu humu wataniogopa ujue!.
      Happiness Begins With Facing Life With A Smile And A Wink.

    10. #10
      Speaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th August 2010
      Posts : 6,178
      Rep Power : 4566
      Likes Received
      2003
      Likes Given
      5101

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Asante sana kwa salam za sikukuu kaka.
      Mjinga mpe cheo...

    11. #11
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default

      Quote By Mtazamaji View Post
      Sisi huku kanda ya ziwa tunao pia wavuvi. wale wanao tumia kokoro(Nyavu zinazotumika kutega samaki) na mtumbwi(tena mitumbiw sio ya engineya kasia) .Aisee kazi yao ni ngumu sana. Japo tunafurahia utamuwa samhawa jamaahuwa sometime hawalali usikuhata wiki nzima .USiku kwao ni mchana namchana ni usiku

      kuna kundi lingine tata na linazua mjadala na gumzo japo siliungimkono kutokana ugumu wa kazi zao na "demokrasia ya kizungu "inabidi tukubali kweli wamejitoa.Ni madadapoa na makaka poa. Kuna mmoja nasikia aliuwawa kwarisasi na mteja wake pale makaburini kinondoni

      Kuna mmoja nasikia aliuwawa kwarisasi na mteja wake pale makaburini kinondoni
      Kuhusu wavuvi, ilibaki kidogo niwagusie, ila sijui shatwain gani akanipitia, kuna mahala nilitaja wafanyabiashara wa samaki, cha ajabu nikawasahau wanaowawezesha, ukizingatia huku kwetu uvuvi bado haujahodhiwa na makampuni makubwa.

    12. #12
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 26,193
      Rep Power : 25454
      Likes Received
      14894
      Likes Given
      15864

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Ni kweli, makundi ya muhimu sana haya japo husahaulika.
      No matter how hot your anger is, it can not cook yams-Nigeria

    13. #13
      Mtazamaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th February 2008
      Location : global village
      Posts : 5,979
      Rep Power : 1779
      Likes Received
      1326
      Likes Given
      2661

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Quote By Mphamvu View Post
      Kuhusu wavuvi, ilibaki kidogo niwagusie, ila sijui shatwain gani akanipitia, kuna mahala nilitaja wafanyabiashara wa samaki, cha ajabu nikawasahau wanaowawezesha, ukizingatia huku kwetu uvuvi bado haujahodhiwa na makampuni makubwa.
      MphamvuNa hao wengine niliowataja .mbona umewapotezea teh teh teh.Nasikia kupitai kipato chao walianzisha pub . Moja iikuwa inaitwa kamana pub.( Hii niliiona kabisa ) na nyingine ushuzi pub . Hii ya ushuzi nadhani wangeweza kupata msaada Ubalozi wa ........

      Si ndio demokrasia atiiiiii
      Tazama michezo live katika gym nayotumia kukuzia misuli ya IT- http://teknohama.x10.mx/live-sports/


    14. #14
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default

      Quote By Mtazamaji View Post
      MphamvuNa hao wengine niliowataja .mbona umewapotezea teh teh teh.Nasikia kupitai kipato chao walianzisha pub . Moja iikuwa inaitwa kamana pub.( Hii niliiona kabisa ) na nyingine ushuzi pub . Hii ya ushuzi nadhani wangeweza kupata msaada Ubalozi wa ........

      Si ndio demokrasia atiiiiii
      Loh?
      Hawa inakuwa vigumu kuwakumbatia kwa kuwa kazi zao sio halali, for they are not enforced by law. Kwa sasa sitakuwa nao mpaka sheria itakapoainisha vingine, sory to say that. Unajua Afrika si Ulaya wala Marikani, kwetu sisi, maisha yako ni ya familia yako, ukoo na pengine kijiji chako. Uchangudoa au ushoga wako unakuwa ni fedheha kwetu wote tunaohusika na maisha yako. Wenzetu wazungu walishajikataa kila mtu anaishi maisha yake binafsi, babako au mamako akizeeka unampeleka kituo cha kulea wazee, regardless vyenye alikulea.
      Ningekuwa na uwezo?

    15. #15
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default

      Quote By Mamndenyi View Post
      Mmmh kubwa mno jamani.
      Nini kubwa Mamndenyi?

    16. #16
      gambachovu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2011
      Posts : 1,865
      Rep Power : 2196
      Likes Received
      256
      Likes Given
      379

      Default

      Quote By Mphamvu View Post
      Dah, kweli nimewasahau, unajua inategemea na jinsi unavokuwa na exposure, mimi sijawahi kuingia bandarini na masokoni sio mtenbeleaji sana kwa hiyi wakanitoka kidogo.
      Samahani kwa hilo mkuu gambachovu...
      Kwa hiyo hata kile kitabu cha Fasihi Andishi cha Kuli nacho hukuwahi kukisoma mkuu Mphamvu?

    17. #17
      gambachovu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2011
      Posts : 1,865
      Rep Power : 2196
      Likes Received
      256
      Likes Given
      379

      Default

      Quote By Mtazamaji View Post
      MphamvuNa hao wengine niliowataja .mbona umewapotezea teh teh teh.Nasikia kupitai kipato chao walianzisha pub . Moja iikuwa inaitwa kamana pub.( Hii niliiona kabisa ) na nyingine ushuzi pub . Hii ya ushuzi nadhani wangeweza kupata msaada Ubalozi wa ........

      Si ndio demokrasia atiiiiii
      We unajitafutia ban... Eidha kwa kujua,ama bila kujua!

    18. #18
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,863
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22555

      Default Re: My Mei Mosi shoutouts... (Hutaki unaacha)

      Umewasahau ma TX!. Ma HG ambao licha ya kufanya kazi za ndani, pia huwa mayaya kutulelea watoto wetu, na wengine huwasaidia hata wa mama wenye nyumba kumhandle yule "mtoto mkumbwa"!.

    19. #19
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default

      Quote By gambachovu View Post
      Kwa hiyo hata kile kitabu cha Fasihi Andishi cha Kuli nacho hukuwahi kukisoma mkuu Mphamvu?
      Sikuwahi kukisoma mkuu,
      ingawa nakifahamu, mara kadhaa nimekikuta kwenye marejeo ya kazi ninazozisoma (since I deal with isimu na fasihi ya Kiswahili), lakini bado nasisitiza kuwa sijakuwa karibu na kundi hili kiasi cha kuandika kwa kina kuhusu wao, ningepiga blah blah na bashiri za uongo na kweli, kitu ambacho ni kinyume na maadili ya uandishi.

    20. #20
      Mphamvu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Pale pale kwa JANA!
      Posts : 7,340
      Rep Power : 18686
      Likes Received
      1117
      Likes Given
      1064

      Default

      Quote By Pasco View Post
      Umewasahau ma TX!. Ma HG ambao licha ya kufanya kazi za ndani, pia huwa mayaya kutulelea watoto wetu, na wengine huwasaidia hata wa mama wenye nyumba kumhandle yule "mtoto mkumbwa"!.
      Loh?
      Umegusa penyewe hasa, hawa nawafananisha na kiungo namba 6 uwanjani, wanafanya kazi kubwa sana lakini hawaonekani. Na kwa familia zetu za Kiswahili, all the credits wanapata ni masimango, makaripio na mshahara wa Sh.T 20000/=
      Kwa mtu ambae ndio ana dhamana ya kukulelea wanao, ana access na chakula unachokula, unatakiwa uwe more than fair to her, basi tu ni vile hatujui hatari ya position zao endapo zitatumiwa vibaya, God forbid.
      Kuhusu kumlea mtoto mkubwa, thats a help of its kind, you're right, Pasco.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...