Naam wanajukwaa
Nafurahi kujiunga na JF, nachukulia jukwaa hili kama ni sehemu ya kujifunza.
Takwimu za tanzania zinaonyesha kuwa kuna watanzania zaidi ya 1.2m wanaoishi nje ya nchi [rejea ripoti ya Tanzania Law Review Commission]. Naam hii ni karibu 3% ya taifa zima.
Nadhani wakati umefika sasa serikali ikapitisha sheria kuruhusu raia hawa kuweza kufaidi matunda ya uraia wa nchi mbili kwani kwa sasa wengi wanakwazwa na kuwa wakiamua kuchukua uraia mwingine inabidi waamue kuachia uzalendo wao.
Swali hili niliwahi kumuuliza mheshimiwa Sumaye alipokuja hapa Uingereza mwaka jana akakiri kuwa ni muhimu kuruhusu lakini hakuweza kutoa sababu kwa nini hasa mpaka sasa Tanzania imeshindwa kuwa sheria ya kuruhusu uraia wa nchi mbili.
Sasa hivi watanzania wengi wanaoishi Uingereza na nchi nyinginezo za Magharibi wanaweza kupata misaada kadhaa ya kuwekeza nchini mwao lakini kwa vile wengi wameamua kuwa na uraia wa nchi mbili bila kuachia uraia wao wa TZ basi inakuwa hawawezi kuwekeza nyumbani na kama watawekeza wataweka katika mfumo usio rasmi kama vile kuwatumia ndugu na jamaa pesa ili waweze kuwekeza,matokeo yake ni kuwa kwa vile ndugu hana uwezo wa biashara au kutokuwa muaminifu inakuwa ndio hivyo tena hela zinakwenda na hakuna linalofanyika,hii ina athari zaidi kwani mtu huyu hutotegemea akamhimiza mwenzie wa tanzania kuwa kawekeze nyumbani.
Naam mniwie radhi wanajukwaa nadhani ngwe yangu hapa mtandaoni italelemea zaidi katika kuwawezesha na kuwajali raia wote wa tanzania na kwa vile tuna asilimia 3% ya hawa wapo nje basi nao inabidi waainishe hoja zao ikiwemo na matatizo wayapatao,mwishowe waweze kuwa nao ni washiriki wazuri wa shughuli za kiuchumi Tanzania.
Mfano wa China ututoshe:
Kuna wachina 48 milioni nje ya nchi yao.Kuna wizara ya kushughulikia wachina waliopo nje ambayo inakuwa ni kama kiambatanishi cha wizara ya mambo ya nje ambapo wana jukumu la kuhakikisha kila mchina mwenye uwezo wa kutoa mchango kwao anawezeshwa bila vikwazo na pia wachina waliopo nje waweze kuwa wanapata habari na taarifa sahihi kuhusu hali ya uchumi,siasa,jamii nk wakati wote.
Angalia kwetu:
Balozi zetu zipo mbali na watanzania au tusema baadhi zimejitenga sana,ni kwa sababu kuwa karibu au mbali kunategemea na hulka ya balozi husika,kama ni mtu wa watu basi watu 'watajichanganya' kama sivyo basi watu hola! Nukta ni nini hapa? ni kuwa inabidi kuwe na ainisho maalum kwenye kazi za balozi katika kuwashughulikia watanzania.
Inatokea Rais anakuja kwenye nchi husika balozi anamkimbiza asionane na watanzania!
Natumai Ari mpya haitokuwa hivi na mabalozi nao watawajali watanzania hawa. Maoni yanakaribishwa, ''i stand to be corrected''


Reply With Quote
Follow Us Here