Ujenzi wa barabara ya Sam Nujoma - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jamii Intelligence


Jamii Intelligence Serious reports & Discussions on Corruption, Politics etc recommended to our clients! Detailed discussions which you need not to miss


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 4th July 2007, 05:10 PM   #1
Ujenzi wa barabara ya Sam Nujoma
Morani75 Morani75 is offline 4th July 2007, 05:10 PM

Salaaam wana Jamii Forums...

Ni majuzi nilipita pale kwenye barabara mpya ya Sam Nujoma. Kwa kweli barabara hii imejengwa/inaendelea kujengwa vizuri sana. Lakini kuna baadhi ya mambo ambayo kwa kuangalia inaonekana kama kuna mtabaruku kidogo. Suala lenyewe ni kwamaba inaonekana mjenzi (Chinese company) wameamua kujenga kile tunachokiita lami nene (minimum 10cm thick, single lift). Tatizo lenyewe ni kwamba kwa wale amabao tumeweza kufanya kazi hizi za lami (asphalt concrete, both AC and AG), njia hii sio nzuri na ina madhara makubwa kwa ufanisi (life span) and utendaji (performance) ya barabara hii. Cha ajabu ni kwamba mheshimiwa huyu contractor na consultant wake hawajui vifuatavyo:

1. Hali ya hewa ya joto (temperate climate) inahitaji lami hii iwe kwenye unene mdogo kuzuia kiitwacho temperature softening ya lami. Hii itasababisha barabara yetu kubomoka kabla ya wakati na kuzuia ni labda kama wameweka/wametumia ile inayoitwa teknolojia ya kutumia "high performance binders"

2. Vifaa wanavyotumia siku nilipopita pale (na siku nyingine mbili tatu zaidi ni kandamizo yenye matairi laini (pneumatic roller) moja na kandamizo gumu (steel drum roller) moja. Kwa unene wa layer kwa kweli vifaa hivi ni vidogo/vichache kwa kutimiza mkandamizo unatakiwa kabla lami haijapoa na kuanza kuwa "rigid" na hivyo kuna uwezekano kukawa na "under compaction" itakayoelekea kuruhusu maji kuingia na kusababisha "premature failure"

3. Kiutendaji, barabara ya lami inatakiwa kutokuwa na migongo au miyumbo. Kwa unene wa layer uliowekwa tayari barabara imeanza kuwa na miyumbo. Mara nyingi hii inatokana na lami labda kutoshindiliwa vizuri (traffic indiced consolidation/compaction), layer kuwa nene sana na vifaa kushindwa kupata "even compaction/smoothness" kutokana na kuwa na uwezo mdogo, paver kuwa na "poor sensors". Kwa harakaharaka kwa ule upande ambao tayari wameshamwaga lami kwa kweli inaonekana kuna mapungufu sababu tayari barabara ina miyumbo hata kabla ya barabara kufunguliwa.

Sasa mimi nashangaa ina maana walivyoshinda kazi hii serikali haina wataalamu ambao wangeweza kuona mambo haya?? Na hii kampuni ya China iliyoshinda mradi huu ina maana waliweka vifaa vichache (walipataje kazi??) au ni kwamba hawajaleta vifaa vyote?? Mwisho, ina maana tunachohitaji ni kuona barabara mpya au tunahitaji pia kupata "quality of work worth of our money invested??".

Kwa habari tuzipatazo kutoka mikoani ikiwemo Singida - Manyoni amabapo kampuni nyingine ya Kichina imeshindwa kutimiza mkataba na malalamiko ya wananchi kuhusu utendaji kazi wa makampuni haya inakuwaje bado tunaendelea kuyaona yakipata kazi hapa nyumbani?? Kibaya zaidi barabara hii ipo mbele ya macho ya watu wengi vikiwemo vyombo vya kusimamia wahandisi, makampuni na vinginevyo vingi??

Tumsaidie mheshimiwa Rais kataka kutimiza miradi na vilevile tujionee huruma sisi walipa kodi.

Naomba kuwasilisha...

Morani75
JF Senior Expert Member
Points: 212,316, Level: 100 Points: 212,316, Level: 100 Points: 212,316, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Thu Mar 2007
Location: Duniani
Posts: 662
Thanks: 6
Thanked 3 Times in 3 Posts
Views: 3346
Reply With Quote
  #2  
Old 4th July 2007, 09:31 PM
Shy Shy is offline
Shy is yours
Banned
Points: 2,380,404, Level: 100 Points: 2,380,404, Level: 100 Points: 2,380,404, Level: 100
Activity: 9% Activity: 9% Activity: 9%
 
Join Date: Thu Nov 2006
Posts: 4,258
Thanks: 0
Thanked 170 Times in 112 Posts
Rep Power: 0
Shy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enough
Send a message via Yahoo to Shy
Default

Hello Morani

Karibu Na Ahsante Kwa Mada Yako Nzuri

Kwa Mimi Ninavyojua , Hii Barabara Ya Sam Nujoma Kwanza Tenda Yake Ina Utata Inasemekana Hiyo Kampuni Ya Kichina Ilipata Hiyo Tenda Kutokana Na Gharama Zake Kuwa Ndogo Lakini Inashangaza Kwa Sababu Wafadhili Wa Barabara Hii Ni European Union Sasa Sijui Hapa Ilikuaje Kuaje Na Hawa Eu Wana Masilahi Gani Hapa Mpaka Wakachagua Kampuni Kama Hii .

Pili Mimi Binafsi Huwa Napita Barabara Hii Karibu Kila Siku , Hata Sasa Hivi Nimepia Barabara Hii Wakati Nakuja Kupumzika Na Sasa Ni Usiku Ujenzi Unaendelea , Ujenzi Huu Wa Usiku Ndio Unatia Mashaka Pengine Ndio Siri Zinafichwa Sana Hapa Kwa Sababu Usiku Huu Hukuti Mainjinia Wa Kitanzania Ni Wachina Tu Na Vibarua Wao Sasa Wazalendo Wetu Wako Wapi ? Jibu Wanalo

Tatu Hatujui Norplan Wana Uzoefu Gani Na Usimamizi Wa Miradi Ya Ujenzi Wa Barabara Hata Hii Kampuni Ya Kichina Pia Hii Nayo Inaweza Kuchangia Mambo Ya Experiance Au Unasemaje ?

La Mwisho Na Kumalizia Ni Kwamba Tangia Barabara Hii Inaanza Kujenga Hakuna Mtaalamu Wowote Wa Kitanzania Amewahi Kuongelea Suala Hili Kiutaalamu Zaidi Au Hizi Kampuni Hazina Press Conference Za Kuelezea Maendeleo Ya Maradi Huu Ili Wananchi Waweze Kuuliza Na Kuelimishwa

Halafu Mradi Huu Haujulikani Kwa Watu Wengi Zaidi Ya Njia Tu Hakuna Picha Maalumu Akilini Mwa Watu Yaani Njia Itakuwaje Au Utafanyaje Kazi , Wangeleta Simulation Ya Kuelezea Jinsi Mradi Utakavyokuwa , Adhari Zake Kwa Jamii Na Kadhalika

Vyote Hivi Hatuna

Lakini Mradi Unaendelea

Usiku Mwema
Reply With Quote
  #3  
Old 4th July 2007, 09:35 PM
Phillemon Mikael Phillemon Mikael is offline
Phillemon Mikael has no status.
JF Premium Member
Points: 644,679, Level: 100 Points: 644,679, Level: 100 Points: 644,679, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Sun Nov 2006
Location: mwanza,/uk/santa clara
Posts: 3,015
Thanks: 23
Thanked 332 Times in 153 Posts
Rep Power: 30
Phillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enough
Default

safi sana mtaaluma ,hii inatakiwa ..kweli jf ni kisima na ma engneer tunao..yupo pia engneer mohamed...
__________________
Reply With Quote
  #4  
Old 6th July 2007, 06:01 PM
Kigarama Kigarama is offline
Kigarama ni Kabwela mzururaji
JF Senior Expert Member
Points: 236,434, Level: 100 Points: 236,434, Level: 100 Points: 236,434, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Apr 2007
Posts: 364
Thanks: 7
Thanked 9 Times in 5 Posts
Rep Power: 23
Kigarama will become famous soon enoughKigarama will become famous soon enoughKigarama will become famous soon enoughKigarama will become famous soon enoughKigarama will become famous soon enoughKigarama will become famous soon enoughKigarama will become famous soon enoughKigarama will become famous soon enough
Default

tuanahitaji ufafanuzi kama huo kwa maendeleo ya nchi yetu!
Reply With Quote
  #5  
Old 30th November 2007, 01:05 PM
Morani75 Morani75 is offline
Morani75 has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 212,316, Level: 100 Points: 212,316, Level: 100 Points: 212,316, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Mar 2007
Location: Duniani
Posts: 662
Thanks: 6
Thanked 3 Times in 3 Posts
Rep Power: 25
Morani75 will become famous soon enoughMorani75 will become famous soon enoughMorani75 will become famous soon enoughMorani75 will become famous soon enoughMorani75 will become famous soon enoughMorani75 will become famous soon enoughMorani75 will become famous soon enoughMorani75 will become famous soon enough
Angry Ujenzi wa Barabara ya Sam Nujoma, Dar

Salaam kwa WanaJambo wenzangu!! Wengi tutakumbuka kuwa muda si mrefu sana uliopita niliweka "post" kuhusu barabara yetu hii ya Sam Nujoma. Nakumbuka wakati ule pamoja na kwamba ujenzi ulikuwa unaendelea, mambo yalikuwa ahueni kuloko sasa. Mheshimwa Rais anajaribu kuweka mandhari mzuri kwa uwekezaji na maendeleo lakini tatizo ni kwamba kuna tatizo kwenye mtandao mzima. Sio madini pekee yanahitaji marekebisho, pia kwenye vitu kama miundombinu kuna matatizo zaidi.... Sasa hatimaye dakika ya 89 ya mechi ya hii barabara imewadia. TANROADS (under new management and technical skills) wanarushiana mpira na wizara husika, kunani??? Someni wenyewe habari hii niliyopata kutoka "www.ippmedia.co.tz" leo:


Quote:
Makabidhiano ya barabara Sam Nujoma bado ni kitendawili
2007-11-30 08:26:27

Na Dunstan Bahai


Hatima ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya Sam Nujoma ya jijini Dar es Salaam ambayo ilikuwa ikabidhiwe kuanzia wiki ijayo, haijajulikana baada ya Wizara ya Miundombinu na Wakala wa Serikali wa Barabara (TANROADS) kurushiana mpira.

Kwa upande wa TANROADS, Ofisa mmoja mwandamizi aliyekataa kutaja jina lake, alisema, Wizara ya Miundombinu wamewakataza kuzungumzia barabara hiyo na badala yake wenye mamlaka ni wizara.

Hata hivyo, Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Makongoro Mahanga alisema, ofisi yake haina taarifa ya kuwakataza Tanroads kuzungumzia barabara hiyo.

`Mimi sina taarifa zozote juu ya wao kukatazwa kuzungumzia matatizo na mafanikio ya barabara hiyo kwani wao ndiyo wasimamizi wakuu, walikuwa kwenye nafasi nzuri ya kuizungumzia,` alisema Naibu Waziri juzi jijini Dar es Salaam.

Aidha alimuahidi mwandishi kuwa angeweza kuzungumzia hatma ya barabara hiyo jana baada ya kuwasiliana na maofisa wa TANROADS kwa vile hakuwa anaelewa vizuri kutokana na kuwa nje ya ofisi yake kwa muda mrefu.

Hata hivyo jana alipoulizwa, alisema hayuko kwenye nafasi nzuri ya kuzungumzia na badala yake alimuomba mwandishi kuwasiliana na maofisa hao wa TANROADS au Katibu Mkuu wake ambaye hakuweza kupatikana jana.

Mkurugenzi Mkuu wa Tanroads, Bw. Ephraim Mrema kwa upande wake alisema, eneo alilokutwa katikati ya jiji halikuwa muafaka kuzungumzia suala hilo, ingawa hakusema eneo muafaka ni lipi.

Barabara hiyo imekuwa ikileta maswali mengi kuliko majibu kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam kutokana na ujenzi wake kuchukuwa muda mrefu.

Aidha makabidhiano ya ujenzi wa barabara hiyo yamekuwa yakiahirishwa mara kwa mara na serikali imekuwa tayari kuiongezea muda kampuni inayoitegeneza kwa zaidi ya mara tatu ambapo mara ya mwisho ni mwezi Desemba unaoanza kesho.

SOURCE: Nipashe

Last edited by PainKiller; 30th November 2007 at 04:15 PM.. Reason: Quoting..
Reply With Quote
  #6  
Old 30th November 2007, 01:56 PM
Misterdennis Misterdennis is offline
Misterdennis has no status.
Senior Member
Points: 88,473, Level: 100 Points: 88,473, Level: 100 Points: 88,473, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Jun 2007
Posts: 144
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 23
Misterdennis will become famous soon enoughMisterdennis will become famous soon enoughMisterdennis will become famous soon enoughMisterdennis will become famous soon enoughMisterdennis will become famous soon enoughMisterdennis will become famous soon enoughMisterdennis will become famous soon enoughMisterdennis will become famous soon enough
Default Re: Ujenzi wa Barabara ya Sam Nujoma, Dar

Tatizo ni serikali kukumbatia cheap contracts ... na zinazoruhusu baadhi ya maofisa watoa tenda /wasimamizi kuchukua chao katika hizi contracts. Matokeo wakandarasi wanaishia kufanya sarakasi tuu kwenye saiti bila ujenzi wa maana kuonekana.
kampuni za kichina zimetokea kupewa kazi nyingi za ujenzi siku za karibuni lakini utendaji wao umekuwa si mzuri sana. Barabara ya singida walinyan'ganywa wakapewa konoike.. !!
Reply With Quote
  #7  
Old 30th November 2007, 04:45 PM
Katibu Tarafa Katibu Tarafa is offline
Katibu Tarafa a president to be
JF Senior Expert Member
Points: 147,270, Level: 100 Points: 147,270, Level: 100 Points: 147,270, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Fri Feb 2007
Posts: 1,130
Thanks: 1
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power: 26
Katibu Tarafa will become famous soon enoughKatibu Tarafa will become famous soon enoughKatibu Tarafa will become famous soon enoughKatibu Tarafa will become famous soon enoughKatibu Tarafa will become famous soon enoughKatibu Tarafa will become famous soon enoughKatibu Tarafa will become famous soon enoughKatibu Tarafa will become famous soon enough
Default Re: Ujenzi wa Barabara ya Sam Nujoma, Dar

tatizo la bongo,pakishakuwa na tatizo tu basi kila mtu atakwambia sio msemaji lakini penye kutafuta ujiko kila mtu atazungumsa hata bila kuulizwa,mimi nafikiri mtu ambaye alipaswa kuzungumzia hii barabara ni site maneger na sio mtu mwingine.yeye ndio anajua mbivu na mbichi,lakini utakutwa anaulizwa waziri au mkurugenzi yeye anajua nini hapa.
Reply With Quote
  #8  
Old 30th November 2007, 05:23 PM
Roya Roy's Avatar
Roya Roy Roya Roy is online now
Roya Roy always on the feet
JF Premium Member
Points: 159,756, Level: 100 Points: 159,756, Level: 100 Points: 159,756, Level: 100
Activity: 9% Activity: 9% Activity: 9%
 
Join Date: Sat Mar 2007
Location: Home
Posts: 873
Thanks: 49
Thanked 104 Times in 74 Posts
Rep Power: 25
Roya Roy will become famous soon enoughRoya Roy will become famous soon enoughRoya Roy will become famous soon enoughRoya Roy will become famous soon enoughRoya Roy will become famous soon enoughRoya Roy will become famous soon enoughRoya Roy will become famous soon enoughRoya Roy will become famous soon enough
Default Re: Ujenzi wa Barabara ya Sam Nujoma, Dar

Nilishangaa watu kuaminishwa kwamba barabara ya Sam Nujoma ingemalizika kujengwa kwa muda huu.. kazi kwenye ile barabara ni kubwa. Inajumuisha kujenga daraja kazi ambayo ni vigumu kuiarakisha. Muda uliokadiriwa nadhani ulikua sio "realistic".
Tuendelee kusubiri, ila watu waache kukurupuka kusema mambo ya kufurahisha umma lakini hayapo "realistic".
Reply With Quote
  #9  
Old 30th November 2007, 05:52 PM
Idimi Idimi is offline
Idimi a hydropower specialist
JF Senior Expert Member
Points: 580,982, Level: 100 Points: 580,982, Level: 100 Points: 580,982, Level: 100
Activity: 8% Activity: 8% Activity: 8%
 
Join Date: Sun Mar 2007
Location: Bremen
Posts: 1,715
Thanks: 118
Thanked 140 Times in 91 Posts
Rep Power: 27
Idimi will become famous soon enoughIdimi will become famous soon enoughIdimi will become famous soon enoughIdimi will become famous soon enoughIdimi will become famous soon enoughIdimi will become famous soon enoughIdimi will become famous soon enoughIdimi will become famous soon enough
Default Re: Ujenzi wa Barabara ya Sam Nujoma, Dar

We Roy,
Muda wa ujenzi wa barabara uliopangwa na kukubaliwa kati ya mkandarasi na mtoa tenda (mmiliki wa barabara)ulijumuisha ujenzi wa daraja, sasa kama wewe unasema daraja linachukua muda mrefu kukauka na kukamilika, ina maana halikuhesabiwa katika muda wa ukamilifu wa kazi?
Sioni mantiki hapa. Hii ni tiktak kama zilivyo nyingine katika sirikali yetu, hapa lazima mtu awajibike. Nashangaa kipande cha kilometa nne kinachukua miaka kujengwa, hataka kama ni nia nne, kwa nini? Barabara ya kupitia chuo kikuu inayoanzia pale kituo cha mafuta hadi Ubungo maji, kupitia Survey na chuo cha ardhi ilitengenezwa na Konoike kwa muda usiozidi miezi mitano, kwa nini hii ichukue muda mrefu namna hiyo?
Kuna namna hapa.
__________________
Help make the world a better place.
Idimi@jamiiforums.com
Reply With Quote
  #10  
Old 1st December 2007, 08:11 AM
Dotori Dotori is offline
Dotori has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 159,888, Level: 100 Points: 159,888, Level: 100 Points: 159,888, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Sat Nov 2007
Posts: 481
Thanks: 21
Thanked 7 Times in 5 Posts
Rep Power: 23
Dotori will become famous soon enoughDotori will become famous soon enoughDotori will become famous soon enoughDotori will become famous soon enoughDotori will become famous soon enoughDotori will become famous soon enoughDotori will become famous soon enoughDotori will become famous soon enough
Default Re: Ujenzi wa Barabara ya Sam Nujoma, Dar

Bottom line, we are not serious!
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
barabara, nujoma, sam, ujenzi


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Ukabila IKULU, UJENZI, MAMBO YA NJE, MIPANGO, TRA, BoT + OFISI NYETI ZA SERIKALI Samvulachole Jamii Intelligence 1548 24th February 2010 05:46 PM
Barabara ya Morogoro yawa kero kwa watumiaji MziziMkavu Habari na Hoja mchanganyiko 21 27th October 2009 10:30 AM
Wafundisheni CHADEMA balance & separation of powers Kulikoni Jukwaa la Siasa 24 26th June 2009 07:42 PM
Mimi ninadhani Lowasa anakurupuka mno bila ya kufikiria wewe unasemaje? tibwilitibwili Jukwaa la Siasa 24 17th October 2006 09:28 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 08:43 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com