Jamii IntelligenceSerious reports & Discussions on Corruption, Politics etc recommended to our clients! Detailed discussions which you need not to miss
Aliingia madarakani kwa haki bila rushwa wala kununua vyombo vya habari. Alikuwa na hoja na alieleza WAZI nia yake ya kugombea urais.
Alianza kazi kwa kasi hakungoja wiki mbili au zaidi kupanga baraza la mawaziri.
Aliunda serikali ndogo kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Alikuwa na falsafa binafsi, dira na msomi aliyependa kusoma na kujifunza.
Akapambana kijemedari kwelikweli na misukosuko ya Reli, MV Bukoba, Elnino na majanga mengine. Akapunguza mfumuko wa bei toka 48% 1994 na kubakia single digit enzi zote za utawala wake.
Akaboresha utumishi wa umma; kapunguza wafanyakazi hewa na kuboresha maslahi.
Akapunguza deni la nje na kuipa Tanzania heshima.
Akajenga miundo mbinu hususan barabara kwa kasi kubwa
Akavutia wawekezaji wenye tija kama TBL, NBC n.k
Akajenga EPZ alipanga zijengwe 22 nchi nzima
Akaimarisha majeshi yetu kwa kuwapatia motisha vitendea kazi na makazi.
Akajenga Uwanja wa Taifa
Akajenga Benki kuu Twin towers na kule Zanzibar. Twin Towers kama Bank of Canada, Toronto (kwa wanaojua)
Alikuwa na hoja zenye mashiko.
Alikuwa kiongozi kweli jasiri, mwenye kujiamini na hakuogopa mihadhara: iwe ya vyama vya siasa, vyuo vikuu au kimataifa. Alikuwa full of substance.
Ujasiri wake hata vita ingetokea enzi zake angetuongoza vyema sana kumshinda adui.
Hakuwa mwongo katika kauli na ahadi zake.
Alikuwa na maadili na na hekima na aliheshimu mamlaka na taratibu zilizopo.
Akawapa nguvu na haki zaidi wanawake.
Alipigania utandawazi kuwanufaisha wengi.
Alikuwa mchapakazi hakuwa mvivu.
Alikuwa makini na alipinga na kukwepa sana matumizi yasiyo lazima ya serikali.
Alisafiri ng’ambo pale tu ilipobidi. Alikaa ofisini na kufanya kazi.
Alijiheshimu hakuwa Fataki.
Hakuwa ombaomba, bali alipenda kujenga uwezo, kujitegemea na kuwasaidia ombaomba.
Akanunua ndege bora ya Rais, mafisadi wakaipinga.
Akanunua rada ya nguvu, mafisadi wakaipinga.
Alikuwa na vyeti vya nguvu na alifuzu vyema masomo yake. Alionyesha uwezo. Alikuwa na speech za kisomi.
Alihakikisha nchi inakaribia kupaa ndio akaikabidhi kwa JK. Tukadhani itapaa.
Na mengine mengi.
Huyo ndiye Benjamin William Mkapa, Rais ninayemkubali na kumrank second. Angekuwepo mpaka leo Tanzania ingekuwa emerging economy I am sure.
Mnaomsema vibaya mshindwe ka kulegea. Hamna shukrani. Ni kiongozi ambaye wanaokumbuka, tunamshukuru sana.
__________________ 'The rich of the future are those who are rich in mind'. Winston Churchill
Mkapa alifanya kitu ambacho kama tungekuwa tunasapoti juhudi hai na endelevu basi tusingemsahau kwa mambo mazuri aliyoyafanya huyu jamaa.
JK anaonekana kutofanya kitu kwa sababu mapengo yanayohitaji kuonekana kama yamefanywa na kiongozi yalizibwa tayari na Mkapa.
Kinachotushinda saa hizi ni sisi wenyewe hakuna wa kumlaumu, matatizo yote ni sisi wenyewe wala hakuna wakulaumiwa, kwanza tujinyoshee vidole sisi wenyewe, sisi tuna matatizo makubwa ambayo hatutaki kuyakubali
Unajua kuna uwezekano mkubwa sana vizazi vijavyo vikafukua makaburi yetu ili kufanyia uchunguzi mafuvu yetu na kuangalia tulikuwa wapumbavu kiasi gani mpaka mambo yote haya tuliweza kuyaacha tu. KIWIRA Coal Mine na Mkapa ni ndugu moja lakini wabunge wetu wamekaa kimya tu wa hawachukui hatua yoyote ile ya kisheria dhidi ya Mkapa.
__________________ Be not afraid of growing slowly, be afraid only of standing still. -- Chinese Proverb
Aliingia madarakani kwa haki bila rushwa wala kununua vyombo vya habari. Alikuwa na hoja na alieleza WAZI nia yake ya kugombea urais.
Alianza kazi kwa kasi hakungoja wiki mbili au zaidi kupanga baraza la mawaziri.
Aliunda serikali ndogo kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Alikuwa na falsafa binafsi, dira na msomi aliyependa kusoma na kujifunza.
Akapambana kijemedari kwelikweli na misukosuko ya Reli, MV Bukoba, Elnino na majanga mengine. Akapunguza mfumuko wa bei toka 48% 1994 na kubakia single digit enzi zote za utawala wake.
Akaboresha utumishi wa umma; kapunguza wafanyakazi hewa na kuboresha maslahi.
Akapunguza deni la nje na kuipa Tanzania heshima.
Akajenga miundo mbinu hususan barabara kwa kasi kubwa
Akavutia wawekezaji wenye tija kama TBL, NBC n.k
Akajenga EPZ alipanga zijengwe 22 nchi nzima
Akaimarisha majeshi yetu kwa kuwapatia motisha vitendea kazi na makazi.
Akajenga Uwanja wa Taifa
Akajenga Benki kuu Twin towers na kule Zanzibar. Twin Towers kama Bank of Canada, Toronto (kwa wanaojua)
Alikuwa na hoja zenye mashiko.
Alikuwa kiongozi kweli jasiri, mwenye kujiamini na hakuogopa mihadhara: iwe ya vyama vya siasa, vyuo vikuu au kimataifa. Alikuwa full of substance.
Ujasiri wake hata vita ingetokea enzi zake angetuongoza vyema sana kumshinda adui.
Hakuwa mwongo katika kauli na ahadi zake.
Alikuwa na maadili na na hekima na aliheshimu mamlaka na taratibu zilizopo.
Akawapa nguvu na haki zaidi wanawake.
Alipigania utandawazi kuwanufaisha wengi.
Alikuwa mchapakazi hakuwa mvivu.
Alikuwa makini na alipinga na kukwepa sana matumizi yasiyo lazima ya serikali.
Alisafiri ng’ambo pale tu ilipobidi. Alikaa ofisini na kufanya kazi.
Alijiheshimu hakuwa Fataki.
Hakuwa ombaomba, bali alipenda kujenga uwezo, kujitegemea na kuwasaidia ombaomba.
Akanunua ndege bora ya Rais, mafisadi wakaipinga.
Akanunua rada ya nguvu, mafisadi wakaipinga.
Alikuwa na vyeti vya nguvu na alifuzu vyema masomo yake. Alionyesha uwezo. Alikuwa na speech za kisomi.
Alihakikisha nchi inakaribia kupaa ndio akaikabidhi kwa JK. Tukadhani itapaa.
Na mengine mengi.
Huyo ndiye Benjamin William Mkapa, Rais ninayemkubali na kumrank second. Angekuwepo mpaka leo Tanzania ingekuwa emerging economy I am sure.
Mnaomsema vibaya mshindwe ka kulegea. Hamna shukrani. Ni kiongozi ambaye wanaokumbuka, tunamshukuru sana.
mkapa ni stainles steel spoon...haipati kutu ikichafuliwa unaosha ..then twende kazi...kila siku tunatumia na kuichafua lakini inasafishika!!!
wanaompinga mkapa walikuwa na ajenda ya siri ...na walifikiri kazi ya kuongoza nchi ni rahisi...wamegundaa kuwa hafunikiki kwa hila wanaaza kujikomba kwake...tunawajuwa..na kila kitu kinajulikana ....MUNGU ANAMSIMAMIA!!!...hapo ieleweke wazi kuwa mkapa pia si malaika ni mtu ..anayo makosa na alikiri alipoaga...lakini asilani hastahili kusutwa na wajinga wasiojuwa kazi zaidi ya kuongea....ukitaka kumsuta mkapa fanya kazi zaidi yake .....msute kwa kujenga uchumi na miundombinu na maendeleo kwa ujumla .....zaidi ya hapo ni mikingamo isiyokwisha....ukweli utasimama!!...
HONGERA MKAPA ..TUPO NYUMA YAKO WENGI KAMA PISHI LA MCHELE!!!
Alimkabidi mkewe mama Mkapa aka first lady funguo za ikulu yetu akawaenzi akina Maro, akutuibia kwa kutumia mifuko ya kiserilikali, akawapa nduguze tender za kiwizi, akajenga majumba ya kifahari kwa kodi zetu.
umenikumbusha ile kampuni ya S.Africa iliyokuwa inaendesha TANESCO ambapo Maro anasadikiwa kuwa Mkurugenzi. E Bana e
Alikuwa ana uwezo wa kufikiria na kurusha makombora kwa wapinzani wake kuwa wana wivu wa Kike, Japo Mkapa alikuwa kiongozi mzuri ana mapungufu yake na haya matatizo yote yanamtoa kuwa Kiongozi hodari na kuwa kiongozi mla rushwa na ufisadi, madudu yote
1 Anben, fonisick, Bank M, Meremeta, EPA, Kuuza nyumba za Serikali, na Madudu mengine kibao ndio yanamtoa Mkapa katika ulingo wa Siasa,
Jamani WanaJF, Hivi wakati ule walitoa watu walikuwa wanamsifu Mkapa kuwa Kiongozi safi mara baada ya kutoka haohao wanaanza kusema kuwa alikuwa Mla Rushwa mkubwa?? Najua hata Mzee mzima wa Kaya JK atakapotoka Madarakani watakuja kusema alikuwa mla rushwa kwasababu serikali katika kipindi hicho iliangushwa na ufisadi wa Richmond, Sisi tunataka watoke sasa na sio Kesho. tuache kuwa Wanafiki kiasi hicho katika siasa zetu
Tatizo la nchi hii hakuna hata kiongozi mmoja mwenye vision. Hakuna ambaye anawaza kwenye akili yake tunataka kujenga Tanzania ya namna gani! Hakuna kiongozi ambaye anafikiria Nitaifanyia nini nchi yangu!! Wanachofikiria ni nini nitapata katika muda nitakaokuwa madarakani!!
Hivyo kampeni za sasa za kujaribu kufunika mabaya yake zinazofanywa na watawala ni njia ya wao vile vile kufunika mabaya yao ili ionekane ni utaratibu wa kawaida na halali kuiibia nchi wakati ukiwa madarakani!!!
Jamani WanaJF, Hivi wakati ule walitoa watu walikuwa wanamsifu Mkapa kuwa Kiongozi safi mara baada ya kutoka haohao wanaanza kusema kuwa alikuwa Mla Rushwa mkubwa?? Najua hata Mzee mzima wa Kaya JK atakapotoka Madarakani watakuja kusema alikuwa mla rushwa kwasababu serikali katika kipindi hicho iliangushwa na ufisadi wa Richmond, Sisi tunataka watoke sasa na sio Kesho. tuache kuwa Wanafiki kiasi hicho katika siasa zetu
If you win a hundred times people will keep showering prise on you. If you loose once the same people will forget they ever know you
Wengi wetu tuna mtupia Mkapa lawama nyingi mno,ni kweli amefanya mengi mazuri sana ya kukumbukwa,na amefanya mengi ambayo sasa ndio tunaona hadhari zake.kwangu binafsi naona Mkapa ni rais ambae ametutoa kwenye hali mbaya ya umaskini na kutufikisha hapa tulipo sasa.Mkapa uwezi kumlinganisha na JK.Jamani tusiwe wachoyo wa fadhila,tuangalie ni uhuzo alioufanya mkapa kwenye kipindi chake cha miaka kumi,na tuangalie uhozo uliofanyika kwa kipindi cha miaka 4 ya JK.Hapo ndipo utakapo pata jibu sahihi.
__________________ Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki,na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.
Pamoja na matatizo yote ya Mkapa, kuna mtu anaweza kutupa walau mambo 10 tu ambayo rais wetu mpendwa JK amelifanyia taifa hili tunapoelekea kufikisha mwaka wa tano?
Binafsi nasema JK is a failure compared to Mkapa. Hata kina Mpendazoe ambao Phillemon Mikael anawakandia wanatumiwa na JK kumwandama Mkapa ili kuficha mapungufu ya JK.
Nipende au nichukie lakini binafsi sifurahishwi na utendaji wa serikali ya JK ambayo ilikuwa inatafuta namna zote za kumpunguza Magufuli lakini Mungu wa Israel na Mungu wa Yakobo bado anamsimamia mtumishi wake Pombe Magufuli.