TiGo Maps
    Show/Hide This

    Topic: Tamko la Rostam dhidi ya Mengi na yatokanayo

    Report Post
    Page 1 of 41 12311 ... LastLast
    Results 1 to 30 of 1227
    1. #1
      Companero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2008
      Posts : 3,698
      Rep Power : 1266
      Likes Received
      449
      Likes Given
      501

      Exclamation Tamko la Rostam dhidi ya Mengi na yatokanayo

      Mbunge wa Igunga na Mweka hazina wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rostam Aziz, hatimaye amejibu rasmi madai mazito yaliyotolewa na Reginald Mengi kuhusu "mafisadi papa". Tamko hilo rasmi linapatikana katika ukurasa wa 6 wa gazeti la 'The Citizen' la leo Alhamisi, tarehe 30 Aprili 2009. Wakati tunamsubiri nakala yake tupate dondoo hii kutoka kwenye hitimisho la tamko hilo:

      "I am therefore calling upon Mr. Mengi to either surrender whatever evidence he has to support his wild accusations and to appoint the appropriate legal bodies or state organs to act accordingly. Alternatively he is it to apologize to me personally within 48 hours, failing all of which, I reserve the right to exercise any appropriate actions in order to expose his wrongdoings"

      Wakati huo huo gazeti hilo linaripoti kuwa mfanyabiashara maarufu, Yusuf Manji, yeye ameshachukua hatua ya kufungua kesi dhidi ya Reginald Mengi ambapo anadai fidia. Maswali ya msingi ya kujiuliza ni : Je, katika mpambano huu ile methali ya "wapiganapo tembo nyasi huumia" itatimia au nyasi ndio zitapata fursa ya kustawi zaidi? Je, mpambano huu utaishia kuwa mchezo wa kuigiza au utazitimizia hizo nyasi methali ya "avumaye baharini papa kumbe wengi wapo"?

      TAMKO LAKE HILI HAPA:


      Last edited by Invisible; 30th April 2009 at 11:36. Reason: Enclosed the doc
      "Each generation must, out of relative obscurity, discover its mission, fulfil it, or betray it"/Kila kizazi, katika utata wa kipindi chake, lazima kiutambue wajibu wake na kiutekeleze au kiusaliti - Frantz Fanon


    2. #2
      Burn's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 3rd December 2008
      Posts : 1,520
      Rep Power : 0
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Quote By Companero View Post
      . Alternatively he is it to apologize to me personally within 48 hours, failing all of which, I reserve the right to exercise any appropriate actions in order to expose his wrongdoings
      Appropriate Actions according to who? MAFIOSO

    3. #3
      Kikojozi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2009
      Posts : 338
      Rep Power : 532
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      RA, kafungue kesi haraka ili tujue ukweli. Go for the bait.
      "A failure is a man who has blundered, but is not able to cash in on the experience." - Elbert Hubbard

    4. #4
      Dina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th September 2008
      Location : Ulimwenguni
      Posts : 511
      Rep Power : 594
      Likes Received
      60
      Likes Given
      17

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Mmh something doesn't click, '...any appropriate actions in order to expose his wrongdoings...' Kwa hiyo malengo siyo kusafishiwa jina bali yanaenda mbele zaidi kuibua na yeye yale yote ayajuayo kuhusu mzee Mengi! Hapa naona ni biashara ya ntaje nkutaje (umemwaga mboga nami namwaga ugali).

      I wish Mzee Mengi awe na bulungutu la ushahidi, aumwage..hapo ndio movie itakuwa worth kutazamika....

    5. #5
      Mpendanchi-2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th April 2009
      Posts : 308
      Rep Power : 525
      Likes Received
      16
      Likes Given
      9

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Kwanza wamechelewa kupeleka hata huko mahakamani, mbona Mengi mpiganaji aliwambia wapeleke siku ileile!!! Wanatafuta njia ya kujiosha lakini waangalie mtu mzima hawezi kusema kitu hovyohovyo tu, anajua anachosema na wasije wakaoga maji machafu bila kutegemea!!
      No one will help to build your Future Tanzania !!!! It's you and me , START NOW !!!

    6. #6
      Ochu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th May 2008
      Posts : 950
      Rep Power : 701
      Likes Received
      18
      Likes Given
      9

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      kwa nini huyu bwana ni muoga sana kuongea hadharani? si bungeni au mbele ya waandishi wa habari....aliongea mara moja tu ile ya mtikila kwa vile alikuwa na ushahidi!!!!!

    7. #7
      Mpita Njia's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 5,535
      Rep Power : 2970
      Likes Received
      451
      Likes Given
      320

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Nilichokibaini kwa upande mwingine ni kuwa, kama ukisoma katikati ya mistari hiyo statement ya RA, anamtukana Mengi matusi mabaya sana
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    8. #8
      The Invincible's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 6th May 2006
      Location : Online
      Posts : 1,597
      Rep Power : 935
      Likes Received
      39
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Naona magazeti mengi ya leo yana hilo tamko la Rostam kwenda kwa Mengi....kichwa chake kwa kiswahili chasema:

      "POROJO ZA MENGI"

      Mmmmhhhhhhh! Naongeza stock yangu ya ze laga.
      Watanzania mbumbumbu wamemchagua raisi dhaifu ajenge taifa la watu wasiojiamini, 2010/2015 - Tafakari

    9. #9
      kinepi_nepi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th August 2007
      Posts : 818
      Rep Power : 720
      Likes Received
      147
      Likes Given
      84

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Nimechoka na kelele nataka vitendo.
      "Power never takes a back step only in the face of more power. Nobody can give you freedom, equality or justice or anything. If you're a man, you take it."

    10. #10
      ByaseL's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 1,592
      Rep Power : 853
      Likes Received
      45
      Likes Given
      1

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Jana asubui nilifanikiwa kuona interview TBC1 ya Waziri Sophia Simba kuhusu sakata la Mengi na wale aliowaita mafisadi papa. Mambo aliongelea kama waziri ndio msimamo wa serikali. Binafsi naona msimamo huo wa serikali una kasoro.

      1) Kama serikali ilitaka kutoa tamko ingemtafuta waziri ambaye ni "eloquent" wa kuweza kuzungumzia swala nyeti kama hili la ufisadi. With due respect kwa Mheshimiwa Simba alijigonga gonga kuhusu maswali aliyokuwa anaulizwa. Majibu yake hayakuwa "factual" enough na hivyo kuoneka anapwaya! Kwa mfano mdogo, Marin Hassan alimuuliza dhana ya kutengenisha baishara na siasa na yeye akajibu kwamba katika wale watuhumiwa watano hakuna mwana siasa hata mmoja! Duinia nzima inajua kwamba Mhe. Rostam Aziz ni mbunge wa Igunga na mjumbe wa kamati Kuu ya CCM na alikuwa Mweka Hazina wa CCM. Juzi Mama Simba amenukuliwa kwenye gazeti akisema kwamba Kamati ya Maadili ya Viongozi haipaswi kujishugulisha pesa za viongozi zilizoko nje ya nchi! My foot!! Maoni yangu ni kwamba serikali ikiachia watu kama waziri Simba kuelezea msimamo wake katika mambo nyeti kama hili tunaweza tukaishia kama swala la Zitto Kabwe na Buzwagi. That issue was mishandled by the government at a high political cost.

      2) Historia inatukumbusha kwamba mwaka juzi wakati swala la EPA lilipoibuka kwenye mtandao na Dr. Slaa kulileta Bungeni, Waziri Meghji (akiwa waziri-Fedha) na Spika walimbeza (skepticism) wakisema hakuna ushaidi na hayo ni mambo ya mitandao. Waingereza wanasema " It came to pass". Leo hii kesi za EPA zinanguruma mahakamani na waziri Meghji sio waziri tena!

      3) Katika nchi yetu sio mara ya kwanza kutaja wazi wazi majina ya watuhumiwa wa ufisadi. Septemba 2007 Dr. Slaa na wenzake walitaja majina kumi ya watuhumiwa wa ufisadi pale MwembeYanga, Temeke. Baadhi yao walicharuka na kutishia kwenda mahakamani kwa kuchafuliwa na wengine wakasema hakuna ushaidi. Mpaka leo hakuna hata kesi moja ilifunguliwa mahakamani kwa "uzushi" huu! Leo hii Mhe. Lowassa, Karamagi na Chenge wako nje ya Baraza la Mawaziri kwa tuhuma kama walizosema kina Dr, Slaa. Mhe, Mramba, Yona na Mgonja wako mahakamani kwa tuhuma kama hizo. Rais mstaaafu Ben Mkapa halali usingiz mzurii kwa kutuhumiwa na umma kwa kutumia madaraka vibaya. Kinachoshangaza wakati wote huu sijaona serikali ikitoa msimamo wake mkali (kama Mama Simba) kuhusu watuhumiwa wa Dr. Slaa. Kulikoni sasa waziri anakuja mbogo kwa kutajwa mafisadi watano tu? Labda kwa kuwa limeongezeka neno " papa"? Mbona serikali haijatoa tamko kuhusu kutuhumiwa Rais mstaafu?

      4) Mhe. Rostam Aziz amekuwa akitajwa tajwa katika haya mambo ya ovyo. It is not by coincedence, I believe. Alitajwa Mwenbeyanga, anatajwa katika wizi wa EPA, alitajwa na Tume ya Mwakyembe kuhusu Richmond na Dowans na sasa anatuhumiwa na Mengi kuwa ni fisadi "papa" . Huyu ni sawa na "Yuda Iscariot" kwa kuisaliti CCM hapaswi kula meza moja na viongozi wetu labda kama nao ni "birds of the same feathers"? Kwa nini asitolewe kamati kuu CCM hadi hatakapojitakasa? Bila hivyo maswali yataulizwa tu. Wakubwa wapende wasipende.

      5) Tanil Somaiya amefadhili uchaguzi wa juzi wa UV-CCM kwa "mchango" wa shs. 400 milioni. Je waziri Simba hakuona kwamba kwa utetezi wake kwa hawa watuhumiwa kunaweza kukatafusiriwa kwamba serikali ya CCM inalipa fadhila? Je wananchi wakisema CCM imetekwa na matajiri kuna wakubisha?

      6) Mama Simba anasema Mengi kama ana ushahidi aupeleke kwenye vyombo husika hususan TAKUKURU. Tunauliza TAKUKURU ipi? Hii inayoongozwa na Hosea? Kuna azimio la Bunge kuhusu kiongozi huyu kwa kuboronga uchunguzi wa ufisadi Richmond. Mengi kama mtu mwelevu hawezi kupeleka kesi ya nyani kwa ngedere. Na hata wananchi hawana imani na Polisi katika mambo haya. Kama imani ingekuwepo serikali hii isengeitisha kura za maoni kutafuta wauaji wa Maalbino. Watu wangewataja watuhumiwa kwa jeshi la polisi na Polisi wangeisha maliza tatizo hili. Iko wapi ile orodha ya wauza unga aliyotuaaidi Mhe. Mwapachu akiwa waziri wa Usalama wa Taifa?

      7) Sio mara ya kwanza wala haitakuwa ya mwisho kwa Mengi kuzozana hadharani na wafanya biashara wenzake. Walikwaruzana na Yusuf Manji mpaka wakafikishana mahakamani. Mengi alizozana na Rostam kuhusu Rostam kuzindua album katika kanisa moja la Kiluteri mpaka (tunaambiwa) mchungaji akachukuliwa hatua. Hakuna jipya na sisi hatuoni kwa nini serikali inaigilia mzozo huu. Kuna sheria zinazohusu kafsha na kama waliotajwa na Mengi wanafikiri wameonewa Mengi kwa kauli yake atafurahi kukutana nao. Manji ameshatinga mahakani ni Rostam aende huko. Why is the minister poking her nose in the affairs that do not concern her? Ana kihele hele. Kwa hili yeye ndie KACHEMSHA na aambiwe hivyo.

      8) Swala la Ubaguzi wa rangi halina mashiko. Hatuwezi kuogopa kutajana na kusutana eti tutaambiwa ni wabaguzi. Kama Wahaya kumi ni wezi wa mali ya Umma nawatajwe. Mbona wachaga wanasemwa kwa kujazana TRA kwa misingi ya Ukabila na hawajalalama? Lipumba na wenzake walikuwa wapi wakati Salum Mohamed Salum akibaguliwa wazi wazi wakati wa mchakato wa Urais ndani ya CCM 2005 na hakuna aliyenyosha kidole? Rostam should not hide behind racism veil to justify his misdeeds.

      Nimalizie kwa kutoa mfano wa Biblia. Yesu alipowasema sana mafarisayo, mazudakayo na wakuu wa dini ya kiyahudi walipanga njama ya kumuua. Na katika kuhalilisha kifo chake Kuhani Mkuu wa wakati ule jina lake Keyafa aliwashauri kwamba " inabidi mtu mmoja afe kwa ajili ya wengi". Baadhi ya magazeti yamesema Mengi kwa kufanya alichofanya anajitoa mhanga. Inawezekana lile neno likatimia. Hatuwezi kuendelea na uoza huu katika nchi yetu. Tanzania bila Ufisadi inawezekana.

    11. #11
      Invisible's Avatar
      Robot Array
      Join Date : 11th February 2006
      Location : Here...!
      Posts : 8,759
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      2877
      Likes Given
      1892

      Default

      Nimeliambatanisha hapa tamko la Rostam (nimeliweke kwenye 1st post pia):


      Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako!
      24/7 Email SUPPORT: support@jamiiforums.com



    12. #12
      Exaud Minja's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th March 2009
      Posts : 82
      Rep Power : 483
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Chukua kumi byasel umenikuna sana hapo.

      Asante sana kweli Tanzania bila Ufisadi inawezekana.

    13. #13
      Bill's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Posts : 1,357
      Rep Power : 813
      Likes Received
      145
      Likes Given
      57

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Hii inafurahisha sana, huyu jamaa anaposema ana reserve right ya kutaja maovu ya Mengi anataka kutufikishia ujumbe gani? Huku ndo kupiga mbizi ukiwa umeshika kwenye kingo. Teheee!!!!

    14. #14
      Gagnija's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th April 2006
      Posts : 1,080
      Rep Power : 833
      Likes Received
      213
      Likes Given
      92

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Kauli ya Rostam baada ya press conference ya Mengi ilikuwa kwamba kiumri, Mengi ni sawa na mzazi wa Rostam, hivyo isingekuwa busara kujibizana naye. Ni washauri gani waliombadilisha huyu hadi kutoa tamko hilo?
      If you are neutral in situations of injustice, you have chosen the side of the oppressor. Tutu



    15. #15
      Skills4Ever's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 2,463
      Rep Power : 1077
      Likes Received
      122
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Labda umri umepungua sasa....baada ya maji kuwa shingoni.
      "No matter how far down the wrong road you've gone,TURN BACK"

    16. #16
      TIMING's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 18,658
      Rep Power : 4797
      Likes Received
      5195
      Likes Given
      5895

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Quote By bill View Post
      Hii inafurahisha sana, huyu jamaa anaposema ana reserve right ya kutaja maovu ya Mengi anataka kutufikishia ujumbe gani? Huku ndo kupiga mbizi ukiwa umeshika kwenye kingo. Teheee!!!!
      Kweli hii kali; Sijui hizo rights alipata wapi hakimiliki yake inawezekana hata cosota kawekeza na kuchukua haki zote

      Truely, his statements seems to be cautious and it looks like he is already scared

      Duh!!!
      ..... Just a thought!!

    17. #17
      Future-Tanzania's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2008
      Posts : 331
      Rep Power : 546
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Quote By Gagnija View Post
      Kauli ya Rostam baada ya press conference ya Mengi ilikuwa kwamba kiumri, Mengi ni sawa na mzazi wa Rostam, hivyo isingekuwa busara kujibizana naye. Ni washauri gani waliombadilisha huyu hadi kutoa tamko hilo?
      Ndugu yangu haya mambo ya umri tuyaweke pembeni. Tanzania tumekaa miaka mingi tukifikiria umri mkubwa ndio busara na njia ya kukomboa nchi and what we got from those old people ni baraha tupu.

      Simtetei RA ila anahaki ya kujitetea bila kuangalia umri, umri is nothing coming to ufisadi au biashara. Ila huyu RA ajiangalie asitegemee watanzania tutanunua huu utetezi usio na miguu wala mikono.

    18. #18
      Dilunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th April 2009
      Posts : 683
      Rep Power : 599
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Rostam nae anachemka. Anasema kama Mengi ana ushahidi basi Mengi ateue chombo cha kisheria au cha serikali kichukue hatua zinazotakiwa. Mengi kawa Director of Public Prosecution? duuu

      Halafu Rostam anasema mtu anae toa opinion kwa kesi ambayo iko mahakamani basi hiyo kisheria ni contempt of court. Rostam anahitaji msaada wa wakili, awali ya yote, kama kaandika mwenyewe hivi vitu.

      Ila Mengi ane alichemka kurudia rudia wimbo wa Manji na Patel, na Mithun Chakraborty na Shashi Kapoor... anauimba toka the 1990s.
      Last edited by Dilunga; 30th April 2009 at 12:17.

    19. #19
      Nkamangi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : No man's land
      Posts : 644
      Rep Power : 647
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Mwanasheria wa Mengi ni nani?

    20. #20
      LazyDog's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2008
      Posts : 2,182
      Rep Power : 20968
      Likes Received
      8
      Likes Given
      23

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Quote By Companero View Post
      Mbunge wa Igunga na Mweka hazina wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rostam Aziz, hatimaye amejibu rasmi madai mazito yaliyotolewa na Reginald Mengi kuhusu "mafisadi papa". Tamko hilo rasmi linapatikana katika ukurasa wa 6 wa gazeti la 'The Citizen' la leo Alhamisi, tarehe 30 Aprili 2009. Wakati tunamsubiri nakala yake tupate dondoo hii kutoka kwenye hitimisho la tamko hilo:

      "I am therefore calling upon Mr. Mengi to either surrender whatever evidence he has to support his wild accusations and to appoint the appropriate legal bodies or state organs to act accordingly. Alternatively he is it to apologize to me personally within 48 hours, failing all of which, I reserve the right to exercise any appropriate actions in order to expose his wrongdoings"
      LOL
      Bwa ha-ha-ha-ha-hah, Bwa ha-ha-ha-ha-hah!


      Mbavu sina!

      Attached Thumbnails Attached Thumbnails Click image for larger version. 

Name:	mbavu sina.PNG 
Views:	176 
Size:	13.8 KB 
ID:	4458  
      A person who won't read has no advantage over one who can't read. -Mark Twain

    21. #21
      wajinga's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th June 2008
      Posts : 152
      Rep Power : 534
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      In other words in 48 hrs Mengi and the like will be dead or what????? This justify Mengis paranoia that they want to kill me.It will be Rostam wants to kill me. How fablous. Thats why the whole government is afraid of him????? Blackmailing them and if it wont work he will kill them eh.

    22. #22
      Steve Dii's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 25th June 2007
      Location : Kihesa - Iringa
      Posts : 6,571
      Rep Power : 3087
      Likes Received
      701
      Likes Given
      2065

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      "I am therefore calling upon Mr. Mengi to either surrender whatever evidence he has to support his wild accusations and to appoint the appropriate legal bodies or state organs to act accordingly. Alternatively he is it to apologize to me personally within 48 hours, failing all of which, I reserve the right to exercise any appropriate actions in order to expose his wrongdoings"
      Inakuwaje hii nchi inakuwa na viongozi wanaojua kuwa kuna mtu ana maouvu lakini hawasemi au kuwafikisha waovu hao mbele ya sheria? Statement kama hii inatosha kabisa kumwondoa mtu katika uongozi. Hafai kuwa kiongozi wa Watanzania.

      Kama anajua maovu ya Mengi, angelikuwa mstari wa mbele kuyapeleka kwenye vyombo vya sheria yashughulikiwe na siyo asubirie maovu yake yatajwe ndiyo naye aseme "mbona huyu naye ana maovu."

      Hadi Amir Jeshi Mkuu naye ana style hii hii ya kuwa na orodha za wauza unga na watoa rushwa.... Kama wanajua maovu kwanini wasiyapeleke kwenye vyombo vya sheria mara moja? Wanasubiria aina gani ya mabaya yatokee ndiyo hayo maovu tuyajue?

      What a bunch of disgraced leaders! Shame.



      Jamii ijuayo uwiano thabiti kati ya dharau, ubinafsi, chuki na ustaarab dhidi ya jamii nyingine na baina ya watu wake ni jamii yenye maendeleo. Isiyojua ni dumazi. SD1-09.

      Fikra ni nyenzo endelezi au potofu. Changamoto tuliyonayo ni kuchanganua na kutenganisha kati ya fikra endelevu na fikra potofu, kwani mwisho wa fikra ni matendo pale fikra hazibakii kuwa fikra. SD6-07Rev.2-09.



    23. #23
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,304
      Rep Power : 1153
      Likes Received
      262
      Likes Given
      82

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      "I am therefore calling upon Mr. Mengi to either surrender whatever evidence he has to support his wild accusations and to appoint the appropriate legal bodies or state organs to act accordingly."
      Mengi alishasema kwamba kama itawachoma wao waende mahakamani na hapo ndipo atakapotoa huo ushahidi, sasa tunashangaa huyu mbwana anasema anaonewa na anataka Mwengi hampe ushahidi, inaelekea huyu bwama upeo wake wa kuelewa mambo yaliyo nje ya Ufisadi ni mdogo sana, kama kweli kaonewa na anataka kuprove kwa wananchi kuwa kaonewa basi aende mahakamani hapo ndipo tutakapomwana mengi kama ni uzushi au ni mambo ya kweli

    24. #24
      Nsesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2008
      Posts : 298
      Rep Power : 546
      Likes Received
      18
      Likes Given
      23

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Hapa jamaa kachemsha na inaonekana hata washauri wake ni wavivu wa kufikiri kwani aya ya mwisho inamuonyesha kuchanganyikiwa hivyo kujaribu kumtisha Mengi kuona kama kweli atamuomba radhi ili iwe njia ya kujisafisha. Heri angekaa kimya, maisha magumu!

    25. #25
      Dark City's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 18th October 2008
      Location : Roaming
      Posts : 7,797
      Rep Power : 2146
      Likes Received
      2851
      Likes Given
      5291

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Quote By Nsesi View Post
      Hapa jamaa kachemsha na inaonekana hata washauri wake ni wavivu wa kufikiri kwani aya ya mwisho inamuonyesha kuchanganyikiwa hivyo kujaribu kumtisha Mengi kuona kama kweli atamuomba radhi ili iwe njia ya kujisafisha. Heri angekaa kimya, maisha magumu!

      Huyu jamaa naona anataka waanze kucheza kidali po! Nani atalala nacho? Kwa hiyo naye atamtuhumu Mengi ili Mengi ndiye aende mahakamani. Hii ngwe bado sana! Ila kama serikali ingekuwepo sasa tungepata mapapa 6 badala ya 5. Mengi alitaja 5 na RA anamwongeza Mengi wenye orodha. Serikali iko wapi jamani? Orodha hiyo tayari inatosha, kwa nini hatuanzi kazi?

    26. #26
      Field Marshall ES's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 27th April 2006
      Posts : 13,392
      Rep Power : 3739
      Likes Received
      228
      Likes Given
      167

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      - Rostam Aziz, mbunge na mjumbe wa CC aliyeapa kulinda taifa, siku zote hizi anafahamu kwamba Mengi kama raia na mfanyabiashara amekwua akivunja sheria za jamhuri ambazo yeye kama mbunge ameapa kuzilinda kwa nguvu zake zote lakini ameshindwa, sasa anangojea nini kujiuzulu?

      - Kwa nini anatishia nyau, badala ya ku-deal straight with the ishu ya Mengi kwamba yeye ni fisadi? Wananchi tunataka ukweli nothing but the truth bila kujali sura ya mtu hapa, wala rangi hii ishu haina siasa ila ni ufisadi tu, nani ni fisadi na nani siye!

      - Wananchi wa Tanzania tumechoshwa na Ze-Comedy, sasa ukweli uwekwe wazi, Rostam aende kwenye sheria aseme ya kwake na Mengi ajibu, tusije tena kusikia busara za Spika.

      Siasa zisiingizwe kwenye hii ishu ambayo ni 100% legal, na wananchi tusiyumbishwe hapa kwa kuweka mayai yetu yote kwenye kikapu kimoja, tunachotaka ni ukweli bila ya kujali sura ya mtu, Mengi alianza kwa maneno, Rostam amejibu kwa maneno na vitisho, sasa next step iwe kwenye sheria! Kwa sababu Rostam ndiye aliyeanza kulilia sheria, sasa ni wakati wa yeye kuwahi Kisutu! Ingawa record yake hapa inamsuta sana maana kwa kawaida yake angeshausema wazi ukweli alinao mbona kwenye Mtikila hakudai kuombwa radhi na kutishia sheria this time ana ushahidi dhidi ya Mengi lakini anataka radhi kwanza?

      Something is not right!

      FMES

    27. #27
      Ndahani's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 5,363
      Rep Power : 1579
      Likes Received
      997
      Likes Given
      1667

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Watu wameanza kutapatapa. Msaada wa utawala bora unahitajika haraka kunusuru mifadhaiko

    28. #28
      Steve Dii's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 25th June 2007
      Location : Kihesa - Iringa
      Posts : 6,571
      Rep Power : 3087
      Likes Received
      701
      Likes Given
      2065

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      From that signed statement, the guy is everything but SMART!



      Jamii ijuayo uwiano thabiti kati ya dharau, ubinafsi, chuki na ustaarab dhidi ya jamii nyingine na baina ya watu wake ni jamii yenye maendeleo. Isiyojua ni dumazi. SD1-09.

      Fikra ni nyenzo endelezi au potofu. Changamoto tuliyonayo ni kuchanganua na kutenganisha kati ya fikra endelevu na fikra potofu, kwani mwisho wa fikra ni matendo pale fikra hazibakii kuwa fikra. SD6-07Rev.2-09.



    29. #29
      Halisi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th January 2007
      Posts : 2,953
      Rep Power : 1184
      Likes Received
      327
      Likes Given
      165

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Kama sikosei Pinda kaweka sawa mambo bungeni katika maswali ya papo kwa papo!!!???

    30. #30
      Field Marshall ES's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 27th April 2006
      Posts : 13,392
      Rep Power : 3739
      Likes Received
      228
      Likes Given
      167

      Default Re: Rostam Aziz Ajibu Mapigo - Atoa Tamko Rasmi

      Quote By SteveD View Post
      From that signed statement, the guy is everything but SMART!
      - Mkuu Steve, Smart? with all due respect not really ila kwa sababu ni Tanzania tu!

      FMES

    Page 1 of 41 12311 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Yatokanayo na Kamati Kuu ya CHADEMA-Tamko Rasmi la Chama
      By Regia Mtema in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 115
      Last Post: 21st March 2011, 15:47
    2. Rostam vs Mengi
      By Nyani Ngabu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 30th July 2009, 19:37
    3. Tamko la Serikali dhidi ya Mengi na Rostam
      By mnozya in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 52
      Last Post: 12th May 2009, 11:10

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...