Jamii IntelligenceSerious reports & Discussions on Corruption, Politics etc recommended to our clients! Detailed discussions which you need not to miss
Mbunge wa Igunga na Mweka hazina wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rostam Aziz, hatimaye amejibu rasmi madai mazito yaliyotolewa na Reginald Mengi kuhusu "mafisadi papa". Tamko hilo rasmi linapatikana katika ukurasa wa 6 wa gazeti la 'The Citizen' la leo Alhamisi, tarehe 30 Aprili 2009. Wakati tunamsubiri nakala yake tupate dondoo hii kutoka kwenye hitimisho la tamko hilo:
"I am therefore calling upon Mr. Mengi to either surrender whatever evidence he has to support his wild accusations and to appoint the appropriate legal bodies or state organs to act accordingly. Alternatively he is it to apologize to me personally within 48 hours, failing all of which, I reserve the right to exercise any appropriate actions in order to expose his wrongdoings"
Wakati huo huo gazeti hilo linaripoti kuwa mfanyabiashara maarufu, Yusuf Manji, yeye ameshachukua hatua ya kufungua kesi dhidi ya Reginald Mengi ambapo anadai fidia. Maswali ya msingi ya kujiuliza ni : Je, katika mpambano huu ile methali ya "wapiganapo tembo nyasi huumia" itatimia au nyasi ndio zitapata fursa ya kustawi zaidi? Je, mpambano huu utaishia kuwa mchezo wa kuigiza au utazitimizia hizo nyasi methali ya "avumaye baharini papa kumbe wengi wapo"?
TAMKO LAKE HILI HAPA:
__________________
"Each generation must, out of relative obscurity, discover its mission, fulfil it, or betray it"/Kila kizazi, katika utata wa kipindi chake, lazima kiutambue wajibu wake na kiutekeleze au kiusaliti - Frantz Fanon
Last edited by Invisible; 30th April 2009 at 11:36 AM..
Reason: Enclosed the doc
In other words in 48 hrs Mengi and the like will be dead or what????? This justify Mengis paranoia that they want to kill me.It will be Rostam wants to kill me. How fablous. Thats why the whole government is afraid of him????? Blackmailing them and if it wont work he will kill them eh.
"I am therefore calling upon Mr. Mengi to either surrender whatever evidence he has to support his wild accusations and to appoint the appropriate legal bodies or state organs to act accordingly. Alternatively he is it to apologize to me personally within 48 hours, failing all of which, I reserve the right to exercise any appropriate actions in order to expose his wrongdoings"
Inakuwaje hii nchi inakuwa na viongozi wanaojua kuwa kuna mtu ana maouvu lakini hawasemi au kuwafikisha waovu hao mbele ya sheria? Statement kama hii inatosha kabisa kumwondoa mtu katika uongozi. Hafai kuwa kiongozi wa Watanzania.
Kama anajua maovu ya Mengi, angelikuwa mstari wa mbele kuyapeleka kwenye vyombo vya sheria yashughulikiwe na siyo asubirie maovu yake yatajwe ndiyo naye aseme "mbona huyu naye ana maovu."
Hadi Amir Jeshi Mkuu naye ana style hii hii ya kuwa na orodha za wauza unga na watoa rushwa.... Kama wanajua maovu kwanini wasiyapeleke kwenye vyombo vya sheria mara moja? Wanasubiria aina gani ya mabaya yatokee ndiyo hayo maovu tuyajue?
What a bunch of disgraced leaders! Shame.
__________________
Jamii ijuayo uwiano thabiti kati ya dharau, ubinafsi, chuki na ustaarab dhidi ya jamii nyingine na baina ya watu wake ni jamii yenye maendeleo. Isiyojua ni dumazi. SD1-09.
Fikra ni nyenzo endelezi au potofu. Changamoto tuliyonayo ni kuchanganua na kutenganisha kati ya fikra endelevu na fikra potofu, kwani mwisho wa fikra ni matendo pale fikra hazibakii kuwa fikra. SD6-07Rev.2-09.
"I am therefore calling upon Mr. Mengi to either surrender whatever evidence he has to support his wild accusations and to appoint the appropriate legal bodies or state organs to act accordingly."
Mengi alishasema kwamba kama itawachoma wao waende mahakamani na hapo ndipo atakapotoa huo ushahidi, sasa tunashangaa huyu mbwana anasema anaonewa na anataka Mwengi hampe ushahidi, inaelekea huyu bwama upeo wake wa kuelewa mambo yaliyo nje ya Ufisadi ni mdogo sana, kama kweli kaonewa na anataka kuprove kwa wananchi kuwa kaonewa basi aende mahakamani hapo ndipo tutakapomwana mengi kama ni uzushi au ni mambo ya kweli
Hapa jamaa kachemsha na inaonekana hata washauri wake ni wavivu wa kufikiri kwani aya ya mwisho inamuonyesha kuchanganyikiwa hivyo kujaribu kumtisha Mengi kuona kama kweli atamuomba radhi ili iwe njia ya kujisafisha. Heri angekaa kimya, maisha magumu!
Hapa jamaa kachemsha na inaonekana hata washauri wake ni wavivu wa kufikiri kwani aya ya mwisho inamuonyesha kuchanganyikiwa hivyo kujaribu kumtisha Mengi kuona kama kweli atamuomba radhi ili iwe njia ya kujisafisha. Heri angekaa kimya, maisha magumu!
Huyu jamaa naona anataka waanze kucheza kidali po! Nani atalala nacho? Kwa hiyo naye atamtuhumu Mengi ili Mengi ndiye aende mahakamani. Hii ngwe bado sana! Ila kama serikali ingekuwepo sasa tungepata mapapa 6 badala ya 5. Mengi alitaja 5 na RA anamwongeza Mengi wenye orodha. Serikali iko wapi jamani? Orodha hiyo tayari inatosha, kwa nini hatuanzi kazi?
- Rostam Aziz, mbunge na mjumbe wa CC aliyeapa kulinda taifa, siku zote hizi anafahamu kwamba Mengi kama raia na mfanyabiashara amekwua akivunja sheria za jamhuri ambazo yeye kama mbunge ameapa kuzilinda kwa nguvu zake zote lakini ameshindwa, sasa anangojea nini kujiuzulu?
- Kwa nini anatishia nyau, badala ya ku-deal straight with the ishu ya Mengi kwamba yeye ni fisadi? Wananchi tunataka ukweli nothing but the truth bila kujali sura ya mtu hapa, wala rangi hii ishu haina siasa ila ni ufisadi tu, nani ni fisadi na nani siye!
- Wananchi wa Tanzania tumechoshwa na Ze-Comedy, sasa ukweli uwekwe wazi, Rostam aende kwenye sheria aseme ya kwake na Mengi ajibu, tusije tena kusikia busara za Spika.
Siasa zisiingizwe kwenye hii ishu ambayo ni 100% legal, na wananchi tusiyumbishwe hapa kwa kuweka mayai yetu yote kwenye kikapu kimoja, tunachotaka ni ukweli bila ya kujali sura ya mtu, Mengi alianza kwa maneno, Rostam amejibu kwa maneno na vitisho, sasa next step iwe kwenye sheria! Kwa sababu Rostam ndiye aliyeanza kulilia sheria, sasa ni wakati wa yeye kuwahi Kisutu! Ingawa record yake hapa inamsuta sana maana kwa kawaida yake angeshausema wazi ukweli alinao mbona kwenye Mtikila hakudai kuombwa radhi na kutishia sheria this time ana ushahidi dhidi ya Mengi lakini anataka radhi kwanza?
From that signed statement, the guy is everything but SMART!
__________________
Jamii ijuayo uwiano thabiti kati ya dharau, ubinafsi, chuki na ustaarab dhidi ya jamii nyingine na baina ya watu wake ni jamii yenye maendeleo. Isiyojua ni dumazi. SD1-09.
Fikra ni nyenzo endelezi au potofu. Changamoto tuliyonayo ni kuchanganua na kutenganisha kati ya fikra endelevu na fikra potofu, kwani mwisho wa fikra ni matendo pale fikra hazibakii kuwa fikra. SD6-07Rev.2-09.