Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Unaishi kwa kipato chako?

    Report Post
    Page 2 of 5 FirstFirst 1234 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 84
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default Unaishi kwa kipato chako?

      Kutokana na hali ngumu ya kiuchumi imenilazimu kuanza kibarua kingine ku "supplement" ajira yangu kuu. Gharama ya nyuma, makadi kibao, na vitu vingine ninavyolipia ambavyo hata sivihitaji imenifanya nijikute nabadilisha sana mtindo wa maisha.

      a. Hakuna kwenda sinema kila weekend;
      b. Hakuna kula out (imebidi nijifunze kupika kitu kingine zaidi ya wali na maharage ya makopo)
      c. Hakuna kwenda mjini kwa gari (naendesha hadi Mall, napaki nakuchukua UDA - SmartBus) siku nikiwa na mizunguko mingi


      Sasa tatizo kubwa lililopo nikilinganisha na nilipokuwa nyumbani ni kuwa hapa kwenye kibarua kikuu na hata hicho cha pili "hakuna mitkasi" ya kuweza kusupplement kipato changu na hasa shughuli nyingi nizifanyazo. Wakati mwingine hali inakuwa ngumu na ninatamani kungekuwa na "njia" ya mkato ya "kibongo bongo" kuweza kujipatia "kipato cha ziada" bila kuhenyeka sana.

      Sasa hili limenifanya nijiulize mtumishi wa umma au hata sekta binafsi (ambaye si mmiliki) anatumia njia gani kusupplement kipato chake na kuafford lifestyle yake? Hivi kwa kipato chako peke yake unaweza kumudu maisha yako au itabidi ufanye mabadiliko makubwa ya jinsi unavyoishi? Je yawezekana kumbe wengi wetu tukipewa nafasi ya kula, tutatafuna bila kukaribishwa na kumegua bila hata kunawa mikono? Je yawezekana baadhi yetu ambao tunatamani kushika nafasi fulani ya kiuongozi tuna upotential fisadism wa aina fulani?

      Endapo mianya yote ya ulaji ikifungwa (no per diems, posho nyingine kama za vikao, za safari, za hali ngumu n.k) utafanya nini? Itakuwaje kama bosi wako anataka uwepo kazini kweli kwa masaa nane na usiende kushughulikia "miradi" yako wakati wa kazi? Vipi kama yule mtu wa supply akiamu kuzingatia sheria na kuhakikisha kitu hakitoki isipokuwa kwa saini na kwa idadi kamili; yaani njia zote za ujanja za kujipatia kipato zikibanwa utaweza kuishi kwa kipato chako au kutafuta shughuli nyingine halali katika muda wako wa ziada?

      Je yawezekana tunaishi katika utamaduni wa kijanja janja kiasi kwamba ufisadi siyo suala la wenye nguvu tu bali pia watu wa chini ambao maisha yao yote wamejifunza "kuula" na hivyo kila mtu anapopata nafasi ya kutumikia kitu cha kwanza anachofikiria ni jinsi gani nafasi hiyo itampa kipato zaidi ya kile kilichoko kwenye mkataba?

      Bila njia za ujanja ujanja tunaweza kweli kuishi kwa kipato chetu cha kawaida.
      bona and NAKAMO like this.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. RukaaJuu Final

    3. #21
      WildCard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 6,455
      Rep Power : 1980
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      59

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Kuishi kwa mishahara yetu kwa MAHITAJI MUHIMU pekee tunaweza. Kinachotuponza Watanzania ni matumizi ya ziada na yasiyo ya lazima kama vile nyumba kubwa(sio ndogo, maana ni ghali sana kuziendesha!), pombe, michango na sadaka za kijinga kama vile harusi, birthday, vipaimara,..., utalii wa ndani, umiliki wa vyombo kama magari bila kuzingatia uwezo wako, kutokuwa wakweli kuhusu vipato vyetu kwenye familia na mambo mengine mengi ya kipuuzi.

    4. #22
      Baba_Enock's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Bunju "B"
      Posts : 5,818
      Rep Power : 1900
      Likes Received
      1162
      Likes Given
      977

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Wakuu wote mliochangia,

      Koleo ni Koleo, and Kijiko ni Kijiko...

      Yule anayeTENGENEZA warsha, semina, kongamano, e.t.c ili aweze kupata posho, nakadhalika ni SAWASAWA na Yule anayeandikisha/anzisha kampuni fake ili aweze kupata kuchota pesa Benki fulani!!!! Tofauti yao kubwa ni "UBUNIFU" na "WINGI" wa pesa watakazopata kwa mkupuo.

      Hawa wote wawili wana NIA CHAFU and ni WABINAFSI!!!!. Hawa wote wawili neno "TAIFA LA KESHO" halipo katika vichwani, wanafikiria zaidi leo na their "families" and "extendend families".

      Tukatae au tukubali - TAIFA ALIWEZE KUFIKA POPOTE kama the working class - either in PUBLIC or PRIVATE SECTOR waendesha maisha yao kwa kutegemea "Per DIEM" au "FAKE BUSINESS DEALINGS". We need a sustainable way of life for ALL OF US (I repeat ALL OF US).

      Nawakilisha
      Ad Majorem Dei Gloriam - "For the greater glory of God"

    5. #23
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22279

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Wakuu wote mliochangia,

      Koleo ni Koleo, and Kijiko ni Kijiko...

      Yule anayeTENGENEZA warsha, semina, kongamano, e.t.c ili aweze kupata posho, nakadhalika ni SAWASAWA na Yule anayeandikisha/anzisha kampuni fake ili aweze kupata kuchota pesa Benki fulani!!!! Tofauti yao kubwa ni "UBUNIFU" na "WINGI" wa pesa watakazopata kwa mkupuo.

      Hawa wote wawili wana NIA CHAFU and ni WABINAFSI!!!!. Hawa wote wawili neno "TAIFA LA KESHO" halipo katika vichwani, wanafikiria zaidi leo na their "families" and "extendend families".

      Tukatae au tukubali - TAIFA ALIWEZE KUFIKA POPOTE kama the working class - either in PUBLIC or PRIVATE SECTOR waendesha maisha yao kwa kutegemea "Per DIEM" au "FAKE BUSINESS DEALINGS". We need a sustainable way of life for ALL OF US (I repeat ALL OF US).

      Nawakilisha
      This is not realistic. If one makes shake deals for survival its not a sin but a sin is to make surplus out of shake deals.

      Naamini kumwezesha mwandishi kwa kibahasha cha nauli ya cha 20,000 kila akija kwenye story sio rushwa na sio dhambi ili mradi mwandishi huyo afanye kazi yake kwa objectivity na sio kufagilia kwa ajili ya kile kijibahasha. Bila uwezeshaji hakuna investigative journalism, jee hii nayo ni rushwa?. Jee uweseshaji wa Ikulu kwa local media to cover presidential visits, nayo hii ni rushwa?. Its not.

      Mwandishi anayekwenda kwa kiongozi na kusema anayo skendo ya kiongozi huyo na kupanga bei ili asiitoe, hii ni blackmail na rushwa mbaya ambayo ni dhambi.
      Ama editor atakayepokea kijibahasha cha 50,000 ili makala zangu za PR za makampuni zitoke, is doing me justice wakati editor huyo huyo akivuta fungu nene ili kuzuia habari fulani isitoke, this is sin.

      Hakuna ubishi kuhusu maisha magumu ya mtumishi wa serikali. Wale wenye kuweza kuongeza kipato kihalali kwa safari, vikao, semina, warsha na makongamano, they are doing the right thing. Wale wanaotumia njia zisizo halali kama kwenye deals za zabuni, they are doing the wrong thing.

      Amini usiamini Per Diem ya serikali kwa mwaka juzi ilikuwa ni 45,000 kwa ofisa wa juu. Hii ndio per diem ya katibu mkuu, waziri mpaka rais!. Kinachowakomboa ni posho na stahili mbalimbali ikiwemo kulipiwa hoteli full board na mengineyo and its not wrong. Its only wrong kama unatafuta hiyo per diem kwa makaratasi tuu huku safari halisi haipo.

      Katika hali kama hii, dhana ya MMKJJ ya kidole kimoja kikielekezwa kwa fisadi na vitatu ukivielekeza kwako ni ya ukweli mtupu. The truth life is a struggle for existance and survival for the fittest. What matters more is 'The End Justify The Means'.

    6. #24
      Susuviri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2007
      Posts : 2,333
      Rep Power : 1063
      Likes Received
      65
      Likes Given
      67

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Outlier
      Samahani Bosi lakini naona unatania maisha ya watu wa maeneo hayo, ama hujawahi kufika!
      How can you possibly, sensibly say watu kule wanaishi maisha mazuri?!
      % ngapi wana access na clean water? Je, huduma ya afya? Umeme? Transport? Akina mama wanakufa wakati wa kujifungua kisa mbali na huduma ya afya, ama wakienda hakuna wataalam. Hospitali daktari afanya upasuaji kwa kibatari- wagonjwa kibao wanakufa.
      na nyumba walizojenga, ni nyumba bora au bora nyumba!
      Acha kutania, maisha ni mabaya- watu hawana alternative, inabidi wayapende hivyo hivyo.
      Mkuu Outlier, sijasema watu wa Rukwa wanaishi maisha mazuri hebu soma vizuri nilichoandika, nilisema mtu mwenye kipato cha 150,000 anaweza kuishi maisha mazuri katika mikoa hiyo. Na yes, nimezitembela mikoa hii mwaka jana, I have seen. Unafikiri ufukara wa kule ni kutokana na watu kupata sh 150,000 kwa mwezi? Watu pale hawaoni hata hiyo 40,000 kwa mwezi. So 150,000 ni pesa nyingi sana, that was my point, please usipotoshe niliyoyaandika!
      That is why I find it so unacceptable for people to demean a 150,000 shs monthly salary!!
      "It is said that power corrupts, but actually it's more true that power attracts the corruptible." - David Brin

    7. #25
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,708
      Rep Power : 3256
      Likes Received
      985
      Likes Given
      760

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Kibunango
      Unataka kuhalalisha kitu gani Kamanda?
      nadhani tukihalalisha itakuwa vema zaidi. Kwa sababu kwa ujanjaujanja watu wanajipatia kipato cha ziada na hakuna panapoonyesha (dhahiri) kuwa pameibwa na hata kama inaonyeshwa kuwa mahali pameibwa hakuna hatua zinazochukuliwa, itakuwa ni vema tukahalalisha malipo haya ya ujanjaujanja na kuyaingiza katika mfumo rasmi ili kuvifanya vipato hivi viwe 'halali.'
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    8. Miaka 50

    9. #26
      Sober's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th June 2008
      Posts : 290
      Rep Power : 641
      Likes Received
      38
      Likes Given
      31

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Mimi nafkiri hali ya watu kufanya ujanjaujanja inatokana na mfumo wa maisha bongo kwa ujumla, pamoja na aspirations za binadamu wengi kutaka kuishi vizuri(naongelea decent life).

      Wengi wangependa wamiliki fenicha nzuri, walau kibanda, usafiri na wasomeshe. Haya ndio malengo ya wengi. Na utakuta wengi wanamshahara ambao si mbaya kihivyo... Tatizo la bongo ukitaka kujenga basi udundulize kimshahara chako, ukitaka fenicha udundulize, ukitaka usafiri udundulize, tuition udundulize na wakati utamkuta mtu ana kazi ya uhakika, amepangisha nyumba analipa 70,000 kwa mwezi, atakaa hapo miaka 20 anampa faida baba mwenye nyumba.

      Kungekua na mifumo mizuri(sio predatory kama TUNAKOPESHA LTD), hii 70,000 mtu angekua analipa wakati anaishi akijua ni nyumba yake, na ataimiliki fully in 15 or 20yrs,.Vivo hivyo kwenye usafiri n.k.... bila hivyo itakua lawama tu as mishahara ya majority ya wafanyakazi bongo HAIDUNDULIZIKI!....

      Mi naamini ukimwambia mtumishi anaelipwa say 250,000...kua kila mwezi utamkata 70,000 kwa kummilikisha nyumba in 20 yrs (mortgage financing)na say 30,000 kwa kumiliki kausafiri(kama wanavyifanya dunia nzima), itampunguzia taharuki ya kujiona anaweza kuwa mtumishi maisha yake yote na kustaafu akiwa hana kitu kabisa.

      Hii taharuki ya kustaafu apeche alolo ndio mwanzo wa mishemishe nyingi...hapa sikusudii kundi linalotaka kumaintain maisha ya matanuzi au kuishi lifestyle za juu.
      Last edited by Sober; 21st January 2009 at 10:00.
      Haangaliwi Mtu Usoni...

    10. #27
      Susuviri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2007
      Posts : 2,333
      Rep Power : 1063
      Likes Received
      65
      Likes Given
      67

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Pasco
      Katika hali kama hii, dhana ya MMKJJ ya kidole kimoja kikielekezwa kwa fisadi na vitatu ukivielekeza kwako ni ya ukweli mtupu. The truth life is a struggle for existance and survival for the fittest. What matters more is 'The End Justify The Means'.
      Sina muda wa kuchambua uliyotasema yote lakini nilichonukuu ni summary ya fikra zako - very sad way of thinking and this is what is causing Tanzania to go to the dogs! Kama wewe ungekuwa kweli fukara wa Rukwa ambaye unategemea 40,000 ya bahatibahati ungeweza kusema hivyo, but I am sure the poor do not say that, save for those who sell their mothers, fathers, sistrers, brothers, daughters and sons who are albinos to be slaughtered for the color of their skin. Unapoiba na vijidili vyako na kuwauza ndugu zako maalbino or any obnoxious deal na kusema eti 'the end justifies the means' You are basically saying 'screw every other human being as long as I can live the life I want, even if I cannot afford it' . It is your right but it is to be condemned and it is despicable.
      I think that from this point of view you are right, you are like the mafisadiz that we are all complaining about! At least you are honest. I personally am ready to say that I have never accepted bribery and have only been forced to give in unusual circumstances. And I am proud of it and I let everyone know, hata nikiitwa -----!
      "It is said that power corrupts, but actually it's more true that power attracts the corruptible." - David Brin

    11. SMU
      #28
      SMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th February 2008
      Location : Mavurunza
      Posts : 4,534
      Rep Power : 3811
      Likes Received
      1312
      Likes Given
      1916

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Pasco
      This is not realistic. If one makes shake deals for survival its not a sin but a sin is to make surplus out of shake deals.

      Naamini kumwezesha mwandishi kwa kibahasha cha nauli ya cha 20,000 kila akija kwenye story sio rushwa na sio dhambi ili mradi mwandishi huyo afanye kazi yake kwa objectivity na sio kufagilia kwa ajili ya kile kijibahasha. Bila uwezeshaji hakuna investigative journalism, jee hii nayo ni rushwa?. Jee uweseshaji wa Ikulu kwa local media to cover presidential visits, nayo hii ni rushwa?. Its not.

      Mwandishi anayekwenda kwa kiongozi na kusema anayo skendo ya kiongozi huyo na kupanga bei ili asiitoe, hii ni blackmail na rushwa mbaya ambayo ni dhambi.
      Ama editor atakayepokea kijibahasha cha 50,000 ili makala zangu za PR za makampuni zitoke, is doing me justice wakati editor huyo huyo akivuta fungu nene ili kuzuia habari fulani isitoke, this is sin.

      Hakuna ubishi kuhusu maisha magumu ya mtumishi wa serikali. Wale wenye kuweza kuongeza kipato kihalali kwa safari, vikao, semina, warsha na makongamano, they are doing the right thing. Wale wanaotumia njia zisizo halali kama kwenye deals za zabuni, they are doing the wrong thing.

      .

      Pasco, nimeshindwa 'kukuelewa'.

      Inawezekanaje mwandishi 'aliyehongwa' kuweza ku retain/maintain objectivity?

      Mwandishi anamtumikia nani? mwajiri? mtoa habari? au msomaji (mteja)? Kama serikali inatakja kufanya uwezeshaji basi iwe ni kwa vyombo vya habari kwa ujumla na si kwa individual journalists. Hii kwa kiasi inaweza kupunguza bias.

      Investigative journalism kwa maoni yangu inatakiwa igharimiwe na chombo cha habari chenyewe and then wana-recover hiyo cost kutoka kwa msomaji (mteja).

      Safari,semina, makongamano etc yasiyo na tija nadhani ndio hasa maana halisi ya ufisadi.
      "Rather than love, than money, than fame, give me truth" ----Thoreau

    12. #29
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,805
      Rep Power : 44131
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1430

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Mpita Njia
      nadhani tukihalalisha itakuwa vema zaidi. Kwa sababu kwa ujanjaujanja watu wanajipatia kipato cha ziada na hakuna panapoonyesha (dhahiri) kuwa pameibwa na hata kama inaonyeshwa kuwa mahali pameibwa hakuna hatua zinazochukuliwa, itakuwa ni vema tukahalalisha malipo haya ya ujanjaujanja na kuyaingiza katika mfumo rasmi ili kuvifanya vipato hivi viwe 'halali.'
      Unapoelekea kuna tisha Kamanda
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    13. #30
      Ncha's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th July 2008
      Posts : 234
      Rep Power : 601
      Likes Received
      12
      Likes Given
      34

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      kama unaona kipato chako ni kidogo sioni tatizo la kutafuta njia za kuongeza ilimradi ni halali. ukiwa na biashara yako nyingine amabyo ukitoka kazini unaisimamia na kuikagua ni njia nzuri ya kuishi.

      Pia unaweza jijengea mazingira mazuri ya kujiajiri kwa njia hiyo. biashara ikikua unaweza amua kufanya kazi zako full time. Ni ngumu kama huna mtaji kujitosa kwenye biashara/kujiajiri kwa kuacha kazi bila kujua kama utafanikiwa.

      Kwa nini per diem isilipwe kama umeenda safari halali ya kikazi. Ni taratibu za kawaida.

    14. #31
      Masaki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 3,043
      Rep Power : 1285
      Likes Received
      333
      Likes Given
      770

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By WildCard
      Kuishi kwa mishahara yetu kwa MAHITAJI MUHIMU pekee tunaweza. Kinachotuponza Watanzania ni matumizi ya ziada na yasiyo ya lazima kama vile nyumba kubwa(sio ndogo, maana ni ghali sana kuziendesha!), pombe, michango na sadaka za kijinga kama vile harusi, birthday, vipaimara,..., utalii wa ndani, umiliki wa vyombo kama magari bila kuzingatia uwezo wako, kutokuwa wakweli kuhusu vipato vyetu kwenye familia na mambo mengine mengi ya kipuuzi.
      Umepiga Ikulu....Hivyo vyote nimevitoa na vingine nimevipunguza kwenye NEW YEAR resoulution yangu!
      Ability may get you to the top, but it takes character to keep you there.

    15. #32
      Leoleo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th July 2008
      Posts : 16
      Rep Power : 557
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Swali la msingi ni kuwa hivi kweli ikiingia serikali makini ikakata mianya yote ya "kipato cha ziada" na kulazimisha watu kuishi kwa malipo yao ya mwezi, wangapi kati yetu wataipigia kura serikali hiyo?

      Kama kuna wapiga kura wa dhati kabisa wenye kupiga kura kwa dhamira halisi inayosukuma matumaini yasiyo ya kinafiki juu mustakabali wao nategemea wachache sana wataipigiakura serikali hiyo kwa sababu kwa mahesabu yoyote malipo ya mwezi ya waliowengi hayatoshelezi mahitaji halisi ya msingi ya familia zao.

    16. #33
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,708
      Rep Power : 3256
      Likes Received
      985
      Likes Given
      760

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Kibunango
      Unapoelekea kuna tisha Kamanda
      Kipi kinachotisha mkuu?
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    17. #34
      Susuviri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2007
      Posts : 2,333
      Rep Power : 1063
      Likes Received
      65
      Likes Given
      67

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Ncha
      kama unaona kipato chako ni kidogo sioni tatizo la kutafuta njia za kuongeza ilimradi ni halali. ukiwa na biashara yako nyingine amabyo ukitoka kazini unaisimamia na kuikagua ni njia nzuri ya kuishi.

      Pia unaweza jijengea mazingira mazuri ya kujiajiri kwa njia hiyo. biashara ikikua unaweza amua kufanya kazi zako full time. Ni ngumu kama huna mtaji kujitosa kwenye biashara/kujiajiri kwa kuacha kazi bila kujua kama utafanikiwa.

      Kwa nini per diem isilipwe kama umeenda safari halali ya kikazi. Ni taratibu za kawaida.
      Ndugu yangu, umenena, sijui kwa nini tunapenda njia nyepesi ya vi-dili. Kuna kazi nyingi halali za kufanya.
      "It is said that power corrupts, but actually it's more true that power attracts the corruptible." - David Brin

    18. #35
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,805
      Rep Power : 44131
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1430

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Mpita Njia
      Kipi kinachotisha mkuu?
      Kuhalalisha ulaji batili, ambao ndio umezaa ufisadi unaopigiwa kelele leo hii.
      Last edited by Kibunango; 21st January 2009 at 13:18.
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    19. #36
      Hofstede's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2007
      Posts : 3,604
      Rep Power : 21341
      Likes Received
      981
      Likes Given
      988

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Kibunango
      Iwapo patatokea serikali makini katika mfumo wa sasa wa maisha, na kubana miaya yote ya mapato ya ziada haitopata kura yoyote toka kwa wafanyakazi. Ingawa asilimia 80 ya Watanzania ni wakulima, sidhani hata hao wakulima kama wataweza kuipigia kura, kwani kwa namna moja ama nyingine nao hufaidika kuwa na ndugu zao wafanyao kazi serikalini.
      Mimi kwa mtazamo wangu ni kwamba wafanyakazi wa serikali wanaweza kuishi kwa kipato chao halali kabisa. Kinachoitafuna bongo sasa hivi ni tamaa. Tamaa ndiyo inafanya maisha yawe magumu bongo.

      99.9% ya wabongo wana ndoto za kuishi maisha ya luxury, hivyo kufanya watu wasiridhike na wanachopata. Na hili ni tatizo la kimfumo kwani mfumo wetu upo hivi ( Serikali, Mfanyakazi wa umma, Mfanyakazi wa sekta binafsi, mfanyabiashara(including wenye nyumba), mkulima, kibaka) hawa ndiyo players wa ugumu wa maisha ya bongo.

      1. Kibaka, huyu yeye anatamani sana kuwa na maisha bora ila ni mvivu wa kufikiri kipato halali na hivyo kuzivia vya wenzake na kufanya uharibifu. Huyu yeye angeweza kudhibitiwa kwa kuwezeshwa na serikali makini kielimu na hata kupewa mbinu za kujitegemea kama kilimo n.k

      2.Mkulima, huyu yeye ndiyo moyo na maisha kwa wote kwani anasaidia kulisha taifa, ila mtu huyu hapo mwanzo alikuwa anakopwa bidhaa zake na vitengo vinavyoanzishwa na serikali isiyo makini, wafanyabiashara pia wanamlipa pesa kidogo kiasi kwamba anaona kilimo hakifai na kupunguza tija na matokeo ni supply kuwa ndogo na vitu kupanda bei.

      3.Mfanyabiashara/mwenye nyumba; huyu yeye anachofanya ni kunyonya kotekote yaani kwa mkulima anamlipa kidogo na mlaji anamcharge sana. Tena hawa wao wanafanya kazi zao zaidi kwa kuangali nini wanapata wafanyakazi. Mshahara ukiongezwa na serikali isiyo makini (ambayo hufanya hivyo kisiasa kwa kutangazia uma) basi hawa huhakikisha kuwa wanachukua zaidi toka kwa mfanyakazi, wenye nyumba nao kila mwaka wanapandisha kodi by 40% - 100% wakishirikiana na madalali bila sababu (free market hiyo).

      4. Mfanyakazi sekta binafsi; hawa wapo makundi mawili, kubwa ni lile la wanaonyonywa sana kwa kulipwa mshahara chini ya kiwango cha kuishi hata kwa siku tano, hawa nao wakipata mwanya lazima waibe, mfano wa kituo cha mafuta wanauza 0.65litre kwa bei ya 1litre(ujanjaujanja).
      Kundi la pili ni wale wanaolipwa vizuri sana, wao hawa ndiyo wanaishi kwa kipato chao halali, kwani wanatumika ipasavyo, hawana muda wa ziada.

      3. Mfanyakazi wa uma. Huyu yeye ndiyo buyu la wanasiasa. kila May Day wanatangaza kuongezewa mishahara kwa kuanzi na Tshs 100, mpaka Tshs 20,000. Sasa hawa ndiyo target ya wafanya biashara, mshahara ukitangazwa umeongezwa kwa hakika shs 100, wao hupandisha bidhaa kwa shs 1000, kuna gap ya shs 900 hapo, hii itatoka wapi? (Jibu sahihi lipo, tumia nafasi uliyonayo kwa kuziba gap hilo na hutaulizwa na serikali kwani wao pia wanajua hilo).


      Kwa serikali makini ikiziba mianya yote nilitaja hapo juu, hakika itapata kura nyingi sana, kwani kinachoongelewa hapa si nominal income (yaani unampa mtu mshahara wa millioni kumi, wakati kodi ya nyumba ni million 11) haisaidii, hapa kinachotakiwa ni Real income ( uwezo wa fedha kununua bidhaa) kama unampa mtu mshahara wa shs 10,000, kodi ya nyumba shs 1000 hata pata wazo la kuziba gap. Serikali makini ni lazima iangalie wafanyakazi katika mtazano wa Real income na si Nominal income. Pia waache kutumia mishahara ya wafanyakazi wa umma kisiasa, kwani kutangaza ni ku-alert "mafisi, vultures (wafanyabiashara) kuwa cha bure kipo.

      Serkali makini lazima itumie sheria kulinda wananchi na si kuitumia pale panapokuwa na manufaa kwao. Naam! Bongo mtu unaweza kuishi kwa kipato halali kama hayo yatafanyika, vinginevyo tutaendelea kuziba GAP.

    20. #37
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,708
      Rep Power : 3256
      Likes Received
      985
      Likes Given
      760

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Kibunango
      Kuhalalisha ulaji batili, ambao ndio umezaa ufisadi unaopigiwa kelele leo hii.
      Hili wala haklitishi Mkuu iwapo utaliangalia kwa mtazamo mwingine. Just fikiria ambavyo watu wanakula fedha lakini hakuna anayeonekana kuwa anaiba. kwa nini vipato hivyo vya kijanja visihalalishwe? kwa sababu hata sasa hivi havionekani kama ni tatizo (kwamba hakuna anayewajibishwa).
      tena vikihalalishwa kutakuwa na multiplier effect-serikali itapata kodi nyingi zaidi (kutoka Paye), vipato vya watu vitapanda-tuta[pungua migomo na maandamano ya wafanyakazi, mzunguko wa fedha utaimarika
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    21. #38
      Caroline Danzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th December 2008
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,723
      Rep Power : 1076
      Likes Received
      652
      Likes Given
      214

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      I salute you susuviri,

      Watanzania tulio wengi hatuna utaratibu wa kufanya sevings, kila siku kwetu ni sikukuu. Fikiria katika hali ya kawaida mtu anayepata kiasi kidogo tsh. 200,000 ana nyumba na familia ya zaidi ya watu 5, anasomesha na kusaidia extended family wakati mtu mwenye mshahara wa milioni 2 hajui hata afanyie nini hela yake, hana familia, hana nyumba etc.

      Tatizo ninaloliona familia nyingi hatuna mikakata endelevu, hatuoni mbali, tumeataliwa na mambo ya kizungu wakati wazungu wenyewe hawana starehe kama zetu. Inasikitisha tunapokaa chini na kulalama eti tusahauliwa wakati ukiulizwa hata unachokipata unakitumije huna majibu sahihi.

      Tujitahi kuwa na mikakati endelevu.

    22. #39
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,805
      Rep Power : 44131
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1430

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Mpita Njia
      Hili wala haklitishi Mkuu iwapo utaliangalia kwa mtazamo mwingine. Just fikiria ambavyo watu wanakula fedha lakini hakuna anayeonekana kuwa anaiba. kwa nini vipato hivyo vya kijanja visihalalishwe? kwa sababu hata sasa hivi havionekani kama ni tatizo (kwamba hakuna anayewajibishwa).
      tena vikihalalishwa kutakuwa na multiplier effect-serikali itapata kodi nyingi zaidi (kutoka Paye), vipato vya watu vitapanda-tuta[pungua migomo na maandamano ya wafanyakazi, mzunguko wa fedha utaimarika
      Naona bado sijakufahamu vizuri, labda tujadili hili kwa mifano halisi kwa yale yanayotokea kila siku katika sehemu mbalimbali za kazi.

      Mfano wakusanyaji kodi za kila siku(service charge) wa Manispaa, hasa sokoni(marikiti). Hawa wana tabia ya kuwa na vitabu viwili viwili ya stakabadhi, ambapo kimoja ni kwa ajili ya mapato yake na kimoja ni kwa ajili ya kupeleka mapato ofisi kwake. Aina hii ya wizi unawaweka katika kundi gani? na aina hii ya ufisadi ukuhalalishwa utaisadia vipi Manispaa na serikali kuu kwa pamoja?
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    23. #40
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,805
      Rep Power : 44131
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1430

      Default Re: Unaishi kwa kipato chako?

      Quote By Hofstede
      Mimi kwa mtazamo wangu ni kwamba wafanyakazi wa serikali wanaweza kuishi kwa kipato chao halali kabisa. Kinachoitafuna bongo sasa hivi ni tamaa. Tamaa ndiyo inafanya maisha yawe magumu bongo.

      99.9% ya wabongo wana ndoto za kuishi maisha ya luxury, hivyo kufanya watu wasiridhike na wanachopata. Na hili ni tatizo la kimfumo kwani mfumo wetu upo hivi ( Serikali, Mfanyakazi wa umma, Mfanyakazi wa sekta binafsi, mfanyabiashara(including wenye nyumba), mkulima, kibaka) hawa ndiyo players wa ugumu wa maisha ya bongo.
      Kwa ufupi ipo haja ya kuandaa mfumo wa aina moja katika nchi na hasa katika sekta ya kutoa huduma na wazalishaji viwandani. Hawa ndio wenye tamaa na tamaa hizo ni za lazima kwao.

      Kila mfanyakazi anapenda kuwa na nyumba yake na kuwa na maisha yanayoringana na nafasi yake kikazi na kifamilia. Hivyo iwapo serikali itaweza kuhakikisha kuwa mahitaji muhimu ya wafanyakazi wake yanapatikana pasipo kadhia ya aina yoyote itakuwa ni rahisi sana kwa wafanyakazi hao kuridhika na maisha yake. Hii kwa upande mwingine itapunguza mambo mengi mno ambayo yanawazonga wafanyakazi.

      Kuna mdau hapa kaandika vizuri namna serikali itakavyoweza kuondoa tamaa za msingi za wafanyakazi. Iwapo hilo likiwezekana then kwa mara ya pili Watanzania wafanyakazi wataweza kuishi kutokana na mapato yao.
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    Page 2 of 5 FirstFirst 1234 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 0
      Last Post: 25th November 2011, 22:27
    2. Je unamiliki mali zaidi ya kipato chako?
      By Nazjaz in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 13
      Last Post: 9th May 2011, 00:23
    3. Kinyesi chako
      By Washawasha in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 13
      Last Post: 26th February 2011, 04:19
    4. Replies: 5
      Last Post: 27th November 2008, 01:33

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...