Re: Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

By
Mzee Mwanakijiji
Kwa mara nyingine tena hoja ya Bunge kupitisha sheria ya kurudisha ofisi ya Kadhi Mkuu linajitokeza tena huku waislamu wakitaka Bunge litunge sheria ya kutambua uwepo wake na wakristu wakipiga kelele kuwa kufanya hivyo ni kuvunja Katiba. Hoja yangu leo ni kuwa, Waislamu hawahitaji kibali cha serikali kuanzisha ofisi ya Kadhi Mkuu kushughulikia mambo yao yanayoendana na sheria za Kiislamu.
Waislamu wakae wao wenyewe wapitishe uwepo wa ofisi hiyo na kuendelea na shughuli zao. Ilimradi tu, maamuzi ya ofisi yao hiyo hayaingilii uhuru wa Mtanzania mwingine au utendaji kazi wa sheria zetu za makosa ya uhalifu na jinai. Pia waelewe ya kwamba uwepo wa ofisi ya Kadhi Mkuu ni subject ya Katiba ya Muungano na Mtanzania yeyote kimbilio lake la mwisho ni mahakama ya Kiraia. Zaidi ya yote, watakapoanzisha ofisi hiyo, wajue kuwa isiwalazimishe waislamu wote kutatua matatizo yao kupitia ofisi hiyo isipokuwa wale ambao kwa hiari yao wanataka kufanya hivyo.
Kanisa Katoliki kwa mfano linayo mahakama yake na sheria zinazoliongoza kanisa hilo (Canon Law) na mahakama yake hiyo ina ngazi za rufaa hadi Vaticano. Hata hivyo Mkatoliki ana haki ya kutumia sheria hizo kuhusu masuala mbalimbali ya kanisa lake, lakini anapofanya kosa la jinai, sheria za kiraia (civil law) zinakuwa na mamlaka. Hivyo basi, waislamu wasisubiri Bunge kupitisha ofisi ya Kadhi Mkuu bali waianzishe wao wenyewe huku wakiweka bayana kabisa kuwa ofisi hiyo haitahusika na makosa ya jinai au kupingana na Katiba ya nchi. Then, hakutakuwa na haja ya kugongana!!!
Mwanakijiji,
Awali ya yote ulitakiwa ujuwe waislam wa Tanganyika walikuwa wanahitaji nini. Znz mambo hayo yameshafanyika. Upande wa Malalamiko yao makubwa ni kuwepo kwa mahakama ya Kadhi ambapo mahakama hiyo itambulike kisharia kwani kinachotakiwa hapa ni maamuzi yake yanayotokana na Mahakama hizi yaweze kutambuliwa kisharia za Tanzania. Sasa huwezi hata siku moja kuanzisha mahakama zako Tz na maamuzi yake yakatambulika kisharia pasi na kutambuliwa mahakama au kubainishwa na Katiba yenu.
Lakin pia waislam hao wameenda mbali zaidi kuwa mambo watakayoshughulikiwa na mahakama hizo ni miradhi, ndoa na Talaka tu. mengine yote yatafuata utaratibu wa Serikali.
Na wameomba Serikali izingatie kuwa waislam nao ni miongoni mwa walipa Kodi hivyyo nao wapewe ruzuku kama inayopewa kanisa katika kuongoza Hospitali zake kama KCMC, Bugando na nyinginezo au hata Universities za kanisa.
Hoja zao zimeenda skuli sana inahitaji uwe makini sana kuwafahamu na kutoa majibu. na sio kutoa majibu mepesi katika masuala mazito.
Mimi nafikiri waTz muanze kufikiri nje a box kama mlivyoweza katika Sharia zenu za Bank na kuruhusu Islamic banking.
Last edited by Barubaru; 11th July 2012 at 13:03.
Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.
Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul
Follow Us Here