Jamani wanajumuiya ya Wa-Tanzania tuishio British Virgin Islands tumeshutushwa na habari kuwa kuna baadhi ya viongozi wetu serikalini wana shahada za PhD kutoka kisiwani hapa. Ukweli hapa hakuna chuo kama hicho. Hiki kisiwa ni kidogo mno kuna wakazi wapatao 23,000. Kisiwa hiki kina secondary 2 na community collage moja.
Uchumi wa kisiwa hiki unategemea sana Utalihi na Financial services which includes offshore banking and registration of companies. Baada ya kutembelea web site ya Commonwealth Open University, Ni kweli nimegundua kuwa imekuwa registered hapa. Cha ajabu address yao ni ya hapa(box no.) lakini, Palm Chambers ambalo ni jengo halipo hapa. Kuonyesha kuwa ni fake, hawakutoa simu yao, ila wametoa fax number. Kutokana na fax number hizi number ni za USA (Florida).
Baadae nilikwenda kwa msajiri wa makampuni nilielezwa kuwa Commonwealth Open University imekuwa registered kama kampuni lakini haina Learning Institution yoyote. Baada ya kuuliza zaidi information hizo, niliambiwa nijaze form harafu nitapewa details baada ya kulipia $ 25.
Registry Of Corporate Affairs,
P.O . Box 418,
Road Town, Tortola, British Virgin Islands.
Fax 1 284 494 6331:
Simu 1 284 494 5491:
E-mail
corporateregistry@bvifsc.vg Website
www.bvifsc.vg
Sikuweza kulipia ili nipate maelezo hayo. Baada ya kujadiliana na wenzangu hapa tumejua kuna watu wajanja wachache wanatumia mwanya huu kuwaibia fedha watu na kuwapa degree baada ya kuwalipa pesa. Hicho chuo hakipo, hao jamaa ni matapeli.
Naomba serikali, Wizara ya Elimu, UTUMISHI mjue kuwa hakuna chuo kama hicho hapa. Kama kingekuwa ni chuo basi tungeweza kuona hizo ofisi zao hapa. Kuna Mtanzania mwenzetu ambaye amekaa hapa zaidi ya miaka kumi. Hajawahi kuona ofisi hiyo (Palm Chambers).
Tuko tayari kushirikiana na mtu yoyote ili kukomesha ununuaji wa yeti fake hasa kwa viongozi wetu.
Shukrani.