Nimepitia post nyingi sana na yapo mambo muhimu ambayo yanahitaji majibu. Kwa bahati mbaya maswali mazito yamekuwa hayajibiwa kikamilifu bali yanababaishwa. Tunaomba majibu kwa ktoka kwa yoyote anayedhani ataweza kutusaidia.
Mohamed Said, nimepitia hoja zako nyingi kwa umakini. Napenda nikukukumbushe msemo wa kiingereza unaosema '' If you have a problem and you can't solve it, you're the problem in first place''.
Bakwata: MS- 'serikali ilipiga marufuku uanzishaji wa taasisi nyingine'. Mabadiliko yametokea na leo kuna Bakwata, Taasisi ya waislam, shura ya maimam, haki na mali za waislam(ponda), haki za waislam (khalifa) n.k. MS 'amesema wamejifunza kutoweka mayai katika kapu moja'
Nakuhakikishia MS huna ufaham wa dhati kuhusu taasisi hizi. Nyingi ni za maslahi binafsi na si waislamu (ushahidi upo) . Hoja ya mayai katika vikapu tofauti si sahihi, mengine si mayai ni visa.
MS,hakuna anayekataa kuwa wazee wetu waliotoa mchango katika harakati za uhuru. Ni asiye na ufaham atakayeamini kuwa AA, TAA au TANU vilianza na Nyerere. AA ilikuwepo kuanzia 1920 hata kabla ya Nyerere kuzaliwa. Viongozi wengi walikuwa waislam, hakuna ubishi. Tatizo ni pale pasiposemwa ukweli. Mfano, eti hakukuwa na wapagani enzi hizo! eti Nyerere alikuwa muovu tu hakuna jema alilofanya na wazee wenzake. Eti, mfumo wa Nyerere umedumaza elimu ya waislam,mbona hatuelezwi hali ilikuwa vipi wakati wa ukolon?Eti, ni waislam peke yao walioleta uhuru! n.k.
Kama kitabu chako kingekuwa na mizania sawa, na kisingekuwa na chambe za udini na kuficha ukweli, kingesomwa sana duniani. Bahati mbaya sana kwa maneno yako ya ' wame, hawa, wao,sisi n.k umelenga kundi fulani la jamii kuwa wasomaji wako na watakubali tu kwasababu wanajua wewe ni MS. Unapoteza sehemu kubwa sana ya wasomaji ambao kwa kujua ukweli wangekuwa sehemu ya 'solution' ya matatizo unayoainisha.
Unaposema historia ya wazee wako na Nyerere sasa ni 'Classic', kwa kukwepa au kushindwa kujibu au kukiri udhaifu na mapungufu fulani kunaondoa thamani ya neno 'classic' na kuwa replaced na ''controversy'.
MS, kwa weledi wako mzuri sana ninashangaa unapohoji vitu kana kwamba wasomaji ni mbumbumbu. Huko mitaani walikoishia darasa la 4B au 7 D watakuelewa ukisema '' kwanini wanakataa tusijiunge na OIC'. Hapa JF ni tofauti sana. Kujiunga na OIC sio tatizo, suala ni je kuna faida? kuna hasara? tunaweza kufanya hivi bila kuathiri mfumo wetu wa maisha? tunaweza kukubaliana bila matatizo?, si suala la mbona msumbiji wamejiunga na ni wakristo? yes, wamejibu maswali yanyokidhi haja ya jamii zao kwanza.
MS, umesema mbona hawataki ijengwe shule 'Darul Iman', jiulize katika mvurugano wa jumuiya lukuki za kiislam nani anaweza kuhoji kwa niaba ya waislam? Ni Ponda, ni Khalifa, ni Bakwata, ni Kundecha au sheikh wa kibaha! Tatizo si 'wao' ni nyinyi (nachukia kusema hivi).
Jiulize pale kibaha kuna shule ya WHIPAS si ya waislam ile! Lakini jambo la muhimu zaidi ni kujiuliza kwanini unadhani kuzuiwa shule kunarudisha maendeleo ya waislam nyuma na usijiulize haya yafuatayo.
1. Kwanini shule za waislam zinzotegemewa kuwa na maaadili zinaongoza kwa utovu wa nidham? (Ushahidi ninao).Jiulize hivi ile shule ya Ali Hassan Mwinyi Dodoma ina wanafunzi 250 na walimu 2, unategemea miujiza gani hapo kama si kufeli 'big time', kabla ya kulalamika kuhusu Darul Islam mmefanya nini kuhusu Ali Hassan Mwinyi sekondari.
Jiulize, ilikuwaje Al haramain ilipokuwa na walimu 'serious' waliwahi kuingiza wanafunzi Chuo kikuu karibu asilimia 80 ya darasa, nini kimetokea baada ya hapo! kwanini walimu walikimbia.(nina ushahidi na hili).
MS, kwanini usiangalie kuwa shule mbovu kwa matokeo ni za Waislam, na ni hizo hizo zina walimu 'unqualified' 3 na wanafunzi 400.
MS, jiulize kwanini mtoto wa kiislam anayesoma Marian pale bagamoyo anakuwa wakwanza kitaifa? Jiulize ni kwanini waislam wenye uwezo wapeleke watoto wao shule ya masista kule Morogoro? Je umewahi kufanya ziara ya utafiti katika seminari na kuona tofauti!
MS, unaposema wamezuia Darul Islam, tuambie hizi zilizopo zina ubora gani! je suala ni wingi au ubora?
Kama kunadhuluma ya kujenga chuo kikuu huko nyuma hiyo ni historia kama ya wazee wako, sasa tuambie kile cha Morogoro kinaendeleaje na kwanini wahadhiri wanakimbia tena ni waislam? why!
Vyombo vya habari: Mimi nadhani ni vigumu kuvilaumu. Leo Ponda anasema hili, kesho halifa anajibu hivi keshokutwa Shaaban simba anasema hivi, siku nyingine Kundecha anajibu hivi, sasa ninani mwenye kauli juu ya waislam. Pili kauli zingine zinaashiria kuvuruga taifa. Hebu fikira MS yupo katika TV anasema '' wao wametudhulum wamechukua asilimia 85% ya viti vya ubunge, Sisi tunasema wao wasije n.k.
Wabunge hawateuliwi Mohamed, wanapigiwa kura na ninawapongeza wananchi kwa kuchagua watu na si dini. Nigeria haijawasiaidia hata kidogo. Simamisheni watu wanaokubalika na jamii. Ukisimamisha mgombea kwasababu ni muislam, tayari unapoteza nusu ya wapiga kura. Na miongoni mwa wapiga kura wako wapo watakaokukataa.
Kuna mbunge mwislam anakubalika katika jimbo lenye wakristo wengi kwasababu ya weledi wake si dini yake.(ushahidi upo)
Matatizo mengi yapo ndani ya jamii ya waislam, lakini kuna njia za kutaka kukwepa ukweli kwa kutumia visingizo tu. Narudia msemo '' If you can't solve a problem, you're the problem in the first place'
Ahsante
Follow Us Here